Tetesi: TANESCO 'kwazizima' Makamba kuhamishwa Nishati. Waendelea na 'mfungo'

Tetesi: TANESCO 'kwazizima' Makamba kuhamishwa Nishati. Waendelea na 'mfungo'

Katika hali ya kustaajabisha, maafisa na wafanyakazi wa kawaida wa Kampuni ya Umeme Tanzania (TANESCO) walirukaruka kwa furaha baada ya kusikia na kujua uhamisho wa aliyekuwa Waziri wa Nishati Januari Makamba. Maafisa na watumishi hao wa Makao Makuu ya TANESCO walionesha furaha yao ya wazi kwakuwa walikuwa 'hawamtaki' Waziri Januari Makamba.

Wana-TANESCO wanashukuru na kumkaribisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Daktari Doto Biteko na kujiapiza kufanya naye kazi vyema. Hatahivyo, watumishi hao wamedai kuwa wanaendelea na maombi na mfungo wao ili Mungu amuongoze Rais Samia kumuondoa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Maharage Chande.

Makamba na Chande ambao ni marafiki wa karibu wa muda mrefu walikuwa hawakubaliki na wafanyakazi wa TANESCO kwa kile kinachosemwa kuwa wana kiburi, dharau na waligusa na kuondoa haki mbalimbali za wafanyakazi zikiwamo kufutwa kwa safari za kikazi. Nyaraka za ki-TANESCO zinaonesha kuwa kuna safari nyingi-hata zile zenye umuhimu ambazo zimefutwa na Chande kwa maelekezo ya Makamba.

Maombi ya wana-TANESCO yatafanikiwa?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Huku mtaani tume furahi zaidi maana alikuwa ana watu wake wa kuingiza mafuta na kuya uza bei wanazo taka wao.
 
Kutokana na kazi kubwa aliyoifanya January Makamba TANESCO lazima wamchukie.

Kabla ya Makamba, mchakato wa kuunganishiwa umeme uligubikwa na urasimu uliowekwa makusudi kurahisisha rushwa.
Wateja wapya walilazimishwa kumkodia gari surveyor wa TANESCO ili aje akague jengo lako.
Mchakato wa kumpata surveyor ulichukua wiki moja mpaka mwezi na zaidi.
Surveyor waliomba rushwa ili wakurahisishie kupata umeme.
Ukikaidi utakutana na vikwazo vya kila aina, ikibidi utaorodheshewa nguzo kadhaa ili kuongezewa gharama na pia kurefusha mchakato wa kupata umeme.
Ukimalizana na surveyor utakutana na kigingi kwenye idara ya ufundi. (Service line).
Hapa utaambiwa waya hatuna, bolt zimeisha, Luku zimeisha.

Wakati wewe unahenyeshwa kwakuwa hutaki kutoa rushwa wenzako watapata huduma ingawa wewe ndiye uliyeanza kuomba.

Na hata hizo Luku zikifika utaambiwa gari bovu, mafundi wameenda kwenye operesheni hii au ile, Subiri wiki mbili.
Kitengo cha dharula nacho hakikuachwa nyuma.
Ukipata Emergency utapiga simu masaa kadhaa, akipokea atakuuliza jengo liko wapi? Ukimwambia niko Mbagala Kisewe utasubiri mwezi mzima.
Upuuzi wote huo umekomeshwa na Makamba.
Hivi sasa nchi nzima tunapiga simu makao makuu Dodoma kwa namba moja tu 0748 550 000 kupata huduma.
Simu inapokelewa kwa wakati na huduma za kuunganishiwa umeme pamoja na ile ya dharula zote zinapatikana kwa wakati.
Kwa utendaji wake huo, amekata ulaji wa mameneja na mainjinia wa vitengo, wasimamizi wa kazi, (supervisor) mafundi pamoja na Vishoka.
Watu hawa hawawezi kumpenda.

Kuhusu kukatika katika umeme, jambo hilo haikwepeki.
Umeme unasafirishwa kama tunavyosafirisha vyombo vya moto.
Hivyo kuna ajali.
Nguzo hugongwa na magari, nguzo au waya hulipuka moto nk.
Lakini hata ukitaka kurekebisha mifumo ya njia za umeme lazima uzime.
Kwahiyo kudai utaongoza wizara ya nishati au Shirika la Umeme bila kukatika umeme ni uongo na Unafiki mtupu.
Mi najua kuwa January Makamba ni mwanasiasa, kwa sababu hiyo ana maadui wengi, lakini NAMPONGEZA kwa mengi mazuri aliyofanya hasa kuisafisha TANESCO.
Namtakia kheri kwenye kazi yake mpya.
 
Wazawa wazalendo tunafikilia muondoke mnaolilia Safari tanesco ingizwe ktk ushindani wa kihiashara na ujuzi ibakie na idara mbili tu ya kuza umeme na kukusanya mapato Kodi serikali idara zingine zote ziondolewe kuanzia usambazi umeme na matengenezo na kunganisha wateja ktk sekta binafsi wakandarasi wafanye kazi iyo kwa ushindani kunga wateja na sekta binafsi wauze vifaa vya service line mpaka nguzo na meter isajiriwe Kama line sm technical information on line technology kisasa nyie muondoke mnatutia asala Kaz kulilia Safari ufikili wateja umeme unakatikatika kwasababu kukosa ujuzi mhandis ajui ata transformer Ina wateja wangapi na kila phace ina wateja wangapi before new customer connection muondoke sekta binafsi ilete tija kwa taifa ktk ushindani wa kibiashara wakandarasi kuleta mapato ya taifa amtoshi kuanzia wakurugenzi mpaka bodi amfikili kulingiza shirika ktk ushindani wa kibiashara wakandarasi sekta binafsi kuongeza kazi usambazi umeme na matengenezo kunga wateja kwa wingi amtoshi ipo siku mungu atamzindua mkuu wa mzalendo kuvunja shirika libaki kuza umeme tu na kukusanya mapato Kodi
Mkuu acha jazba, umeandika bila hata kuweka koma wala nukta!
 
Hao wafanyakazi wa TANESCO kama walizowea wizi wasidhani makamba kuondoka ticket ya uwizi imerudi Doto atawanyoosha. Mkurugenzi hatabadilishwa na bodi ya TANESCO haitavunjwa kwa sasa.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Jembe la ufisadi? Biteko ahakikishe huyo Maharage Chande nae anakwenda wizara ya mambo ya nje amfuate boss wake his partner in their crime syndicate!

. Rostam akipenda iwe itakuwa!
 
. Rostam akipenda iwe itakuwa!
Nimesikia Mkwere ndio mwenye REMOTE CONTROL kumbe na Rostam pia!! Msipomsimamisha bibi anaipeleka nchi kubaya! Better late than never.
 
Kutokana na kazi kubwa aliyoifanya January Makamba TANESCO lazima wamchukie.

Kabla ya Makamba, mchakato wa kuunganishiwa umeme uligubikwa na urasimu uliowekwa makusudi kurahisisha rushwa.
Wateja wapya walilazimishwa kumkodia gari surveyor wa TANESCO ili aje akague jengo lako.
Mchakato wa kumpata surveyor ulichukua wiki moja mpaka mwezi na zaidi.
Surveyor waliomba rushwa ili wakurahisishie kupata umeme.
Ukikaidi utakutana na vikwazo vya kila aina, ikibidi utaorodheshewa nguzo kadhaa ili kuongezewa gharama na pia kurefusha mchakato wa kupata umeme.
Ukimalizana na surveyor utakutana na kigingi kwenye idara ya ufundi. (Service line).
Hapa utaambiwa waya hatuna, bolt zimeisha, Luku zimeisha.

Wakati wewe unahenyeshwa kwakuwa hutaki kutoa rushwa wenzako watapata huduma ingawa wewe ndiye uliyeanza kuomba.

Na hata hizo Luku zikifika utaambiwa gari bovu, mafundi wameenda kwenye operesheni hii au ile, Subiri wiki mbili.
Kitengo cha dharula nacho hakikuachwa nyuma.
Ukipata Emergency utapiga simu masaa kadhaa, akipokea atakuuliza jengo liko wapi? Ukimwambia niko Mbagala Kisewe utasubiri mwezi mzima.
Upuuzi wote huo umekomeshwa na Makamba.
Hivi sasa nchi nzima tunapiga simu makao makuu Dodoma kwa namba moja tu 0748 550 000 kupata huduma.
Simu inapokelewa kwa wakati na huduma za kuunganishiwa umeme pamoja na ile ya dharula zote zinapatikana kwa wakati.
Kwa utendaji wake huo, amekata ulaji wa mameneja na mainjinia wa vitengo, wasimamizi wa kazi, (supervisor) mafundi pamoja na Vishoka.
Watu hawa hawawezi kumpenda.

Kuhusu kukatika katika umeme, jambo hilo haikwepeki.
Umeme unasafirishwa kama tunavyosafirisha vyombo vya moto.
Hivyo kuna ajali.
Nguzo hugongwa na magari, nguzo au waya hulipuka moto nk.
Lakini hata ukitaka kurekebisha mifumo ya njia za umeme lazima uzime.
Kwahiyo kudai utaongoza wizara ya nishati au Shirika la Umeme bila kukatika umeme ni uongo na Unafiki mtupu.
Mi najua kuwa January Makamba ni mwanasiasa, kwa sababu hiyo ana maadui wengi, lakini NAMPONGEZA kwa mengi mazuri aliyofanya hasa kuisafisha TANESCO.
Namtakia kheri kwenye kazi yake mpya.
January unajisifia mwenyewe!!
 
Mkuu sio safari zote hazina tija. Nyingine ni muhimu kwa ajili ya kujenga uwezo wa Taasisi katika kushughulikia masuala inayotekeleza.
Safari zina umuhim gan TANESCO miaka nenda rudi ipo stagnant! bado wanatumia technologies za Zaman, wanatumia minguzo ya miti wanashindwa hata na vinchi vidogo kama Malawi!
 
Hawa wapumbavu mbwa kabisa ,Kwahiyo wao safari ni muhimu kuliko kubana matumizi na kuleta tija na ufanisi kwenye kutoa huduma au sio ?
 
Pambio ... YESU NI BWANA.. hapo hakuna wa Isaka wala wa Ishmael
 
Unalalamika masilai binafsi ya Safari sio masilai ya nchi kwasababu kila mkoa tanesco ipo na full idara unalilia Safari nini
Si ndio hapo ? , Safari za nini wakati kila mkoa kuna vitengo vya TANESCO na idara zake ? ,upuuzi gani huo ? ,
 
Katika hali ya kustaajabisha, maafisa na wafanyakazi wa kawaida wa Kampuni ya Umeme Tanzania (TANESCO) walirukaruka kwa furaha baada ya kusikia na kujua uhamisho wa aliyekuwa Waziri wa Nishati Januari Makamba. Maafisa na watumishi hao wa Makao Makuu ya TANESCO walionesha furaha yao ya wazi kwakuwa walikuwa 'hawamtaki' Waziri Januari Makamba.

Wana-TANESCO wanashukuru na kumkaribisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Daktari Doto Biteko na kujiapiza kufanya naye kazi vyema. Hatahivyo, watumishi hao wamedai kuwa wanaendelea na maombi na mfungo wao ili Mungu amuongoze Rais Samia kumuondoa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Maharage Chande.

Makamba na Chande ambao ni marafiki wa karibu wa muda mrefu walikuwa hawakubaliki na wafanyakazi wa TANESCO kwa kile kinachosemwa kuwa wana kiburi, dharau na waligusa na kuondoa haki mbalimbali za wafanyakazi zikiwamo kufutwa kwa safari za kikazi. Nyaraka za ki-TANESCO zinaonesha kuwa kuna safari nyingi-hata zile zenye umuhimu ambazo zimefutwa na Chande kwa maelekezo ya Makamba.

Maombi ya wana-TANESCO yatafanikiwa?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Ukiangalia kwa jicho jepesi unaweza fikiri wamefurahi kwa manufaa ya nchi la hasha.
Kipindi cha Makamba na Maharage wamepunguza sana matumizi ya ndani ya shirika(Ya tenda mimi sijui).
Madereva na maofisa wengine ambao walikua wanasafiri kila leo kila sehemu haya mambo hayapo tena.
Walikua wananunua vifaa vya Simiyu mzabuni anaambiwa adeliver Dar then wanatuma madereva kibao kusombelea kupeleka Simiyu. Kwa sasa mzabuni anapeleka vifaa kule vinakohitajika.
Si makamba tu hata Maharage wanatamani aondoke leo au hata afe leo.
Binafsi mipango ya Maharage naiona kabisa na naikubali kwa mfano;
1. Kubadili structure ya Shirika
2. Kupunguza matumizi ya ndani
Wazee sasa wanalia jamaa hafai kabisa hiyu kisa kawabana safari sizizo na tija na utendaji wa kutumia mfumo.

Kwa hiyo ikiwa watu wanafurahi kuondoka kwa kiongozi inabidi uangalie mara mbili je walikua wananyanyaswa au walikua wanabaniwa upigaji.

Wakati watu wengine wakiwa wanabanwa kula keki basi na wewe uone namna bora ya kupunguza matumizi hadi kwenu wakubwa.

Pamoja na yote wachache wenye shukurani wanashukuru ya kwamba uliongeza mishahara ndio ukaondoa ufanisi wa hovyo uliokua unaongeza gharama.

Maharage wafanyakazi wote waliokua wananufaika na safari na mapigo hawakutaki take care nadhani umenisurika mara 2 hivi kuwa macho tunaweza tusione ukifanyacho kesho tutakuelewa tu.
 
Mkuu sio safari zote hazina tija. Nyingine ni muhimu kwa ajili ya kujenga uwezo wa Taasisi katika kushughulikia masuala inayotekeleza.
Tatizo ni hao wafanyakazi. Safari si lazima, madam wanalipwa mishahara. Inavyoonekana walibaniwa upigaji.
 
Back
Top Bottom