Tanzania Economic Freedom Advocacy (TEFA)

Hatuna natural gesi refinery ndo maana mpaka sahivi serikali inatafuta mwekezaji sasa unavyosema zipo tayari unashangaza
Umeshawah jiuliza ile budget ya usd billion 40 ni ya nini kama kila kitu kipo unavyosema
Hiyo budget ni ya kujenga LNG Plant sio ya Natural Gas Refinery. Natural gas Refineries zipo Mtwara na Lindi. Moja ipo Madimba na Nyingine ipo Songo Songo. Natural Gas Refinery ni kiwanda cha kuchakata gesi asilia ili ifae kwa matumizi. LNG Plant kazi yake kubwa ni kubadili gesi asilia kuwa kimiminika ili iwe rahisi kuisafirisha kwa njia ya meli.
 
Unafikra za kijamaa kila kitu ifanye serikali hakuna nchi dunia yenye uwezo wa kufanya miradi mikubwa peke yake hata china iliendelea kwa sababu ya wawekezaji kutoka nchi za magharibi kwenda kuwekeza china
Aliyesema kila kitu ifanye Serikali ni nani ? Hivi wewe na akili zako unaweza ukasema Nchi inashindwa ku raise funds?

Na unadhani watu binafsi pesa wanatoa wapi kwenye briefcases ? Au na wao wanakopa tena kutumia mradi wako kama collateral ? Mkuu jitahidi kutafuta information na jielimishe hii ni karne ambayo information zipo wide open kukosa ufahamu ni uzembe...
 
Kuna mambo mengi huyajui
 
Kuna mambo mengi huyajui
Hivi ndio vioja badala ya kuelezea hayo ambayo siyajui wewe unaendelea kuelezea kwamba siyajui sasa huoni kwamba tunajaza posts bila sababu ? Kwahio tuanze kongelea ufahamu wangu.

Kuhusu ufahamu wangu ni kweli sifahamu mengi tu....

I am the Wisest Man Alive.., for I know One thing and that is I Know Nothing.....; Hence am more knowledgeable today than I was yesterday, kwa kuendelea kujifunza on a daily basis....
 
Nimeshakuelezea ila umekataa kuelewa mimi nifanyaje ila taratibu taratibu utaelewa
 
Angalia hii diagram utanielewa namaanisha nini point yangu ni kwamba natural gas refinery inatoa ethane, probane na butane ambazo kwenye crude oil refinery unazipata kupita napthaView attachment 3262315
Unajua kitu kinaitwa comperative advantage ? Huo mradi wako wa kutengeneza hizo petrochemicals hata ukishakamilia return on investments na masoko inakuwaje ? Kumbuka hapo wengine hawaanzi kufanya production ili wapate hizo petrochemical products bali hizo ni kama wastes za kitu wanachofanya kwahio kwa kutengeneza kwao hizo ni kama ziada...; It's not a venture in itself....

Ni kama wewe unapika chakula na kutoa moshi (Waste) lakini ukagundua kwamba hata ule moshi unaweza ukaukusanya na kukaushia nyama...
 
Makampuni makubwa ya mafuta ya binafsi ya kimataifa ndio yenye uwezo wa kujenga refinery
Hakuna serikali duniami yenye uwezo huo

Hata uarabuni refinery zimejengwa na makampuni binafsi makubwa ya kimataifa
Hakuna shida yeyote kama mikataba ingekuwa ni ya win win situation !
 
Mkuu Logikos ... Naomba umwelewe Mtoa mada ya kuwa hataki kuongeza chochote kwenye kuelewa wake anaamini kuwa yupo sahihi asilimia mia moja ..
Hataki challenge hataki Criticism...

Ninaweza sema umwache Lakini Ameleta mada hapa kwenye Open forum sasa sijaelewa alitaka ipite bila kupingwa au lah...

It's all about sustainability
 
Ni budget ya kujenga offshore drilling na refinery
 
Tukae hapa
@Meneja wa Makampuni
Upo wapi kati ya hizo taasisi ulizozitaja mkuu? GASCO, TPDC, TANOIL? Wamekufikisha uwanja wa nyumbani...shule kubwa nimepata
Hao TPDC, TANOIL au GASCO kipi cha maana walichofanya hawana mtaji wowote ndo changamoto yao
Hivi vitu vinahitaji fedha na sio maneno mengi
 
Unajua ukiwa na petrochemical plant unajua huitaji tena ku-import polythylene n.k kutoka uarabuni na tutakuwa tunawauzi nchi za sadc kumbuka hakuna nchi yenye petrochemical kwa nchi za sadc sasa unasemaje haina faida

Na viwanda vyote vya plastic vitakuwa vinanunua malighafi hapa Tanzania na sio ku-import kama wanavyofanya sasa unasemaje petrochemical haina faida

Watu wenye fikra kama zako ndo wamejaa serikali kila ukipeleka wazo wanalipiga chini kwamba ooh haiwezekan mara halina faida ilihali nchi ni maskini ya kutupa baada ya miaka 60+ ya uhuru
 
Hao TPDC, TANOIL au GASCO kipi cha maana walichofanya hawana mtaji wowote ndo changamoto yao
Hivi vitu vinahitaji fedha na sio maneno mengi
Mkuu, unataka kusema huko Songosongo na Madimba sio vitu vya maana? Si ni TPDC hao au?
 
Saafi sana Sana, wekeni na website sasa. Kumeanza kuchangamka Wallah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…