DOKEZO TAKUKURU na Usalama wa Taifa, fuatilieni haya; nchi inahujumiwa. Kuna rushwa, urasimu na ufisadi mkubwa

DOKEZO TAKUKURU na Usalama wa Taifa, fuatilieni haya; nchi inahujumiwa. Kuna rushwa, urasimu na ufisadi mkubwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Nchi ikishakua na namba moja alafu kilaza na asieweza fanya maamuzi basi nchi hiyo inakua imefeli sana. Hilo swala la nida nakiri kweli wanazingua japo sina ushahidi wa mtu kutoa hela ila wanausumbufu njoo kesho njoo kesho mpka ukipata namba umesota na bado vitambulisho vikifika serikali za mtaa kukutafuta napo uanze kuomba sana yaani tabu tupu
 
Sajo,

Tatizo ni kubwa. Unacheka kama mazuri.

Nimekumbuka kitu... Mtihani wenyewe wa Hisabati Darasa la 7 ni multiple choice (wa kuchagua).

Imagine kitu kama hicho kilipata 'clearance' ya watu wa TISS huko , Hisabati mtihani wa kuchagua, kweli?!

Leo nchi tuna watoto hawajui kuhesabu, wame pass.
Yani inafika hatua unazisoma comment humu hadi unasikitika tu, kwasababu huna cha kufanya na inaumiza sana.
 
Kuhusu mafuta utayaona Jumatano maana bei itapanda sana kutokana na dollar
 
Kuna mahali nimekuta waganda kama 20 wasiojua hata kuongea kiswahili vizuri, cha ajabu wote wana Tanzania ID
Sasa wa Rw, ndio husema waziwazi, kwamba ukiwa na hela ya kutosha, unapata tu bila shida.

Na kweli wameunga unga makaratasi na wanavyo.

Tumepuuza mambo makubwa na ya msingi sana nchi hii
 
Kwanza nikupe hongera sana mwandishi kwa uzalendo!!

Mara kadhaa nimekuwa nikitoa lawama kwa watu wa usalama kushindwa kulisaidia taifa katika mambo mengi sana.

Mifano ni mingi sana lakini hili la rasilimali za taifa kutumiwa hovyo na watu kwa maslahi ya watu wachache linaumiza sana. Juzi kati tu tumeshuhudia wazawa wakihamishwa kwenye makazi yao rasmi waliopatiwa na mwenyezi Mungu ili tu mwekezaji wa nje apewe hilo eneo afanye kwa manufaa yake, nchi yake na wale waliompatia. Inaumiza sana watu wa usalama ambao kwa kweli ndiyo wanatakiwa kuona ustawi wa mwananchi mmoja mmoja unaheshimiwa lakini wamegeuka kuwa watafutaji na walinzi wa wezi wa rasilimali za taifa.

Hatujakaa vizuri kuna hii issue ya bandari naona nayo kuna upigwaji mkubwa kwa taifa. Hata kama haujui sheria lakini ukiwasikiliza watu wa serikali na ukasikiliza wale wanaooupinga kwa facts unaona kabisa upande upi uko kwa maslahi ya nchi na upi unaangalia matumbo ya watu wachache.

Kuna wakati hii idara inatakiwa isiangalie sura ya mtu ijikite katika kuliangalia taifa maana sisi sote tutapita lakini taifa hili litaendelea kuwepo. Kwanini idara isione kuwa mwaka 2500 taifa letu litakuwa linaiongoza dunia? Nasema hivyo nikimaanisha kwamba lazima waone kuwa rasilimali za taifa hili zikisimamiwa vizuri zinaweza kuifanya nchi kupiga hatua kubwa baadaye. Mfano Magufuli japo alikuwa na madhaifu yake lakini kuna namna alilifanya taifa lianze kuonekana linapiga hatua kwa kasi na usimamizi wa rasilimali za nchi ulikuwa unaona angalau huyu mtu anajali. Hata mirafi mingi ya kimkakati ilikuwa inawapa moyo sana wananchi na ndiyo maana walianza kulipenda sana taifa lao.

Tiss tafadhali msipuuze yanayosemwa na watu nyinyi viapo vyenu ni kwa ajili ya maslahi ya taifa na si kwa ajili ya maslahi ya chama fulani au kikundi fulani cha watu.
 
Ila kumbuka TISS kazi yao si kutekeleza, wao ni kutafuta taarifa,kuchakata ,kisha kuzipeleka kwa boss wao
Hilo nalijua wazi kabisa.

Ila tusibeze nguvu yao ya ushauri, wana njia nyingi za kuhakikisha ushauri wenye manufaa unafanyiwa kazi
 
Kwanza nikupe hongera sana mwandishi kwa uzalendo!!

Mara kadhaa nimekuwa nikitoa lawama kwa watu wa usalama kushindwa kulisaidia taifa katika mambo mengi sana.

Mifano ni mingi sana lakini hili la rasilimali za taifa kutumiwa hovyo na watu kwa maslahi ya watu wachache linaumiza sana. Juzi kati tu tumeshuhudia wazawa wakihamishwa kwenye makazi yao rasmi waliopatiwa na mwenyezi Mungu ili tu mwekezaji wa nje apewe hilo eneo afanye kwa manufaa yake, nchi yake na wale waliompatia. Inaumiza sana watu wa usalama ambao kwa kweli ndiyo wanatakiwa kuona ustawi wa mwananchi mmoja mmoja unaheshimiwa lakini wamegeuka kuwa watafutaji na walinzi wa wezi wa rasilimali za taifa.

Hatujakaa vizuri kuna hii issue ya bandari naona nayo kuna upigwaji mkubwa kwa taifa. Hata kama haujui sheria lakini ukiwasikiliza watu wa serikali na ukasikiliza wale wanaooupinga kwa facts unaona kabisa upande upi uko kwa maslahi ya nchi na upi unaangalia matumbo ya watu wachache.

Kuna wakati hii idara inatakiwa isiangalie sura ya mtu ijikite katika kuliangalia taifa maana sisi sote tutapita lakini taifa hili litaendelea kuwepo. Kwanini idara isione kuwa mwaka 2500 taifa letu litakuwa linaiongoza dunia? Nasema hivyo nikimaanisha kwamba lazima waone kuwa rasilimali za taifa hili zikisimamiwa vizuri zinaweza kuifanya nchi kupiga hatua kubwa baadaye. Mfano Magufuli japo alikuwa na madhaifu yake lakini kuna namna alilifanya taifa lianze kuonekana linapiga hatua kwa kasi na usimamizi wa rasilimali za nchi ulikuwa unaona angalau huyu mtu anajali. Hata mirafi mingi ya kimkakati ilikuwa inawapa moyo sana wananchi na ndiyo maana walianza kulipenda sana taifa lao.

Tiss tafadhali msipuuze yanayosemwa na watu nyinyi viapo vyenu ni kwa ajili ya maslahi ya taifa na si kwa ajili ya maslahi ya chama fulani au kikundi fulani cha watu.
Point kubwa sana uliyosema kwamba sisi na watoto wetu tutapita, lakini Taifa na vizazi vijavyo vitakuwepo.

Kuna mambo makubwa sana ya msingi hao wenye viapo wameyapuuza.

Leo elimu yetu haizalishi watu wenye ujuzi. Imekuwa elimu ya ovyo.

Leo umaskini unazidi viwango kila siku.


Wengine wana tozwa tozo. Wengine wanaiba hizo hizo tozo.
Ukihoji, Waziri mzima anakwambia hamia Burundi. Huyo ni Waziri kabisa wa serikali.!
 
Ni usiku mnene. Naamua kuandika DOKEZO hili.
Kwa uchungu wa yanayoendelea katika nchi yangu.

Katika mada hii, nitaomba wachangiaji kujadili kwa uwazi kabisa, na kuongezea mifano mingine baada ya hii nitakayokuwa nimeiweka hapa.

Lengo ni Nia njema kabisa kurekebisha pale tulipokosea na kusaidia WaTz ambao wanakosa kufaidi matunda ya nchi yao.

Hapa chini ni jinsi ambavyo mambo ya ovyo yanafanywa wazi na TISS wala hawafanyi kazi yao iliyotukuka.

1. NIDA na Utoaji wa NAMBA/Vitambulisho vya Taifa.

Hili jambo ni kubwa sana. Mimi nimelithibitisha. Na wote wanaofika kuhudumiwa katika ofisi zote za NIDA nchi nzima wanasema wazi.
Iko hivi, huwezi kufanikisha kupata namba ya NIDA ikiwa huna kiasi flani cha fedha. Na huwezi kupata ile ID ikiwa huna kiasi kikubwa zaidi cha fedha.
Yani utaenda utafuata taratibu zote na kuwa na viambatanisho vyote, lakini huwezi kupata kimojawapo kati ya hivyo bila fedha.
Kiufupi hadi mlinzi wa getini anajua hilo.
Baadhi ya Ofisi za NIDA DSM kupata namba ya NIDA inaanzia sh. 150,000/-. Kupata ID ni kuanzia sh. 500,000/-
Lakini kadri utakavyoongeza dau maana yake utawahishiwa zaidi mchakato wako.

Kwanza hakuna huduma pale, zaidi ukifika upangwe foleni na walinzi, ukiingia unakuta mtu anachat tu, hadi jioni uambiwe njoo tena kesho.

Haya yana muda mrefu yanafanywa wazi kabisa. Hatari hii ni kwamba sasa hata mgeni je, akiwa na milion zake mbili si anapewa zake ID kama MTz??

Mh. Rais wetu ni msikivu, je, ulishasikia amepewa ripoti hii akashindwa kuifanyia kazi?!

Nani wa kumpelekea ripoti kama sio TISS?

2. Mradi wa mwendokasi Mbagala.
Huu mradi nendeni mchunguze, ni mbovu na umejengwa chini ya viwango vibaya mno.

Uchunguzi unaonesha baadhi ya miundombinu kuanza kuharibika hata kabla ya matumizi rasmi kuanza.
Wasichokijua ni kwamba hii miradi ya miundombinu ya barabara huwa na zaidi ya miaka 20 ya uhai kabla ya marekebisho.
Sasa ukifika pale ukakuta baadhi ya beacon zimeanguka, kumeguka, n.k, Unajiuliza shida ni nini? Bajeti ndogo ya ujenzi? Lakini hilo linakataa kwa sababu hizi fedha ni mkopo tumepata kutoka Benki ya Dunia (WB), hawawezi kutenga fedha chini ya inayotakiwa.!
Sasa vile vituo vya abiria ndio utacheka kabisa. Mabati ni chini ya viwango, hizo frame walizichomelea ni chini ya viwango, uchomeleaji wenyewe ni wa dizaini za fundi maiko.

Hata wakibisha, nawahakikishieni, barabara ya mwendokasi ya Posta KIMARA itadumu, na hii ya Mbagala itakuja kuharibika mapema kabla yake. Tuko hapa mtakuja kuthibitisha panapo uhai.

Sasa kwa hali hii, utasema Rais wetu alivyo msikivu, ana hii ripoti mezani kweli? Na hatujasikia akichukua hatua zozote?

3. UHABA wa petrol sasa hivi nchini.

Hapa siandiki sana.
Fahamuni kwamba mafuta yapo. Si mlisikia hata Waziri anasema hakuna upungufu wa petrol. Si amesema mara nyingi tu!

Sasa Mimi na wewe tuulizane, Waziri anasema yapo, vituoni ukifika hakuna, yapo wapi? Eeh...

Jamaa wana mafuta, ila hawatoi kuyauza. Wanasubiri bei mpya za August, zipande usiku wa leo tarehe 31/07/2023 ndio wataanza kutoa mafuta.

Sasa "syndicate" ya namna hii, hapo unasema TISS wapo na wananchi, au wametuma ripoti Rais hajachukua hatua?!

Achaneni na mambo ya ooh Dola $ kuadimika, hiyo inaathiri uagizaji wa mzigo mpya. Sio stock iliyopo ambayo huagizwa miezi mitatu au zaidi nyuma.

4. Nauli za mabasi za LATRA.

Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!

USHAHIDI upo.

Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!

Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.

Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.

Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.

Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!

Narudia ripoti hii ni kwa Nia njema ya kujenga Taifa letu.

Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.

Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.

Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.
Ndugu umefanya vizuri kuandika haya! Lakini kwa sisi wazee wa zamani kidogo tunachojua ni kuwa TISS haipo tena kwa maslahi ya taifa! Rais Mwinyi alijitahidi kuboresha kwa kuajiri wataalamu wazuri na kuanzisha idara kamili ya TISS kila wilaya, Mkoa na Taifani. Akawapa vitendea kazi vya kutosha nakumbuka mapajero 500 yaliagizwa mwanzoni!. Muda unavyokwenda hawa jamaa wakawa sehemu ya ufisadi na uasi dhidi ya wananchi. Unakumbuka wasiojulikana na madhara yake? Sasa nani kama mama amewapa nguvu na kinga ya kutoshtakiwa! Aliwarudisha ikulu wamlinde yeye anapouza nchi na raslimali za taifa! Hakuna aliyeshitukia haya.

Wanachoweza ni Ulevi tu kila club wapo wanalewa 24/7 hours. Na kuonyesha vibastola vyao!

Wa kuaminiwa ni TPDF na idara yake ya Intelgence! \Tutafute namna ya kuwafikia!
 
Nimesoma ripoti yote hakuna la uongo hata moja
1. Kwenye hilo la NIDA mpaka 50 watu wanapokea.. Rushwa!
2. La mbagala hili lilishasemwa sasa! Mpaka namna tenda ilivyopatikana.. Rushwa!
3. La petrol kuna andiko limeichambua vizuri mno.. Rushwa!
4. La LATRA ni mulemule.. Rushwa..!

Ni rushwa ni rushwa ni rushwa mwanzo mwisho! Lakini si tunakumbuka angalizo la mkuu wa kaya kuhusu kula kwa urefu wa kamba? Dosari ilianzia hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
So ni Rushwa kwa kwenda mbelee ..
 
Sasa wa Rw, ndio husema waziwazi, kwamba ukiwa na hela ya kutosha, unapata tu bila shida.

Na kweli wameunga unga makaratasi na wanavyo.

Tumepuuza mambo makubwa na ya msingi sana nchi hii
Kuna siku akili itatukaa sawa
 
Ndugu umefanya vizuri kuandika haya! Lakini kwa sisi wazee wa zamani kidogo tunachojua ni kuwa TISS haipo tena kwa maslahi ya taifa! Rais Mwinyi alijitahidi kuboresha kwa kuajiri wataalamu wazuri na kuanzisha idara kamili ya TISS kila wilaya, Mkoa na Taifani. Akawapa vitendea kazi vya kutosha nakumbuka mapajero 500 yaliagizwa mwanzoni!. Muda unavyokwenda hawa jamaa wakawa sehemu ya ufisadi na uasi dhidi ya wananchi. Unakumbuka wasiojulikana na madhara yake? Sasa nani kama mama amewapa nguvu na kinga ya kutoshtakiwa! Aliwarudisha ikulu wamlinde yeye anapouza nchi na raslimali za taifa! Hakuna aliyeshitukia haya.

Wanachoweza ni Ulevi tu kila club wapo wanalewa 24/7 hours. Na kuonyesha vibastola vyao!

Wa kuaminiwa ni TPDF na idara yake ya Intelgence! \Tutafute namna ya kuwafikia!
Kwani tunapuuza mambo ya msingi kama nchi.?!

Hivi kweli unaweza tazama tu mradi mkubwa kama wa Mbagala mwendokasi unajengwa chini ya viwango?!

Na hujali! Then unajiita na kuji proud sisi, ndio TISS.

Kuhusu Military Intelligence umesema la maana, ila je , unajua ni mara ngapi imezidiwa nguvu ya siasa na hii TISS iliyopo! Anyway tuishie hapo,
 
Kwa hali hii ambayo nchi inapitia, uongozi mbovu, rushwa, ubinafsi, ufisadi, nepotism na vetting mbovu, uonevu nk tatizo ni TISS.

Chanzo cha tatizo ni muundo usiofaa tulio nao, yaani tunachagua mtu mmoja (Rais)wakati wa uchaguzi mkuu halafu anakuta pale ikulu timu ya watu (TISS) wengine wana miaka hata 20 wako hapo.

Cha kushangaza TISS siku zote wanadai kazi zao ni ngumu, hivi kuna mtu anapenda kufanya kazi ngumu kwa muda mrefu, hata km analipwa vizuri, kwanini hatuoni wao TISS kuomba kubadilishiwa kazi kwa sabab ya kazi ngumu wanazofanya? hapa kuna hila na Kati ya mambo wanamwambia Rais mpya ni kuwa wao (TISS) ndio wamefanya yeye Rais afike hapo, maana yake, bila wao asingefika hapo na hivyo wao ndio wanao urais wake.

Rejea maneno ya Rais wa awamu ya 5 akilalamikia kuwa anachomekewa watu wasiofaa kwenye uteuzi(waziri mpya kushindwa kusoma kiapo) na imetokea Rais mstaafu anakuwa na watu wake wengi ndani ya TISS ili aendelee kuongoza ndicho kinachotokea Tanzania na inavyoonekana TISS inaundwa na kundi kubwa la vijana yaani ni under age kulingana na nature ya kazi wanazopaswa kufanya TISS kwa nchi, ndii maana uonevu ni mwingi sana Tanzania.

Kuna nchi moja ndani ya SADC Rais mpya alipoingia ikulu kwanza alibadilisha intelligence team yote, tumeona hata Rais Tinubu amefanya hivyo..

Pili, Rais huyo mpya aliteua intelligence team wote wapya na kazi ya kwanza aliyowaambia wafanye ni kwenda kila kata na kijiji ndani nchi kufanya mikutano ya hadhara ili kuwaambia wananchi KAZI ZAO NI ZIPI KWA NCHI.

Hivi tunavyoongea Rais mstaafu wa nchi hiyo na baadhi ya maafisa wakubwa wastaafu akiwemo chifu wa intelligence mstaafu wako uhamishoni wamekimbia nchi.

Hivi ndivyo wanaojua uongozi na wana ajenda ya maendeleo wanapochaguliwa hufanya mara tu wanapoanza urais.

Tanzania imekwama sabab kubwa ni vested interest za wastaafu kupitia TISS angalia baadhi ya mawaziri hata tu tathmini ndogo ya face value judgement kuona km wanastahili kuwa mawaziri inakupa jibu HAWASTAHILI..lakini hao ndio TISS inawataka wale wasiojielewa anasukumwa tu km boya!

Hii shida ya bandari kutokuwa na tija inayopelekea kutafuta wawekezaji chanzo ni TISS angalia huyo DG wa sasa wa TPA bado mtoto hana sifa kabisa za nafasi hiyo, na sabab za kuweka mtu wa aina hii ni wao TISS kuwa na access ya kuinfluence utendaji na maamuzi yake throughout, a similar case hata kwa spika wa bunge, taifa lenye umri zaidi ya miaka 60 eti halina watu wazima wenye sifa za kuwa spika au DG wa TPA..si kweli!

Dawa ni wananchi kudeal na issue ya TISS wanavyopatikana wakati Rais mpya akichaguliwa na kazi zao kwa ujumla..tusipofanya hivi, nchi itakwama zaidi ya hapa tulipo.
Umedadavua mambo mengi ya maana sana.

Halafu hii kila mara wakikosolewa wanakimbilia kudai wewe hujui, kazi yetu ngumu sana, tunakesha tunakulinda, wewe umelala usingizi. . .kama ulivyosema mbona wamo tu kila siku kama kazi ni ngumu, lakini si ndio wanalipwa kwa kazi hiyo?!

Na mengi uliyosema, ueledi unapuuzwa sana kwa sababu ya maslahi binafsi, hata ya mtu asiyekuwa serikalini, ana access na hawa wana intelligence, wananchi watakuwa manamba na watumwa ktk nchi yao
 
Back
Top Bottom