Tanzania na China zasaini mkataba wa uendelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR kutoka Mwanza - Isaka

Tanzania na China zasaini mkataba wa uendelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR kutoka Mwanza - Isaka

Kuidharau China kuwa ni tajiri uchwara sio hoja ya msingi. Utapeli wa taifa la China upo wapi? Unatakiwa China imrkuwa na msaada mkubwa sana kwa Tanzania usio na harufu ya kibeberu miaka nenda rudi.

China inawalea viongozi makatili wa Afrika, kwa sababu viongozi hao wanawapa miradi mingi, bila kuhoji ubora wa miradi hiyo. Hivyo hapo China inalindana na viongozi kwa kuwapa 10%, na wao kufaidika na fedha za wananchi kwa miradi substandard. Nenda kaangalie kwenye takwimu deni kubwa la nchi hii ni la mabeberu au wachina, na ni wapi wametoa misamaha zaidi?
 
DED wa Geita alinunua gari la milioni 400.

Waziri wa Mambo ya nje wa China katoa msaada wa milioni 380.
Nipo nje ya maada
Hata kama uko nje ya mada, hoja yako ina mantiki.

Viongozi wetu sijui tusemeje?

Akili zao hazina akili ama wanawapenda beberu wa kichina?

Wanajua wao, siye yetu macho
 
China inawalea viongozi makatili wa Afrika, kwa sababu viongozi hao wanawapa miradi mingi, bila kuhoji ubora wa miradi hiyo. Hivyo hapo China inalindana na viongozi kwa kuwapa 10%, na wao kufaidika na fedha za wananchi kwa miradi substandard. Nenda kaangalie kwenye takwimu deni kubwa la nchi hii ni la mabeberu au wachina, na ni wapi wametoa misamaha zaidi?
Viongozi makatiri wa Afrika? Hapa Tanzania tuna kiongozi katili? Ten %? Kwenye miradi? Kwa hiyo hata ujenzi wa Sgr unaofanyika kuna 10%? Miradi sustandard?
 
Viongozi makatiri wa Afrika? Hapa Tanzania tuna kiongozi katili? Ten %? Kwenye miradi? Kwa hiyo hata ujenzi wa Sgr unaofanyika kuna 10%? Miradi sustandard?
Unauliza au unapigia majibu mstari?
 
Mchina kwa reli tumepata mtu sahihi. Hivi vijamaa vinafanya maajabu ya ujenzi wa reli huko kwao utastaajabu.. Unakuta vinajenga reli inapita bonde la urefu wa ghorofa kadhaa inaibukia ndani ya mlima, unachanwa reli inapita inakwenda kupita juu ya mto/ziwa flani then inafika destination mji flani maelfu ya km kadhaa ndani ndani huko. Na hizi project hata hazichukui miaka mingi project imekabidhiwa..

Kama tumekuwa makini kwenye mikataba basi tusiwe na wasi upele umepata mkunaji.. Wanaweza
 
Mbona wameruka kipande Cha Makutupora Hadi Tabora na Tabora Hadi Isaka?
Kama nilimsikia vizuri msemaji wa kampuni ya kichina iliyopewa ujenzi wa reli ya kutoka Mwanza kwenda Isaka, alizingumzia kuhusu vipande ulivyo taja hapo juu, kwamba wanaweza kusaidia katika ujenzi wa sections hizo wakitakiwa kufanya hivyo, vile vile nilimsikia Waziri wa miundo mbinu na ujenzi akigusia kwa mbali sections hizo tajwa na kutoa impression as if watapewa Wachina kuzimalizia itakapo bidi - I might be wrong lakini reading between the lines naona huko ndiko tutakapo elekea eventually ni suala la muda tu, Wachina hawakwepeki - binafsi hilo naona ni sawa tu tunacho taka ujenzi wa reli ukamilike kama ilivyo pangwa tangu mwanzo.
 
Mchina kwa reli tumepata mtu sahihi. Hivi vijamaa vinafanya maajabu ya ujenzi wa reli huko kwao utastaajabu.. Unakuta vinajenga reli inapita bonde la urefu wa ghorofa kadhaa inaibukia ndani ya mlima, unachanwa reli inapita inakwenda kupita juu ya mto/ziwa flani then inafika destination mji flani maelfu ya km kadhaa ndani ndani huko. Na hizi project hata hazichukui miaka mingi project imekabidhiwa..

Kama tumekuwa makini kwenye mikataba basi tusiwe na wasi upele umepata mkunaji.. Wanaweza

Hawa jamaa kitu kingine kabisa - wamepewa tuzo lukuki Duniani kutokana na ubunifu wa ujenzi wa madaraja ya reli na barabara - ujenzi mwingine una-defy laws of physics, wao ndio wana ongoza Duniani katika ujenzi wa reli pamoja na uundaji wa trains za umeme wa mwendo kasi ikifuatiwa na Japan na Ujerumani. Watu wengi ambacho hawajui ni kwamba Wachina ndio walikuwa watu wa kwanza Duniani kubuni na kutumia mataruma (sleepers) za zege wakati wa utawalawa Mao-Tse-Tung, hivi sasa Dunia inatumia ubunifu wa Wachina kuzalisha Concrete Sleepers.

Bottom line is: tukishirikiana na watu hawa kwa akili watatufikisha mbali sana kimaendeleo.
 
Kumbe sisi sio matajiri tena. Lol! Wakitusamehe madeni na serikali isisahau kuwasamehe wananchi inaowadai. Mfano watu waliokopeshwa na bodi ya mikopo ya Elimu ya juu ambao mpaka Sasa deni lao linaongezeka kila siku bila kujali kuwa hawajapata ajira ya kudumu.
 
Hapa watakuwa wanalenga kuendeleza uchumi wa kanda ya ziwa mapema ...sasa huko makutupora-Tabora labda kama wanataka kubeba ubuyu.

Kanda ya ziwa hipi wakati Mkoa wa Kagera haupo kwenye equation ya utandazaji wa reli, sisi tutakuwa tunaisikia kwenye radio tu, wanajenga branches za kwenda, Mpanda, Rwanda, Burundi na DRC lakini sio Bukoba bwana!!

Mtu ungetegemea kwamba walao branch moja ya reli ingepitia Bukoba kwenda Mbarara na kujiunga na reli ya Uganda hivyo kupunguza utegemezi wa meli inayo beba mabehewa kwenda Port Bell Uganda ikitokea Mwanza na Mkoa wa Kagera ungefahidika kwa usafirishaji wa mizigo na passengers.
 
Si kweli, waziri wa Mambo ya nje wa China amewahi kwenda Congo hakupokelewa na Rais
lakini pia hata Tanzania hivi juzi wakati wa msiba wa Mkapa kuna Marais walipokelewa na mawaziri
Jifunze kuelewa tofauti za shughuri, msiba siyo shughuri ya kikazi au kiserikali, Rais wa nchi nyingine anaweza akaja kutembelea mbuga za wanyama kimyakimya na akaondokea huko huko kimyakimya. Hivi tunakwamawapi kwenye kujua namna ya kupambanua mambo!
 
Back
Top Bottom