TAKUKURU, Polisi waja na muarobaini wa rushwa za barabarani wakishirikiana na wadau

TAKUKURU, Polisi waja na muarobaini wa rushwa za barabarani wakishirikiana na wadau

Kila trafik anapiga hesabu amiliki harrier tk la nyani..... Usipime
Trafik anafanya Kazi kwa siku afunge hesabu kama ataingiza 50000 au 70000
Kuna wakati kulikuwa na tuhuma ya matrafik Kupeleka hesabu kwa wakubwa zao nao?
Nkirudi kwenye suala la rushwa tz ni ngumu kuondoka

Ova
 
Ila wazee ma ofisa wa takukuru na ma police hawapendani sana aisee wakikutana kwny anga zao.

Kuna jamaa wa takukuru alipiga mzinga usiku akiwa na harrier yake tako la nyani alikua mtungi,jamaa wa police walivyokuja kupima wakawa wako fresh tu kwny mambo ya 'favour' ila walivyoambiwa tu jamaa ni takukuru wakasema safi sana ngoja tumnyooshe.

Aisee report ilitolewa bila chenga chenga kama ilivyo,jamaa alikua amelipia comprehensive insurance ya gari yake so hakulipwa chochote kwa report ile ya majamaa.
 
Daah basi kama ni hivyo rushwa haiwezi tena kuisha mkuu, maana kipindi hiki kipindi hiki mishahara hata wiki 2 kufikisha ukiwa bado upo ni chamgamoto sana.

Nilidhani kwa mjeda kupewa u-boss pale Takukuru basi rushwa itapungua/kuisha kabisa lkn naona bado imetamalaki.
Rushwa na njaa vinaendana
 
Hahah kuna jamaa yangu walimkamata na escudo yake short chasis wakamwambia ndg yangu mbona unatembelea ka gari ka zamani hivi aisee,umekapiga rangi mpk kamegomaa kung'aa jitahidi ununue hata Noah basi hahah.

Kila trafik anapiga hesabu amiliki harrier tk la nyani..... Usipime
Trafik anafanya Kazi kwa siku afunge hesabu kama ataingiza 50000 au 70000
Kuna wakati kulikuwa na tuhuma ya matrafik Kupeleka hesabu kwa wakubwa zao nao?
Nkirudi kwenye suala la rushwa tz ni ngumu kuondoka

Ova
 
Hahah kuna jamaa yangu walimkamata na escudo yake short chasis wakamwambia ndg yangu mbona unatembelea ka gari ka zamani hivi aisee,umekapiga rangi mpk kamegomaa kung'aa jitahidi ununue hata Noah basi hahah.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Ova
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) leo imefanya maongezi ya kimkakati na Wadau mbalimbali wakiwemo Sekta Binafsi, Sekta za Umma, Asasi za Kiraia, Taasisi za Dini, Vyombo vya Habari, Viwanda vya Uchapaji na Uchapishaji, Kampuni za Simu, Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri, Wasanii, Madereva wa Vyombo vya Moto na Wananchi kuelezea Kampeni inayotarajiwa kuzinduliwa ya kupunguza ama kutokomeza kabisa rushwa Barabarani.

TAKUKURU imeeleza kuwa Kampeni hiyo imepewa jina la ‘UTATU’ ikimaanisha ni muunganiko wa pande Kuu tatu: TAKUKURU, Jeshi la Polisi na Wadau

Imedaiwa kuwa lengo kuu la kampeni ni kuzuia rushwa za barabarani ambayo imebainika ni kisababishi kimojawapo cha ajali zinazotokea barabarani; tatizo ambalo limekuwa likikemewa sana na viongozi mbalimbali wa Serikali. Aidha imesema UTATU huo unatakiwa kuweka mikakati ya pamoja na endelevu ya kutibu tatizo la ajali badala ya kulaumiana na kunyoosheana vidole.

Kampeni hiyo imejiwekea mambo malengo mahususi manne, ikiwa kila lengo linatakiwa kutekelezwa na kila mdau kwa nafasi yake:
  • Kudhibiti vitendo vya rushwa miongoni mwa wasimamizi wa sheria za barabarani
  • Kuandaa mkakati wa kuzuia vitendo vya rushwa barabarani
  • Kushirikisha Umma kuzuia vitendo vya rushwa barabarani
  • Matumizi ya TEHAMA kudhibiti vitendo vya rushwa barabarani
Kuhusu matumizi ya TEHAMA kudhibiti vitendo vya rushwa barabarani, TAKUKURU imesema tayari limeanza kutekelezwa kwa kutengeneza mfumo utakaotumika kuchukua matukio ya vitendo vya rushwa kwa kutumia simu ya mkononi (Mobile App).

Mfumo huo (Mobile App) utakaozinduliwa pamoja na Kampeni hii ya UTATU, utapakuliwa kutoka Play Store au App Store ya simu ya mkononi kisha mtu ataweza kupiga picha za video, mnato au sauti na kuzituma TAKUKURU.

Baadhi ya Majukumu ya Wadau wa Kampeni hii yametajwa kuwa:

Wasimamizi wa sheria na miundombinu ya Barabara (TANROADS, TARURA, LATRA na wengine)
Wanalo jukumu la kusimamia ubora wa miundombinu na Vyombo vya Usafiri ikiwa ni pamoja na
  • Kuboresha sheria, kanuni na miongozo
  • Kuboresha miundombinu ya barabara na mizani
  • Kusimamia usajili wa Vyombo vya Usafiri
  • Kuhakikisha alama za usalama barabrani zinaonekana vizuri
  • Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa barabarani
Wasanii wa fani mbalimbali
  • Wana jukumu la kuhamsisha watumiaji wa barabara kupitia Sanaa zao zinazosisimua na kuburudisha huku ujumbe wao ukisaidia kubadili mitazamo ya watumiaji wa barabara kuacha vitendo vya rushwa
  • Wanatarajiwa kutoa michango yao ya kuandaa Sanaa zitakazohusiana na kampeni ya UTATU

AZAKI wao wametajwa kuwa wahamasishaji ambapo majukumu yao yatakuwa:
  • Kuhamasisha wananchi kutuma taarifa za vitendo vya rushwa barabarani
  • Kuhamasisha wananchi waache uoga wa kutoa taarifa za rushwa
  • Kutumia mtandao wao kutoa taarifa za vitendo vya rushwa
  • Kuhamasisha wananchi kuacha kutoa rushwa kwa masimamizi wa sheria za usalama barabarani
Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri ambao majukumu yao ni
  • Kusimamia Vyombo vya Usafiri ili kutoruhusu magari mabovu kuingia barabarani
  • Kuajiri madereva wenye sifa na kuwalipa vizuri
  • Kuacha kutoa Rushwa ili wapate leseni bila kufuata utaratibu
  • Kuwachukulia hatua madereva wazembe
  • Kuwasimamia madereva kuacha kutoa rushwa kwa wasimamizi wa sheria za usalama barabarani
Wamiliki wa Vyombo vya Habari ni kundi lingine ambalo katika Kampeni hii majukumu yake yamebainishwa kuwa
  • Kuelimisha wananchi kupitia Vyombo vyao vya Habari
  • Kusaidia kutoa nafasi kwenye Vyombo vya Habari na kurusha matangazo kuhamasisha kampeni
  • Kutoa taarifa za vitendo vya Rushwa

Wamiliki wa Viwanda vya Uchapishaji na Uchapaji wao wataweza kushiriki kwa:
  • Kusaidia kuchapa machapisho ya kuhamasisha kampeni
  • Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa
Vingozi wa dini wao wana majukumu muhimu ya
  • Kufundisha maadili kwa waumini wao ili wasitoe rushwa kwa wasimamizi wa sheria za usalama barabarani
  • Kutumia Vyombo vya Habari vinavyomilikiwa na dini zao ili kuhamasisha kampeni
  • Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa

Katika mkutano huu, wadau walioshiriki kutoa maoni wamedokeza haya:-

Kwanza, wamesema Rushwa ni mtazamo wa ndani ya Polisi na nje ya Polisi, watu wanaona Polisi ni fursa. Kwenye vitengo vinavyoongoza kwa rushwa ni pamoja na kwenye kutoa leseni, ukaguzi wa barabarani. Polisi walio kwenye Pikipiki maarufu kama ‘tiGO’ na madereva wa magari ya Kirikuu wanaodai kuwa wakipita ni lazima wasimamishwe na kuombwa rushwa

Aidha, wengine wamehoji kwanini TAKUKURU hawapo barabarani? Huku wengine wakisema ni bora adhabu ziongezwe kwenye makosa ya barabarani na adhabu ya fedha iondolewe kabisa.

Wengine wakiwemo Viongozi wa Dini wametoa maoni kuwa hofu ya Mungu ndio suluhisho pekee la tatizo la rushwa kwa wananchi wanaweza kuwaepuka TAKUKURU na Polisi ili wasikamatwe kwenye masuala ya rushwa. Pia, Polisi wakiwa na hofu ya Mungu wanaweza kukataa rushwa na kuwakamata wanaotaka kutoa na hivyo kuzuia rushwa.

Lakini, kuhusu App TAKUKURU waliyozungumzia wadau wamesihi sana kuwa kunatakiwa kuwe na elimu ya awali itakayotolewa kwa Wananchi kabla ya kuanza kutumia App hiyo na pia kuwapa muda Wananchi kuielewa.

Wametaka pia Makamanda wa Polisi na watumishi waboreshewe maslahi kwa kuwa hiyo inaweza kuwa njia mojawapo ya kuzuia rushwa.

Mtoto acha kupiga mayowe. Cheza watu waone wenyewe
 
Kudhibiti rushwa ni rahisi sana. Ikithibitishwa askari wa barabarani amembambikia kosa dereva afukuzwe kazi baaasi
 
Wazo zuri kwa kiasi chake lakini ni wazo na mikakati ya ajabu kama taifa kutafuta tiba ya rushwa 'BARABARANI' ikiwa rushwa 'BARABARANI' inachagizwa na utuamiaji wa vyombo vya moto na watumiaji wa vyombo vya moto hawazidi 25 asilimia kama taifa. Ni ajabu!

Mikakati hiyo ingeelekezwa kila sekta na taifa kwa ujumla maana rushwa 'BARABARANI' ni theluthi tu. Zipo rushwa katika ofisi, shule na huduma mbalimbali za kijamii zinazochagiza theluthi kubwa.

Tiba ya rushwa 'BARABARANI' ni kufumua na kuanzisha jeshi la polisi upya, utuamiaji wa teknolojia, maisha bora na kutengeneza sheria zinazoendana na karne ya 21.
 
Labda itungwe sheria ya kunyongwa akipatikana mtu Ana Toa ama kuchukua rushwa!
Hapo rushwa ndiyo itapungua nchi hii

Ova
 
TAKUKURU imeeleza kuwa Kampeni hiyo imepewa jina la ‘UTATU’ ikimaanisha ni muunganiko wa pande Kuu tatu: TAKUKURU, Jeshi la Polisi na Wadau

Ni hilo tu au kuna agenda za siri?

Kwanini kampeni hiyo ipewe jina "utatu" ambalo hakuna asiyefahamu kuwa ni neno la msingi kwa imani ya kanisa.

Uislam umekuja kuweka sawa kuwa "utatu" ni shirki.

Wabaduli jina hilo. Halikubaliki na Watanzania wote.

Kampeni ni njema nia ni ovu.

Ntawashangaa sana Mashehe waliokaribishwa kuzungumzia kampeni hii kama hilo la "utatu" watalikalia kimya.

Binafsi sijaafiki kampeni hii kupewa jina hilo na nalipinga hadharani.

Jina hilo libadilishwe na liwekwe jina ambalo halihusiki na imani za watu wa Tanzania ili kuepusha fitna.
 
Rushwa=umasikini + ukosefu wa maadili.

Cctv camera kama zitafungwa maeneo wanaposimama trafiki zinaweza kusaidia kwa namna moja au nyingine.

Njaa ya mapolisi ikiwa ni pamoja na mishahara midogo ni miongoni mwa vichocheo vya vitendo vya rushwa kwa trafiki polices na ndio mzizi wa vitendo vya rushwa.

Ukosefu wa maadili nalo pia ni tatizo sugu kwenye hili swala la rushwa na imani hayo mambo hapo jui yakiboreshwa tunaweza kupiga hatua kadhaa kwenye hii vita.
 
Threat of self review. Same police who take bribe are the one who form part of the task force for the issue.

Citizen who require a meccy from police officers by being un qualified for road running are the one who also a part of the team.

Simba kapewa ulinzi wa mbuzi zizini.
 
Serikali haijaamua kutokomeza rushwa .. Hawa Askari wakifungwa Kama 20 hivi na kesi zao zikaenea nchi nzima rushwa itapungua kwa kasi.

Sehemu zote za rushwa zinajulikana na hao takukuru wanayajua Ni issue ya kisiasa tu kujifanya hawajui hayo maeneo.

Hakuna taasisi ya hovyo Kama takukuru huwa sioni kazi Yao kabisa.. Wanashindwa kuingia field wakamate watoaji na watoa rushwa eti wanasubiri alieombwa rushwa ndio aende kutoa report kwao.. Huu Ni ujinga...

Case nyingi mtaani Ni mtoaji na mtoa rushwa wanashirikiana.. kusubiri muombwaji aende takukuru huku Ni kutojua wajibu wao. Maana yake Ni kwamba wametoa room mombaji na mtoa rushwa wafanye business as usual.

Takukuru ivunjwe Kama si kurekebishwa sijawahi kuona kazi Yao ya maaana.. inabidi wawe kila sehemu kufuatilia utolewaji na utoaji wa rushwa na sio kukaa maofisini kusubiri muombwaji wa rushwa aje ...
 
Huku Moshi ndio kumeoza kabisa. Hiace inasimamisha abiria hapa hapa stendi kwenye askari wa barabarani waliopangwa kuangalia usalama wa abiria.

Magari yanatoka vijijini yamepakia abiria na madumu ya pombe (mbege). Abiria wakilalamika wanadharauliwa kwa sababu kuna wakubwa wanawalinda hao wamiliki wa magari. Tunapata tabu sana hasa magari ya Kibosho Kirima na Umbwe.
 
YEHODAYA, Yaani TAKUKURU kwa hili wanatuhadaa. Sidhani kama hawajui tatizo la trafiki . Hii ni kauli ya kinafiki. Mimi mke wangu ameamua haendeshi tena gari Arusha. Maana hata gari haina kosa lazima utoe pesa. Kuendesha gari Arusha ni kero.
 
Back
Top Bottom