Tanzania na China zasaini mkataba wa uendelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR kutoka Mwanza - Isaka

DED wa Geita alinunua gari la milioni 400.

Waziri wa Mambo ya nje wa China katoa msaada wa milioni 380.
Nipo nje ya maada
Hapo ni sawa na mkurugenzi kununua v8 cash likija swala la ujenzi wa madarasa wanachangishwa wananchi
 
Mkuu, kwani unadhani makamanda hawayajui hayo? Wanaujua huo ukweli, ila bongo zao walikabidhi kwa tundu na akaondoka nazo kwenda kwa shoga yake Amsterdam huko ubeberuni!
 
Nashukuru umeliona hili na wewe...unajua nimejiuliza sana nini hiki? Anyways akili ya mwafrika utategemea nini? Na mchina atamaliza ndio wakati hata hatujaunganisha dodoma-isaka.
 
Swali; kwanini waanzie Mwanza na sio Dodoma kuja Isaka? Hauoni kuna shida sehemu? Ningeelewa kama tender zingekuwa zimetangazwa za dodoma isaka.
 
Wachina ni binadamu kama sisi ila wanatoka sayari nyingine. Wamepambana kushinda zabuni ya ujenzi kwa eneo lenye madini mengi, naona hata wakitujengea bure watakuwa wamejilipa maradufu
 
Ni vizuri lakini kutumia neno wameshinda zabuni wakati zabuni haijatangazwa ukweli ni kwamba wametoa mkopo tukawapa wajenge lakini sio kweli kwamba wameshinda zabuni!
Zabuni zilitangazwa mkuu. Watendee haki. Si vema kusema uongo. Kama hujui uliza kwanza ujulishwe.
 
DED wa Geita alinunua gari la milioni 400.

Waziri wa Mambo ya nje wa China katoa msaada wa milioni 380.
Nipo nje ya maada
Hilo la DED halikubaliki, ni wendawazimu. Ila pia ujue kua akija rafiki yako tajiri nyumbani kwako akakupatia chunvi ya sh 500 utakuwa mwendawazimu pia kukataa.
 
Mkuu, lengo la kugawa mradi kwenye vipande vingi ilikuwa pamoja na mambo mengine kuweka kandarasi tofauti kila kipande. Nielewe vema, kandarasi tofauti na si mkandarasi tofauti. Hivyo kwa mfano, lots one na two zina kandarasi tofauti hata kama mkandarasi ni kampuni moja.

Kuwapa Wachina lot 5 haizuii kuwapa wengine lots 3 na 4. Usishangae Mturuki akapewa tena lot mojawapo. Kila tenda hutangazwa kivyake.

Pia walichoombwa Wachina kwenye lots 3 na 4 ni kutusaidia financing. Hakuna aliyewahakikishia kuwa tenda watapewa wao.
 
Safi sana kwa maelezo marefu yasiyochosha. Nadhani bro Magu anajua kinachoitesa TAZARA ndiyo maana aliagiza upelekwe bungeni muswada wa kuruhusu kila nchi mshirika iwajibike kuendeleza upande wake wa reli.
 
Swali; kwanini waanzie Mwanza na sio Dodoma kuja Isaka? Hauoni kuna shida sehemu? Ningeelewa kama tender zingekuwa zimetangazwa za dodoma isaka.
Mkuu, hapo lengo ni kuwahakikishia Waganda na potential financiers kuwa mradi utatekelezwa ili isitutokee kama inayowatokea Wakenya. Uganda wana maamuzi yao ya kufanya juu ya wapi wanaelekeza reli yao kwanza; Tz au Kenya.

Sijui ni kwa vipi watu wanaoonekana wazi wana zero understanding na masuala haya wanakesha hapo kuponda hiki au kile. Kuna mwingine eti anauliza tenda ilitangazwa lini! Sasa huyo si zero brain anapaswa kusoma tu kimya kimya kama library!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…