Tanzania na China zasaini mkataba wa uendelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR kutoka Mwanza - Isaka

Tanzania na China zasaini mkataba wa uendelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR kutoka Mwanza - Isaka

Toka Makutupora mpaka Tabora. Na Tabora Isaka kampuni gani wanajenga?
 
“Nimemuomba Waziri wa Mambo ya Nje China Wang Yi, akafikishe salamu zangu kwa Rais Xi Jinping kwamba watusamehe madeni ikiwemo deni la nyumba za Askari USD 137 M, na deni la kiwanda cha urafiki USD 15 M, nimeomba watufutie kwasababu China ni Rafiki zetu, pia wao ni Matajiri”-JPM

Hivi ule utajiri Jiwe alikuwa akituaminisha umepotelea wapi?
 
Kwani hicho nacho umeambiwa hakina mfadhili
Hapa tunazungumzia kukabidhiana kazi kwa WAKANDARASI walioshinda Zabuni ya ujenzi wa kipande husika, SIYO WAFADHILI. Huyo waziri wa China, kama Rais wetu Magufuli, wapo hapo kushuhudia zoezi hilo. Pesa za ujenzi ni ZETU! Sisi ndio tunawalipa hao Wakandarasi toka China walioshinda hiyo zabuni! Sijui somo limeeleweka?!
 
909765.jpg
 
Dar-Moro=300Km

Moro-Makutupora=426Km

Makutupora-Isaka=435Km

Isaka-Mwanza=220Km

Isaka-Rusumo=371Km

Kwa nini kazi zisiende kwa mfuatano ili hata ngoma ikikwama njiani ruti iwepo ya kuishia hata Isaka.

Wachina watamaliza na kukabidhi Isaka-Mza huku kipande cha Makutu-Isaka kikiwa bado hata tenda haijatangazwa halafu anaingia Rais mwingine na kusema reli siyo kipaumbele chake,mradi unaachwa kwenye mataa kama katiba mpya tunakuwa tumepoteza pesa bure.
 
Mbona wameruka kipande Cha Makutupora Hadi Tabora na Tabora Hadi Isaka?
Hapa watakuwa wanalenga kuendeleza uchumi wa kanda ya ziwa mapema ...sasa huko makutupora-Tabora labda kama wanataka kubeba ubuyu.
 

 
Duh kumbe Bado tunadaiwa urafiki na reli ya tazara!!!??
 
Ni vizuri lakini kutumia neno wameshinda zabuni wakati zabuni haijatangazwa ukweli ni kwamba wametoa mkopo tukawapa wajenge lakini sio kweli kwamba wameshinda zabuni!
 
kila siku anazindua havifanyiki...wapi bomba la wese kutoka ug
 
Naona hatimaye China imemlegeza sasa atakubali kunywa matapishi yake. Ujenzi wa Bagamoyo Port haukwepeki. Kwa mbali naona JK akipasuka mbavu.
Kwa akili yako mgando
Kuna uhusiano gani hapo?
 
Back
Top Bottom