Tamko la waumini wanaopinga Parokia ya Kawe kuendeshwa kinyume cha taratibu za Kanisa Katoliki


Nina maandiko mawili kwenu katika magomvi yenu ya wenyewe kwa wenyewe;

1 Corinth 14: 33; 33 For God is not a God of disorder but of peace—as in all the congregations of the Lord’s people.

Mathew 7:21-23: 21“Not everyone who says to me, ‘Lord, Lord,’ will enter the kingdom of heaven, but only the one who does the will of my Father who is in heaven. 22 Many will say to me on that day, ‘Lord, Lord, did we not prophesy in your name and in your name drive out demons and in your name perform many miracles?’ 23 Then I will tell them plainly, ‘I never knew you. Away from me, you evildoers!’
 
Nilisoma juzi ila sikutoa maoni. Kanisa Katoliki tunabahati ya kuwa na viongozi wa ngazi kwa ngazi mpaka kumfikia Papa au Baba Mtakatifu.

Haya matatizo yangepelekwa kwa kiongozi wake ambae ni Askofu, akishindwa kuyatatua yangeenda kwa Kadinali.

Kuweka haya matatizo hapa ni kuanika nguo chafu nje kwenye kamba.
 
Halafu uone walivyo na tabia ambayo sijaipenda, yaani kwenda siku moja tu kuambia Mzee Rwaichi hayupo tayari wamekata tamaa. Utadhani hawajui kuwa baba anaumwa
 
Yaani nyie ni kamati ya ufuatiliaji tu! na vipi Halmashauri yenu ya walei? mbona wao hawako nanyi kwenye hili? Fateni sera za kanisa katoliki mambo ni kwa hirakia tuu?
Kama hayo malalamiko Yenu mlisha yapeleka ngazi husika na hata Askofu wa jimbo mmekutana naye.... Sasa huku JF umeyaleta ya nini? Maana ukweli unabaki kuwa mwenye uamuzi wa mwisho juu ya Parokia na hata nani awe paroko ni Askofu wa jimbo
Baraza la Walei nadhani ni chombo cha kumsaidia paroko kufanikisha maendeleo ya Parokia kiimani na ki uchumi Ila si kumuongoza paroko au kumuongoza
Kanisa katoliki halina utamaduni wa waumini kumkatalia padre kuongoza Misa.. lina utaratibu wa kukabiliana na migogoro ya ndani
Kama kwenye Parokia hiyo mmefikia kufanya hayo mliyoyafanya.. basi kuna kila sababu ya sisi tuliosoma post yako hii kuamini kuwa baraza la Walei la Parokia hiyo lina tatizo kubwa na yawezekana kwa sehemu kubwa ndio wanaochangia mgogoro huo ( kama upo kweli) na mtoa post hii ni among the Ring learders.
 
Hapo walei wametafuta mwanya wa kupiga sadaka na miradi ya kanisa Padre anaonekana kathibiti kila kona sasa wanaamua kumpiga majungu. Nani aliwaambia kuwa kuna demokrasia katika kanisa? kuna usemi wa kilatini usemao ROMA LUCUTA CAUSA FINITO maana yake ni kwamba kiongozi wa juu katika kanisa akitamka hakuna kupingwa, linguine kanisa ni tajiri wa waumini haliangaingi kufanya promo ta maupako, kutoa mapepo wala kubeba waamini kwa magari, kama kanisa limewashinda? kuna makanisa mengi hapo mjini akina gwajima , mzee wa upako, kakobe ,mwamposa wote wanataka waumini na kule mtapata hiyo democresia ya kuwapangia mapato na matumizi
 
Munahangaika na sadaka hakuna lolote
 
Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba kijana anayeandaliwa kuwa padre uanzia seminari ndogo akiwa darasa la tano, yaani darasa la sita na la saba ndio seminari ndogo kisha f1 hadi fvi na kuendelea huko....pamoja na kuchukuliwa akiwa mdogo bado vitu kama familia anamotoka huangaliwa kwa umakini sana. Malezi ya mapadre wa kule hayaishii hapo jamaa wanaangaliwa sana hdi kwenye parokia zao....nimeandika haya baada kuona kunautofauti sana kati ya Mapadre wa jimbo la Bukoba, na majimbo mengine.

Hapa nilipo kina Padre Nicholas Bahati Kundy ni wengi sana hadi waumini wengi tunaanguka kiimani!
 
Wakatoriki nao wamekuwa kama walokole. Migogoro kibao. mmetia aibu. lakini bado ni kanisa stable kama wakitatua migogoro hii mapema mapema.
Jimbo kuu la Dar es salaam Lina Parokia zaidi ya 75. Hiyo Ni Parokia Moja tu.
 
Kwenye kuungama hakuna kutaja jina la uliyeshiriki naye kutenda dhambi. Acha kupotosha.
 
Jimbo kuu la Dar es salaam Lina Parokia zaidi ya 75. Hiyo Ni Parokia Moja tu.
Sasa zipo parokia 120. Hiyo kamati tendaji ya parokia ya Kawe ndio wanaochochea huo mgogoro kati ya paroko na waumini. Wamebanwa kuchakachua sadaka na kuwapa marafiki zao tenda za ujenzi wa ukumbi. Njaa mbaya sanaaa.
 
Mkuu Nalendwa,

Kwa Mtazamo wangu; waamini inaonekana wana kiburi. Kanisa lina njia za kutatua migogoro kama hii:

• Walipaswa kuwa watii kwa kiongozi na Mchungaji Mkuu wa Jimbo. Kama wamepangiwa appointment na ikashindikana, haiwapi tiketi ya kutafuta umaarufu.

• Hakukuwa na sababu ya press release kwa mambo ya ndani na ambayo yanafuatiliwa. Athari yake kwa Mama Kanisa ni kubwa kuliko faida.

• Hata kama mtu amekosea, kuna namna ya kuwasilisha hoja hizo kwa unyenyekevu, busara na Ukristu wa hali ya juu. Hakuna mkamilifu, ninakuhakikishia, hata wao sio wakamilifu.

• Waamini hawana subira na wana mihemuko mithili ya vijana wanaobalehe. Hawalijui vizuri Kanisa letu.

• Wanapaswa kujua kuwa mwenye maamuzi ya mwisho juu ya Jimbo ni Askofu ambaye hawezi kuingiliwa na Askofu mwingine yeyote, hata Askofu wa Roma (Baba Mtakatifu), hivyo, wanapaswa kumheshimu Kiongozi wa Kanisa Mahalia.

• Zaidi ya yote; Kanisa Katoliki siku zote huwa halina haraka, na haliendeshwi kwa kufuata hisia za waamini.

Huwa linachukua muda kujihakikishia ukweli kabla ya kufanya uamuzi. Kwanini wanashindwa kuwa wavumilivu?

Kanisa Katoliki sio chama cha siasa.
 
Kuna nini cha kuficha sasa hapo, unatumia kifungu gani cha sheria juu ya hiyo hoja yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…