TANESCO: Tuna upungufu, siyo mgao wa umeme. Wananchi endeleeni kuvumilia

TANESCO: Tuna upungufu, siyo mgao wa umeme. Wananchi endeleeni kuvumilia

Ninacho wakubali awamu hii wanajua kucheza na maneno ili kuliepuka neno mgao.
 
giphy.gif
 
Mmenitia hasara kwenye biashara zangu nyie, vigogo wote mnaotuchezea huu mchezo wa kishetani nawalaani, maisha yenu yajae laana tupu.
 
Its too much sasa, yaani tangu wakate saa 12 asubuhi hadi sasa giza 🙆🙆🙆

Hakika mama anaupiga mwingi.
 
Maharage anaweza kuwa ni mchapa kazi mzuri (sina uhakika kilichomweka hapo) lakini siyo msemaji mzuri na hajuwi kujieleza.

Nakumbuka zamani, enzi za Kikwete kama siyo TANESCo basi wizara ya nishati na madini ilikuwa na msemaji mmoja mtoto wa kike, Badra Masoud, alikuwa anajuwa kufikisha ujumbe, tena wakati huo ndiyo ilikuwa tuna shida kweli ya umeme lakini alikuwa akifikisha ujumbe anaeleweka.

View attachment 2753879
mashallah, mabinti wa kiislam wanamuogopa Mungu ndomaana wakiongea wanaeleweka
 
Niseme tu kwamba, Mkurugenzi hana la kutuambia
Kupewa na kukosa umeme kwa muda maalumu kila siku huo ni mgao
 
Kiukweli maharage ukimuangalia ni msemaji wa tanesko na hana sifa ya kua mkurugenzi amekua akiongea sana bila utendaji, swala la umeme hapa kwetu imekaa kisiasa zaid tuliambiwa gesi ya mtwara ulikua unatosha kuzalisha umeme mwingi ila badala yake bado tumebaki pale pale, halafu TANESCO huwa hawaoni aibu kudanganya, niamini mimi bwawa la Nyerere sio suluhisho la umeme Tanzania hii hilo bwawa ni siasa kama zile za makamba.
 
Akizungumza leo September 18 katika kipindi cha #Supa Breakfast cha East Africa Radio, Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO ndugu Maharage Chande amedai kuwa Tanzania hakuna kabisa mgao wa umeme bali kuna upungufu

Wateja na wananchi watuvumilie katika kipindi hiki najua ni kigumu kuvumilika na kuelekeweka lakini wafanyakazi wanajitahidi, wizara inajitahidi na serikali inajitahidi kuhakikisha tunatatua changamoto, vile vile uchumi unakua sana kwahiyo ni vizuri na mahitaji ya umeme yanaongezeka, tuko katika kushindana kuzalisha na matumizi ambayo ni mashindano mazuri kwa ustawi wa nchi yetu

Katika mitandao ya umeme hitilafu huwa zinatokea mara kwa mara maeneo mbalimbali huwezi kusema utakuwa na mtandao wa umeme isitokee hitilafu na pale zinapotokea wateja wetu huwa wanafahamishwa lakini pale ambapo tunapata upungufu"

Siyo kwamba nchi nzima hakuna umeme, kuna baadhi ya meeneo yanakosa na pia tunatoa taarifa kwenye hayo maeneo, ni vizuri mwananchi apate taarifa na tumekuwa tukitoa taarifa na tutaendelea kufanya hivyo.


View attachment 2753272
Huu umropo, ropo ropo yake hii baada ya "kuvimbewa maharage ya wapi" umemnyang'anya tonge mdomoni dadeki!

Aende Ttcl nako akayafanye aliyoyafanya Tanesco waTz tutayapokea tu, kwa kuwa sasa hatuna mtetezi.

Rais Samia kuendelea kukumbatia hawa mumiani badala ya kufukuza inamharibia taswira na haiba yake sana.

Inaonekana dhahiri hayuko na wananchi, bali yuko upande wa genge la hawa wezi na ananufaika nao.

Hatua anazochukua za kuuma na kupuliza kwa mtindo wa panya, asidhani anawafurahisha waTz, aelewe kuwa anawakera na kuwaudhi pakubwa sana waTz!

Wana mizizi gani imara hawa mafisadi kushindwa kung'olewa hata wanaponajisi hadharani taaluma na ajira zao?

Je yeye Rais Samia anakuwa ananufaika na nini katika madhila wanayoyapitia wananchi kwa sasa kutokana na utendaji mbaya wa hawa wahuni hadi aendelee kuwalinda kwa mtindo wa: "wa huku peleka kule na wa kule lete huku"?

Mtindo huu wa uteuzi na utenguzi umemtia doa kubwa sana Rais Samia katika utawala wake huu na kuzirudisha imani za raia zinazoendelea kuporomoka kila uchao itahitaji nguvu za ziada!

Mgao wa umeme na maji kila kona ya nchi ulivyotamalaki, tafsiri yake ni nini kwa mtawala kama huyu kuendelea kukaa kimya huku akicheka na nyani?

Maswali yote haya yasiyokuwa na majibu ina maana yeye Rais hazisikii kero hizi!

Tukisema Ccm imeshindwa kuongoza nchi, hatusemi kwa chuki bali tunasema kwa kufuata mnyororo wa matukio haya mabaya ya kiuongozi na kiutawala yanayoivua Serikali nguo.
 
Akizungumza leo September 18 katika kipindi cha #Supa Breakfast cha East Africa Radio, Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO ndugu Maharage Chande amedai kuwa Tanzania hakuna kabisa mgao wa umeme bali kuna upungufu

Wateja na wananchi watuvumilie katika kipindi hiki najua ni kigumu kuvumilika na kuelekeweka lakini wafanyakazi wanajitahidi, wizara inajitahidi na serikali inajitahidi kuhakikisha tunatatua changamoto, vile vile uchumi unakua sana kwahiyo ni vizuri na mahitaji ya umeme yanaongezeka, tuko katika kushindana kuzalisha na matumizi ambayo ni mashindano mazuri kwa ustawi wa nchi yetu

Katika mitandao ya umeme hitilafu huwa zinatokea mara kwa mara maeneo mbalimbali huwezi kusema utakuwa na mtandao wa umeme isitokee hitilafu na pale zinapotokea wateja wetu huwa wanafahamishwa lakini pale ambapo tunapata upungufu"

Siyo kwamba nchi nzima hakuna umeme, kuna baadhi ya meeneo yanakosa na pia tunatoa taarifa kwenye hayo maeneo, ni vizuri mwananchi apate taarifa na tumekuwa tukitoa taarifa na tutaendelea kufanya hivyo.


View attachment 2753272
Bado huyu mtu kwangu namuona ni mweledi, mbunifu,mchana kazi asiyechoka na mzalendo kwa nchi yetu Tanzania.
 
Back
Top Bottom