Tanganyika iiombe radhi Zanzibar?

Tanganyika iiombe radhi Zanzibar?

Kitabu hicho kililetwa humu na tukakichambua kuuonyeshea urongo wake wa wazi mchana kweupe!. Mapinduzi ya Zanzibar: Ukweli ni Upi?
P
Pamoja na kukichambua, bado ukweli uliomo kweye vitabu hivyo utabakia kuwa ukweii. Sifa moja kuu ya uchambuzi wa Mapinduzi huwa unategemea mtazamo wa mchambuzi husika na huu ndio utaratibu wa uchambuzi.
 
Pamoja na kukichambua, bado ukweli uliomo kweye vitabu hivyo utabakia kuwa ukweli.
Kwanza nakubaliana na wewe, uongo ulioandikwa kwenye kitabu, utabakia kuwa ndio ukweli mpaka kitabu kingine kitakapo kosoa na kuusema ukweli wenyewe halisi kuukosoa huo uongo.
Sifa moja kuu ya uchambuzi wa Mapinduzi huwa unategemea mtazamo wa mchambuzi husika na huu ndio utaratibu wa uchambuzi.
Naunga mkono hoja, ila uchambuzi wa historia unaotegemea fasihi simulizi kuigeuza fasihi andishi, siku zote una udhaifu wa kuchomekewa urongo!.

Mwandishi Dr. Ghasani hakuyashihidia Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar bali amehadithiwa kwa fasihi simulizi na mashuhuda wa Mapinduzi Matukufu yale, na kuuageuza fasihi andishi akaandika kitabu chenye urongo. Mimi nimekupa fursa ya kusikiliza shuhuda wa Mapinduzi Matukufu yale, na wewe kumsikia kwa masikio yako akielezea ukweli wa Mapinduzi Matukufu yale, wewe utamwamini nani?.

Nakushauri mwamini shuhuda unayemsikiliza kwa masikio yako na sio mrongo aliyesimuliwa urongo, akaandika urongo bila kuwa na uhakika mrongo ni nani kati ya aliyemsimulia, au aliyeandika, anaweza kabisa kuwa alisimuliwa ukweli, lakini mwandishi akaandika urongo kwa malengo yake. Msikilize shuhuda huyu
P
 
Capture.JPG
 
Kwanza nakubaliana na wewe, uongo ulioandikwa kwenye kitabu, utabakia kuwa ndio ukweli mpaka kitabu kingine kitakapo kosoa na kuusema ukweli wenyewe halisi kuukosoa huo uongo.

Naunga mkono hoja, ila uchambuzi wa historia unaotegemea fasihi simulizi kuigeuza fasihi andishi, siku zote una udhaifu wa kuchomekewa urongo!.

Mwandishi Dr. Ghasani hakuyashihidia Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar bali amehadithiwa kwa fasihi simulizi na mashuhuda wa Mapinduzi Matukufu yale, na kuuageuza fasihi andishi akaandika kitabu chenye urongo. Mimi nimekupa fursa ya kusikiliza shuhuda wa Mapinduzi Matukufu yale, na wewe kumsikia kwa masikio yako akielezea ukweli wa Mapinduzi Matukufu yale, wewe utamwamini nani?.

Nakushauri mwamini shuhuda unayemsikiliza kwa masikio yako na sio mrongo aliyesimuliwa urongo, akaandika urongo bila kuwa na uhakika mrongo ni nani kati ya aliyemsimulia, au aliyeandika, anaweza kabisa kuwa alisimuliwa ukweli, lakini mwandishi akaandika urongo kwa malengo yake. Msikilize shuhuda huyu
P
Mkuu Mayalla, unaonaje ukaandika na wewe kitabu kitakachoeleza KWELI TUPU za MAPINDUZI NA MUUNGANO?

Nishazisoma bandiko zako kadhaa. Ni wazi kuwa unayafahamu mengi, na umekuwa ukiyawasilisha, wakati mwingine, kimafumbo.

Unaonaje ukiweka kila kitu wazi kwa njia ya kitabu?

Najua wewe ni mtu "mkubwa!" Huogopi.

Mwaka 2016, ulithubutu kumwuliza Amiri Jeshi Mkuu swali ambalo wenzako, pengine wasingethubutu kuliuliza!

Mwaka 2018, ulidiriki kuandika kile unachokiamini ni sahihi bila kujali kuwa kutamkasirisha mkuu wa moja ya mihimili nchini!

Bila shaka, uliyafanya hayo yote kwa maslahi mapana ya Taifa!

Unaonaje ukaandika na kitabu kitakachokuwa na KWELI TUPU, tena bila mafumbo, kuhusu MAPINDUZI NA MUUNGANO?

Ukifanya hivyo, utakuwa umetoa zawadi kubwa sana kwa vizazi vya sasa na vya baadaye!

Tafadhali mkuu, andika kitabu, na usiweke mafumbo! Tafadhali 🙏🙏🙏
 
Kinanachosikitisha ni hao CCM kuuza nchi mchana kweupe kwa waarabu!

lakini si ndio tunaambiwa CCM kwa kupitia vyama vyao viliotangulia ndio waliwafukuza waarabu? Sasa ni kuwa wanawarejesha tu walipowakuta.
 
Viongozi kutoka Zanzibar hata rais wa Zanzibar ndio wanaojua madhara ya kuvunja muungano, hao wengine wanajisemea tu. Zanzibar haijaweza bado kujitegemea kifedha siku wakiweza muungano utavunjika hapo hapo!

kwahiyo Tanganyika ndio inaweza kujitegemea ama?
 
Honestly speaking, tuache unafiki na ubabaifu. Huo muungano hauna kero yoyote; bali ni MBOVU, period. Zaidi ya kujadiliana (to negotiate) kuwa na serikali moja tu, mengine yote ni UBATILI mtupu.

Aidha, muungano lazima uwe na lengo la kimkakati. Miaka yote 60 lengo la muungano huu “halijadiliki”; ni “siri”; ni “nyeti”; limefunikwa na kivuli cha kutisha na kufisha cha Mwalimu JKN kinacholindwa na wakuu wa CCM wasio na maadili. Ukweli ni kuwa maradhi hayafichiki milele. Tusubiri kilio tu. Na bado.
Serikali 1 ✓

Serikali 2 = No

Serikali 3 ✓
 
Kama inaitegemeza Zanzibar sio haba ila haitegemei fedha kutoka Zanzibar.

Sasa kwanini munainyonya Zanzibar? kwanini mpaka leo mnagoma kuipa mgao wake kutoka BOT? kwanini kwa miaka mingi mumekuwa hamuwapi mgao wao wa pato la muungano wa 4.5%?
 
Sasa kwanini munainyonya Zanzibar? kwanini mpaka leo mnagoma kuipa mgao wake kutoka BOT? kwanini kwa miaka mingi mumekuwa hamuwapi mgao wao wa pato la muungano wa 4.5%?
Zanzibar ndio kupe kwa Tanganyika. Jana tu shs trillion 1 zinakwenda kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa Pemba na barabara kilometer 800 Zanzibar yote. Fedha hizo zinatoka Tanganyika. Huu muungano hauwafai watanganyika kabisa.
 
Zanzibar ndio kupe kwa Tanganyika. Jana tu shs trillion 1 zinakwenda kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa Pemba na barabara kilometer 800 Zanzibar yote. Fedha hizo zinatoka Tanganyika. Huu muungano hauwafai watanganyika kabisa.

acha mihemko mkuu.
 
Serikali 1 ✓

Serikali 2 = No

Serikali 3 ✓
Sawa. Lakini ukweli ni kwamba serikali 3 kiuhalisia ni kuuvunja muungano; itakuwa ni kuthibitisha hatuna nia ya kuungana. Rais wa JMT ataishia kuwa a lame duck president!

Fikiria. Zanzibar hadi leo wanatambua katiba yao ndiyo yenye nguvu juu ya ile ya JMT! Muungano wa kweli unahitaji kukubaliana katiba moja na serikali moja tu. Nje ya hapo tutaendelea kupigiwa porojo za “kero za muungano” zikiambatana na “kamati za usuluhishi” zikitengewa posho za mabilioni ya walipa kodi mazuzu.
 
Tulichofundishwa shuleni kuhusu Muungano, ni tofauti na ninayoyasikia Sasa!

Inasemekana, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar haikuwa takwa la wananchi, bali la Karume na Nyerere, lakini zaidi, Nyerere.

Inasemekana, hata yale yanayoitwa Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar, yalikuwa ni mauaji katili, na yaliratibiwa na kusaidiwa, kwa sehemu kubwa, na Tanganyika. Hata silaha zilizotumika kwenye mapinduzi zilitoka Tanganyika.

Inasemekana, mapinduzi hayakulenga kumwondoa Mwarabu, bali Serikali halali kwa lengo la kukiweka madarakani Chama kilichokuwa kikiungwa mkono na Tanganyika.

Inasemekana, tokea mfumo wa Vyama vingi uanze, chama kinachoungwa mkono na Tanganyika kimekuwa kikishinda uchaguzi bila ridhaa ya wapiga kura. Kwamba kishinde kisishinde, lazima kiingie madarakani, maadam tu kinaungwa mkono na Tanganyika.

Inasemekana, hata huu Muungano uliopo kwa sasa si Muungano bali ni Ukoloni. Kwamba Tanganyika inaitawala nchi nyingine kimabavu.

Inawezekana, kama Zanzibar ingekuwa na uwezo, ingeshajitoa kwenye Muungano. Kuenedelea kwake kuwepo kwenye Muungano ni kwa sababu tu inalazimishwa na Tanganyika.

Yameshasemwa mengi na kuandikwa mengi.

Uungwana ni vitendo. Ikiwa hayo yote yanayosemwa ni kweli, basi Zanzibar wana haki ya kuulakamikia Muungano.

Kama ni kweli, nini kifanyike?

Mosi, Tanganyika iiombe radhi Zanzibar kwa yote inayoamini imeitendea Zanzibar ndivyo isivyo, na kwa yale ambayo Zanzibar inailalamikia.

Pili, kura ya maoni iitishwe kwa wananchi wa nchi ya Tanganyika na Zanzibar kuamua juu ya mustakabali wa Muungano.

Tatu, maamuzi ya wananchi yaheshimiwe.
Muungano ulikuwa 'CIA' project ya kuimeza Zanzibar ndani ya Tanganyika kama njia ya kuua ukomunisti huko Visiwani.
 
Back
Top Bottom