Tanzania bado nchi masikini sana, kwa miaka 8 watanzania wameagiza magari 561,875

Tanzania bado nchi masikini sana, kwa miaka 8 watanzania wameagiza magari 561,875

Wakati namba D ikielekea kuisha tujikumbushe idadi ya magari yaliyoagizwa chini ya namba D.

Kwa mfano, Namba T100DAA, ili kubadilika na kua T100DAB inahitajika magari 899, herufi ziko 25 kutoa herufi I. Hivyo kubadili herufi moja inahitajika magari 899 mara herufi 25 unapata magari 22,475.

Kubadili kabisa herufi kutoka DAA kwenda EAA inahitaji magari 22,475x25 sawa ma magari 561,875. Kwa maana kwamba kwa namba D ambayo imeanza mwaka 2014 na inaisha mwaka 2022 ni miaka 8 Tanzania imeagiza magari 561,875.

Kwa maana kwamba kwa mwaka Tanzania wastani tunaagiza magari 70,234 ama magari 5,852 kwa mwezi sawa na magari 195 kwa siku.

Hii ina maana kwamba kwa wastani wa watu milioni 60, milioni 30 ikiwa ni nguvu kazi tunaagiza gari 5,852 kwa mwezi ni ishara ya umasikini mkubwa sana.

Mbaya zaidi magari hayo 95% ni second hand ya miaka mingi. Ukiangalia Watanzania wanaagiza magari ya mwaka 2000 hadi 2008. Hayo ni ya kutembelea, ya usafiri kama daladala ni ya kuanzia mwaka 1995 hadi 2000.

Magari ya kuanzia 2010 Tanzania ni ya kutafuta kwa tochi. Serikali pekee na watanzania wachache sana wanaagiza magari ya kuanzia 2018 na kuendelea.

Mimi mwenyewe kimkweche changu ni cha mwaka 1999 niko vidudu😂. Aibu ya mwaka.

Hii nchi miaka 62 ya uhuru bado ni maskini wa kutupwa. CCM imenajisi hii nchi kwa kiwango kisicho na mfano.
Nani kakwambia watanzania ni masikini?
Umasikini uo kwa mtu binafsi.
 
Watu kwa ground wanauziana magari hum hum bongo, maelfu kwa maelf, kama huamn fuatilia utitili wa platform mbalimbal za madalali wanaopromote na kuuza magari ndipo utajua ukwel.

Kinachofanya watu wasiagize nje ni hiyo tabia ya kotoza kodi ndefu ambapo kihalali haikutakiwa iwe hivyo,so bora tuuziane humu humu
Hayo yanayouzwa humu humu yanayoka wapi?
 
Wewe ni zero brain.
Nchi inaundwa na watu na kama idadi kubwa ya watu wanaounda hiyo nchi ni masikini hiyo nchi itakuaje tajiri?
Okay big brain.
Na wanaotembelea ma V8 binafsi na serikali na hai waliiagiza magari laki sita unawaweka wapi.
 
Hivi hili suala la.kodi za magari kuwa sawa au zaidi na bei ya kununulia gari hakuna wakulisemea??

#MaendeleoHayanaChama

Hakuna. Nchi hii ni ya ajabu sana. Unataka maendeleo lakini vitu vya kuchochea maendeleo huvipi vipaumbele, unavipiga vita, unavikwamisha kwa makusudi kabisa.

Kuweka kodi kubwa kwenye magari, mafuta, mbolea, tozo, kwenye miamala, luku jitihada za serikali kupunguza Kasi ya maendeleo ya watu ili kuwafanya wabaki maskini.

Serikali yetu inaonekana inapambana Sana kupunguza Kasi ya maendeleo Kwa Mtanzania kupitia sera, Kodi, tozo, vipaumbele visivyo rafiki wala kumsaidia Mtanzania zaidi ya kumkamua na kumrudisha nyuma kimaendeleo
 
Sana tutapokezana za humu humu ndani maana waagizaji watakuwa wachache.
Fikiria Fuso ya mwaka 1988 kuiingiza nchini ujipange na pesa si chini ya million 75+. Je ya mwaka 2012 utailipia pesa ngapi.[emoji28]

Ukiangalia daladala nyingi, gari nyingi Tanzania zimechoka balaa. Ajali nyingi zinasababishwa na gari zilizochoka.
 
Kwa ulimwengu wa SAsa ant dumping ni useless principal.sababu antidumping uja kumezwa na scrapping principal yaani kitu au gari likifika mwisho linaenda screpa kukatwa chuma chakavu then linarudi kiwandani kama raw materials ya kuzalisha tena gari.
Yangebaki huko wanakozalisha
 
Wakati namba D ikielekea kuisha tujikumbushe idadi ya magari yaliyoagizwa chini ya namba D.

Kwa mfano, Namba T100DAA, ili kubadilika na kua T100DAB inahitajika magari 899, herufi ziko 25 kutoa herufi I. Hivyo kubadili herufi moja inahitajika magari 899 mara herufi 25 unapata magari 22,475.

Kubadili kabisa herufi kutoka DAA kwenda EAA inahitaji magari 22,475x25 sawa ma magari 561,875. Kwa maana kwamba kwa namba D ambayo imeanza mwaka 2014 na inaisha mwaka 2022 ni miaka 8 Tanzania imeagiza magari 561,875.

Kwa maana kwamba kwa mwaka Tanzania wastani tunaagiza magari 70,234 ama magari 5,852 kwa mwezi sawa na magari 195 kwa siku.

Hii ina maana kwamba kwa wastani wa watu milioni 60, milioni 30 ikiwa ni nguvu kazi tunaagiza gari 5,852 kwa mwezi ni ishara ya umasikini mkubwa sana.

Mbaya zaidi magari hayo 95% ni second hand ya miaka mingi. Ukiangalia Watanzania wanaagiza magari ya mwaka 2000 hadi 2008. Hayo ni ya kutembelea, ya usafiri kama daladala ni ya kuanzia mwaka 1995 hadi 2000.

Magari ya kuanzia 2010 Tanzania ni ya kutafuta kwa tochi. Serikali pekee na watanzania wachache sana wanaagiza magari ya kuanzia 2018 na kuendelea.

Mimi mwenyewe kimkweche changu ni cha mwaka 1999 niko vidudu[emoji23]. Aibu ya mwaka.

Hii nchi miaka 62 ya uhuru bado ni maskini wa kutupwa. CCM imenajisi hii nchi kwa kiwango kisicho na mfano.
Umesahau kwamba mpaka miaka ya karibuni piki piki na magari yalikua yana share number. Means kama ingekua kama sasa kwamba gari zisimame zenyewe inawezekana namba E ingesogea mpaka miaka 4 mbele, so piga hesabu upya.
 
Wahuni hawapunguzi kodi kila kukicha wanaona gari ni anasa na pia wale madarali wa Toyota wanawapiga kwa kuwauzia bei ya kilimo kwanza ambayo Nchi zingine hawaagizi kwa bei yetu wao wanaona sawa maana wapo wanaokula 10% kwa Serikali kupigwa..Nimeona pale Kasumulu mpaka wa Malawi gari za kumwaga na matoleo ya sasa hivi kwa sababu ya kodi yao ni rafiki gari ndogo halizidi Tsh 2m wakati hilo gari Tanzania ni 12m kodi yake...
 
Kununua gari ndo dalili ya ukwasi wa mtu binafsi?
Shule umetoka lini?
Umeshawahi kufanya kitu kinaitwa wealth ranking huko kwenye vijiji au mitaa yetu?? Ukitaka kujua economic status ya jamii fulani unaipimaje kama siyo kutumia vigezo vya mtu kumiliki vitu??
 
Back
Top Bottom