Tamasha la WCB Mtwara ladhihirisha Uchumi unazidi kuimarika! Watanzania wana pesa mifukoni

Tamasha la WCB Mtwara ladhihirisha Uchumi unazidi kuimarika! Watanzania wana pesa mifukoni

Mkuu, embu jaribu kutumia akili yako japo pengine hauna au ipo kidogo, hivi kweli watu kujaa fiesta ni indicator ya kupima kuimarika kwa uchumi au ubora wa maisha wa watu?
Ofcoz, ni evidence mojawapo. Mtwara toka imezaliwa haijawahi tokea ile, is that not improvement ya maisha ya watu.
 
Mkuu Je hao walijaa kwenye hivo viwanja ni % ngapi ya watanzania wote ?
Mkuu mbona unauliza maswali magum Sana, ivi unategemea mtu aliyetoa post Kama hii akakupa jibu kwel? Hawez kukupa hata
 
Unafikiri Tamasha lingekosa watu ungesemaje wewe dada?
 
Dah, watanzania bado tuna safari ndefu sana, yaani kila kitu ni siasa tu.....!!!
 
Wanatamani kuandamisha Watu lkn hawana Watu wamebaki na smartphone kutangaza nchi yetu vibaya hata kama mm nitalala njaa nitalala njaa na nchi yangu Tanzânia
 
Pangua hoja
Ivi hapo Kuna hoja gan Sasa, mbona hakuna hoja yeyote zaidi ya upuuzi, ivi Tanzania in watu wangap? Hapo kwenye hivyo viwanja wameenda watu wanagap, na kiingilio kilikua Bei gani? Hebu tuanzie hapo
 
Huyu mwehu tumemvua nguo fb, kumbe na huku yupo na anatumia I'd hii.
Fb watu siku hizi naona wamekua sana kuliko jf.
Jf kuna wastaarabu sana huku.
Kule kalala mutini
Mkuu hebu muanike Hapa tumjue ni Nani maana wajinga Kama vizur kuwaanika ili wajulikane
 
Tamasha mtu anasimama zaidi ya masaa 4 na hana hata kinywaji achilia mbali msosi. Kujazana huko ndio dalili ya umaskini na ni kweli haijapata kutokea watu kuwa maskini namna hii.

Nyie hata mafao ya 25% mnasema mnatetea wanyonge, mmeidandia timu ya taifa kutafuta kick sasa inapumulia mashine ila wakati wenu huu endeleeni kuonyesha upumbavu wenu.
Ila timu ya taifa ingeshinda Kuna mtu angepewa sifa Sana kama vile na yeye alikua anacheza pale uwanjan, tumefungwa kimyaaaa
 
Uwanja kujaa inapogeuka kuwa kipimo cha uchumi kukua - maajabu mengine.

Kuna siku tukila sahani imejaa msosi aka "mlima" basi tutaambiwa uchumi unapaa tunakula tunashiba.
 
Uwanja kujaa inapogeuka kuwa kipimo cha uchumi kukua - maajabu mengine.

Kuna siku tukila sahani imejaa msosi aka "mlima" basi tutaambiwa uchumi unapaa tunakula tunashiba.
Mbona usipojaa mnasema ni kigezo cha watu kukosa hela na uchumi kubana?
 
Jana kule Mtwara kumefanyika tamasha la wasafi ambalo limeacha historia kwa kufurika watu kwa kiasi ambacho haijapata kutokea watu kujaa namna ile kwenye uwanja wa Nangwanda.

Pia kule wilaya ya Kahama msanii Ali Kiba naye amefanya tamasha ambalo limeacha gumzo kwa kujaa watu.

Kitendo cha watu kujaa kwenye matamasha haya kimeenda kinyume kabisa na CHADEMA ambao wamekuwa wakieneza propaganda kuwa uchumi umeshuka na watu hawana pesa mfukoni.!!
Chadema ,hasa Tundu Lisu wamefikia hatua ya kuichafua nchi kimataifa kuwa eti Tanzania kwa sasa hali ni mbaya kiasi kwamba watu wanashindia mlo mmoja.!

Sasa tuwaulize nyie chadema ,hivi mtu ambaye anashindia mlo mmoja atatoa wapi hela ya kulipia tamasha na kushangilia mwanzo mwisho kama tulivyoona kule Mtwara na Kahama?

Ifike mahali mkubali tu kuwa kasi ya rais Magufuli ni kubwa kuliko uwezo wenu wa kufikiri.
Kwa hiyo mmewalenga sababu mnajua wamepokea hela ya korosho eti? Mbona hamkwenda kufanya fiesta yenu mwezi Julai?

Halafu we jamaa kweli hukwenda shule kabisa. Kufurika kwa watu kwenye fiesta ndio dalili ya kuimarika kwa uchumi???? Hahahahahahaha......
Nacheka kwa dharau!!!!!!!
 
Naona wachumi wa jiwe wameongeza indicator mpya ya kukua kwa uchumi.Ndiyo maana Mwijage alitumbuliwa maana na yeye alikuwa na fikra sawa na huyu ndugu.
 
Ujinga na ubwege umewajaa nyumbu wanaoamini watu wenye kauli mbili, leo wanasema hivi kesho vile. Lakini bado nyumbu zinaamini. Hao ndio ujihoji wamelishwa nini
Kweli kabisa. Mara waseme wafanyabiashara wasinunune mara wanaita tena waje wanunue!! HIzi Kauli mbili mbili zinaligharimu taifa!!
 
Kule wameuza korosho huku mahindi yetu yamekatazwa kutoka nchini
 
Sijui CCM hutumia mbinu gani kupandikiza ujinga na ubwege kwenye vichwa vya watanzania wenzetu!!




Furaha na amani ya nchi yetu ndiyo MBINNU ambazo CCM ina tumia kupandikiza maendeleo ya ya nchi yetu kwa vijana wetu bila kusahahu uthubutu wa Rais wetu Mpendwa Magufuli kudhibiti Rushwa, Ufisadi, Wizi wa rasilimali zetu, uporaji na matumizi mabaya ya fedha za umma na ufufuaji wa viwanda na mashirika ya umma.
 
Maneno Meier hayo mambo mabaya yote uliyoyaorodhesha wakati yanafanyika ni chama gani kilikuwa madarakani kama si CCM? Na wakati huo Magufuli si alikuwepo kama Waziri, Mbunge na Mjumbe wa vikao vya CCM?

Huu utetezi wako unanirudisha kwenye kushangaa, hivi mna nini nyie watu!?
 
Mkuu, embu jaribu kutumia akili yako japo pengine hauna au ipo kidogo, hivi kweli watu kujaa fiesta ni indicator ya kupima kuimarika kwa uchumi au ubora wa maisha wa watu?
Ndiyo CHADEMA na Tundu Lissu, Zitto Kabwe na wengineo wote wametuchafua sana nje. Hawa watu walitakiwa wasionekane tena katika hii nchi. Sio watu wazuri kwa nchi yetu.

Wewe unaweza ukakata tawi ambalo unalikalia? Hawa watu sio tu wanamhujumu Magufuli bali lengo lao ni kututeketeza sisi.

Ina maana nyie mnakubali matanzania mwenzetu aziombe serikali za EU na Ulimwengu wasisaidie Tanzania kwa sababu Rais aliye chaguliwa kuongoza nchi ni wa CCM?
 
Back
Top Bottom