Tanzania iruhusu watu binafsi kujenga nyumba za kuhifadhia maiti (Mortuary rooms)

Mkuu sema tu nipo apeche alolo ningekuwa nina hela ningewekeza kwenye hiyo idea yako maana naiona potential ya hiyo fursa ni kubwa sana.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
zipo privates zaidi ya 4 mpaka sasa
 
viungo vyetu vitauzwa huko private bora kuachia serikali. private analenga faida akitokea mtu anataka figo au dushe watauziwa.. marehemu kapigwa suti kumbe watu washang'oa kila kitu, siafiki hili wazo.
 
viungo vyetu vitauzwa huko private bora kuachia serikali. private analenga faida akitokea mtu anataka figo au dushe watauziwa.. marehemu kapigwa suti kumbe watu washang'oa kila kitu, siafiki hili wazo.
Mbona hospitali kubwa za private nyingi zina mortuaries zao na hawauzi hivyo viungo mkuu? Kinachotakiwa ni kuwepo kwa standards na ufuatiliaji wa kinachofanyika na mamlaka zinazohusika kuhakikisha kila kitu kinafanyika kwa weledi, na kikifanyika kitu kinyume na weledi hatua zinachukuliwa haraka.
 
Serikali wala haijakataza funeral homes kuanzishwa tatizo biashara ndogo watanzania hawafi kwa wingi kama nchi zingine
 
Sio lazima wawe wao unaweza ukaanzisha ukawaajiri km part time yaani anafanya kazi hospital akitoka anaunganisha shift nyingine kwenye ofisi yako km madaktari wanavyofanya

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Huoni madaktari wengi wanafungua hospitali zao, mafamasia wanafungua famasi zao nk
 
Kwa nchi yenye wasiojulikana ni hatari kuwa na vitu hivyo.
 
Kwa nchi yenye wasiojulikana ni hatari kuwa na vitu hivyo.
Kwa nini mkuu? Mbona hospitali za private zina mortuary?
Na ukifuatilia huu uzi pia wadau wamesema zipo private mortuaries, hadi sasa mimi nimezipata tatu tayari, na natarajia kwenda kuzitembelea kujifunza mambo mawili matatu ili nianzishe na mimi.
 
Kuna biashara za kufanya. Binafsi siwezi fanya hiyo Biashara ni bora nife na umaskini wangu.
 
Wakati nakua nilikua na mawazo ya kijamaa ukizingatia mfumo wetu wa maisha na kukosa exposure kwa wenzetu ila nilipopata fursa ya kutoka nje nikagundua kumbe private investors wana uwanda mpana sana wa kuwekeza tofauti na mawazo yangu kuwa serikali ina wajibu wa kuwekeza kila kitu. Rejea wa JK ( kama sijakosea) kuna rhino alipelekwa SA kutibiwa tena kwenye taasisi binafsi. Nyama pori namibia 🇳🇦, private security companies,
Nadhani tanzania 🇹🇿 tumechelewa sana, serikali iandae sera tu

kuna siku natoka, nikapita bank A kujua kama acc yangu naweza kuitumia nje japo ina MasterCard wakasema mpaka niandike barua etc, kikubwa nikaenda kuchukua acc ya nje ambayo naweza kuaccess ATMs zao basi.
 
Umeongea vizuri sana aisee.... Na ndo negative comments nyingi unazoziona hapa nyingi ni matunda ya mawazo ya kijamaa!!
 
Hadi issue za mortuary kuanzia kuhifadhi maiti.... na ile nyumba walihama ikakaa muda imekosa mpangaji wanataka kuiuza haijauzika ikabidi wa wawauzie hao hao!!
Daaahhh...!!
Wabongo tuna imani kali!
 
Au akifa mtu maarufu unaomba kumuhifadhi bure kwa hiyo wakati wakiitangaza tangaza hiyo taarifa lazima waseme na alikohifadhiwa na itapata media coverage ya kutosha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…