Are you sure Ngwajima anamshauri Raisi? Sio kila anayekutana na Raisi ndie mshauri wake.
Vita na gwajima utaiweza?
"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
Hiyo ya corona kuletwa na 5G mbona ni agenda worldwide... Hata nduguzo wanaiongelea.
Ona kinacho fanyika kwa mabwana zenu kule,Kote inazungumzwa na watu wa vijiweni lakini sio kitu cha kutangazwa kwa umma, kwa maelfu ya watu, tena na mtu ambaye ni maarufu na ana access hadi ikulu. Halafu amekusanya watu kanisani, maelfu akiwaambia pumba kama hizo, hamna tahadhari yoyote, watu bado mnakusanyika.
Mkuu MPE tu vidonge amevitaka mwenyewe hata mimi ninavyo vidonge kibao vya video clip lakini namsubiria kidogo nimpe ameze ili apone ugonjwa wake wa slavery mentality.Ona kinacho fanyika kwa mabwana zenu kule,
Si huwa hadi kitu kifanyike kwa mabwana zenu ndio mzinduke,
Utanikwepa ila nitakufata nikudunge huko huko.
Huyo ni msemaji wa waumini wake na wala si msemaji wa watz... Ukiamua kumsikiliza poa, ila mimi huwa simtilii maanani.Kote inazungumzwa na watu wa vijiweni lakini sio kitu cha kutangazwa kwa umma, kwa maelfu ya watu, tena na mtu ambaye ni maarufu na ana access hadi ikulu. Halafu amekusanya watu kanisani, maelfu akiwaambia pumba kama hizo, hamna tahadhari yoyote, watu bado mnakusanyika.
Atajuta kufungua huu uzi.Mkuu MPE tu vidonge amevitaka mwenyewe hats mimi ninavyo vidonge kibao vya video clip lakini namsubiria kidogo nimpe ameze ili apone ugonjwa wake wa slavery mentality.
Na hao mabwana zetu wanaosema hivyo? Nenda YouTube utawasikia na kuwaona. Tatizo la ndugu zetu Wakenya ni kujifanya mnaelimu wakati hakuna kitu mnawasujudia sana wazungu kiasi mnajitoa hata ubinadamu wenu. Miaka ya nyuma nilifanyakazi hapo Nairobi na nilikuwa naishi Westland karibu na Saliti Centre nilikuwa naona jinsi gani wakenya weusi wanavyonyanyaswa na weupe wakishirikiana na wakenya wachache ilikuwa inaniumiza sana. Kuna uwezekano wewe ni kati ya wakenya wachache unaokula matunda ya Kenya ila waliowengi wanapata shida sana huko mitaani. Kwahiyo mkuu Watz wengi tunajitambua sana pamoja na kuwa bado tuko nyuma kimaendeleo lakini sisi tunajari UTU kwanza!! Ndiyo maana hata sasa hivi tunapambana na corona kiutu zaidi siyo nyinyi hapo kutandikana kama wanyama na wanapigwa ni wakenya weusi sioni weupe akipigwa na uhakika ukienda Westland utakuta weusi wanaendelea kula nchi tu ya wakenya.
hivi kwa nini kwenye awamu hii occupants wengi wa nyumba muhimu ni psychiatric cases - makanisa na maboma (wilaya, mikoa hadi taifa)???Ukiona kauli ambazo Watanzania huwa nazo humu JF utajua kweli hawa ndugu zetu elimu yao ina mapungufu makubwa sana, hebu waza huyu mchungaji maarufu sana Tanzania yote, anategemewa na maelfu ya Wabongo, na mara moja moja hutinga ikulu kwenda kushauri (kama kwenye hii picha), ndiye anadiriki tena kwa akili zake mwenyewe kusema Corona inaletwa na teknolojia ya 5G.
Huwa sishangai nikiwaona Watz humu na kauli zao, maana hapa ndio elimu yao ilikofikia, hata wataalam wote kimya wanapoambiwa Corona ni 'kaugonjwa'.
He might be right,sema labda namna ya kuwasilisha kwa njia rahisi imekua ngumu, tafuta noti ya Euro 20 , uione ikoje, ina nini na nini
Hii symbol ya corona ipo
chini yake ni minara ya 5G
je ni coincidence au kuna ujumbe nyuma ya pazia? una google...uliza huko
Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi karibuni kumetokea uvumi katika mitandao ya kijamii kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya ugonjwa wa corona na Teknolojia ya 5G.Miongoni mwa hoja zinazotolewa ni kama zifuatazo:-
1. Kuwa karibu na 5G kuna sababisha corona, ndio maana nchi zilizo athirika zaidi ni zile zilizoanza kutumia teknolojia hii.
2. Teknolojia ya 5G inatoa miaonzi ambayo inasababisha kansa, na kuharibu kabisa vinasaba (DNA) vya binadamu.
3. Kuna dhana kuwa Corona imeanza China kutokana na China kuwa ya kwanza kujenga minara ipatayo 100,000 kwa ajili ya 5G.
4. Ipo dhana kuwa kinga dhidi ya corona itakuwa na kipandikizi cha kielekroniki (micro chip) kitakachopandikizwa kwenye mwili wa binadamu kuzuia athari za 5G. Ndio maana Bill Gate anadhamini utengenezaji wa dawa na kinga ili zisambazwe kwenye nchi maskini kwa malengo ya kiusalama.
Dhana zote hizi ni uongo, na ukweli kuhusu mfumo wa mawasiliano wa 5G ni unapatikana katika sayansi ya mionzi pamoja na ile ya mawasiliano kama ifuatavyo:-
Mfumo wa 5G kama ilivyo mifumo mingine kabla yake, mfano 2G, 3G, na 4G ambao mpaka sasa hivi unatumia/kusafiri kwa njia ya mawimbi ya redio (radio waves) ambayo ni aina moja wapo ya mionzi isiyo ainishi (non ionizing radiation) kama ilivyo katika spectra ya mionzi (electromagnetic spectrum).Mfano wa mionzi iliyo katika kundi hili la mionzi isiyo ainishi ni ile inayotumika katika microwave, ile ya jua (ultraviolet) nk.
Mionzi ainishi ambayo inaweza kuleta madhara kwenye mwili wa binadamu ni ile ya x-ray, alpha, betta, gamma ray na neutron na ile ya ultra-violet light ambayo ipo mwisho wa spectra ya mionzi (electromagnetic spectrum). Mionzi inayotokana na 5G haipo katika kundi hili.
Kwa kuwa mionzi inayotokana na 5G sio ainishi, ni wazi kuwa mionzi hii haiwezi kusababisha madhara ya cancer, kubadili kinasaba au kusababisha matatizo ya mifumo ya kupumua au yanayofana na hayo ndani ya mwili wa binadamu.
Madhara yanayoweza kupatikana katika teknolojia ya 5G ni kama yale yanayoweza kupatikana katika teknolojia ya 2G, 3G, na 4G, ambayo pia yanaweza kupatikana katika microwaves, ultraviolet ambayo ni kuongeza joto la seli.
Mfano ukiongea na simu kwa muda mrefu unapata maumivu kwani seli za sehemu za sikio ni laini. Vivyo hivyo tunashauriwa kutopakata laptop ili joto linaloongezeka kutokana na kupakata laptop lisiathiri sehemu za uzazi ambazo seli zake ni laini na ni rahisi kuathiriwa na joto.
Binafsi ninaweza kutoa mjumuisho ufuatao katika hili:-
Moja kuna upotoshaji unaofanyika kwa makusudi au kwa kutokujua kuhusu mionzi na corona, upotoshaji huu unaweza kuwa na madhara ya kiafya kwa watu kutokuchukua tahadhari stahiki kwa ugonjwa huu wa corona na kuongeza hofu ambayo haipo.
Pili, upotoshaji huu unalenga pia kujipatia kipato kwa wale wanaotafuta idadi kubwa ya watu wanaosoma makala zao katika mitandao ya kijamii.
Tatu, upotoshaji huu unaweza kuwa unafanywa na mataifa makubwa kama Marekani na washirika wake ambayo yanahofu na China kwenye Teknolojia ya 5G.
Vile vile upotoshaji huu unaweza kuwa na athari za kuhofia Teknolojia ya 5G ambayo ndio dunia inapoelekea na hivyo kuwabakisha watu nyuma.
Wewe umezidi kutapatapa, huyu huyu alipokua anapambana na Makonda ulikua unamtetea na kumshambulia Makonda, baadae huyu huyu aliposambaza picha za ngono mitandaoni, POLISI wakamtetea, wewe ukaikadhifu POLISI kwa kumtetea wakati ni kweli ile video inaonyesha ni yeye.Inasikitisha sana kwa kweli.....japo yote haya yalitabiriwa.
Mkuu, kwahiyo maelezo/mtazamo wa mtu wewe umechukulia ndio Alpha na Omega ?? kwamba yeye alilosema ndio hilo Hilo? kwa mantiki hiyo tunachoona kwenye Noti ya Euro 20 tukitupilie mbali tubaki na mtazamo wa huyu jamaa?? this is too low from you , ulipoamkia leo sio kabisaKuna jamaa ametole maelezo vizuri sana bora mkasoma uzi wake mtaelewa, hamna kitu kama hicho na haiwezekani, uliza mtaalam yeyote, hebu fuata uzi wa huyu jamaa huku
Upotoshaji uliopo kati ya uhusiano wa teknolojia ya 5G na corona - JamiiForums