Tanzania: Hatukupiga kura sababu tulichotaka kati ya Urusi vs Ukraine hakikutokea!

Tanzania: Hatukupiga kura sababu tulichotaka kati ya Urusi vs Ukraine hakikutokea!

Kutokupiga kura kuunga mkono upande wowote kidiplomasia maana yake ni kuwa na upande lakini tunaogopa kuunyosha wazi wazi.

Na katika hili la sasa maana yake Tanzania tumechagua upande wa Vita, tunawaunga mkono Urusi kwa 100%, hivyo huyo waziri wa mambo ya nje wa Tz aache kutufanya sote wajinga.

Na katika hili tujiandae kulipa gharama.
Kwani tuliwahi kupewa nafasi ya kupiga kura juu ya iraq, Libya, syria nk pia?

Uwepo wa Urusi ni muhimu sana ili kubalance shobo za wazungu.

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Kutokupiga kura kuunga mkono upande wowote kidiplomasia maana yake ni kuwa na upande lakini tunaogopa kuunyosha wazi wazi.

Na katika hili la sasa maana yake Tanzania tumechagua upande wa Vita, tunawaunga mkono Urusi kwa 100%, hivyo huyo waziri wa mambo ya nje wa Tz aache kutufanya sote wajinga.

Na katika hili tujiandae kulipa gharama.
Nchi imekosa mwelekeo. Kwenye hili huwezi kuwa na neutral position.
 
Kwa mujibu wa vitabu vitakatifu- Mungu hapendi kauli kama hizi, hata ktk vita ya malaika Gabriel na Lucifer - wale malaika wote walio kaa kando kuangalia mshindi ni nani ili wajiunge naye - waliswekelewa mbali pamoja na kundi la Lucifer...

Yaani Ukraine inavamiwa na inajitetea kutetea sovereignty yake na bado sisi kama nchi tunasema tuko neutral...je ikitokea sisi tukavamiwa na majirani na kupewa kauli kama hii, tutaona ni Sawa?
Kwani wewe ni mtoto?

Tz iko upande wa Urusi!

Ingekuwa enzi za Magu angekuwa anashambuliwa kwa matusi humu kwamba yuko upnde wa dikteta Putin.

Ndio maana mimi huwa naidharau sana hii mianaharakati uchwara ya tz

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Kwa nini Ukraine anataka kuvunja kiholela makubaliano na Urusi kwamba asijiunge NATO?
Hakukuwa na makubaliono yoyote ya namna hiyo. Soma historia ya jambo hilo kwa ukamilifu wake, usikimbilie kumeza maneno ya Putin ambayo ni uwongo mtupu.

Mwaka 1949 baada ya vita iliyokuwa imeanzishwa na na Ujerumani, dunia ilikuwa imegawanyika makundi mawili, moja lilikuwa linaongozwa na muungano wa nchi za Urusi, na la pili lilikuwa linaongozwa na muungano wa nchi za magharibi. Kwa vile Ujerumani ndiyo iliyokuwa imeanaisha vita ile, ilivunjwa vipande viwili, kimoja kikawa chini ya muungano wa Magharibi, na kingine kikawa chinia ya muungano wa Urusi. Nchi kadhaa za Magharibi (siyo zote) zilingia mktaba wa kushirikiana iwapo mmoja wao atashambuliwa, mkataba huo ndio unaoitwa NATO leo, vile vile nchi saba za mashariki zikaingia mkataba wao wa kuwa na ulinzi wa pamoja ulioitwa Warsaw Pact ambazo zilikuwa zinatawaliwa kikomunist. Nchi kadhaa za Ulaya hazikutaka kuingia mktaba wowote kati ya hiyo miwili: nchi hizo ni pamoja na Austria, Cyprus, Finland, Ireland, Malta, na Sweden.

Miaka 40 tangu ya kuanzishwa kwa NATO na WP, nchi zilizokuwa chini ya NATO ziliendelea sana kiuchumi wakati zile zilizokuwa chini ya WP zikirudi nyuma sana kiuchumi na maisha kuwa magumu kila siku. Mwaka 1987 Gorbachev akiwa Katibu Mkuu wa chama cha kikomunist alihimiza mabadiliko ya kiuchumi ya Perestroika, ambapo pamoja na mambo mengine alihimiza nchi wanachama wa USSR na wale wa WP kufanya maamuzi yao ya kiuchumi wenyewe badala ya kusubiri kuamuliwa na viongozi wa juu (Perestroika) na kutaka serikali ziongoze kwa ukweli na uwazi (glasnost). Hiyo ilisababisha nchi zilizokuwa chini ya WP kuanza kuachana na uchumi wa kikomunist, hali iliyopelekea kuanguka kwa tawala za kikomunist katika nchi zote za WP ambapo kule Romania rais wa nchi ile pamoja na mke wake walinyongwa hadharani. Mabadiliko hayo yakazikumba hata nchi za Afrika ambapo Msumbiji waasi wa Renamo wakaanza kupambana na utawala wa kikomunist wa Frelimo, serikali ya kikomunist ya Haile Mariam huko Ethiopia nayo ilipinduliwa na hata China kukawa na Maaandamano ya Tianamen Square kupinga utawala wa kikomunist.

Kutokana na mabadiliko hayo nchi za Ujerumani Magharibi na Mashariki zikaonyesha nia ya kuungana tena kuwa nchi moja, na katika mchakato huo kukawa na tatizo kuwa kwa vile Ujerumani Magaribi iko chini ya NATO, na Ujerumani Mashariki bado iko chini ya WP, itakuwaje zikiungana. Kulikuwa na alternative mbili: ama zote ziachane na mikataba hiyo, au zote ziwe chini ya mkataba mmoja. Waziri Mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher hakutaka ziungane, Rais Reagan wa Marekana akasema iwapo zitaungana basi ziwe chini ya NATO, Chancellor wa Ujeruman Helmut Kohr naye alitaka ziwe chini ya NATO. Hivyo mazungumzo yakafanyika kati ya Reagan, Kohr na Gorbachev aliyekuwa anaongoza WP wakati huo kuhusu swala hilo. Gorbachev alitaka iwapo zitaungana basi zijitoe katika mikataba hiyo. Hata hivyo baadaye Reagan na Kohr walimshawishi Gorbschev akakubali Ujerumani iungane na kuwa nchi moja chini ya NATO lakini baada ya muungano huo, NATO isichukue nchi nyingine yoyote ya WP, na pande zote tatu zikakubaliana hivyo.

Mwaka 1991, Muungano wa Soviets (USSR) ulivunjika, jambo lililosababaisha hata Mkataba wa WP nao kufa. Kufuatia hali hiyo nchi zilizokuwa chini ya USSR zikaanzisha mkataba wao wa ulinzi ulioitwa Collective Security Treaty Organization (CSTO) ambao ulianza na nchi za Armenia, Kazakhstan, Kyrgyzstan, Urusi, Tajikistan na Uzbekistan, baadaye zikafuatiwa na Georgia pamoja na Belarus. Ukraine haukujiunga na CSTO kabisa. Baadaye nchi za Azerbaijan, Georgia and Uzbekistan zilijitoa kwenye hiyo CSTO, na badala yake zikaunda kundi lao la GUAM (Georgia, Ukraine, Azerbaijan and Moldova) ambalo halikutaka kuingiliwa na Urusi kwa namna yoyote; na hata lugha yao ya mikutano walikataa kutumia kirusi bali wakawa wanatumia kiingereza. Hatua hiyo ya nchi hizo kukataa kuwa chini ya influence ya Urusi ndicho kilichoiudhi Urusi, siyo kwa sababu ya NATO hata kidogo. Serikali ya Urusi ilipoanza kuwa hostile kwa nchi hizo za GUAM vitisho vya namna hiyo vikazifanya nchi hizo na nyingine zinazopakana na Urusi kutafuta uanachama wa NATO. Utaona kuwa Urusi ilishazishambaulia nchi hizo za GUAM moja baada ya nyingine lakini haikuwahi kuzishambulia Latvia, Lithuania au Estonia zilipoomba kuwa wanachama wa NATO na baada ya muda wakakubaliwa. Ilishaishambulia Georgia, Azerbaijan (kupitia Armenia), Ukraine kwa mara tatu sasa na kwenye plani yao ya vita iliyovujishwa na rais wa Belarus ilionyesha kuwa walikuwa pia na mpango wa kusihambulia Modova; yaani nchi zote za GUAM!

Hiyo ndiyo historia halisi kwa ufupi, usilishwe propaganda za Putin nawe ukaona ni haki watu wa Ukraine kuuwawa bila hatia yoyote. Baada ya USSR kufa, WP nayo ilikufa, hivyo hakuna mkataba wowote au makubaliano yoyote yaliyosema kuwa nchi zilizokuwa chni ya WP zisikubaliwe kuwa chini ya NATO; in fact ni nchi zenyewe zinazoomba kuwa wanachama, hawalazimishiwi na NATO. Makubaliano baina ya Gorbachev na Reagan/Kohr yalikuwa ni kati ya NATO na WP ambayo haipo tena leo hii.
 
Kwani tuliwahi kupewa nafasi ya kupiga kura juu ya iraq, Libya, syria nk pia?

Uwepo wa Urusi ni muhimu sana ili kubalance shobo za wazungu.

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Wewe una akili ya ubaguzi, jambo ambalo dunaia inalipinga sana. Unachukulia kuwa maisha ya watu wa Ukraine hayana thamani kwa vile wao ni wazungu. Elewa kuwa Putin naye ni mzungu kama walivyo wazungu wa Ufaranza, wazungu wa ujerumani yeye pia ni mzungu wa urusi.
 
Sera yetu tokea enzi na enzi na hiyo, beberu Watuache!
Put-in atatuchamba Sana na bunduki Used hatotuuzia,

Wao wenyewe wanamgwaya Put-in, mkurungwa kaingia Kwa jirani, jirani hajarogwa kurusha japo kombora moja Moscow, hii inanifanya niwaone wale wa Houthi wa Yemen ni wababe, mikombora wamepiga mpaka Saudi!

Tutajadiliana Tu mitandaoni inatosha!

Hao mabalozi watuache mara chanjo mara kutugombanisha na rafiki zetu wanaogombana!
Inabdidi tufikirie tena iwapo huwa tunanunua vifaru na magari ya kijeshi kutoka urusi kwani vimeonakana kama ni karatasi tu mbele ya Ukraine. Mpaka sasa hivi Urusi wameshapoteza vifaru na magari ya deraya kwa jumla zaidi ya 600! Tusinunue vifaru kutoka urusi tena! Tutakuwa tunapoteza hela zetu za mkopo.
 
Wewe una akili ya ubaguzi, jambo ambalo dunaia inalipinga sana. Unachukulia kuwa maisha ya watu wa Ukraine hayana thamani kwa vile wao ni wazungu. Elewa kuwa Putin naye ni mzungu kama walivyo wazungu wa Ufaranza, wazungu wa ujerumani yeye pia ni mzungu wa urusi.
Ahaaa.. Kumbe watu ni wa Ukraine tu, ila Walibya, iraq, na syria wao siyo watu?

Hiyo dunia si ndio iliungana kuwaua walibya mpaka leo wanaishi kwa shida?

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Kwa mujibu wa vitabu vitakatifu- Mungu hapendi kauli kama hizi, hata ktk vita ya malaika Gabriel na Lucifer - wale malaika wote walio kaa kando kuangalia mshindi ni nani ili wajiunge naye - waliswekelewa mbali pamoja na kundi la Lucifer...

Yaani Ukraine inavamiwa na inajitetea kutetea sovereignty yake na bado sisi kama nchi tunasema tuko neutral...je ikitokea sisi tukavamiwa na majirani na kupewa kauli kama hii, tutaona ni Sawa?
Unadhan tz ina msaad gan katk hyo vta hata ingemuung mkono ukraine!ama maamz ya putin kuivamia ukrain yamechagzwa na tanzania!MIND YOUR OWN BIZNEZ,n statement fup yenye maan pana sana,ish humo.
 
Kwani wewe ni mtoto?

Tz iko upande wa Urusi!

Ingekuwa enzi za Magu angekuwa anashambuliwa kwa matusi humu kwamba yuko upnde wa dikteta Putin.

Ndio maana mimi huwa naidharau sana hii mianaharakati uchwara ya tz

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Asante kwa taarifa ndugu yangu
 
Unadhan tz ina msaad gan katk hyo vta hata ingemuung mkono ukraine!ama maamz ya putin kuivamia ukrain yamechagzwa na tanzania!MIND YOUR OWN BIZNEZ,n statement fup yenye maan pana sana,ish humo.
Nimekuelewa...ngoja tu mind our business- tuwe neutral...ikiwaka mulika na ikizima papasa...ndio mpango kwa sasa...
 
Ahaaa.. Kumbe watu ni wa Ukraine tu, ila Walibya, iraq, na syria wao siyo watu?

Hiyo dunia si ndio iliungana kuwaua walibya mpaka leo wanaishi kwa shida?

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile ap

Ongea ukiwa na facts zako vizuri. Libya na Syria yalikuwa ni mapigano ya wenyewe kwa wenyewe- waasi dhidi ya serikali; hawakuvamiwa na nchi za nje. Huko Libya urusi ilikuwa na jeshi lake ardhini kusaidia upande wa Gadaffi na NATO ikawasidia waasi kuwa kuwapa air cover, lakini vita halisi ilikuwa ni kati ya waasi dhidi ya serikali ya Gaddafi. Kule Syria, ina fact ni Urusi iliyopeleka jeshi likalobomoa mji wote wa Allepo uliokuwa unampinga Assad na kuwamwagia hewa ya sumu. Tafuta factsa zako vizuri kuhusu vita za Libya na Syria

Kuhusu vita Iraq, tulilaani sana uvamizi ule. Kama hujui tafuta kwenye records zako; serikali ya Mkapa ilitoa tamko la kupinga uvamizi ule na hata kura ilipoleklwa kwenye umoja wa Mataifa, Tanzania tulipinga, hakukaa neutral!
 
Ongea ukiwa na facts zako vizuri. Libya na Syria yalikuwa ni mapigano ya wenyewe kwa wenyewe- waasi dhidi ya serikali; hawakuvamiwa na nchi za nje. Huko Libya urusi ilikuwa na jeshi lake ardhini kusaidia upande wa Gadaffi na NATO ikawasidia waasi kuwa kuwapa air cover, lakini vita halisi ilikuwa ni kati ya waasi dhidi ya serikali ya Gaddafi. Kule Syria, ina fact ni Urusi iliyopeleka jeshi likalobomoa mji wote wa Allepo uliokuwa unampinga Assad na kuwamwagia hewa ya sumu. Tafuta factsa zako vizuri kuhusu vita za Libya na Syria

Kuhusu vita Iraq, tulilaani sana uvamizi ule. Kama hujui tafuta kwenye records zako; serikali ya Mkapa ilitoa tamko la kupinga uvamizi ule na hata kura ilipoleklwa kwenye umoja wa Mataifa, Tanzania tulipinga, hakukaa neutral!
Mkuu usitufanye watoto hapa!

Unafiki wa wazungu tunaujua na Putin anaungwa mkono na wengi sababu wanajua hiyo vita ingetokea popote katika afrika au uarabuni hungeona matamko yote hayo

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Inabdidi tufikirie tena iwapo huwa tunanunua vifaru na magari ya kijeshi kutoka urusi kwani vimeonakana kama ni karatasi tu mbele ya Ukraine. Mpaka sasa hivi Urusi wameshapoteza vifaru na magari ya deraya kwa jumla zaidi ya 600! Tusinunue vifaru kutoka urusi tena! Tutakuwa tunapoteza hela zetu za mkopo.

Kwa sababu hii hii serikali badala ya kuomba msaada wa dawa za corona Uturuki. Waangalie ni vipi wanapata drones za Uturuki zimepeleka kilio kikubwa Kremlin. Punit pamoja na jeuri yake yote leo ndio anagundua katika Uongozi wowote chini ya jua hamna kitu kama "Absolute Power" You have to relly on others. Punit uso umemshuka kwelikweli. Nguvu alizobaki nazo ni kubadilisha wasaidizi wake wa karibu 1000 na kumuweka mkuu wa ujasusi wa Urusi under house arrest. Hawezi kumlisha sumu kama alivyozoea na washirika wake wa karibu wanamuonesha wazi kuwa Mkuu wako wa ujasusi ndiye atakurithi your days are numbered.
 
Kutokupiga kura kuunga mkono upande wowote kidiplomasia maana yake ni kuwa na upande lakini tunaogopa kuunyosha wazi wazi.

Na katika hili la sasa maana yake Tanzania tumechagua upande wa Vita, tunawaunga mkono Urusi kwa 100%, hivyo huyo waziri wa mambo ya nje wa Tz aache kutufanya sote wajinga.

Na katika hili tujiandae kulipa gharama.

Wewe ndo Mjinga ukifikiri anakufanya mjinga
 
Inabdidi tufikirie tena iwapo huwa tunanunua vifaru na magari ya kijeshi kutoka urusi kwani vimeonakana kama ni karatasi tu mbele ya Ukraine. Mpaka sasa hivi Urusi wameshapoteza vifaru na magari ya deraya kwa jumla zaidi ya 600! Tusinunue vifaru kutoka urusi tena! Tutakuwa tunapoteza hela zetu za mkopo.
Ukraine je? Una takwimu zake?
 
Mkuu usitufanye watoto hapa!

Unafiki wa wazungu tunaujua na Putin anaungwa mkono na wengi sababu wanajua hiyo vita ingetokea popote katika afrika au uarabuni hungeona matamko yote hayo

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
True!
Hili ndilo lililofanya nchi nyingi za Afrika na Arab na South America kuuchuna, wao huwa hawalaani Israel anavyoshambulia Palestine!
 
Mkuu usitufanye watoto hapa!

Unafiki wa wazungu tunaujua na Putin anaungwa mkono na wengi sababu wanajua hiyo vita ingetokea popote katika afrika au uarabuni hungeona matamko yote hayo

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Hauwngi na wengi mzee; pitia zile kura za umoja wa mataifa uone tena. Anaungwa mkono na nchi chache tu, wengine kadhaa ni wale wasiokuwa na msimamo kama Tanzania, na sioyo wengi, halafu wasiomuunga ndio wengi.

Angalia kuwa anabomoa majengo na kuuwa rai wa Ukraine kwa mizinga ya mbali tu huku vifaru vyake na askari wake wakioowamo magejerali na makanali akiuawa kama mbwa koko kwenye vita ya ana kwa ana. Halafu Putin asivyokuwa na akili timamu, hataki kurudisha miili ya askari wake waliouwawa nyumbani kwao wakazikwe kwa heshima. Anajali vifo vya majenerali tu
 
Ukraine je? Una takwimu zake?
Ukraine ilipoteza ndege kadhaa wakati vita inaanza kwa vile walivamiwa ghafla zikiwa uwanjani zikapigwa mizinga. Lakini wao hawajatumia vifaru vyao kwenye vita hiyo, kwa hiyo hawajapoteza hata kifaru kimoja. Urusi inatumia vifaru na magari ya deraya, yanabomolewa kama vibuyu. Halafu kuna wakati kambi ya Ukraine ilipigwa mizinga usiku, ikauwa askari wapato 50 hivi, kwenye vita ya ana kwa ana urusi imekuwa inapoteza askari kama sisimizi waliomwagiwa mafuta ya petroli. leo hii Mnowari yao kubwa imebomolewa ikiwa bandarini na kuuwa askari wengi wa navy pamopja na Navy Commander wao.
 
Back
Top Bottom