Tangu nipatwe na Matatizo kazini, mke wangu amebadilika tabia

Tangu nipatwe na Matatizo kazini, mke wangu amebadilika tabia

Chief jiandae visa vya makusudi apo anatafuta sababu za kutemana .

Hii same story imenitokea juzi tu KWA wife niliempenda na kumuamini .
Badala uchumi kuyumba alitengeneza mazingira ya niwe nakasirika mda wote (namshukuru mungu sikuwahi kumgusa ata singi )
Atatengeneza mazingira ya uwe unamnyenyekea Ili ukasirike .
Vitimbwi vyote atakuletea mwisho wa siku mume utakuwa na hasira zako na tendo la ndoa utalikinai (Izo ni plan baadaye sana ndio utakuja kugundua zilikuwa za makusudi )
Jiandae na vikao maana ataenda kulalamika humtimizi haja zake tendo na huduma za ndani .

Ukweli nilipigana vitimbwi na dharau mwisho wa siku anajitangazia kwao nimemuacha na mbaya zaidi alishapakaza mbaya kwao akaja home kimya kimya akabeba vitu .

Usiku narudi home nakuta godoro tu niliumia sana sikutaka purukushani kupiga piga simu najua sababu mti wa pesa umekauka yote haya yametokea.

Ila yote na yote Jipange Ili usije ukakonda KWA mawazo. Good luck budy
Duh! Pole mkuu. Maisha kwa sasa yapoje upande wako
 
Pole sana. Toka nje katafute pesa mangi, hakuna heshima yeyote utakayopata kwake kama huna pesa especially kama amekuzidi kipato. Baada ya hizo dharau itafuata usaliti ulio waziwazi. Changamka man.
Mleta maada kasema hata Kama anashinda home lakini mkwanja unaiingia Kama kawa,sema labda Mke wake anataka Jamaa awe na kipato Cha Kama Cha boss wake kisa tu labda anahongwa na huyo boss wake vijicenti ndiyo maana anamzarau Mume wake!!!
 
Piga udayworker,kabebe mizigo,kachanganye zege,kachimbe mitaro,kaombe ukondakta nk..
Kwani mleta maada kasema hana pesa!? Mbona pesa anayo hadi anahudumia familia! Sema wife anataka kuona akitoka asubuhi kwenda kazini na kurudi Jioni, yaani anataka Mume wake awe na ajira, ndiyo Mwanamke alivyo kariri Maisha ya 8 to 5 job!

Wakati Dunia Sasa imebadilika,watu wengine wanaingiza pesa hata wakiwa wamelala kitandani au Yuko sebuleni anaangalia tv huku mishe za pesa zinaingia kupitia simu yake!
 
Yupi Bora, Mwanaume anae shinda Nyumbani huku anaiingiza pesa,au Mwanaume anae damkaa asubuhi na kwenda kuzurula bila plani na kurudi home bila kitu na kesho akiamka anaomba tena nauli kwa wife na kwenda kuzurula tena bila mipango!!??
Hujanielewa point yangu mkuu, kazi anaweza asiwe nayo daily kwa sisi wapambanaji sio kila siku ukitoka unapata(vice versa is true), unaweza usitoke kila siku ina uafadhali kuliko kutokutoka kabisa. Kuna watu mwezi unaisha hajatoka kabisa, mishe unazifuata/unazitafuta, hazikutafuti ndio maana ni vyema kutoka.
 
Duh! Pole mkuu. Maisha kwa sasa yapoje upande wako
Nilipitia kipindi kigumu ndani pale kulikuwa na nondo iliyojitokeza kila siku nikilala nilihisi ndio sahihi ya maamuzi (kujiuwa ) nilikonda sana kwa mawazo mtu ulimpa kila kitu mwisho wa siku anakusaliti kisa uje drop kimaisha.

Nashkuru Mama alinipokea japo mama ilimuuma sana cz nilimuuminisha ni mke wa maisha. Kwa sasa naanza upya maisha from 25m to 0 balance.

Nilimpenda sana wife wangu mpaka sasa
 
Narudia kauli yangu, MKE wangu mtarajiwa atafanyiwa VETTING yakibabe sana.. Ili ndoa ikija kuwa NDOANO nisilaumu mtu wala kujilaumu bali nitasema "MUNGU NDIO KAPANGA HILI"
 
Ajira uliyopoteza ulidumunayo kwa muda gani..?
Halafu mbali na hiyo ajira ulikua na mishe gani nyingine iliyokuwa inakuweka town..?
Na bank or mobile account unabalance ya bei gani..?
 
Habari za jioni wanajukwaa wa MMU, ikiwa mmetoka katika mihangaiko akili na mwili vimechoka nawaletea jambo jingine hili tupate kulijadili.

Mimi na mke wangu ni waajiliwa yeye ni mtumishi wa umma na mimi ni mtumishi wa sekta binafsi, ndoa yetu ina miaka mitatu sasa na tuna mtoto mmoja (asante sana MUNGU kwa hili).

Shida iliyonileta kwenu ni kuwa hapa karibuni nimepata matatizo ya kikazi sasa imenibidi niwe nashinda nyumbani kwa sababu mimi siyo mtu wa kukaa nje sana nahisi ndipo matatizo yalipoanzia. Tangu nipatwe na hii hali mke wangu amebadilika tabia sijui kama ni makusudi au lah.

Niwe muwazi kuwa mke wangu amenizidi mshahara lakini pamoja na hayo sijawahi kuona tabia hizi kwake hadi hapo nilipopatwa na hizo shida kazini.

Tabia zipo nyingi ila naleta tatu zilizonishitua;

~ Kwanza amekuwa hataki kushiriki nami tendo.

~ Pili sababu huwa nashinda na mtoto huwa napika kwa ajili yangu na mtoto ambapo ye akirudi anapika kwa ajili ya wote kwani anasema sijui kupika. Sasa hapo juzi kati alinambia itabidi nijifunze kupika kama nataka kuendelea kuwa naye.

~ Tatu ni kuwa tuna machine ya kufulia sasa imeharibika, nikamuomba kuwa nikipata hela tutafanya matengenezo akanijibu kama ni hivyo basi niwee namfulia nguo zikiwemo chupi zake daah.

Mimi nimefikiria uamuzi wa kuachana naye licha ya kuwa na mtoto naye, kwani sina mpango wa kumpiga na hiyo juzi ilibaki kidogo nipige arudi kwao Vunjo Mashariki na ulemavu wa uso alivyosema niwe namfulia.

Nauliza tu wanawake wa humu haya anayofanya mwenzenu ni halali kweli?
Huyo mke wako hawana tofauti na wale wa love connect ambao kigezo chao kikuu umeajiriwa au umejiajiri. Na hawa wapo wengi sana.
1. Alikujibu kuwa uanze kujifunza kupika km unataka kuwa naye

2. Uanze kumfulia nguo ikiwemo chupi
Ningekuwa mimi ningemfukuza siku hiyo hiyo. Hii ni dharau iliyopitiliza alitakiwa awe mfariji wako kwa sasa
 
Kuna vitabia vya kivivu kaviona kwako vinamboa.hata kama huna kazi amka saa 12 kapambane sio unalala mpaka saa tano ukiamka unashindia kwenye TV.All in all wanawake wengi wanadharau sana unapokosa kipato.
Siwezi kuishi kumfurahisha mwanamke. Uzunguke ili ubembeleze ndoa na kumfurahisha mwanamke?

Ndoa inajengwa na upendo na kuvumiliana kwa kila hali. Ningekuwa mimi ndoa ingevunjika siku hiyo hiyo.
 
Back
Top Bottom