Tanzania Motorbike Road Trip - Tanga | Safari ya Tanga

Tanzania Motorbike Road Trip - Tanga | Safari ya Tanga

Yeah wakati nipo Tanga kuna mtu aliniambia kuna shortcut hiyo uliyosema.. nikamuuliza ni barabara ya rami akasema hapana..[emoji1787][emoji1787] nikasema mmh hiyo hapana ata kama ni shortcut
Hiyo ni vumbi kipande kirefu lami inaishia Tanga mjini,unapiga vumbi mpaka Pangani,Mwera,Mkwaja,Saadani unatokea Bagamoyo. Mbugani usipite usiku na hiyo njia kwa bike yako haifai utachoka njia ina rasta ndogo ndogo
 
Kuna wale jamaa zangu matoyo wa chuga walishindana kwenda Moshi na kurudi asee walikufa kadhaa ile kitu sio
Nilicho jifunza Ukiwa unaendesha pikipiki kwa safari ndefu:

1. Hakikisha umebeba maji ya kunywa ya kutosha na unywe sana maji

2. Hakikisha usibane sana mdomo muda wote muda mwingi jitahidi kuachama au kuongea ongea tu inasaidia misuli isikaze na meno yasipate ganzi.

3. Vaa koti zito ambalo litazuia upepo kuingia mwilini

4. Vaa Buti na hilo buti usifunge kamba kama unafunga kiatu maana ukifunga kama unafunga kiatu utafanya ukaze na mzunguko wa damu utakuwa mdogo sana miguuni kupelekea kuchoka miguu

5. Hakikisha ndani vaa Vesti tu au nguo nyepesi hii inasaidia wewe uwe huru na mwili kuwa huru.. maana ukivaa shati zito afu ukavaa na koti juu mwili utakosa kupumua na kujikuta unachoka haraka.

6. Vaa helment yenye kioo tena kioo kigumu sana.

7. Utakapo hisi njaa au kiu hakikisha unaupatia mwili hitaji lake usilazimishe safari kwenda mbele wakati unahisi mwili kupata joto.

8. Usile hovyo hovyo.. nunua biskuti au chocolate na maji au zile Energy Drinks

9. Zingatia sana tena sana Side Mirror uwiiiii madereva Side Mirror ni muhimu kuliko ata chochote

10. Ukihisi umechoka pumzika tena pumzika kwa kujilaza chini na sio kusimama au kukaa (hii itakusaidia sana uone utamu wa safari)

11. Hakikisha kiuno chako usifunge na kukazaa.. kama suruali ya mkanda basi funga kiuno chako kiwe relax kabisa kisibanwe na chochote

12. Hakikisha haumwi chochote ata mafua yaani upo na afya njema

MENGINE NITAONGEZA YALE NILIYOJIFUNZA
 
3. Niliondoka Dar saa 11 asubuhi.. sikumbuki Pale Mkata nilifika muda gani (sikuangalia saa pale ila nahisi ilikuwa kama saa 3 au 2) nilikaa pale kama lisaa limoja kwa ajili ya kuvuta pumzi na kuacha magari ya mikoani yapite kwanza..

Tanga niliingia saa 7 mchana (hapa njiani nilikuwa nasimama sana mara ninywe maji, mara nikute kivutio flani nipige picha so nilikuwa mtu wa kusimama simama hovyo [emoji1787][emoji1787] Utalii wa ndani mara nipige na kibao karibu Tanga hope unaelewa )
Ulitembea km ngap mpaka kufika Tanga?
 
Nilicho jifunza Ukiwa unaendesha pikipiki kwa safari ndefu:

1. Hakikisha umebeba maji ya kunywa ya kutosha na unywe sana maji

2. Hakikisha usibane sana mdomo muda wote muda mwingi jitahidi kuachama au kuongea ongea tu inasaidia misuli isikaze na meno yasipate ganzi.

3. Vaa koti zito ambalo litazuia upepo kuingia mwilini

4. Vaa Buti na hilo buti usifunge kamba kama unafunga kiatu maana ukifunga kama unafunga kiatu utafanya ukaze na mzunguko wa damu utakuwa mdogo sana miguuni kupelekea kuchoka miguu

5. Hakikisha ndani vaa Vesti tu au nguo nyepesi hii inasaidia wewe uwe huru na mwili kuwa huru.. maana ukivaa shati zito afu ukavaa na koti juu mwili utakosa kupumua na kujikuta unachoka haraka.

6. Vaa helment yenye kioo tena kioo kigumu sana.

7. Utakapo hisi njaa au kiu hakikisha unaupatia mwili hitaji lake usilazimishe safari kwenda mbele wakati unahisi mwili kupata joto.

8. Usile hovyo hovyo.. nunua biskuti au chocolate na maji au zile Energy Drinks

9. Zingatia sana tena sana Side Mirror uwiiiii madereva Side Mirror ni muhimu kuliko ata chochote

10. Ukihisi umechoka pumzika tena pumzika kwa kujilaza chini na sio kusimama au kukaa (hii itakusaidia sana uone utamu wa safari)

11. Hakikisha kiuno chako usifunge na kukazaa.. kama suruali ya mkanda basi funga kiuno chako kiwe relax kabisa kisibanwe na chochote

12. Hakikisha haumwi chochote ata mafua yaani upo na afya njema

MENGINE NITAONGEZA YALE NILIYOJIFUNZA
namba 12 nimepiga chafya😂😅😅😅
 
msuyaeric mbona tanki lako la mafuta dogo sana. Inakunyima uhuru wa kutembea safari ndefu mpaka ubebe mafuta. Boxer Dar Mpaka Tanga anatumia lita 9 tanki ni lita 11. Honda Crf250 na CB400 za carburetor ni lita 10 safari yote
Ni kweli mkuu Tank ni dogo ila pikipiki haili Mafuta Kabisa nilibeba kidumu kuhofia ila nipokuwa natoka Tanga kurudi Dar sijabeba kidumu Mkuu
 
Kwa huo umbali mbona umetumia mafuta mengi sana kufika?

Pikipiki ilikua na shida gani?
Mkuu pikipiki yangu haina dashbod ya mafuta hivyo huwa nikataka kujua mafuta yamefika wapi huwa nafungua tank la mafuta sasa nilikuwa nikiona mafuta yamepungua kidogo huw naongeza ndo maana.

Ila kipindi narudi Dar nimejaza mara mbili tena nimejaza sababu sipendi kuishiwa mafuta safarini ukizingatia dashbod yangu haisomi mafuta
 
Mkuu pikipiki yangu haina dashbod ya mafuta hivyo huwa nikataka kujua mafuta yamefika wapi huwa nafungua tank la mafuta sasa nilikuwa nikiona mafuta yamepungua kidogo huw naongeza ndo maana.

Ila kipindi narudi Dar nimejaza mara mbili tena nimejaza sababu sipendi kuishiwa mafuta safarini ukizingatia dashbod yangu haisomi mafuta
Nimepiga hesabu nimepata ulipaswa kutumia angalau lita 10 tu.
 
Kidumu usibebe mkuu unajiongezea mzigo, piga hesabu mafuta kwa Km unazotembea ujue sheli za kuongeza njiani
Ujue mkuu kabla sijapanga safari nilianza kuangalia Map ya Njia ya Tanga na Vituo vyake vya Mafuta..

Nikajakujua vituo vya mafuta vipo mbalimbali sana yaani kituo cha mafuta utakipata street unayokutana nayo ambayo hiyo street kwa tanga ni Mkata, Segera, muheza na nyingine sikumbuki..

Sina elimu ya KM kwenye Mafuta hivyo ikanilazimu kubeba kidumu kama emergenc
 
Nimepiga hesabu nimepata ulipaswa kutumia angalau lita 10 tu.
Labda pikipiki yangu inakunywa mafuta na sijui.. nitaenda kwa fundi aniangalizie vizuri shida itakuwa nini
 
Back
Top Bottom