Inabidi muwache ushindani wakijinga kwani united nation kwa wao slum ni sehemu yeyote ambayo haijapimwa, tatizo lilokuwepo Kenya especially in Nairobi watu wa hali ya chini hawana jinsi ya kujenga nyumba za bei nafuu
Wakati Dar Es salaam watu Wenye hali ya chini wanauwezo wakujenga.Kenya inabidi isaidie watu wake zaidi kwani Nairobi inaitaji nyumba zaidi ya 2 million za bei nafuu, inawezekana kujenga nyumba zote kwa kutumia Saccoss ilikuwapa watu mortgage za bei nafuu.
Watu wanaishi Slum za dar ni maskini tu kama wale wanoishi slumza Kibera...... hawana maji safi, mazingira masasi, au uwezo wa kiuchumi....... Lakini kinachofanya kibera iwe mbaya zaidi ni kwavile kibera ni mahali padogo sana ki jiografia (Ukilinganisha na hata mbuga ya wanyama ya Nairobi(Nairobi National Park NNP) ni 117square Kilometer wakati Kibera ni 2.5 sq.km) , hivyo kila kitu kimeshikana..... Tena ukumbuke Dar iko pwani -Upande wa pwani hua kuna design tofauti za kujenga, Mara nyingine si lazima uwe na simiti, Unaezajenga na udongo na ukuta flat nimeona hata mombasa vitongoo duni hua wanafanya hivyo.
---- Tofauti na kibera, pale wanaokaa kwa hayo mabati, si yao, wanakodisha na kulipa from 300,400-700Ksh kwa mwezi, ukipatengeneza unatengezea mkodishaji,mwezi ujao ukishindwa kulipa atakuhamisha!
Nilikua nasoma kuhusu dar nikaona mahali flani WB inasema suluhisho moja kupunguza uongezeko wa slum dar ni kupanua mipaka ya jiji kama vile swiden au sijui netherlands ilivyofanya...... Naona nairobi ikifuatilia hivyo na ikifanyikiwa kupanua mipaka ya mji pia tutatatua shida kadhaa, manake vile Nairobi ni ndogo, kununua shamba ekari moja ni zaidi ya pesa utakazotumia kujenga nyumba ndogo.. Wakiongeza jiji labda kutakua na nafasi ya kupumua..... Tena isitoshe, Nairobi Ni 684 skq.km wakati NNP ni 117sq.km hii inamaanisha 20% ya nairobi (ambayo ni ndogo tayari) ni mbuga ya wanyama!
Angalia nairobi, Mji mkubwa wenye watu wengi zaidi Kenya, huo mji na pia Mombasa imebewa mipaka midogo sana
Kama Nairobi haitaongezwa mipaka basi ile mipango ya Nairobi Metro iharakishwe ili hata watu wa mapato ya chini wawe na uwezo wa kusafiri kila asubuhi na jioni kwa nauli ndogo kupitia treni au BTR kutoka metro region kwa county jirani kama Kajiado,Kiambuu, Machakos wakija Nairobi ili wawe hawana haja ya kuishi kibera ambapo wanaweza tembea hadi CBD wakitafuta kazi..
Alafu hayo mambo ya sijui morgage ya bei nafuu, hayata saidia, Tayari wakaazi wa kibera walianza kujengewa apartmets hapo kando ya kibera ambapo walikua watalipa bei nafuu(Nafikiri ilikua 1000 kwa mwezi 1 bedroom na 2k for 2 bedroom), Lakini mradi wenyewe ulionekana kufanya zero work, pindi wakazi wa kibera walipoanza kuhamishwa kwa hizo nyumba, walizikodisha 4K-5k kwa wakenya wengine na wakarudi kibera ya mabati ili wapate faida , Kwahivyo suluhisho la kuhamisha wakaazi wa kibera ni mwanzo uwapatie kazi itakayo lipa vizuri
apartment mpya za kibera ndo hizo hapo unaziona zilijengewa hata ukuta na barabara
Zile picha nimeona zikiwekwa hapa za kibera ni za kitambo, sasa kuna barabara (southern by-pass inapita kati kati ya kibera
Ukiangalia upande wa kushoto bado ni hizo appartment mpya zilizojengewa za wakaazi wa kibera, lakini kama nilivyosema, wengine wao walizikodisha na kurudi Kibera ya mabati
ukiangalia hapo wamesafisha wanataka kuongeza apartment zengine, lengo ni kuondoa kibera polepole, lakini serekali imegundua ni vigumu sana