Tanzania iwe upande gani Kama Ethiopia na Misri zinapigania maji ya mto Nile?

Misri duniani niyakumi na moja Israel ya kumi nambili wacha Israel kubebwa ila misri ningumu sana kama unaufahamu mkataba wa Camp David utaelewa tu
Hatuangalii hizo rank za kutenezwa Bali tunaangalia matokeo halisi kwenye field

Matokeo Ni kuwa Israel kamdunda Misri Mara kadhaa japo yeye alikuwa Taifa Changa na dogo zaidi

Kwani Camp David Accords zilisaidia zaidi Misri au Egypt baada ya Vita?.

Au hujui Historia ya Middle East vizuri ndugu

Hivi unajua Misri ndio nchi ya kwanza ya Kiarabu inayoitambua Israel kuwa Ni nchi? Tena Bila kupenda
 
Akionyesha dalili za kutaka kushambulia tu, tunajaza sumu ya panya maji yote kutoka mpaka wa Ethiopia kwenda mbele, tukose wote, akijitoa akili na sisi tunajinyofoa ubongo kabisa, liwalo na liwe!!
Wewe inaonekana huzitakii mema nchi zetu yaani uweke sumu kwenye maji kabisa.
Mkuu hapo ndipo tutachakazwa tuchakae kwelikweli.
Yaani nakwambia tutapotea.
 
Kama Israel ilishinda Camp David accords zilikuwa za nini. Si unajua kilichozungumziwa kule.
Kwanza Sinai ambayo walipigania sasa hivi inamilikiwa na nani na kabla ya vita kuanza ilikuwa chini ya milki ya nani?

Misri anaitambua Israel bila kupenda, kwani kuitambua na kutoitambua kunapunguza au kuongeza nini. Mpaka rais wao akaenda Israel kwenye state visit kisha unasema bila kupenda?

Hatuangalii rank tunaangalia impact, kwahiyo unaona Israel ni viwango sawa na Ethiopia kijeshi mpaka uzilinganishe. Huwezi linganisha Uganda kupigwa na Tanzania kumaanisha inawezwa pigwa na Burundi.

Yani unalinganisha nchi iliyopigwa na kanchi kanaitwa Eritrea dhidi ya Egypt? Maajabu!
 
Hemu
Wewe geography Kama hukupata A aliyesahihisha karatasi yako anatakiwa atandikwe bakora .uko vizuri somo la geography na application yake in the real world .Hukukariri majina ya mito tu
Hemu m-Qoate jibu linaelea
 
We jamaa bana

Sinai Ni sehemu ya Egypt kwa Sasa, baada ya Israeli kurudisha

Camp David Accords ilitoa assurance ya Egypt kuwa anaitambua Israel na hataungana Tena na Waarabu wenzake kuivamia Tena,

Pia Kama unafahamu mgogoro wa Israel na Palestine huwezi kusema eti Egypt kuitambua Israel hakuna tatizo, Israel Waarabu wote wanaiona inaikalia kimabavu Ardhi ya Palestine na haitakiwi ku exist kabisa, na ndio maana nchi za Kiarabu ziliungana na kuivamia Israel

So Egypt kuitambua Israel Ni Kama anasaliti Ile Sababu iliyofanya nchi za Kiarabu kuivamia mwaka 1967

Pia Kama unafahamu Historia vizuri, baada ya Camp David Accords, Egypt alifukuzwa kwenye Arab League kwa kwenda kinyume na nchi nyingine za Kiarabu kuhusu Israel & Palestine

Pia huyo Rais wa Egypt, Sadat aliyeingia mkataba wa Camp David aliuawa na wananchi wenye hasira kwa Sababu aliidhalilisha nchi

Egypt inaweza kuwa nchi yenye nguvu Africa Ila Duniani Ni nchi ndogo sana
 
Ntarudi.....
 
Egypt wanajiona kama wakoloni. Hawatufai. Hata5kutoa maji Ziwa Victoria wanang'aka.

Ethiopia ni wenzetu zaidi. Ni moja ya nchi zilizokuwa upande wetu wakati wa vita dhidi ya Iddi Amin.

Tunajua Egypt wapo kwenye kwenye ujenzi wa bwawa la Stieglers.

Ili tu tusideal na ziwa...
 

Nakumbuka Mjerumani alikataa kuhusishwa na mgogoro kuhusu ziwa Nyasa
 

Kagera river ndio main supplier.
 
Ethiopia Ni wabishi pia tangu enzi za Mfalme Menerik I, nitaifa ambalo halikutawaliwa, nitaifa la wabishi. Ni taifa kakamavu, Ni taifa la kupigana

Linapo kuja suala la Egypt sasa...
 
Tanzania haiwezi kudhurika kwasababu ndo chanzo chenyewe alafu yanashuka uko Ethiopia apo misri anahaki yakupigana kwasabu lazima kina cha maji kitapungua sana misri.
 
Huo ni ujinga, Misri alishwahi kutuzuia eti tusipeleke maji ya ziwa victoria kwa wananchi wa Tabora, hata sijui walipata wapi jeuri ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi yetu, very arrogant, ila Lowassa aliwanyoosha, wakatulia

Hivi maji yalifikia?
 
Huu ugomvi wa maliasili ni mgumu sana.

Huwa nafikiria (theoretically tu) hivi Misri akitutaka tuzuie maji kutoka Victoria yasitiririke kwenda kwake, tutayapeleka wapi? Au tunachimba mto yaende Tanga? Baharini?

[emoji23][emoji23][emoji23]
 

Asee!
 
Nakumbuka Mjerumani alikataa kuhusishwa na mgogoro kuhusu ziwa Nyasa
Ujerumani ilikuwa inatambua ziwa Nyasa kama sehemu ya Malawi. Hata kwenye ramani zao wanaonyesha hivyo, hata ramani iliyokuwa displayed ubalozini kwao ilionekana inaonyesha Nyasa ni ya Malawi. Ndo maana dunia mzima inaliita lake Malawi.
Sijui kwa sasa GER wana msimamo gani.
 
Sasa kama Egypt ni nchi ndogo sana duniani na ni kubwa Afrika, Ethiopia iko Asia?


Then Anwar Sadat hakuuwawa na wananchi wenye hasira kali. Au unamaanisha wananchi wa Misri wanaruhusiwa kumiliki assaurt rifles tena kwenye sherehe za kitaifa.
 
Ujerumani analitambua kama Ziwa Malawi (Milki ya Malawi).

Uingereza analitambua kama Ziwa Nyasa na Ziwa Malawi upande wa Malawi (Milki ya Tanzania na Malawi).
 

Hapo ndio najiuliza sisi weusi tunakwama wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…