Tanzania limejitokeza tabaka la "wenye nchi" ambao wanaona hawastahili kuendesha gari kwenye foleni na wana haki ya kutofuata sheria za barabarani

wana heri hao wanaokimbia masaa yote kama farasi,kuliko wale wanaotukoboresha mahindi saa zima ili wapite wakati wako makwao bado wanakata gogo.

kwanza hawa hawasababishi upotevu wa muda,ila usumbufu na mshtuko tu ambao kiasi unavumilika.

kuna nchi kama germany,foren ikifunga gari zinatanua kuacha nafasi katikati kwa ajiri ya gari za dharula,ila bongo kwa vibarabara vyetu mtihani kiasi.
 
Mwarobaini ulikuwa Magu, mkauponda acha watumie barabara nawe ikikuuma tumia hivohivo
Wakati wa magufuli hakukuwa na magari kibao ya serikali yaliyokuwa yakikiuka speed limits, yakitanua, kupiga ving’ora, kuwasha vimulimuli na kupita taa nyekundu? Wala bila kuwa kwenye misafara inayoongozwa rasmi?
 
Ukiwa na V8 unaweza paki gari kwenye zebra crossing ukaenda shopping na ukarudi usisumbuliwe. Ukipaki IST utakwenda kuikomboa jiji au halmashauri.

Kuna siku (mwaka jana) nilikuwa pale taa za Ohio kuingia Alihasan Mwinyi road. Ikaja landcruiser 76 series inanamba nyeusi hata hazieleweki.

Kwa kuwa kulikuwa na foleni(kutokea Ohio kuingia Alihasanimwinyi) jamaa alipita opposite road akaingia barabara kuu halafu naona katikati akabadili mawazo akaichekecha fasta akapiga uturn kama anarudi tena Ohio, napo nikaona kaingia Zebra crossing akaelekea barabara ya bibititi.

Kimoyomoyo nikajisemea ingekuwa babywalker imefanya ushubwada huo tena kwenye red angepata tabu sana.

 
Wakati wa magufuli hakukuwa na magari kibao ya serikali yaliyokuwa yakikiuka speed limits, yakitanua, kupiga ving’ora, kuwasha vimulimuli na kupita taa nyekundu? Wala bila kuwa kwenye misafara inayoongozwa rasmi?
Rejea mke wa Mahiga na DeD kule Tanga nini kiliwapata.
 
Wakati wa magufuli hakukuwa na magari kibao ya serikali yaliyokuwa yakikiuka speed limits, yakitanua, kupiga ving’ora, kuwasha vimulimuli na kupita taa nyekundu? Wala bila kuwa kwenye misafara inayoongozwa rasmi?
Wapuuzi wapo awamu zote ila ukiona watu wanaandika thread hizi ujue wamezidi.
 
Sawa, lakini kuna siku yao ya arubaini. Ngoja siku ninaendesha kijiko saa za jioni utasikia nilivyowabomonda. Na mazoea ndio yanazaa matukio kama hili hapa chini

 
Rejea mke wa Mahiga na DeD kule Tanga nini kiliwapata.
Suala la marehemu mke wa marehemu Mahiga nalijua. Hata kemeakemea, fokeafokea, tumbuatumbua za viongozi wengine nazıjua.

Ninachouliza, simply, ni hali halisi iliyokuwa barabarani enzi hizo. Rejea mada na comment niliyoiquote. Wakati wa Magufuli, hakukuwa na magari ya serikali/taasisi za umma na wakuu wao nje ya misafara rasmi yaliyokuwa yakikiuka sheria za barabarani with impunity?
 
Na huo ndio ukweli, impunity. Katika hizi zama za Raisi Samia kumekuwa na impunity ya kutisha toka kwa viongozi wa serikali, polisi na Usalama wa Taifa. Sijui ni kwa kuwa raisi ni mwanamke?
 
Kipindi cha Magufuli askari polisi walishagundua jinsi ya kupata vyeo kirahisi toka kwa Magufuli. Na akawa anameza tu kirahisi na kusemampandishe cheo huyu. Jamaa hadi walikuwa wanaambiana jinsi ya kutafuta vyeo vya haraka kwa kitu ambacho raisi atajua, na wakawa hata visa vingine wanatunga. Kwa mfano huyu askari wala hakutukanwa. Alijua alipata fursa ya kupanda cheo na akaitumia barabara, ma Magufuli akaingizwa cha wanawake!
 

Nchi yoyote yenye utawala wa hovyo, hizi ndio ishara na dalili zake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…