Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Kwa hiyo mlitaka JF ndio watoe hiyo taarifa, then Serikali itoe asubuhi baada ya kuweka nadharia za JF?
 
Labda kwa sababu tumezoea ‘breaking news’ za JF sijui raisi ateuewa akina nani.

Raisi ni mtu mkubwa sana kwenye nchi anapotokea yeye mwenyewe usiku mnene kutangaza breaking news ya kitu chochote iwe tumevamiwa, kuna kiongozi kafa or whatever ‘symbolic’ inaashiria umuhimu wa tukio kwa taifa na habari yenyewe trustworthy 100%.

Unataka watu watangaze habari za kifo na press conference sijui na kuvaa nguo sahihi; mambo mengine only in Tanzania, wapi kwengine wanafanya ivyo.

Tangazo la kifo cha Mandela au Nkuranziza likikuwa na press conference?
 
Mtu mwenyewe mbishi na ni mjuwaji wa kila kitu uenda alishauriwa akakataa na hata kusema "usibishane na mimi" sasa mtu wa hivyo utamfanyaje ni kumuacha tu,wito wangu kwa watu wenye madaraka waache viburi dunia ni ya kupita tu haiwezekani binadamu wa kawaida ukajua kila kitu hakuna binadamu wa hivyo.
Una tafsiri vipi kitendo cha raisi kuongea na taifa saa sita ya usiku? Is it normal au ni kutokana na uzito wa habari yenyewe pamoja na wasaidizi wote kwanini waliona atokee mwenyewe.

Watu wa Ikulu walijua wanafanya nini ‘symbolically’ kutaka yeye aongee, sio kwamba walikurupuka.
 
Pascal Mayalla,

Kwa mitandao ya sasa, mida ya saa kumi na mbili asubuhi hiyo isingekua taarifa tena kwa umma maana nchi nzima saa saba au nane ingekua imeshajua! Labda hii ingekua tamko tu la rais ila sio taarifa!

Kuna mida codes tupa kule.
Kwa hiyo serikali inashindana na mitandao ya kijamii nani awahi kukomenti sio...

Tatizo Ni kwamba licha ya uharaka wote huo bado taarifa haikutimia, yule ni kiongozi wa nchi inahitajika uwazi na umakini kuhusu kifo chake.

Mwalimu alifia hospital ya Mtakatifu Thomas pale Uingereza, tuliokuwa tunakua wakati huo mpaka leo hilo jina halitutoki.

Sasa Mheshimiwa amefia wapi kwa ugonjwa gani haijulikani kabisa.
 
Rais mstaafu Mkapa alizidiwa ghafla usiku akiwa kihospitali cha hapo Makumbusho ambako hakuna hata ventilator. Kiukweli alibanwa na mapafu ila timing ikawa mbovu. Mzaha mzaha wa serikali ya Magufuli kuhusu mambo muhimu ya afya za watanzania yanawagarimu wengi.

Halafu Rais wa nchi kutangaza msiba huku umelegea kama umetoka kula ile kitu ya Mshana Jr au mrangi haileti picha ya kuwa Amir jeshi mkuu tena umewahi kuvaa gwanda kabisa. Kutangaza huku unalegeza mwili ili watanzania waone kuwa umeumizwa sana ni ulimbukeni. In short lile tangazo nililiangalia mwanzoni tu nikaachana nalo maana Rais alikuwa very weak! Kuwa vile hakukufanyi kuonekana eti umeumizwa sana na ni udhaifu mkubwa kwa Amir jeshi mkuu.
 
Ni kuhusu Lissu mkuu, mpaka leo wengine hamjajua tu au hamtaki tu kukubali.

Tulishauri aombwe radhi yaishe lakini wapi, matokeo yake ndiyo mambo kama haya....
 
Wanabodi,
Naangalia Kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, kipindi kinajadili Msiba wa Benjamin Mkapa.

Tangazo la Msiba lililotolewa na Rais Magufuli, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu imelaumiwa kwa kutokumsaidia rais kikamilifu kutoa tangazo hili, hali inayotafsiriwa kuwa katika baadhi ya matukio, Kurengenzi hiyo inahitaji kusaidiwa na manguli wazoefu ili waweze kumsaidia rais Magufuli katika baadhi ya matukio.

Manguli wa Mwanza, Dotto Bulendu, Edwin Soko na Moses Mathews, wamesema kwa vile hii ni shocking news, kulipaswa kuwepo kwa muda kidogo wa kumuandaa rais Magufuli kutoa tangazo hilo kulitangazia kuanzia, timing, dress code na content za tangazo lenyewe.

Timing
Kwa vile msiba umetokea usiku, kutoa tangazo saa 6:30 usiku was not the right timing kwa Watanzania, news ya msiba ingekuwa held, halafu Wahariri wakaitwa Ikulu usiku ule, halafu Tangazo litolewe live saa 12:00 asubuhi, rais akiwa na VP na PM.
TCRA kutoa taarifa vyombo vyote vya habari vya k electronic kujiunga na TBC ili hiyo live itangazwe Tanzania nzima.

Dress Code.
Kuna mavazi ya kawaida mtu anaweza kuvaa katika tukio lolote, lakini kuna dress code ya msiba. Wanasema rais Magufuli alipaswa kushauriwa kutoa tangazo hilo akiwa amevaa a proper dress code ya tangazo hilo.

Contents za Tangazo
Tangazo la msiba wa kiongozi wa kitaifa linaongozwa na sheria ya Vifo vya viongozi, sheria imeweka contents za kisheria ambazo lazima liwe na vitu 6
  1. Jina la Kiongozi ni nani
  2. Kifo kimetokea lini
  3. Kifo kimetokea wapi nchini, mkoani, safarini, nje ya nchi
  4. Mahali mahsus, kimetokea nyumba, hospitalini, safarini,
  5. Kama ni hospitalini, hospitali gani
  6. Sababu za kifo, kimesababishwa na nini, maradhi, ajali, usingizini, etc
Tangazo la rais Magufuli kutangaza kifo cha Mkapa, lilikosa, baadhi ya taarifa muhimu za kisheria, hivyo kuleta sintofahamu kwa jamii.

Hajawahi kusikika kuwa Benjamin Mkapa anasumbuliwa na maradhi yoyote, hivyo taarifa kuwa amefariki hospitali ni shocking, hospitali gani na ameumwa nini, ni maswali ambayo taarifa ya rais ilikosa.

My Take
Kwa vile taarifa ya msiba ni shocking news, flaws ndogo ndogo katika tangazo la msiba huo, zinavumilika.

Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu inafanya kazi nzuri katika upashanaji habari wa shughuli za rais, lakini lazima itenganishe matangazo ya kawaida ya rais kwa shughuli za kila siku za kazi za rais na tangazo la taifa, Watu wa Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas walipaswa kuhusishwa, na kwa vile mimi sio mserikali kujua nani alihusika, kama Dr. Abbas alihusika na bado tangazo la rais ndio lile, hii inamaanisha Dr. Abbas anaelemewa naye anahitaji kuwekewa wasaidizi.

Kwa maoni yangu, japo sheria inatamka tatangazo litolewe immediately kunapotokea msiba, kama msiba umetokea usiku wa baada ya saa 6:00, then alfajiri ni immediately kulikuwa hakuna uharaka wa kukimbilia kutangaza usiku mkubwa huo huo ili kutoa nafasi kwa rais kutangaza in a proper way na kufanya mashauriano na watu wawili watatu ili kutoa tangazo kamilifu kisheria, kikanuni na kiutaratibu na sio kumuharakisha rais kutangaza huku he looks sleepy!.

Namalizia kwa kutoa pole kwa Rais wa JMT, Dr. John Pombe Magufuli, Familia ya Mkapa na Watanzania kwa ujumla, kwa msiba huu mkubwa wa rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.

Paskali

Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake!
Leo poti umeweka nukta tupu.
 
Taarifa isingeweza kuvuja family ikisimamiwa isitoe tàrifa,hamna wa kuvujiaha taarifa kubwa kiasi hico


Pascal Mayalla,
Ila pia kuna uwezekano tangazo lingetoka saa kumi na mbili kama mnavyopendekeza sasa, mngekuja na kwa nini mitandao ya kijamii taarifa iko heeani saa sita usiku alafu kurugenzi inachelewa! There is always something to say in a reverse way!
 
Dah! Wakati mwingine unaweza ku-complicate mambo bila sababu za msingi, sasa issue za nguo sijui uwe umevaa hivi au muda angesubiri hadi asubuhi, awaite watu fulani wawepo, nk nk nk, yote haya yangefanyika yangeleta utofauti gani ambao kwa sasa unaonekana umetoweka au umepungua?

Au labda tuendelee kusubiri huko mbeleni litaleta madhara ambayo kwa sasa hayajajitokeza, which I doubt.
Ni mtazamo wangu tu.
 
Pasi nimeshakutabiria mara nyingi tu kuwa nafasi ile ya Gerson ni yako baada ya November,ila Mami usinisahau katika ufalme wako.
 
Wanabodi,
Naangalia Kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, kipindi kinajadili Msiba wa Benjamin Mkapa.

Tangazo la Msiba lililotolewa na Rais Magufuli, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu imelaumiwa kwa kutokumsaidia rais kikamilifu kutoa tangazo hili, hali inayotafsiriwa kuwa katika baadhi ya matukio, Kurengenzi hiyo inahitaji kusaidiwa na manguli wazoefu ili waweze kumsaidia rais Magufuli katika baadhi ya matukio.

Manguli wa Mwanza, Dotto Bulendu, Edwin Soko na Moses Mathews, wamesema kwa vile hii ni shocking news, kulipaswa kuwepo kwa muda kidogo wa kumuandaa rais Magufuli kutoa tangazo hilo kulitangazia kuanzia, timing, dress code na content za tangazo lenyewe.

Timing
Kwa vile msiba umetokea usiku, kutoa tangazo saa 6:30 usiku was not the right timing kwa Watanzania, news ya msiba ingekuwa held, halafu Wahariri wakaitwa Ikulu usiku ule, halafu Tangazo litolewe live saa 12:00 asubuhi, rais akiwa na VP na PM.
TCRA kutoa taarifa vyombo vyote vya habari vya k electronic kujiunga na TBC ili hiyo live itangazwe Tanzania nzima.

Dress Code.
Kuna mavazi ya kawaida mtu anaweza kuvaa katika tukio lolote, lakini kuna dress code ya msiba. Wanasema rais Magufuli alipaswa kushauriwa kutoa tangazo hilo akiwa amevaa a proper dress code ya tangazo hilo.

Contents za Tangazo
Tangazo la msiba wa kiongozi wa kitaifa linaongozwa na sheria ya Vifo vya viongozi, sheria imeweka contents za kisheria ambazo lazima liwe na vitu 6
  1. Jina la Kiongozi ni nani
  2. Kifo kimetokea lini
  3. Kifo kimetokea wapi nchini, mkoani, safarini, nje ya nchi
  4. Mahali mahsus, kimetokea nyumba, hospitalini, safarini,
  5. Kama ni hospitalini, hospitali gani
  6. Sababu za kifo, kimesababishwa na nini, maradhi, ajali, usingizini, etc
Tangazo la rais Magufuli kutangaza kifo cha Mkapa, lilikosa, baadhi ya taarifa muhimu za kisheria, hivyo kuleta sintofahamu kwa jamii.

Hajawahi kusikika kuwa Benjamin Mkapa anasumbuliwa na maradhi yoyote, hivyo taarifa kuwa amefariki hospitali ni shocking, hospitali gani na ameumwa nini, ni maswali ambayo taarifa ya rais ilikosa.

My Take
Kwa vile taarifa ya msiba ni shocking news, flaws ndogo ndogo katika tangazo la msiba huo, zinavumilika.

Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu inafanya kazi nzuri katika upashanaji habari wa shughuli za rais, lakini lazima itenganishe matangazo ya kawaida ya rais kwa shughuli za kila siku za kazi za rais na tangazo la taifa, Watu wa Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas walipaswa kuhusishwa, na kwa vile mimi sio mserikali kujua nani alihusika, kama Dr. Abbas alihusika na bado tangazo la rais ndio lile, hii inamaanisha Dr. Abbas anaelemewa naye anahitaji kuwekewa wasaidizi.

Kwa maoni yangu, japo sheria inatamka tatangazo litolewe immediately kunapotokea msiba, kama msiba umetokea usiku wa baada ya saa 6:00, then alfajiri ni immediately kulikuwa hakuna uharaka wa kukimbilia kutangaza usiku mkubwa huo huo ili kutoa nafasi kwa rais kutangaza in a proper way na kufanya mashauriano na watu wawili watatu ili kutoa tangazo kamilifu kisheria, kikanuni na kiutaratibu na sio kumuharakisha rais kutangaza huku he looks sleepy!.

Namalizia kwa kutoa pole kwa Rais wa JMT, Dr. John Pombe Magufuli, Familia ya Mkapa na Watanzania kwa ujumla, kwa msiba huu mkubwa wa rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.

Paskali

Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake!
With due respect, I beg to differ.
Tufike mahali, tuishi maisha halisi, badala ya maisha ya maigizo.
Mzazi wako anapoaga dunia, wazo la kuangalia aina ya mavazi haliakisi uhalisia wa maisha yetu.
Rais Magufuli, katika kutoa taarifa ya kifo cha Rais wetu mstaafu Benjamin Mkapa, alionyesha utu wake katika uhalisia wake.
Kama alikataa kuwasikiliza 'Washauri' wake kuhusu "dress code" nk, ninamuunga mkono.
Dress code na taratibu nyingine ni "uigizaji" na tofauti na 'waigizaji wanavyojiita kioo cha jamii', uhalisia ni kinyume chake.
Watanzania hawapendi uigizaji bandia.
Ukweli huu umejionyesha kwenye chaguzi za maoni za CCM ambapo hao "wanaojiita kioo cha jamii" wamekataliwa kuwa sehemu ya uongozi wa jamii yetu katika majimbo waliyoenda kuomba ridhaa.
Paskali Mayala, Baruani Muhuza, Steve Nyerere, Mpoki, Pilipili na wengineo wamethibitishiwa kuwa kamwe wao siyo kioo cha jamii.
Kioo cha jamii ni wale wanaojitahidi kuishi maisha ya uhalisia.
Siyo maisha ya maigizo.
Rais Magufuli ameonyesha uhalisia wa machungu anayopata binadamu aliyeondokewa na mzazi wake.
Kwa umri aliofikia wa miaka takriban 82, Mzee Mkapa ni mzazi wa sehemu kubwa ya jamii ya nchi yetu, iliyo na umri chini ya miaka 60.
 
Mimi kwangu sina tatizo na muda hata kama ingekuwa saa nane usiku lakini namna tangazo lilivyotolewa mfano kuna haja gani ya kuficha hospitali alipofia na hata maradhi unaweza kusema hilo ni la familia lakini mtu akiwa kiongozi tena kiongozi mkuu huyu familia yake ni pamoja na wale anaowaongoza hivyo kuna umuhimu na kujua kipi kimemsibu kiongozi wao sasa umeona hata ule mtiririko wa tangazo lenyewe ni kama alikuwa anababaika kuruka ruka maeneo fulani ambayo eti yeye aliona haikustahili kuwekwa bayana.
Labda tumesikiliza clip tofauti mbona alisema mzee Mkapa kafia hospitali ya Dar Es Salaam automatic picha inayokujia ni Muhimbili.

Tatizo ni hawa waandishi wetu mtu anaanza fani mpaka anakaribia kumaliza udhani kama keshawai kukutana na jina Bronislow Malinowski au ata amewahi kushika kitabu chochote cha ‘social anthroplogy’ katika maisha yake kujiongeza kwenye kutafsiri matukio.

Ndio tatizo liliopo hapa hao wachambuzi ni kutokana na tafsiri zao; hila watu wa Ikulu jinsi walivyoitoa habari walizingatia symbolic significance ya raisi kuzungumza. Na big deal kiongozi wa nchi anapotekea usiku mnene. Hawa kukurupuka Ikulu walijua wanachofanya.
 
Wanabodi,
Naangalia Kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, kipindi kinajadili Msiba wa Benjamin Mkapa.

Tangazo la Msiba lililotolewa na Rais Magufuli, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu imelaumiwa kwa kutokumsaidia rais kikamilifu kutoa tangazo hili, hali inayotafsiriwa kuwa katika baadhi ya matukio, Kurengenzi hiyo inahitaji kusaidiwa na manguli wazoefu ili waweze kumsaidia rais Magufuli katika baadhi ya matukio.

Manguli wa Mwanza, Dotto Bulendu, Edwin Soko na Moses Mathews, wamesema kwa vile hii ni shocking news, kulipaswa kuwepo kwa muda kidogo wa kumuandaa rais Magufuli kutoa tangazo hilo kulitangazia kuanzia, timing, dress code na content za tangazo lenyewe.

Timing
Kwa vile msiba umetokea usiku, kutoa tangazo saa 6:30 usiku was not the right timing kwa Watanzania, news ya msiba ingekuwa held, halafu Wahariri wakaitwa Ikulu usiku ule, halafu Tangazo litolewe live saa 12:00 asubuhi, rais akiwa na VP na PM.
TCRA kutoa taarifa vyombo vyote vya habari vya k electronic kujiunga na TBC ili hiyo live itangazwe Tanzania nzima.

Dress Code.
Kuna mavazi ya kawaida mtu anaweza kuvaa katika tukio lolote, lakini kuna dress code ya msiba. Wanasema rais Magufuli alipaswa kushauriwa kutoa tangazo hilo akiwa amevaa a proper dress code ya tangazo hilo.

Contents za Tangazo
Tangazo la msiba wa kiongozi wa kitaifa linaongozwa na sheria ya Vifo vya viongozi, sheria imeweka contents za kisheria ambazo lazima liwe na vitu 6
  1. Jina la Kiongozi ni nani
  2. Kifo kimetokea lini
  3. Kifo kimetokea wapi nchini, mkoani, safarini, nje ya nchi
  4. Mahali mahsus, kimetokea nyumba, hospitalini, safarini,
  5. Kama ni hospitalini, hospitali gani
  6. Sababu za kifo, kimesababishwa na nini, maradhi, ajali, usingizini, etc
Tangazo la rais Magufuli kutangaza kifo cha Mkapa, lilikosa, baadhi ya taarifa muhimu za kisheria, hivyo kuleta sintofahamu kwa jamii.

Hajawahi kusikika kuwa Benjamin Mkapa anasumbuliwa na maradhi yoyote, hivyo taarifa kuwa amefariki hospitali ni shocking, hospitali gani na ameumwa nini, ni maswali ambayo taarifa ya rais ilikosa.

My Take
Kwa vile taarifa ya msiba ni shocking news, flaws ndogo ndogo katika tangazo la msiba huo, zinavumilika.

Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu inafanya kazi nzuri katika upashanaji habari wa shughuli za rais, lakini lazima itenganishe matangazo ya kawaida ya rais kwa shughuli za kila siku za kazi za rais na tangazo la taifa, Watu wa Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas walipaswa kuhusishwa, na kwa vile mimi sio mserikali kujua nani alihusika, kama Dr. Abbas alihusika na bado tangazo la rais ndio lile, hii inamaanisha Dr. Abbas anaelemewa naye anahitaji kuwekewa wasaidizi.

Kwa maoni yangu, japo sheria inatamka tatangazo litolewe immediately kunapotokea msiba, kama msiba umetokea usiku wa baada ya saa 6:00, then alfajiri ni immediately kulikuwa hakuna uharaka wa kukimbilia kutangaza usiku mkubwa huo huo ili kutoa nafasi kwa rais kutangaza in a proper way na kufanya mashauriano na watu wawili watatu ili kutoa tangazo kamilifu kisheria, kikanuni na kiutaratibu na sio kumuharakisha rais kutangaza huku he looks sleepy!.

Namalizia kwa kutoa pole kwa Rais wa JMT, Dr. John Pombe Magufuli, Familia ya Mkapa na Watanzania kwa ujumla, kwa msiba huu mkubwa wa rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.

Paskali

Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake!

Mkuu Pascal unanikumbusha tukiwa wadogo tukienda winda porini na ukaona mbwa anaacha kuwa makini na alichokifuata basi unamstua kwa sauti ya " Hey..Shika shika"
 
Back
Top Bottom