Tanzania Economic Freedom Advocacy (TEFA)

Tanzania Economic Freedom Advocacy (TEFA)

Ukiwa na tabia ya kusikiliza na kuchangajya na yako itafaa zaidi kuliko kufunga ubongo wako Kwa Yale tu unayopenda kuyasikia...Ukimsoma utagundua kuna ujumbe anakupatia ila kwakua hutaki kusikia unasikia kelele tu na siyo ujumbe muhimu anaokusaidia kuung'amua
Huwezi endelea kununua gesi uarabuni na india ilihali unayo hapa Tanzania
 
Gesi asilia ya Tanzania haiwezi kuzalisha petrochemical products zote ulizo andika hapo kwa urahisi, lakini inaweza kutumika kama malighafi kwa baadhi ya bidhaa fulani zinazotokana na gesi, hasa ammonia na methanol.

Hata hivyo, gesi yetu haiwezi kuzalisha kiurahisi polyethylene, polypropylene, thermoplastic polyurethane, ethylene, propylene, benzene, toluene, na xylenes, kwa sababu muundo wake una methane (CH₄) kwa kiwango cha juu sana (90-99%) na haina kiasi kikubwa cha ethane, propane, au butane, ambazo ni malighafi kuu katika uzalishaji wa petrochemicals.

Petrochemicals ambazo Tanzania inaweza kuzalisha kwa kutumia gesi asilia

Ammonia (NH₃)
Inaweza kuzalishwa kutoka gesi asilia kwa kutumia Haber Process, ambapo methane hutumiwa kuzalisha hidrojeni inayochanganywa na nitrojeni kutoka hewani kutengeneza ammonia. Ammonia ni malighafi muhimu katika utengenezaji wa mbolea kama urea. Lakini kabla ya kupata Amonia lazima kwanza uifanyie gesi asilia (Methane) steam reforming kwa kuipiga na mvuke wa maji kwa kutumia catalyst ili upate hydrogen na carbon monoxide. Baada ya hapo utiapiga hydrogen na nitrogen ili upate ammonia. Unaweza kuitumia Ammonia kwaajili ya kutengeneza kemikali zingine. Au unaweza kuipiga Ammonia na carbon monoxide ili upate Urea.

Methanol (CH₃OH)
Inaweza kuzalishwa kutoka methane kupitia Methanol Synthesis Process, ambapo methane inachanganywa na mvuke wa maji na oksijeni kuzalisha gesi ya mchanganyiko (syngas), ambayo hubadilishwa kuwa methanol. Methanol hutumika kama malighafi ya kutengeneza kemikali nyingine na kama nishati.

Petrochemicals ambazo gesi yetu haiwezi kuzalisha kwa urahisi

Gesi asilia ya Tanzania haiwezi kuzalisha kwa urahisi kemikali zifuatazo kwa sababu zinahitaji gesi yenye ethane, propane, au mafuta ghafi (crude oil) kama malighafi kuu:

Polyethylene (PE)
Hutokana na ethylene, ambayo mara nyingi huzalishwa kutoka kwa ethane au mafuta ghafi. Kwa kuwa gesi yetu haina ethane ya kutosha, hatuwezi kuzalisha polyethylene kwa kiwango kikubwa.

Polypropylene (PP)
Hutengenezwa kutoka kwa propylene, ambayo huzalishwa zaidi kutoka kwa mafuta ghafi au ethane/proane iliyopo kwenye gesi yenye mchanganyiko wa hydrocarbons nyingi (wet gas). Gesi yetu ni “dry gas”, hivyo haina propylene ya kutosha kwa uzalishaji wa polypropylene.

Thermoplastic polyurethane (TPU)
Inahitaji isocyanates na polyols zinazopatikana kutoka kwa petrochemical compounds zinazotokana na mafuta ghafi.

Ethylene (C₂H₄) na Propylene (C₃H₆) Zinazalishwa kwa wingi kutoka kwa ethane na propane, ambazo gesi yetu haina kwa kiwango kikubwa.

Benzene, Toluene, na Xylenes (BTX compounds)
Hizi zinapatikana zaidi kutoka mafuta ghafi (crude oil) au gesi yenye mchanganyiko wa hydrocarbons nyingi, ambayo Tanzania haina. BTX compounds hutumika kutengeneza plastiki, rangi, dawa, na vimumunyisho vya viwandani.
Kwamba gesi asilia ya Tanzania ni tofauti na ya nchi nyingine sidhani kama ni kweli

Kuna jambo unachanganya gesi asilia ina methane, maji, probane, butane, kwa pamaja refinery ndo inazitengeneza hizo sasa unasemaje haiwezekani ulichoandika sio sahii

Na kuhusu Benzene, Toluene, na Xylenes unanua malighafi inayoitwa naptha ambayo inazalishwa na crude oil refinery

Kumbuka naptha kwenye petrochemical plant kama raw material inaweza tengeneza
Probane, butane, ethane, benzene, toluene, xylenes
 
Gesi asilia inayopatikana Tanzania, ina kiwango kikubwa cha methane (CH₄) asilimia 90% hadi 99%.

Ethane (C₂H₆) chini ya 5%,
Propane (C₃H₈) chini ya 1%,
Butane (C₄H₁₀),
Hydrocarbons nyingine chini ya 1%, K
Kaboni dioksidi (CO₂) kwa kiwango cha 0.5% - 3%,
Nitrojeni (N₂) chini ya 1%, na
Kiasi kidogo cha hidrojeni salfidi (H₂S).

Hii inafanya gesi inayo patikana Tanzania iwe gesi inayofaa kwa matumizi ya kuzalisha umeme, kupikia kupitia mabomba, na matumizi ya viwandani.

Kwa kuwa haina kiasi cha kutosha cha propane na butane haiwezi kutumika kuzalisha LPG (Liquefied Petroleum Gas).

LPG kwa kawaida huhitaji gesi yenye propane na butane kwa kiwango kikubwa, ambacho Tanzania haina.

Vilevile, gesi yetu haiwezi kuzalisha hidrojeni (H₂) kwa urahisi kama ulivyo andika. Uzalishaji wa hidrojeni kwa kawaida unahitaji gesi zenye mchanganyiko wa hydrocarbons tofauti au maji kupitia electrolysis.

Kwa kuwa gesi yetu ina methane kwa kiwango kikubwa, njia pekee inayowezekana ni Steam Methane Reforming (SMR), ambayo inahitaji mitambo mikubwa na uwekezaji mkubwa.

Hadi sasa, Tanzania haijaweka kipaumbele kwenye uzalishaji wa hidrojeni kutoka gesi asilia.
Kuna jambo amambalo unachanganya LPG kwa asilimia kubwa inazalishwa na crude oil refinery ila gesi zinazounda LIquified Petroleum gesi zinaweza pia kuchakatwa kwenye natural gesi refinery ambazo ni butane na probane kumbuka hizi ndo zinatengeneza LPG
 
Mkuu, kuhusu Gas Refinery, mara nyingi tunaziita Natural Gas Processing Plants. Hizi tulishazijenga; zipo huko Mtwara na Lindi, na tayari zimeshaanza kuchakata au kusafisha gesi asilia. Hii ndiyo gesi tunayoitumia kwenye magari, bajaji, na viwandani.

Pia tunaitumia kuzalishia umeme, na kuna baadhi ya nyumba ambazo tayari zimeshaanza kusambaziwa gesi kwa njia ya bomba kwa ajili ya kupikia. Gesi yetu huwezi kuitumia kupikia ikiwa kwenye mtungi; ni lazima iwe kwenye bomba kwanza.

View attachment 3261861

Tuna:

1. Songo Songo Natural Gas Processing Plant
View attachment 3261844

2. Madimba Natural Gas Processing Plant

View attachment 3261845

Mkuu, Tanzania hatuwezi kuzalisha LPG kwa sasa kwa sababu gesi yetu ina kiwango kikubwa cha Methane. Hivyo, hatuwezi kuitumia kuzalisha LPG.

Ili uzalishe LPG, unahitaji mafuta (crude oil) au gesi yenye kiwango kikubwa cha Butane na Propane. LPG ndiyo gesi pekee inayoweza kutumika majumbani kwa kupikia ikiwa kwenye mtungi, hata katika maeneo ya vijijini yaliyo mbali na visima vya gesi.

View attachment 3261862

Unachokizungumzia hapa ni Liquefied Natural Gas Plant (LNG Plant). LNG Plant siyo refinery, bali ni kiwanda kinachobadili gesi asilia kuwa kimiminika ili isafirishwe nje ya Tanzania na kuuzwa kwenye masoko ya kimataifa.

Gesi asilia inapoozwa kwenye nyuzi joto -162 °C, inageuka kuwa kimiminika cha baridi, kisha inajazwa kwenye mitungi na kupakiwa kwenye meli tayari kwa kusafirishwa kwenda masoko ya nchi za Magharibi, ambako inaweza kununuliwa kwa wingi ili mwekezaji arudishe fedha zake za uwekezaji haraka.

View attachment 3261846
Hatuna natural gesi refinery ndo maana mpaka sahivi serikali inatafuta mwekezaji sasa unavyosema zipo tayari unashangaza
Umeshawah jiuliza ile budget ya usd billion 40 ni ya nini kama kila kitu kipo unavyosema
 
Unapanga vizuri tu kumbuka natural gas refinery inatoa malighafi kama ethane ambayo inatumika na petrochemical plant kama malighafi
Uganda mwenye mafuta kashindwa kujenga refinery sababu ya gharama kubwa ndio maana kaamua a export mafuta ghafi ndio Tanzania tuweze ambapo mafuta yanapita tu toka Uganda kwenda nje

Gharama za kujenga refinery nchi yaweza filisika
 
TUNACHOPIGANIA SASA
Kwenye mradi wa gesi asilia ambao mazungumzo bado yanaendelea tunapendekeza mambo yafuatayo;-
  1. Mwekezaji asijenge tu kiwanda cha kuchakata gesi asilia (natural gas refinery), bali ajenge na kiwanda cha petrochemical kwa pamoja.
  2. Mwekezaji azalishe megawatts laki moja (100,000) za umeme kutoka kwenye gesi asili, na bidhaa zitokanazo na gesi asilia kama hydrogen. Zitasaidia kwenye ukuaji wa viwanda.
  3. Tanzania itafute mwekezaji wa crude oil refinery ambayo itakua Tanga pale ambapo bomba la mafuta la uganda litaishia kutoka uganda.
  4. Shule za msingi za serikali kuongeza wigo wa masomo ya kingereza (english) na kuwa matatu nayo ni kingereza, hesabu kwa kingereza na science kwa kingereza huku kiswahili kikifundishwa masomo mawili kiswahili na uraia-hii haitawaacha nyuma watoto wa kimaskin kama ilivyo sasa kwamba kuna watoto wanamaliza msingi wakiwa na msingi mzuri wa lugha ya kingereza huku wengine wakiwa na msingi mbovu wa lugha ya kingereza na mitihani iwe sawa kwa shule za msingi za serikali na binafsi.
  5. Kuanzisha mamlaka itakayohusika na upimaji wa makazi, ili kuhakikisha watu wanajenga kwa kufuata mpangilio ili iwe rahisi kuwasambazia gesi majumbani, na huduma nyingine za kijamii na itakuwa na kazi zifuatazo;-
  • Kupima nchi nzima.
  • Kuhakikisha yeyote anayejenga anafuata mipango miji.
  • Kuhakikisha kwenye miji, na vijiji kunakuwa na zoning na sio sasa unakuta gesti imejengwa katikati ya makazi ya watu.
  • Kuhakikisha kwenye makazi yote kunapita miundombinu muhimu kama fiber, maji, n.k inapitak kwa kila mwenye nyumba.
  • Kutoa elimu ya mipango miji na faida zake kwa wananchi.
  • Polisi wa mipango miji watahakikisha wanaojenga wanafuata masharti na kuwatia nguvuni wote wanaojenga kiholela a.k.a wakaidi.
  • Mapato yote ya majengo watakuwa wanakusanya wao.
TEFA (Tanzania Economic Freedom Advocacy) ni wakina nani????
Ni jamii yenye malengo ya kupigania Tanzania itumie rasilimali zake kiukamilifu ili kuondoa umaskini unaosumbua kaya nyingi.

MAONO (Vision)
Kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda.
Kwanza miundombinu ya maji machafu tu imetushinda !
Hiyo orodha ndefu tutaiweza ??!
Najaribu kujiuliza tu alakini 😳🙌
 
Gesi asilia ya Tanzania haiwezi kuzalisha petrochemical products zote ulizo andika hapo kwa urahisi, lakini inaweza kutumika kama malighafi kwa baadhi ya bidhaa fulani zinazotokana na gesi, hasa ammonia na methanol.

Hata hivyo, gesi yetu haiwezi kuzalisha kiurahisi polyethylene, polypropylene, thermoplastic polyurethane, ethylene, propylene, benzene, toluene, na xylenes, kwa sababu muundo wake una methane (CH₄) kwa kiwango cha juu sana (90-99%) na haina kiasi kikubwa cha ethane, propane, au butane, ambazo ni malighafi kuu katika uzalishaji wa petrochemicals.

Petrochemicals ambazo Tanzania inaweza kuzalisha kwa kutumia gesi asilia

Ammonia (NH₃)
Inaweza kuzalishwa kutoka gesi asilia kwa kutumia Haber Process, ambapo methane hutumiwa kuzalisha hidrojeni inayochanganywa na nitrojeni kutoka hewani kutengeneza ammonia. Ammonia ni malighafi muhimu katika utengenezaji wa mbolea kama urea. Lakini kabla ya kupata Amonia lazima kwanza uifanyie gesi asilia (Methane) steam reforming kwa kuipiga na mvuke wa maji kwa kutumia catalyst ili upate hydrogen na carbon monoxide. Baada ya hapo utiapiga hydrogen na nitrogen ili upate ammonia. Unaweza kuitumia Ammonia kwaajili ya kutengeneza kemikali zingine. Au unaweza kuipiga Ammonia na carbon monoxide ili upate Urea.

Methanol (CH₃OH)
Inaweza kuzalishwa kutoka methane kupitia Methanol Synthesis Process, ambapo methane inachanganywa na mvuke wa maji na oksijeni kuzalisha gesi ya mchanganyiko (syngas), ambayo hubadilishwa kuwa methanol. Methanol hutumika kama malighafi ya kutengeneza kemikali nyingine na kama nishati.

Petrochemicals ambazo gesi yetu haiwezi kuzalisha kwa urahisi

Gesi asilia ya Tanzania haiwezi kuzalisha kwa urahisi kemikali zifuatazo kwa sababu zinahitaji gesi yenye ethane, propane, au mafuta ghafi (crude oil) kama malighafi kuu:

Polyethylene (PE)
Hutokana na ethylene, ambayo mara nyingi huzalishwa kutoka kwa ethane au mafuta ghafi. Kwa kuwa gesi yetu haina ethane ya kutosha, hatuwezi kuzalisha polyethylene kwa kiwango kikubwa.

Polypropylene (PP)
Hutengenezwa kutoka kwa propylene, ambayo huzalishwa zaidi kutoka kwa mafuta ghafi au ethane/proane iliyopo kwenye gesi yenye mchanganyiko wa hydrocarbons nyingi (wet gas). Gesi yetu ni “dry gas”, hivyo haina propylene ya kutosha kwa uzalishaji wa polypropylene.

Thermoplastic polyurethane (TPU)
Inahitaji isocyanates na polyols zinazopatikana kutoka kwa petrochemical compounds zinazotokana na mafuta ghafi.

Ethylene (C₂H₄) na Propylene (C₃H₆) Zinazalishwa kwa wingi kutoka kwa ethane na propane, ambazo gesi yetu haina kwa kiwango kikubwa.

Benzene, Toluene, na Xylenes (BTX compounds)
Hizi zinapatikana zaidi kutoka mafuta ghafi (crude oil) au gesi yenye mchanganyiko wa hydrocarbons nyingi, ambayo Tanzania haina. BTX compounds hutumika kutengeneza plastiki, rangi, dawa, na vimumunyisho vya viwandani.
Ufafanuzi mzuri sana wa kitaalamu

Tundu Lisu na ujuaji wako na kelele zako za ooh gesi asilia umeeelewa mtaalamu alichoeleza?
 
Ufafanuzi mzuri sana wa kitaalamu

Tundu Lisu na ujuaji wako na kelele zako za ooh gesi asilia umeeelewa mtaalamu alichoeleza?
Kaelezea pumba dunia kote inajulikana gesi asilia inatoa malighafi kwa ajili ya viwanda vya petrochemical kama ethane, butane na probane
 
Kutengeneza drilling na refinery ya gesi asilia ni almost usd billion 40 zaidi ya budget ya Tanzania ya nchi kwa akili yako unamsuli wa kufanya hivyo kama nchi
Wale waliofanya kwenye Nchi zao waliipata wapi Hiyo misuli unayoiulizia ???!

Ndio maana pia Madini ya Dhahabu wakakubali waliokuwepo juu awamu zile kuyaachia yaende kwa kukubali Nchi ipewe asilimia kiduchu ! (3%) 😳

Mwamba alisemaga Tumepigwa !
 
Wale waliofanya kwenye Nchi zao waliipata wapi Hiyo misuli unayoiulizia ???!

Ndio maana pia Madini ya Dhahabu wakakubali waliokuwepo juu awamu zile kuyaachia yaende kwa kukubali Nchi ipewe asilimia kiduchu ! (3%) 😳

Mwamba alisemaga Tumepigwa !
Mwamba alianzisha mradi wa train ya umeme mpaka leo unatutoa damu kama nchi na hujafika hata usd billion 20 sembuse usd billion 40
 
Kwamba gesi asilia ya Tanzania ni tofauti na ya nchi nyingine sidhani kama ni kweli

Kuna jambo unachanganya gesi asilia ina methane, maji, probane, butane, kwa pamaja refinery ndo inazitengeneza hizo sasa unasemaje haiwezekani ulichoandika sio sahii

Na kuhusu Benzene, Toluene, na Xylenes unanua malighafi inayoitwa naptha ambayo inazalishwa na crude oil refinery

Kumbuka naptha kwenye petrochemical plant kama raw material inaweza tengeneza
Probane, butane, ethane, benzene, toluene, xylenes
At what percentage ? Ingekuwa rahisi na economically feasible kwanini hata Biogas zote tusibadilishe na kuziweka kwenye mitungi ? The whole thing itakuwa sio economically viable, ni cheaper na efficient kuitumia kama ilivyo (kama tungekuwa na infrastructure tungeipeleka mpaka kila nyumba kama mabomba ya maji. Ila next alternative is better tuipeleke sehemu moja au chache zikafue umeme.

Mkuu every conversion inatumia Nishati na hata kuifanya gesi asilia kuwa LNG ni sababu ya storage unaipressurize inakuwa liquid katika nyuzi joto ndogo ili uisafirishe kwa urahisi ikifika inapofika bila hio nyuzi joto ndogo inarudi kuwa gesi asilia na mwisho wa siku inatumika tena (mtiririko mzima unatumia Nishati ila bado ni economical kwa wanaonunua sababu wana uhaba wa Nishati tofauti na sisi wenye alternative)...

Mkuu issue sio kuweza kufanya bali je unachofanya kina make economical sense ? Is it sustainable ?!!

Unaongelea Hydrogen kama unaitaka sana kwanini hata wewe usitumie maji na electrolysis utengeneze hio hydrogen (ila bado utajikuta hata storage yake sio that easy na ni gharama)
 
Makampuni makubwa ya mafuta ya binafsi ya kimataifa ndio yenye uwezo wa kujenga refinery
Hakuna serikali duniami yenye uwezo huo

Hata uarabuni refinery zimejengwa na makampuni binafsi makubwa ya kimataifa
Hakuna nchi inayoshindwa kufanya lolote lile..., Miradi yote mikubwa kuliko yote lazima iwe na government / taxpayers money (hapa naongelea miradi kama ya NASA n.k.) kwahio nchi kukosa pesa hio sio sababu...

Issue ni kwa nchi kutumia taxpayers money kwa jambo ambalo halina tija hivyo kuchezea pesa za mlipa kodi; anachokiongelea does not make sense wala return on investment huenda isirudi na tuna better alternatives kama issue ni nishati (kupikia through umeme) na Nishati kuendeshea (through CNG / Gesi asilia).., Na kuhusu miradi na kukopa ngoja nikuulize....

 
At what percentage ? Ingekuwa rahisi na economically feasible kwanini hata Biogas zote tusibadilishe na kuziweka kwenye mitungi ? The whole thing itakuwa sio economically viable, ni cheaper na efficient kuitumia kama ilivyo (kama tungekuwa na infrastructure tungeipeleka mpaka kila nyumba kama mabomba ya maji. Ila next alternative is better tuipeleke sehemu moja au chache zikafue umeme.

Mkuu every conversion inatumia Nishati na hata kuifanya gesi asilia kuwa LNG ni sababu ya storage unaipressurize inakuwa liquid katika nyuzi joto ndogo ili uisafirishe kwa urahisi ikifika inapofika bila hio nyuzi joto ndogo inarudi kuwa gesi asilia na mwisho wa siku inatumika tena (mtiririko mzima unatumia Nishati ila bado ni economical kwa wanaonunua sababu wana uhaba wa Nishati tofauti na sisi wenye alternative)...

Mkuu issue sio kuweza kufanya bali je unachofanya kina make economical sense ? Is it sustainable ?!!

Unaongelea Hydrogen kama unaitaka sana kwanini hata wewe usitumie maji na electrolysis utengeneze hio hydrogen (ila bado utajikuta hata storage yake sio that easy na ni gharama)
Bado uko mbali sana kifikra sio kosa lako
 
Hakuna nchi inayoshindwa kufanya lolote lile..., Miradi yote mikubwa kuliko yote lazima iwe na government / taxpayers money (hapa naongelea miradi kama ya NASA n.k.) kwahio nchi kukosa pesa hio sio sababu...

Issue ni kwa nchi kutumia taxpayers money kwa jambo ambalo halina tija hivyo kuchezea pesa za mlipa kodi; anachokiongelea does not make sense wala return on investment huenda isirudi na tuna better alternatives kama issue ni nishati (kupikia through umeme) na Nishati kuendeshea (through CNG / Gesi asilia).., Na kuhusu miradi na kukopa ngoja nikuulize....

Unafikra za kijamaa kila kitu ifanye serikali hakuna nchi dunia yenye uwezo wa kufanya miradi mikubwa peke yake hata china iliendelea kwa sababu ya wawekezaji kutoka nchi za magharibi kwenda kuwekeza china
 
Back
Top Bottom