Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Nadhani huu ni mjadala mzuri na nimeupenda sana. Katika suala hiili kuna mambo ambayo hatuna budi kuyaangalia moja moja ili kuweza kukielewa kitu kizima. Mara nyingi tunaposikia "Mradi wa Vitambulisho vya Taifa" tunachukulia kuwa ni kitu kimoja bila kuangalia vipande vyake.
a. Ni utambulisho wa nini?
Kuna mtu aliuliza swali hili huko nyuma kuwa hivi vitambulisho hasa vinachotaka kutambulisha ni kitu gani? Kama ni Taifa kama inavyotajwa sasa pasi za kusafiria tayari zipo hivyo ni duplication ya services kwani pasi inamtambulisha x,y kuwa ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo, kitambulisho kingine ni cha nini basi? Tuzingatie kuwa hivi karibuni serikali ilifanya mabadiliko ya vitambulisho vyetu na kuvileta vya "kisasa" ambavyo navyo ni kama vinatumia teknolojia bora zaidi yenye kuzuia kughushi n.k. So, kama sivyo vya kutambulisha taifa vinatambulisha nini?
b. Vitambulisho vya Uraia?
Hili nalo ni kama (a) hapo juu. Kama vitambulisho hivi ni vya uraia na siyo vya kila mtu aliyemo ndani ya Taifa hilo basi bado mradi unaohitajika ni wa vitambulisho vya wageni! kwani Raia tayari wana vitambulisho vyao (pasi). Hivyo, basi kama ni kutaka kujua wageni hili nalo ni rahisi zaidi kutekeleza kwani tayari tuna vituo vya kuingilia nchini na tayari wageni wanapokuja wanakuja na pasi zao n.k Hivyo, kwetu sisi ni kutengeneza mfumo tu wa kawaida wa kuonesha mgeni ni nani na akiwa nchini lazima atembee na kitambulisho hicho. Utaona basi kuwa wageni ni wachache sana kuliko raia na hivyo mradi wa kuwatambulisha wageni nchini mwetu utakuwa wa gharama ndogo zaidi!
c. Mradi wa Kutambulisha Wakazi?
Yawezekana lengo la mradi huu ni kumtambulisha pia mkazi wa eneo fulani. Kwamba ndani ya hizo kadi kutakuwa na anuani ya mtu anaishi wapi. Hili hata hivyo litakuwa gumu sana kwani watu wanahamahama sana, na watu wengi wanaishi katika nyumba za kupanga ambazo si zote zina anuani tofauti ya chumba kwa chumba (apartments) ukiondoa anuani ya nyumba moja.
Kwa mfano, Mtaa wa Mkwepu kuna Nyumba ya Bw. Sadallah ambayo ndani yake kuna wapangaji wanne. Nyumba hiyo kwa nje imeandikwa namba 17xx. Hata hivyo wakazi wake wenye familia zao wakiandika kwenye kitambulisho wanasema kuwa wanaishi kwenye nyumba namba 17xx, lakini zaidi ya hapo hakuna taarifa zaidi. Hata hivyo, jirani ya nyumba hiyo kuna jamaa naye amejenga kibanda chake na hapo ni kwake lakini hakijapimwa na hivyo hana anuani. Kwa muda mrefu ndugu yetu huyo amekuwa akiwaelekeza watu kuwa anaishi "nyumba tatu toka kwa mzee Sadallah". Huyu tutamtambulisha vipi kwenye kadi yetu hii kwamba anaishi wapi?
Hapa basi utaona kuwa kutahitajika mradi mwingine mkubwa wa kupima na kutoa mfumo mpya wa namba za anuani kwa kila jengo na ofisi ambayo inatumiwa na watu au matumizi yoyote rasmi. Kwa kufanya hivyo, mradi mpya wa 'MFUMO MPYA WA ANUANI ZA MAKAZI NA OFISI" utaanzishwa.
lakini wakati huo huo tunatambua kuna halmashauri ambazo zinatoa vitambulisho vya aina mbalimbali kwa wafanyabiashara, wakazi n.k Hivyo utaona Halmashauri kwa kiasi kikubwa ndizo zenye nafasi kubwa na ya kwanza ya kukutana na watu wa kawaida na wageni kuliko serikali kuu. Hivyo, mpango au mfumo wa kutambulisha wakazi na makazi yao utaonekana kufanyika vizuri chini ya Halmashauri za Mitaa na Miji kuliko kwenye serikali kuu.
d. Kumtambulisha mtu?
Hata hivyo kwa kadiri inavyoonekana mradi huu una lengo la kumtambulisha mtu. Yaani huyo mtu ni nani, rangi yake, vinasaba vyake, hali yake ya afya, benki yake, anaishi wapi, ni wa jinsia gani? Hivyo utaona basi kuwa kwa kutambulisha vitu vingi vya mtu mmoja basi mradi huu unafaa sana kwani kwa kutumia teknolojia hiyo ya kompyuta tunaweza kabisa kuweka habari nyingi kwenye kitu kidogo sana.
Hata hivyo tutajiuliza tunafanya hivyo kwa faida ya nani? Je mtu wa kijijini mkulima au mhamaji akishakuwa na kitambulisho hicho kitamfaa vipi wakati kila mvua inyeshapo amehama au yuko sehemu nyingine? Je kila akihakama na ng'ombe wake itabidi aende kuupdate yuko mahali gani na mbuga gani au tutaweka na GPS humo humo ili kumjua mtu huyo yuko wapi kwa sababu hatujui kijiografia yuko wapi?
Kama lengo ni kuyatambulisha yote hayo manne kwenye kikadi kimoja, kwa watu milioni 40 na kutengeneza database, supporting staff, n.k gharama ya bilioni 200 ni kejeli ya akili za watu timamu, na wabunge wanaosapoti mradi huu akili zao tunaweza kuziweka kwenye kundi la "fyatu"!
a. Ni utambulisho wa nini?
Kuna mtu aliuliza swali hili huko nyuma kuwa hivi vitambulisho hasa vinachotaka kutambulisha ni kitu gani? Kama ni Taifa kama inavyotajwa sasa pasi za kusafiria tayari zipo hivyo ni duplication ya services kwani pasi inamtambulisha x,y kuwa ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo, kitambulisho kingine ni cha nini basi? Tuzingatie kuwa hivi karibuni serikali ilifanya mabadiliko ya vitambulisho vyetu na kuvileta vya "kisasa" ambavyo navyo ni kama vinatumia teknolojia bora zaidi yenye kuzuia kughushi n.k. So, kama sivyo vya kutambulisha taifa vinatambulisha nini?
b. Vitambulisho vya Uraia?
Hili nalo ni kama (a) hapo juu. Kama vitambulisho hivi ni vya uraia na siyo vya kila mtu aliyemo ndani ya Taifa hilo basi bado mradi unaohitajika ni wa vitambulisho vya wageni! kwani Raia tayari wana vitambulisho vyao (pasi). Hivyo, basi kama ni kutaka kujua wageni hili nalo ni rahisi zaidi kutekeleza kwani tayari tuna vituo vya kuingilia nchini na tayari wageni wanapokuja wanakuja na pasi zao n.k Hivyo, kwetu sisi ni kutengeneza mfumo tu wa kawaida wa kuonesha mgeni ni nani na akiwa nchini lazima atembee na kitambulisho hicho. Utaona basi kuwa wageni ni wachache sana kuliko raia na hivyo mradi wa kuwatambulisha wageni nchini mwetu utakuwa wa gharama ndogo zaidi!
c. Mradi wa Kutambulisha Wakazi?
Yawezekana lengo la mradi huu ni kumtambulisha pia mkazi wa eneo fulani. Kwamba ndani ya hizo kadi kutakuwa na anuani ya mtu anaishi wapi. Hili hata hivyo litakuwa gumu sana kwani watu wanahamahama sana, na watu wengi wanaishi katika nyumba za kupanga ambazo si zote zina anuani tofauti ya chumba kwa chumba (apartments) ukiondoa anuani ya nyumba moja.
Kwa mfano, Mtaa wa Mkwepu kuna Nyumba ya Bw. Sadallah ambayo ndani yake kuna wapangaji wanne. Nyumba hiyo kwa nje imeandikwa namba 17xx. Hata hivyo wakazi wake wenye familia zao wakiandika kwenye kitambulisho wanasema kuwa wanaishi kwenye nyumba namba 17xx, lakini zaidi ya hapo hakuna taarifa zaidi. Hata hivyo, jirani ya nyumba hiyo kuna jamaa naye amejenga kibanda chake na hapo ni kwake lakini hakijapimwa na hivyo hana anuani. Kwa muda mrefu ndugu yetu huyo amekuwa akiwaelekeza watu kuwa anaishi "nyumba tatu toka kwa mzee Sadallah". Huyu tutamtambulisha vipi kwenye kadi yetu hii kwamba anaishi wapi?
Hapa basi utaona kuwa kutahitajika mradi mwingine mkubwa wa kupima na kutoa mfumo mpya wa namba za anuani kwa kila jengo na ofisi ambayo inatumiwa na watu au matumizi yoyote rasmi. Kwa kufanya hivyo, mradi mpya wa 'MFUMO MPYA WA ANUANI ZA MAKAZI NA OFISI" utaanzishwa.
lakini wakati huo huo tunatambua kuna halmashauri ambazo zinatoa vitambulisho vya aina mbalimbali kwa wafanyabiashara, wakazi n.k Hivyo utaona Halmashauri kwa kiasi kikubwa ndizo zenye nafasi kubwa na ya kwanza ya kukutana na watu wa kawaida na wageni kuliko serikali kuu. Hivyo, mpango au mfumo wa kutambulisha wakazi na makazi yao utaonekana kufanyika vizuri chini ya Halmashauri za Mitaa na Miji kuliko kwenye serikali kuu.
d. Kumtambulisha mtu?
Hata hivyo kwa kadiri inavyoonekana mradi huu una lengo la kumtambulisha mtu. Yaani huyo mtu ni nani, rangi yake, vinasaba vyake, hali yake ya afya, benki yake, anaishi wapi, ni wa jinsia gani? Hivyo utaona basi kuwa kwa kutambulisha vitu vingi vya mtu mmoja basi mradi huu unafaa sana kwani kwa kutumia teknolojia hiyo ya kompyuta tunaweza kabisa kuweka habari nyingi kwenye kitu kidogo sana.
Hata hivyo tutajiuliza tunafanya hivyo kwa faida ya nani? Je mtu wa kijijini mkulima au mhamaji akishakuwa na kitambulisho hicho kitamfaa vipi wakati kila mvua inyeshapo amehama au yuko sehemu nyingine? Je kila akihakama na ng'ombe wake itabidi aende kuupdate yuko mahali gani na mbuga gani au tutaweka na GPS humo humo ili kumjua mtu huyo yuko wapi kwa sababu hatujui kijiografia yuko wapi?
Kama lengo ni kuyatambulisha yote hayo manne kwenye kikadi kimoja, kwa watu milioni 40 na kutengeneza database, supporting staff, n.k gharama ya bilioni 200 ni kejeli ya akili za watu timamu, na wabunge wanaosapoti mradi huu akili zao tunaweza kuziweka kwenye kundi la "fyatu"!