TANESCO inaweza ikatengeneza faida kubwa sana endapo wataanza kukopesha units za LUKU. Hii ni ngumu kwa mteja kukwepa marejesho

TANESCO inaweza ikatengeneza faida kubwa sana endapo wataanza kukopesha units za LUKU. Hii ni ngumu kwa mteja kukwepa marejesho

Kukopesha umeme ni suala gumu ndiyo maana hata ww haujatoa ni njia gani watatumia kukopesha unit ila umeandika wawe wanakopesha.
Mimi nimewapa hints tu, sasa kazi ni kwa wataalam wa uchumi na ICT kukaa na kuona wanaweza vp kutekeleza hilo.

Wanaweza kufanya arrangement ana kampuni husika ya mtandao wa simu kama Vodacom au Tigo kutoka mkopo wa pesa mahsusi kwa kununua units za umeme tu na sio muamala mwingine wowote.
 
Kwanin wakopeshe? Sio kila huduma itolewe kwa mkopo
Wabongo kwenye mikopo sio waaminifu kabisa.
Mbona serikali inakopa? Mbona wapo watanzania wanalipa madeni yao ya bank kwa mikopo bila shurti za mahakama?
 
Ni ngumu na italeta migogoro sana. Fikiria umepangishwa nyumba halafu kuna deni la 40,000 halijalipwa. Hiyo hela anatoa nani?
Hakuna umeme wa dharura wa 40,000/= huu ni uongo. Mikopo ya dharura katika simu haizidi 20,000/= na kiwango hupanda kulingana na uaminifu wa mteja husika.
 
Ibakie hivi hivi kama huna pesa ulale gizani tu ili upate akili vizuri.
Maisha hayaenda kama unavyofikiria ndio maana waliojenga mabondeni kama pale Jangwani wakikumbwa na mafuriko serikali inawaokoa ingawa walifanya kosa kutohamia mabwepande walipopewa viwanja.
 
Kukopesha umeme ni suala gumu ndiyo maana hata ww haujatoa ni njia gani watatumia kukopesha unit ila umeandika wawe wanakopesha.
Ni ngumu na italeta migogoro sana. Fikiria umepangishwa nyumba halafu kuna deni la 40,000 halijalipwa. Hiyo hela anatoa nani?
Ukiangalia thread yako haijajitosheleza. Ni njia gani TANESCO watatumia kukopesha umeme? Kuna nyumba zinapangishwa nzima.
Mkuu mbona ni simpo tu, mathalana tanesco wanaweza kukukopesha umeme wa 15,000. Halafu utakatwa labda 25% kila utakaponunua tena mpaka deni liishe. Au ukiamua unalipa 100%.
 
Mkuu mbona ni simpo tu, mathalana tanesco wanaweza kukukopesha umeme wa 15,000. Halafu utakatwa labda 25% kila utakaponunua tena mpaka deni liishe. Au ukiamua unalipa 100%.
Mkuu, huyo jamaa ana PhD ya ubishi sijapata kuona
 
Ukopeshe watanzania hawa hawa waliofanya TALA akabeba virago vyake, Africa mambo ya postpaid bado sana sisi hata matundu ya vyoo shida
 
Kuna meneja mmoja wa tanesco nilikua naongea nae akaniambia shirika linaenda kufa...coz cost of production n kubwa kuliko mapato.
Alikupa maelezo na ufafanuzi wa kutosha ukijiridhisha? Au umekurupuka tu baada ya yeye kukwambia hivyo? Maana ulitakiwa umuulize vizuri upate maelezo yanayojitosheleza kabla ya kuweka comment yako humu!
 
Alikupa maelezo na ufafanuzi wa kutosha ukijiridhisha? Au umekurupuka tu baada ya yeye kukwambia hivyo? Maana ulitakiwa umuulize vizuri upate maelezo yanayojitosheleza kabla ya kuweka comment yako humu!
Msamehe bure tu huyo mkuu
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu JamiiForums.

Kwanini TANESCO haikopeshi units za umeme wa LUKU kwa wateja wake? Mimi ninaona kama mchakato huu utawawezesha kupata faida kubwa sana kama riba kwa maana ni ngumu sana kwa mteja kukwepa marejesho.

Tofauti ya mteja wa TANESCO na mteja wa mtandao wa simu za mikononi kama Vodacom na Tigo ni kwamba, mteja wa mitandao hii ana nafasi kubwa sana ya kutokulipa deni kwa maana anaweza kubadili simcard au anaweza kufa kisha deni likawa limepotea tofauti na mteja wa TANESCO ambaye deni linakuwa limebebwa na nyumba kiasi kwamba hata akifa, deni litakatwa wakati wa ku-transfer property ownership.

Mteja wa mitandao ya simu za mikononi anaweza akakopa Vodacom kisha akahama mtandao akaanza kutumia Tigo, lakini mteja wa TANESCO hawezi kubadili number yake ya mita ya LUKU. Kama alikopa umeme wa 20,000/= kwa kutumia M-PESA inakuwa ngumu sana kukopa tena kwa kutumia mtandao mwingine kama vile TIGO PESA kwa maana atatumia number ile ile ya mita hivyo computer system itakataa kufanya muamala wa kumpa units.

TANESCO wanaweza kufanya special arrangement na kampuni husika ya mtandao wa simu kama Vodacom au Tigo kutoka mkopo wa pesa mahususi kwa kununua units za umeme tu na sio muamala mwingine wowote. Ukitumia pesa hiyo kwa muamala mwingine inakataa.

Mathalana TANESCO wanaweza kukukopesha umeme wa 15,000. Halafu utakatwa labda 25% kila utakaponunua tena mpaka deni liishe. Au ukiamua unalipa 100%.

Wataalam wa masuala ya uchumi pamoja na ICT mnaweza kulifafanua hili zaidi kwa maana hiyo sio taaluma yangu lakini ninapendekeza number itakayoruhusiwa kukopa iwe moja tu (Mmiliki wa nyumba) hususan kwa nyumba zenye wakazi (wapangaji) wengi

NB: Ndugu zangu waislam, Mungu awatangulie na kuwasimamia katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. Siku zote 30 za mfungo zikawe za kheri na baraka kwenu. Wishing you courage and strength so that you win every challenge of this life.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Nunua umeme tu mdogo wangu
 
Back
Top Bottom