Yah ni kweli. Ila ni bora mtoto akawa mtoto. Mimi binti yangu ana maswali mengi sana lakini ni yale, unaondoka, utachelewa kurudi, unaenda wapi, baba ulikuwa wapi, huyu ni nani, mama atakuja lini kukaa na sisi kama fulani anakaa na baba na mama...Nadhani ni malezi pia au ukuaji wa mtoto mwenyewe
Mpaka hapo kakua ndo anakoelekea pia...mi mwanangu wa kiume ni miaka 9 pia lakini hathubutu kuniuliza maswali ambayo anajua yataniumiza japo najua anatamani kujua mengi ila anahuruma sana...huwa ananiangalia sana machoni kujua hali yangu au mood yangu.Ni mwema sana kwa kweli.Yah ni kweli. Ila ni bora mtoto akawa mtoto. Mimi binti yangu ana maswali mengi sana lakini ni yale, unaondoka, utachelewa kurudi, unaenda wapi, baba ulikuwa wapi, huyu ni nani, mama atakuja lini kukaa na sisi kama fulani anakaa na baba na mama...
Ana image ya family lakini si ndoa wala kuolewa hayo hayaelewi elewi bado.
Pole sana,,Umenena ukweli mtu na licha ya watoto pia ninaudhaifu kuishi mwenyewe hua naathirika Hadi kiafya
Kweli mkuu! Watoto wanatofautina uelewa.Inategemea na mazingira, Binti yangu akiwa na 4yrs alitulazimisha na mama yake tumueleze ukweli unaoleweka tumempataje pataje baada ya kumueleza uongo mara kadhaa.... So Yuko hivo tangu kuzaliwa maana hata Sasa lazima aniulize baba unakoenda utaridi saa ngap na muda ukipita ataomba simu anipigie nimwambie Niko wap... Yaan ni balaa saana huyu mtoto
Najua unaonyesha upendo nimekushauri binti ajaribu kutofautisha upendo unaompa wewe na jinsi ambavyo wazazi wengine wanavyo wapenda wanaoSure binafsi najitahidi kuhakikisha upendo na ndio umetawala kwangu
Aisee🤔 MUNGU amlinde huyo mtoto wa kike.Nnaimani mnaendelea vizuri wanajamii forum,
Kama kawaida yangu kuwaleteeni Mikasa inayonitokea kwenye maisha yangu, sababu hapa ndio sehemu pekee nisiyojulikana uhalisia wangu, napata uhuru zaidi wa kufunguka ili kupata ushauri wa kunikosoa na kuniita moyo.
Ni hivi baada ya kutengana na aliyekua mke wangu, Sasa tunaelekea mwaka wa nne, na muda si mrefu tunakamilisha talaka.
Hapo awali mwanamke aling'ang'ania kukaa na watoto kitu ambacho kiliniumiza saana. lakini nikacheza na akili yake kiasi Cha yeye mwenyewe kutamka kuniachia watoto wangu niishi nao.
Hata hivyo nilishapata mwanamke kutoka nchi jirani ambaye niliamini ataishi vizuri na watoto wangu Hawa wadogo baada ya kua nae kwenye mahusiano kwa kipindi Cha mwaka kabla hajarudi kwao.
Nilimsafirisha kutoka nchini kwao Hadi hapa Tz na Sasa ananilelea watoto, na watoto wangu naona wakipendeza japo huyu Binti angu akibadilika badilika mood.
Mama Yao (mtalaka) aliumia saana kiskia kuna mwanamke naenda kuishi nae, kitu ambacho alitaka aje ampe masharti (kumtisha) huyu mwanamke wangu mpya (step mother) endapo hatoishi vizuri na watoto wake, kitu ambacho Mimi nilimkataza.
akasema anajua atakachofanya kwa watoto maana atawajaza sumu ili wajilinde dhidi ya huyo step mother wao hili nalo nilimuonya lakini nadhani alilifanya kwakua Kuna mambo napambana nayo Sasa nadhani ni matokeo ya hizo sumu.
Binti (9yrs) yangu amekua hamfurahii step mother wake bila sababu ya msingi hata nilipokaa nae kuzungumza nae aliniambia Hana tatizo nae zaidi aliniuliza kwann nimeachana na mama Yake?
Ni desturi yangu kufanya nao ibada pamoja na kuwasaidia masomo Yao hivo wamekua wakiniuliza maswali mbali mbali kwakua wanajua baba Yao hua sifichi.
Mara kadhaa nimekua nikiwasisitizia majukumu Yao ya baadae watakapokua wakubwa kwamba wakiume atakua baba na familia yake na wakike atakua mama wa familia yake.
kila ikifika hatua ya kusema Binti yangu ataolewa na kua na familia yeye anabadilika sura na kukataa kati kati kwamba hato olewa Wala kuzaa nikimuuliza kwann anasema hataki tuu...
Nawaza saana na kujiuliza yule mama yake ni kama mfeminist tuu anakauli za kusema hataki tena kuolewa na haamini katika ndoa na ndoa ni kama utumwa Sasa anaishia kuchapika tuu mjini naona kabisa hiki kilicho kichwani kwa Binti yangu ni matokeo ya kuachana na mama Yao na ndio sumu alizomtia Binti yangu...
Wataalamu nisaidieni nawezaje kumuokoa Binti yangu dhidi ya hili balaa maana Dunia ishaharibika..
Note: kataa ndoa ushauri wenu naujua MSIkomenti.
Imeshatokea sasaMtoto wa Miaka 9 unaongea nae kuhusu mambo ya Kuolewa na Kuzaa?
Aisee☹️Fanya linalowezekana uongee vema na mkeo. Huyo bado ni mkeo, huyo mpya sisi hatumfahamu. 😄
Mh! Endelea kujifanya mjanjaWazazi wakiachana, watoto ndio wanaoteseka.
Poleee sanaa, Lol
Ni kweli kabisa unachosemaMtoto wa miaka 6-8 anauwezo wa kutumia asilimia 80 ya ubongo wake na ndiyo maana wachina huwa wanawaweka pamoja watoto wenye akili wenye umri huo, (incubate), and nurturing
Inatokea kuzungumza kulingana na mada uliyouliza sio from no where... Hata hivyo utamficha vip na anaona kwenye movie na tamthilia??9years is too young to be discussing marriage. Huyo ni mtoto saizi awaze vitu vya umri wake. Friends, shule, masomo hata muwe mnaulizana akikua anataka kua nani, kama anataka kuwa pilot basi maramojamoja unamtreat flight moja kwenda mkoa wa tofauti kuchochea ndoto zake, kama ni kuwa doctor unamnunulia books ama vitu vinaendana na career anayotaka. Unamuelekeza kwenye vitu tofauti kabisa na mambo ya ndoa. Sasa miaka 9 mnadiscuss ndoa kweli 🙄🙄 Hebu kuwa serious baba nanii
Yap mazingira na nafasi Yako kushirikiana nao kwenye mambo muhimu kama ibada na masomo humo ndo maswali hutokeaYah ni kweli. Ila ni bora mtoto akawa mtoto. Mimi binti yangu ana maswali mengi sana lakini ni yale, unaondoka, utachelewa kurudi, unaenda wapi, baba ulikuwa wapi, huyu ni nani, mama atakuja lini kukaa na sisi kama fulani anakaa na baba na mama...
Ana image ya family lakini si ndoa wala kuolewa hayo hayaelewi elewi bado.
Kwa jinsi ulivyoandika inaonekana una experience kwenye hili, hongera kwa kuArchive...Pole sana mkuu, ila unapaswa kujiuliza wewe upo tayari tayari kabisa kumuacha aende?
Katika maisha ya ndoa/uhusiano hua kunakipindi baina ya mmoja huwa anakengeuka. Kipindi hiki huwa ni kigumu sana ambapo kama ikikosekana umakini watu hawa hujikuta wametengana ile hali bado wanapendana.
Kingine ni mtoto anaposema jambo la kikubwa ujue limetoka/kalisikia kwa mtu mzima. Unapaswa ukae na binti yako umueleze ukweli halisi mambo yalivyokuwa kama wewe ndiye mwenye makosa au mama yake. Na usioneshe kumnyooshea zaidi kidole mama yake. Usitie uongo hata kidogo ili wewe uonekane kujisafisha. Yule ni mtoto bado ni malaika, utafanya mambo yawe magumu zaidi.
Fanya linalowezekana uongee vema na mkeo. Huyo bado ni mkeo.
Muulize kama yuko tayari kuona watoto wakiukosa upendo wa baba na mama? Yuko tayari kuruhusu hili ile hali yeye bado yuko hai?
Zungumza naye maneno ya kihisia zaidi... gusa point muhimu..
Yaani dah.. natamani hata ningekutwangia simu nikuelezee... 🤗
Hilo swali la "Kwanini uliachana na mama?" sio la mtoto ni la mama. Yang'amue vizuri maswali anayo kuuliza huyo bintiyo.
Lakini inaonesha wife bado anakuhitaji ila anashindwa ajirudishe namna gani. Hawezi kujirahisisha ataonekana bwege. Mfungulie njia umrudishe.
Hope so japo na Mimi nilishangaa saana reaction yake juu ya Hilo!Pole sana.
Ila kwa umri wa huyo binti yako na masuala ya kuolewa mara kuzaa umemuwahi sana,bado mdogo. Mpe muda baadae atakuwa na maamzi sahihi kwa ajili yake.
Mambo yamebadilika mzeeMtoto wa Miaka 9 unaongea nae kuhusu mambo ya Kuolewa na Kuzaa?
Tabia ya hovyo sana hii.Mtoto wa miaka 9 ushaanza kumpigia hesabu za kuolewa🤔