TANESCO: Taarifa Muhimu kwa baadhi ya wateja kwenye Mikoa ya Dar es salaam na Pwani

TANESCO: Taarifa Muhimu kwa baadhi ya wateja kwenye Mikoa ya Dar es salaam na Pwani

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
UPANUZI WA KITUO CHA KUPOZA UMEME CHA KINYEREZI NA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME YA MSONGO WA KILOVOTI 132 KINYEREZI-GONGOLAMBOTO

Ijumaa 15 Novemba, 2024.

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kuhusu maboresho ya miundombinu yanayoendelea katika Kituo cha Kinyerezi kwa kuongeza transfoma kubwa ya MVA 175 na upanuzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovolti 132 kutoka Kinyerezi hadi Gongo la mboto.

Maboresho haya yataathiri hali ya upatikanaji wa umeme kwa vipindi tofauti kwa baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Mkuranga, maeneo ya Mbagala, Chanika, Kisarawe, Gongo la mboto na Kipawa, kuanzia Jumamosi alfajiri ya tarehe 16 Novemba 2024 hadi Jumanne jioni ya Tarehe 19 Novemba 2024.

Kufanyika kwa maboresho haya kutawezesha umeme mwingi na wa kutosha unaozalishwa kwa sasa nchini kuwafikia wateja wa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam kwa ubora na uhakika.

Shirika linawashukuru kwa uvumilivu wateja wake wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani ambao wataathirika na utekelezaji wa kazi hii muhimu katika kipindi chote ambacho kazi hii itakua inaendelea.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA, TANESCO- MAKAO MAKUU.
DODOMA
www.tanesco.cotz
IMG-20241115-WA0023(1).jpg
 
Kuna habari kwamba bwawa la umeme maji yameshuka na Kuna mgao wa umeme unaendelea kimya kimya

Uzalishaji umepungua katika bwawa la mwalimu Nyerere

Hii imekaaje tanesco njooni mtujibu

Umeme kukatika asubuhi mpaka jioni je hakuna tatizo la mgao wa umeme?
 
Kuna habari kwamba bwawa la umeme maji yameshuka na Kuna mgao wa umeme unaendelea kimya kimya

Uzalishaji umepungua katika bwawa la mwalimu Nyerere

Hii imekaaje tanesco njooni mtujibu

Umeme kukatika asubuhi mpaka jioni je hakuna tatizo la mgao wa umeme?
Tilivo sema kwamba technology ya HEP is outdated ni gharama and unreliable wengi waliona tuna mpinga JPM....huyu jama alikua mkrupukaji kutuingiza gharama zisio za lazima, sijui alipewa je Uraisi.

We angalia mpaka hilo bwawa lianze kufanya kazi kuna unafuu wowote kwenye bei za umeme per unit, kuna hatua ypyote ya maendeleo kiviwanda. Hali ni ile ile, kuongeza deni la taifa bure.
 
Tilivo sema kwamba technology ya HEP is outdated ni gharama and unreliable wengi waliona tuna mpinga JPM....huyu jama alikua mkrupukaji kutuingiza gharama zisio za lazima, sijui alipewa je Uraisi.

We angalia mpaka hilo bwawa lianze kufanya kazi kuna unafuu wowote kwenye bei za umeme per unit, kuna hatua ypyote ya maendeleo kiviwanda. Hali ni ile ile, kuongeza deni la taifa bure.
Ni Upuuzi,,Fitna Na Usimamizi M'bovu Hakuna Cha autidetedi
 
Tilivo sema kwamba technology ya HEP is outdated ni gharama and unreliable wengi waliona tuna mpinga JPM....huyu jama alikua mkrupukaji kutuingiza gharama zisio za lazima, sijui alipewa je Uraisi.

We angalia mpaka hilo bwawa lianze kufanya kazi kuna unafuu wowote kwenye bei za umeme per unit, kuna hatua ypyote ya maendeleo kiviwanda. Hali ni ile ile, kuongeza deni la taifa bure.
Lakini Canada na china ndo wapo kweli ujenzi Sasa sijui kati yako hao nani yupo outdated
 
Tilivo sema kwamba technology ya HEP is outdated ni gharama and unreliable wengi waliona tuna mpinga JPM....huyu jama alikua mkrupukaji kutuingiza gharama zisio za lazima, sijui alipewa je Uraisi.

We angalia mpaka hilo bwawa lianze kufanya kazi kuna unafuu wowote kwenye bei za umeme per unit, kuna hatua ypyote ya maendeleo kiviwanda. Hali ni ile ile, kuongeza deni la taifa bure.
Chawa hawatakuelewa. Ila huu ni ukweli mtupu. Waliofikiria kumpa yule uraisi sijui waliwaza kitu gani haswa
 

Mambo yote yalishaelezwa kwenye huu uzi muda mrefu sana. Ndo ujue nchi hii tuna viongozi wa hovyo sana!

Uzuri wa JF madini yote yapo humu. Ni ukilaza tu wa viongozi wetu kutozingatia maoni mujarab yanayotolewa humu
 
Mafisadi mmeanza kelele baada ya kunyimwa kuongezewa mkataba na kampuni lenu la kifisadi la Richmond
 
Kuna habari kwamba bwawa la umeme maji yameshuka na Kuna mgao wa umeme unaendelea kimya kimya

Uzalishaji umepungua katika bwawa la mwalimu Nyerere

Hii imekaaje tanesco njooni mtujibu

Umeme kukatika asubuhi mpaka jioni je hakuna tatizo la mgao wa umeme?
Nchi za Ulaya na Marekani wanahangaika saivi kutengeneza vyanzo vya umeme vya nyuklia, sisi huku tunapambana na umeme wa maji

Kwa mabadiliko haya ya tabia nchi tukiendelea kutegemea huu umeme wa maji tusitegemee kuondokana na mgao wa umeme kamwe!

Kenya wamepata kibali kutengeneza umeme wa nyuklia. Sisi madini ya Uranium tunayo alafu kila siku tunapoteza mahela kwenye miradi ya umeme wa maji wakati Tume ya Atomic wamekaa tu hawajui hata wafanye nini.

Nchi hii shida ni kuwa na viongozi wasio na akili full stop. Wanaupeo mdogo sana wa kufikiri na kuona mbali.
 
Back
Top Bottom