TANESCO: Mtambo wa kuzalisha Megawati 20 za umeme umewasili Nchini ukitokea Marekani

TANESCO: Mtambo wa kuzalisha Megawati 20 za umeme umewasili Nchini ukitokea Marekani

Ijumaa Desemba 2, 2022, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lilitoa taarifa ya jitihada za muda mfupi zilizokamilika pamoja na zinazoendelea kufanyika katika kukabiliana na upungutu wa umeme.

Leo Jumanne Desemba 6,2022, TANESCO imetoa ripoti kuwa tayari mtambo wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 20 za umeme umewasili Nchini ukitokea Marekani siku ya Jumamosi Desemba 3, 2022.

Mtambo huo utafungwa katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia cha Ubungo namba Ill.

Majaribio ya mitambo miwili katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I yanaendelea vizuri, na kwa sasa mitambo hiyo inaingiza jumla ya Megawati 65 za umeme katika Gridi ya Taifa.

Wamesema kuwa wanategemea hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Desemba 2022, mitambo hiyo itakuwa ikizalisha jumla ya Megawati 90.

“Bado tunaendelea na kazi za matengenezo ya mitambo miwili ya Ubungo namba Ill ambapo baada ya kukamilika mwishonl mwa Desemba 2022, itazalisha jumla ya Megawati 40 za umeme.

Kuhusu jitihada za kati Tanesco wamesema “Tunategemea mitambo mingine miwili kuanza kufanyakazi katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I kuanzia mwezi Februari 2023 ili kuingiza Megawati 90 za umeme katika Gridi ya Taifa.
View attachment 2437844
Kama kawaislda tenesco haijawahi kufanya manunuzi ya maana yanayojali maslahi ya umma hapo lazima kuna ufisadi tiari
 
Wamalizie Plan ya JK ya kujenga Kinyerezi III na Kinyrerezi IV na sio kutegemea hii mipango ya zima kibatari....

Yaani wanachofanya ni kama wanatarajia baada ya muda mfupi mvua zitaanza kunyesha!
Kweli kabisa. Wawekeze zaidi kwenye gesi tuwe na megawat zaidi ya 2500 zinazotokana na Gesi tu
 
Naona tunarudia yale yale ya Dowans/IPTL na Richmond na kashfa ya malipo yao ya shilingi milioni 54 kwa dakika.

Naona watu wanatafuta hela kwaajili ya Uchaguzi 2025.

Kweli Nchi inaliwa na wenye Nchi 🙆
 
Kweli kabisa. Wawekeze zaidi kwenye gesi tuwe na megawat zaidi ya 2500 zinazotokana na Gesi tu
Na hili likifanyika, kitakachobaki ni hofu ya kukatika umeme tu kutokana na miundombinu lakini sio tena uhaba wa umeme eti kisa kuna ukame!

Sijui tunakwama wapi!
 
Kashfa Juu ya Kashfa!
10% juu ya Ten Percent!

Na watanzania tumenyamaza Tuli!
 
Naona tunarudia yale yale ya Dowans/IPTL na Richmond na kashfa ya malipo yao ya shilingi milioni 54 kwa dakika.

Naona watu wanatafuta hela kwaajili ya Uchaguzi 2025.

Kweli Nchi inaliwa na wenye Nchi 🙆
Hamna cha Dowans wala IPTL... ni ujinga tu wa viongozi...

Nchi tayari imeshaingia gharama ya zaidi ya Sh 1 TRILLION kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Kinyerezi.

Ambacho "kinatushinda" ni kujenga tu mitambo ya kuzalisha umeme pale Kinyerezi kwa sababu tayari gesi ipo!

Ukiangalia hiyo mipango yao utaona wazi ni ya kutegea mvua... kwamba mvua ikishanyesha, basi tatizo litapungua!
 
Dharura za umeme Tanzania hazitakaa ziishe kwasababu ndiyo kichaka cha utajirisho!
 
Miaka miwili nyuma kulikuwa na umeme wa uhakika na lugha ilikuwa ya majigambo tunaweza miradi ya megawatts 2000+ na mfano juu.

Leo tumerudi na hadithi za megawatts 20.

R.I.P shujaa Magufuli
Umeme wetu wategemea Mvua na Mwaka huu mvua zimekataa kabisa
 
Wamalizie Plan ya JK ya kujenga Kinyerezi III na Kinyrerezi IV na sio kutegemea hii mipango ya zima kibatari....

Yaani wanachofanya ni kama wanatarajia baada ya muda mfupi mvua zitaanza kunyesha!
Tatizo ni nchi yetu haina succession ya miradi, kila mtu anataka akumbukwe kivyake

Kinyerezi ingetosha kabisa kuzalisha umeme wa kutosha nchi nzima
 
Naona tunarudia yale yale ya Dowans/IPTL na Richmond na kashfa ya malipo yao ya shilingi milioni 54 kwa dakika.

Naona watu wanatafuta hela kwaajili ya Uchaguzi 2025.

Kweli Nchi inaliwa na wenye Nchi [emoji134]
We naye umezidi uongo
 
Mambo ya masandarusi kama kazi !! Walisema mitambo ilikuwa haifanyiwi marekebisho kipindi kile !! Sasa ndio inafanyiwa matengenezo!! Na umeme ndiyo imekuwa shidaa !!
kakojoe kwenye mito ili tupate maji ya kusukuma mitambo.
Unaona kabisa ukame hata maji ya matumizi nyumbani mgogoro bado unawaza umeme wa maji!
 
Tatizo ni nchi yetu haina succession ya miradi, kila mtu anataka akumbukwe kivyake

Kinyerezi ingetosha kabisa kuzalisha umeme wa kutosha nchi nzima
Hilo ndo tatizo... nahisi kila mmoja ni kama anataka aandike historia yake...

Ule Mradi wa Kinyerezi kama ungekamilika, hivi sasa ingekuwa tuna umeme mwingi ambao hatuwezi hata "kuumaliza"

Na uzuri zaidi, hata lile Bwawa la Nyerere lingeweza kujengwa bila pressure hii iliyopo sasa!!!
 
Mmiliki wa huo mtambo ni nani? Tuanzie hapa kwanza. Kama ni TANESCO, sina tatizo! Ila kama ni mabepari wa Richmond, basi tujiandae kupigwa tena na kitu kizito kichwani.
 
Ijumaa Desemba 2, 2022, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lilitoa taarifa ya jitihada za muda mfupi zilizokamilika pamoja na zinazoendelea kufanyika katika kukabiliana na upungutu wa umeme.

Leo Jumanne Desemba 6,2022, TANESCO imetoa ripoti kuwa tayari mtambo wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 20 za umeme umewasili Nchini ukitokea Marekani siku ya Jumamosi Desemba 3, 2022.

Mtambo huo utafungwa katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia cha Ubungo namba Ill.

Majaribio ya mitambo miwili katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I yanaendelea vizuri, na kwa sasa mitambo hiyo inaingiza jumla ya Megawati 65 za umeme katika Gridi ya Taifa.

Wamesema kuwa wanategemea hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Desemba 2022, mitambo hiyo itakuwa ikizalisha jumla ya Megawati 90.

“Bado tunaendelea na kazi za matengenezo ya mitambo miwili ya Ubungo namba Ill ambapo baada ya kukamilika mwishonl mwa Desemba 2022, itazalisha jumla ya Megawati 40 za umeme.

Kuhusu jitihada za kati Tanesco wamesema “Tunategemea mitambo mingine miwili kuanza kufanyakazi katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I kuanzia mwezi Februari 2023 ili kuingiza Megawati 90 za umeme katika Gridi ya Taifa.
View attachment 2437844
another richmond in the making
 
Miaka miwili nyuma kulikuwa na umeme wa uhakika na lugha ilikuwa ya majigambo tunaweza miradi ya megawatts 2000+ na mfano juu.

Leo tumerudi na hadithi za megawatts 20.

R.I.P shujaa Magufuli
Huyo shujaa wako angejaza maji kwa mkojo? Kile kitendo cha kuacha mradi wa gas ambayo ilikuwa tayari kwenye stations ni kununulia tu mitambo na kuifunga ilikuwa wazo mfu kwasababu gas haina msimu kama maji.
Yani nchi iliendeshwa kwa kutumia ndoto za Nyerere za 70s kana kwamba dunia iko vile vile
 
Ijumaa Desemba 2, 2022, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lilitoa taarifa ya jitihada za muda mfupi zilizokamilika pamoja na zinazoendelea kufanyika katika kukabiliana na upungutu wa umeme.

Leo Jumanne Desemba 6,2022, TANESCO imetoa ripoti kuwa tayari mtambo wenye uwezo wa kuzalisha Megawati 20 za umeme umewasili Nchini ukitokea Marekani siku ya Jumamosi Desemba 3, 2022.

Mtambo huo utafungwa katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia cha Ubungo namba Ill.

Majaribio ya mitambo miwili katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I yanaendelea vizuri, na kwa sasa mitambo hiyo inaingiza jumla ya Megawati 65 za umeme katika Gridi ya Taifa.

Wamesema kuwa wanategemea hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Desemba 2022, mitambo hiyo itakuwa ikizalisha jumla ya Megawati 90.

“Bado tunaendelea na kazi za matengenezo ya mitambo miwili ya Ubungo namba Ill ambapo baada ya kukamilika mwishonl mwa Desemba 2022, itazalisha jumla ya Megawati 40 za umeme.

Kuhusu jitihada za kati Tanesco wamesema “Tunategemea mitambo mingine miwili kuanza kufanyakazi katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I kuanzia mwezi Februari 2023 ili kuingiza Megawati 90 za umeme katika Gridi ya Taifa.
View attachment 2437844


Bwawa kuchelewa ndiyo wengine wanapata tender . Mama awe makini sana!
 
Back
Top Bottom