#COVID19 Tanzania kuanza kuzalisha chanjo zake za COVID-19

#COVID19 Tanzania kuanza kuzalisha chanjo zake za COVID-19

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
Rais Samia amesema Tanzania ina mpango wa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza chanjo za UVIKO-19 ikiwa ni juhudi za kupambana na janga hilo pamoja na magonjwa mengine.

Rais Samia amesema hayo wakati akifanya mazungumzo na Rais wa Baraza la Ulaya, Bw. Charles Michel, jijini Brussels nchini Ubelgiji ambapo amemwambia Bw. Michel kuwa Tanzania inalenga kuwa mzalishaji na msambazaji wa chanjo hizo katika nchi za EAC pamoja na SADC.

Akielezea umuhimu wa hatua hiyo, Rais Samia amesema kuna uwezekano wa Tanzania kutumia kiasi cha Shilingi bilioni 216 katika uingizaji wa chanjo ifikapo mwaka 2030.

1644942861146.png
 
Rais Samia amesema Tanzania ina mpango wa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza chanjo za UVIKO-19 ikiwa ni katika juhudi za kupambana na janga hilo.

Rais Samia amesema hayo wakati akifanya mazungumzo na Rais wa Baraza la Ulaya, Bw. Charles Michel, jijini Brussels nchini Ubelgiji.

View attachment 2120325
Wasije tu wakatuchanganyia covido na nimricaf wakatuambia ni chanjo
 
Naamini hatushindwi, tukichanganya mapapai, mapera, maembe, tangawizi, unga wa dona, na hiliki kidogo na nyanya tukisema ndio chanjo yetu nani atakataa?
 
[emoji38][emoji38][emoji38] Nchi ambayo hata pamba ya kuoshea vidonda inaagiza nje eti leo inawaza kutengeneza Chanjo ya corona !
 
Tupeni taarifa ya kiswahili. Vinginevyo, tueleze kama tumepewa kandarasi ya kueneza lugha ya Kiingereza Ulimwenguni. Na sisi kaziI yetu ya kueneza kiswahili tumeiacha ama imetushinda?
 
🤣🤣🤣🤣

This has got to be a joke!
Nadhani watazalisha under license ya watengenezaji wakubwa (kama ni kweli). Ila bado ni usanii tu kwani Tanzania hakuna watu wanaotaka chanjo. Kimsingi walishasahau kabisa kama kuna korona. Hii ni siasa ya kujikomba kwa mabeberu na hakuna kitu serious.
 
Nadhani watazalisha under license ya watengenezaji wakubwa (kama ni kweli). Ila bado ni usanii tu kwani Tanzania hakuna watu wanaotaka chanjo. Kimsingi walishasahau kabisa kama kuna korona. Hii ni siasa ya kujikomba kwa mabeberu na hakuna kitu serious.
Kwa jinsi maisha yanavyoendelea Tanzania, ukweli ni kwamba COVID 19 siyo tatizo kabisa.

99% ya watu [makisio yangu] hawana habari nayo hiyo COVID.
 
IT'S OWN! Ina maana kwa matumizi ya Tanzania tu? Au Kiingereza chao kigumu (primary english).
 
Back
Top Bottom