TANESCO inaweza ikatengeneza faida kubwa sana endapo wataanza kukopesha units za LUKU. Hii ni ngumu kwa mteja kukwepa marejesho

Voda wakikopesha 5,000/= baada ya siku nne mtu anakopa tena Tigo 2,000/= atahama huko na kukopa tena Airtel au Halotel.

Sasa ukikopa LUKU directly kwa kuandika number ya mita, ni ngumu kwa mtu kuweza kukopa zaidi ya mara moja.
Saaaaf sana
 
Ukopeshe watanzania hawa hawa waliofanya TALA akabeba virago vyake, Africa mambo ya postpaid bado sana sisi hata matundu ya vyoo shida
Usijishushe kihivyo boss, au Kama Ni kujishusha sio kwa wingi kiasi unachotaka kuaminisha watu.
Mimi binafsi Ni mteja wa branch inayohusika na kukopesha fedha nilianza na elfu 20 na Sasa naweza kukopa Hadi laki 5 na kuresha bila ya shida. Na wapo wateja wengi qa namna yangu huko.
Hao tala waliondoka kwa mambo yao.
 
Good idea
 
Waweke mfumo wa vocha za kununua luku yaani unaingiza direct kwenye simu umeme unajiconnect.
 
Tanasco hawazalishi umeme "produce" anasambaza "supply".
Yeye pia ananunua huo umeme kutoka kwa wazalishaji.
Pili, Tanesco ili akopeshe umeme lazima awekeze hela ya kununua umeme toka kwa mzalishaji kwa minajiri ya mkopo tuu. Yaani kutakuwa na mtaji wa kuendesha mkopo wa umeme. Unaposikia Mpawa au Songesha katika mitandao ya pesa ujue ile ni "separate legal entity" yenye mandate ya kukopesha. Mara nyingi Kampuni za simu huwapa hilo deal mabenki.
Tatu,kwa kufanya hivyo inabidi Tanesco walipe kodi ya mapato yatakayotokana na mikopo ya umeme kwa muda fulani kitu hivyo hicho unachowaza kwamba ni "faida kubwa" haitakuwepo pesa nyingi italipa kodi (VAT na nyinginezo) na gharama za uendeshaji.
Nne,timing ya kumlipa mzalishaji itakuwa disrupted na mikopo ya umeme. Tanesco ili amlipe umeme mzalishaji lazima auuze. Fuatilia uendeshaji wa hili shirika ndio utajua kwanini selikali ime-monopolize huduma ya umeme. Kwanini hakuna soko huria la umeme. Yani kila mti azalishe na asambaze.
 
Tanasco hawazalishi umeme "produce" anasambaza "supply".
Yeye pia ananunua huo umeme kutoka kwa wazalishaji.
Sisi wateja tunawajua TANESCO ndio anatuuzia umeme hao wengine sio kazi yetu sisi kuwajua. Lakini asante kwa taarifa.
 
Sioni tatizo lolote juu ya hili kama lina manufaa kwa taifa. Watanzania wanakopa kutoka TANESCO na yeye (TANESCO) anakopa kutoka huko anaponunua.

Kwani hayo makampuni ya mitandao ya simu yanayokopesha watu data wao ni main (ISP) suppliers?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…