Tanzania idadi ya watu imeongezeka lakini hali sio nzuri mkoa wa Kilimanjaro

Nimetembelea baadhi ya vijiji huko Kigoma, Katavi, Rukwa nk na kukutana na wasukuma wengi sana, vijiji vingine karibia 70 % ni wasukuma. Sasa wakati nawahoji hawa wasukuma nikagundua kwamba wanapotoka huko kwao wanauza kila kitu na kuhamia maeneo mengine, na sababu kuu wao wanasema huko kwao ardhi imechoka, ukame, uzalishaji mdogo nk hivyo kulazimika kukimbilia maeneo yenye mazingira mazuri. Sasa tofauti na watu wa Kilimanjaro ni kwamba wakati wasukuma wanauza miji/ardhi zao na kuhamia kwingine Kilimanjaro wao hawauzi maeneo yao na badala yake wanayaendeleza huku wakiwa nje ya mkoa wao.
 
Maisha hayapatikani mkoa wa Kilimanjaro?
Kwanza jiulize fursa ni nini? Pili jiulize ikiwa kijiji A kuna fursa nyingi kuliko Kijiji B ni kwa nini uhangaike na Kijiji B? Umejiuliza ni kwa nini watu wanamiminika kila siku Dar kuliko wanavyomiminika Lindi au Kigoma?
 
Kutokana na utaratibu wa wachagga kutokuuza viwanja kama makabila mengine, maendeleo yamezorota maeneo mengi.

Ukibaki kijijini utaishia kuwa mlevi wa mbege
Hapa ni moja ya vijiji vya mkoa wa Kilimanjaro, Kijiji cha Oria, Kata ya Kahe... Hapa ardhi hii hawauzi ila wanakodisha, tena kwa msimu, ambapo ekari moja ni sh laki nne... Watu wanajua umuhimu wa ardhi na pia ardhi ni ndogo hivyo hawawezi kuuza na kumnufaisha mwingine.
 
Acha wapambane na hali yao, na sasa hivi wako kwenye makafara , wanaringishiana utajiri na kafara si wanawake wala wanaume full kafara
 
Kigoma wapo wapo tu, kazi kurogana na kubishana kwa Mambo yasiyo ya msingi.
Yanga nako kila mwanaume amelishwa limwata.
 
ukiona hivyo ujue nimkoa ambao hauna fursa ukibaki huko utabaki maskini. halafu shida nyingine wanaoa kamke kamoja kamoja kamavile nimahanithi unamkuta mtu anavitoto viwilitu vya dawa.
we ni gasho
 
Kusema ukweli mleta mada yupo sahihi kabisa, natoka wilaya ya rombo nadhani huko ndio hali mbaya kabisa hata biashara ndogondogo ni vigumu kufanya kwa sababu hakuna watu, serikali hapa lazima ifanye kitu huu ujinga wa kuzaa kwa mpango hamna tutajikuta siku moja mkoa flan unapoteza origin yake.
 
Ni kweli kabisa hili jambo.sijui hata ufumbuzi wake ni upi
Ubinafsi umezidi, na umimi tatizo, lazima harakati za kifedha zianzishwe na kilimo Cha thamani kubwa kianzishwe, ili kuvuta watu upya ukiangalia kwa makini vijana wengi ni wanywa viroba hapa dar, kilimo Cha vanilla, alizeti, ndizi za kisasa zinazikomaa kwa muda mfupi na vya aina hiyo vianzishwe.
 

Wanatafuta hela hao, wewe unafikiri huko ni kisarawe kutwa kucheza draft?
 
Wachagga wanajitambua, hawazaliani kama panya na hawako tayari kukaa kwenye umaskini wakati kuna fursa nyingi mahali pengine
 
Baada ya miaka kadhaa..kilimanjaro itageuka makaburini tu..kama kinondoni makaburini...


Endeleeni kukimbia kwenu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Kwanini viwanda vyetu vingi vilikufa?
 
Ni kweli kabisa uchaggani sasa panadai urbanization lakini kwa bahati mbaya serikali yetu ipo nyuma sana ya wakati.
 
Hio ndo point yangu na wanapenda December ni wale waliozliwa kule lakin mtu amezaliwa na kukulia dar hauon umuhimu sana wa kwenda kule December wengi wanaenda kwa mkumbo hasa ambao hawajazaliwa kule
Watabisha na hilo mkuu, lakini tatizo lipo na kama wasipolirekebisha litabaki jina tu.
Baadhi ya makabila madogo hayajulikani kabisa kwasababu hizo, muingiliano na kuhamahama kwa watu kunabadili tamaduni halisi za watu.

Mchaga ilikua rahisi kabisa kumtambua kwanza kwa rafudhi yake tu, lakini sasa hivi wengi wamekulia miji mingine ile rafudhi haipo kabisa.
 
Tanzania nzima ndio inatakiwa iwe hivyo, huu ujinga wa ukabila haisaidii chochote zaidi ya kuleta ubaguzi
 
Mikoa migumu zaidi kutoa ardhi ni Arusha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…