Tanzania idadi ya watu imeongezeka lakini hali sio nzuri mkoa wa Kilimanjaro

Tanzania idadi ya watu imeongezeka lakini hali sio nzuri mkoa wa Kilimanjaro

Ukienda mkoa wa Kilimanjaro utashangaa mambo yafuatayo haya matatizo hayako tu uchagani bali hata upareni yapo

Idadi ndogo ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza, huku mikoa mingine wanafunzi wakiwa wengi na wengine wanakaa chini Hali ni tofauti mkoa wa Kilimanjaro idadi ya wanafunzi inazidi kushuka kila miaka inavyozidi kwenda Kuna shule inaandikisha darasa la kwanza wanafunzi 10, Kuna nyingine iliandikisha wa-nne

Nyumba nyingi kuwa empty hili ni tatizo lingine kubwa Kuna idadi kubwa sana ya nyumba hazina watu na ukienda vijijini Hali ndo mbaya Zaid nyumba nzuri nyingine gorofa Ila hazina watu na Hali inakua mbaya pale bibi na babu wakifariki sanasana utamkuta kijana mmoja tu ambaye Yuko kwa ajili ya kuziangalia, vijana kutoka Tanga hasa wasambaa, kutoka singida na manyara wambulu ndo utawakuta wanaangalia zile nyumba nyingi na kulimia migomba

Mfano ukienda upareni ni kawaida sana kuona nyumba imeachwa na kugeuka kuwa kichaka huku manyasi yakiwa yameota ndani huku nyumba ikiwa imebomoka bomoka

Vijiji mkoa wa Kilimanjaro havina watu kama umepanga kwenda kukaa week kwa Ile Hali ya vile vijiji vyao utajikuta umehairisha hakuna watu kabisa yaani in-short mkoa wa Kilimanjaro una ukiwa sio sawa na kipindi tunakua

Changamoto nyingine hakuna vijana Kuna kijiji nilienda kijiji kizima kijana ni mmoja ambaye ni bodaboda wengine waliobaki ni watu wa miaka 40 na kuendelea ni nadra sana kumuona kijana wa miaka 20's
Kijiji gani hicho chenye kijana mmoja? japo kuna uhalizia.
 
Hujaongelea mikoa mingine ila kumbuka ulisema "sehemu nyingine Tz ukimaanisha mikoa mingine usipokuwa Kilimanjaro. Nami nikasema hiyo mikoa mingine na Wachaga wapo, ndio walozaliana kwa wingi na mwisho watarudi Kilimanjaro.
 
Kwasababu mikoa mingi Kuna MIJINI
Pia, Kilimanjaro ni ndogo sana, na udhaifu wa serikali ulivyo wanaofanya maamuzi hawana akili.

Mfano, Kilimanjaro Kuna shule nyingi na zahanati, lakini unashangaa pesa za mgawo wa UVIKO na TOZO wakalazimishwa wajenge Tena madarasa wakati yaliyopo tu hayatumiki yote.

Lakini wangewaacha huru, wangetumia hizo pesa kufanya ukarabati wa majengo mabovu.

Kwa Kilimanjaro, Wilaya moja tu mfano Rombo inalingana na Tarafa mkoa mwingine, kwahiyo usitarajie wakashindwa kuweka umeme mkoa mzima.

Rombo unaweza kuzunguka na pikipiki masaa 6 ukaimaliza yote.

Lakini Wilaya Kama Geita au Mlimba Morogoro huo uwezo haupo leave muda mfupi.
Labda hoja yako inaweza kuwa kweli, ila mimi pointi yangu ya mwanzo nilikuwa namjibu jamaa aliyesema Kilimanjaro kuna hali mbaya ya maendeleo ndio inayochangia watu kuhama,
 
Labda hoja yako inaweza kuwa kweli, ila mimi pointi yangu ya mwanzo nilikuwa namjibu jamaa aliyesema Kilimanjaro kuna hali mbaya ya maendeleo ndio inayochangia watu kuhama,
Maendeleo ya kawaida ya kiserikali yapo sana, maana barabara kubwa Zina Rami, ndogo huwa zinalimwa mara kwa mara zipitike.

Umeme upo zaidi ya Kaya 90% na maji yapo, japo kiangazi ni mgawo.

Nyumba na ubora wa makazi yapo vizuri nadhani kwa 80%.

Kinachofanya watu wakimbie huku ni ugumu wa maisha, na ukosefu wa fursa za kiuchumi. Hata hao wengi wenye pesa na maendeleo binafsi hawatafutii huku.
 
Nice topic, naona wengi wamechangia kwa mazuri, mabaya na changamoto zilizopo.

Kwanza ni declare interest, I am proudly chaga na nakubaliana na mitazamo mingi isipokuwa ile tu ambayo ipo negative na yenye wasiwasi kwa sababu zifuatazo kama ilivyo repotiwa kwenye matokeo yetu ya senza na makazi ya mwaka huu 2022:

1. MVUA: Wengi wameongelea Kilimo lakini takwimu zinaonesha kuwa mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa maeneo yenye mvua chache sana so sio rafiki kabisa kwa kilimo. Ukiangalia, Bukoba: 2245.2mm kwa mwaka, Dar es salaam 971.5mm lakini Kilimanjaro ni only 394.3mm kwa mwaka; kumbuka kilimo ndie mwajiri mkuu hapa Tanzania.

2. IDADI YA WATU: Wapo waliosema, idadi ya watu Kilimanjaro imepungua sana, unless kwa maneno machache lakini sensa inasema idadi ya watu inaongezeka kwa wastani mzuri, mwaka 2002 wakazi Kilimanjaro walikuwa 1.4m, 2012 wakawa 1.6m na mwaka huu 2022 sensa inasema wakazi Kilimanjaro ni 2.0m. Ongezeko hili la watu kwa Kilimanjaro ni la wastani at 2.3% (Tanzania 3.1%) hivyo mlio na wasiwasi tulieni na tuendelee kuonana December mgombani

3. UCHUMI: Pamoja na wale waliokuwa na wasiwasi kuhusu viwanda vya zamani kufa, hali ya uchumi kimkoa nayo ni nzuri at TZS 3.6m regional per capital GDP; hii ni hali ya utajiri wa mkoa gawanya kwa idadi ya watu - tukipitwa na mikoa 3 tu i.e. Dar, Ruvuma na Mbeya.

4. UHALIFU: Nimeshangaa tu hali ya uhalifu, ipo juu sana kufikia jumla ya visa 2981, tunapitwa na Ilala pamoja na Kinondoni pekee ambazo ni kama wilaya, tukifuatiwa na Morogoro kwa mbali.

Taarifa zote ni kutoka kwenye reports za TBS 2022

Nawasilisha
 
Kuna kitu hakipo sawa,hata kama ni kutafuta maisha mikoa mingine ndio iwe hadi watoto wa darasa la kwanza.????
 
Hio ndo point yangu na wanapenda December ni wale waliozliwa kule lakin mtu amezaliwa na kukulia dar hauon umuhimu sana wa kwenda kule December wengi wanaenda kwa mkumbo hasa ambao hawajazaliwa kule
Ni kweli kijana aliyezaliwa dar hawezi kwenda kijijini kwao kwasababu wazazi wake wanaishi dar na wamejenga dar au mikoa mingine na huyo kijana utakuta kapata kazi mkoani uku wazazi wanaishi dar, kwaiyo kijana akipata likizo lazima ataenda dar sehemu ambayo kazaliwa na kakulia uko na wazazi wake wamejenga na kuishi dar.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Nimetembelea baadhi ya vijiji huko Kigoma, Katavi, Rukwa nk na kukutana na wasukuma wengi sana, vijiji vingine karibia 70 % ni wasukuma. Sasa wakati nawahoji hawa wasukuma nikagundua kwamba wanapotoka huko kwao wanauza kila kitu na kuhamia maeneo mengine, na sababu kuu wao wanasema huko kwao ardhi imechoka, ukame, uzalishaji mdogo nk hivyo kulazimika kukimbilia maeneo yenye mazingira mazuri. Sasa tofauti na watu wa Kilimanjaro ni kwamba wakati wasukuma wanauza miji/ardhi zao na kuhamia kwingine Kilimanjaro wao hawauzi maeneo yao na badala yake wanayaendeleza huku wakiwa nje ya mkoa wao.
Wasukuma wao wana uziana wao kwa wao.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Maendeleo ya kawaida ya kiserikali yapo sana, maana barabara kubwa Zina Rami, ndogo huwa zinalimwa mara kwa mara zipitike.

Umeme upo zaidi ya Kaya 90% na maji yapo, japo kiangazi ni mgawo.

Nyumba na ubora wa makazi yapo vizuri nadhani kwa 80%.

Kinachofanya watu wakimbie huku ni ugumu wa maisha, na ukosefu wa fursa za kiuchumi. Hata hao wengi wenye pesa na maendeleo binafsi hawatafutii huku.
Fursa za kiuchumi zipo nyingi tu, sema watu wa kule hawataki kubadilika, maisha yaleyale ya miaka ya 90 ndio wanataka kuishi vile vile
Mfano miti ya kawaha hadi leo unakuta ipo wanakomaa nayo wakati kahawa haina bei
Zao la parachichi ambalo ni deal siku hizi lina stawi sana kule lakini wachache sana ndio wamelima miche ya kisasa
Ndizi pia ni zao ka biashara lakini wapo na ndizi zile zile za miaka ya zamani

Mahindi pia pale wapo mipakani na Kenya wangelima soko lipo karibu tu
 
Fursa za kiuchumi zipo nyingi tu, sema watu wa kule hawataki kubadilika, maisha yaleyale ya miaka ya 90 ndio wanataka kuishi vile vile
Mfano miti ya kawaha hadi leo unakuta ipo wanakomaa nayo wakati kahawa haina bei
Zao la parachichi ambalo ni deal siku hizi lina stawi sana kule lakini wachache sana ndio wamelima miche ya kisasa
Ndizi pia ni zao ka biashara lakini wapo na ndizi zile zile za miaka ya zamani

Mahindi pia pale wapo mipakani na Kenya wangelima soko lipo karibu tu
Watalima wapi, ardhi kiduchu hiyo.

Hata ukiweka wastani wa ekari 2 kwa kila mtu, bado haitoshi kilimo Cha biashara.
 
Watalima wapi, ardhi kiduchu hiyo.

Hata ukiweka wastani wa ekari 2 kwa kila mtu, bado haitoshi kilimo Cha biashara.
Watu wamehama ardhi nyingi ipo tupu, sema mambo yale yale ya ukale yanawarudisha nyuma, mimi kijijini kwetu majirani karibu 4 kati ya 6 wamehama na mashamba hayatumiki ila kuuza hawauzi wala kukodisha
 
hata nchi zinakimbiwa inategemea na akina nani wako katika nchi husika, ukiona watu nwanasepa ujue kuna kitu wameona huko wanakokimbilia.
 
Nice topic, naona wengi wamechangia kwa mazuri, mabaya na changamoto zilizopo.

Kwanza ni declare interest, I am proudly chaga na nakubaliana na mitazamo mingi isipokuwa ile tu ambayo ipo negative na yenye wasiwasi kwa sababu zifuatazo kama ilivyo repotiwa kwenye matokeo yetu ya senza na makazi ya mwaka huu 2022:

1. MVUA: Wengi wameongelea Kilimo lakini takwimu zinaonesha kuwa mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa maeneo yenye mvua chache sana so sio rafiki kabisa kwa kilimo. Ukiangalia, Bukoba: 2245.2mm kwa mwaka, Dar es salaam 971.5mm lakini Kilimanjaro ni only 394.3mm kwa mwaka; kumbuka kilimo ndie mwajiri mkuu hapa Tanzania.

2. IDADI YA WATU: Wapo waliosema, idadi ya watu Kilimanjaro imepungua sana, unless kwa maneno machache lakini sensa inasema idadi ya watu inaongezeka kwa wastani mzuri, mwaka 2002 wakazi Kilimanjaro walikuwa 1.4m, 2012 wakawa 1.6m na mwaka huu 2022 sensa inasema wakazi Kilimanjaro ni 2.0m. Ongezeko hili la watu kwa Kilimanjaro ni la wastani at 2.3% (Tanzania 3.1%) hivyo mlio na wasiwasi tulieni na tuendelee kuonana December mgombani

3. UCHUMI: Pamoja na wale waliokuwa na wasiwasi kuhusu viwanda vya zamani kufa, hali ya uchumi kimkoa nayo ni nzuri at TZS 3.6m regional per capital GDP; hii ni hali ya utajiri wa mkoa gawanya kwa idadi ya watu - tukipitwa na mikoa 3 tu i.e. Dar, Ruvuma na Mbeya.

4. UHALIFU: Nimeshangaa tu hali ya uhalifu, ipo juu sana kufikia jumla ya visa 2981, tunapitwa na Ilala pamoja na Kinondoni pekee ambazo ni kama wilaya, tukifuatiwa na Morogoro kwa mbali.

Taarifa zote ni kutoka kwenye reports za TBS 2022

Nawasilisha
Sensa ya mwaka 2012 Kilimanjaro ilikuwa na watu 1.6, mwaka 2022 wapo 1.8, watu laki mbili tu kwa miaka 10, 2032 itakuwa negative
 
Sensa ya mwaka 2012 Kilimanjaro ilikuwa na watu 1.6, mwaka 2022 wapo 1.8, watu laki mbili tu kwa miaka 10, 2032 itakuwa negative
Hapana, ukichukulia kiwango cha wakazi waliohesabiwa kutoka mikoa mingine, hilo ongezeko ni very sustainable as wengi sana tumehesabiwa kutoka mikoa mingine kama Dar na Mwanza

Wakazi kama wakazi wanaweza kuwa wachache lakini wenyeji tutakuwa tumeongezeka sana.
 
Kutokana na utaratibu wa wachagga kutokuuza viwanja kama makabila mengine, maendeleo yamezorota maeneo mengi.

Ukibaki kijijini utaishia kuwa mlevi wa mbege
Ardhi ndio resource namba moja katika uchumi kusapoti shughuli zingine za kiuchumi ziende. Ukifika katika mji ambao wakazi wake wana masharti ya kichawi na ya ajabu ajabu juu ya ardhi ni ngumu sana kuvutia wawekezaji.

Kuna watu wanataka wanunue ardhi wajenge mashule, wajenge mahoteli, wajenge makampuni na taasisi ila hili swala kwa Kilimanjaro ni ngumu sana kwasababu wenyeji wanang'ang'ania ardhi as if imeshikana na roho zao au wakiuza hawatapata nyingine popote pale. Mtu yupo radhi afe masikini au aishi kifukara ila sio kukabidhi au kuuza ardhi kwa raia mwenzake anapokuja hata na offer nzuri.

Utasikia hiki kiyamba haitakiwi kuuzwa ni za watoto na wajukuu. Khaaaaah. Sasa mnaishije.

Huku Dar mtu akifika Dau unamuachia mjengo au plot unaenda kufanya issue zingine na ndio maana watu wapo vizuri na wanaishi vema bila shida.

Hizi tabia ni za ajabu sana. Wengine wenye mambo ya ajabu ni jamii za wafugaji kama wa masai na wamang'ati. Wanakuwa na mang'ombe weengi halafu hawana matumizi nayo zaidi ya kuwalisha tu na kuwatumia kama display ya utajiri. Ufala sana huu ndio maana wanatuharibia sana mazingira. Kila wanapokwenda jamii ya wafugaji ukame na uharibifu wa mazingira unatokea. Tazama dodoma pale wameharibu mkoa unaonekana ni wa ukame ila sivyo. Tazama maeneo ya Arusha namna wameharibu. Tazama mikoa kama morogoro. Wanaharibu sababu ya overgrazing na kuharibu uoto.

Haya matabia inatakiwa yatungiwe sheria kuyakata. Mtu anang'ang'ania ardhi akiwa hana matumizi nayo kwa zaidi ya miaka 15 au 20 au 30 alazimishwe kuuza akakae huko maporini kwenye ardhi nyingi isiyo na uhitaji mkubwa sio sehemu kumechangamka wewe umekaa na plot ina migomba na mahindi.

Na hawa wafugaji walazimishwe kuuza mifugo wabakie na idadi ndogo wafuge kwa zero grazing sehemu moja kwa lazima watake wasitake.
 
Back
Top Bottom