Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Kuelekea kumalizika msimu wa Ligi Kuu Tanzania TPL, Patashika hiyo kushika kasi kwa viwanja tofauti kupigwa ambapo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mbao FC wanamenyana na KMC, huku Uwanja wa Namfua mkoani Singida wanyeji Singida United wanapapatuana na Mabingwa watetezi Simba SC.
Mchezo wa Singida United dhidi ya Simba SC, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika tisini
Msimu uliopita Simba SC walitangaza ubingwa rasmi kwenye uwanja huo huo wa Namfua Stadium, wakati walipopepeta na Singida United na wenyeji hao kukubali kipigo cha 1-0
Na leo tena Mei 21, 2019 Mabingwa hao wanahitaji ushindi muhimu ili kuweza kutangaza rasmi ubingwa msimu 2018/2019. Je historia itajirudia au Singida United wanaweza kumsimamisha Simba SC kwa muda?
Usikose ukaambiwa..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 jioni na utakuwa mubashara kupitia Azam Sports 2.
Naaaaaaam mpira umeanza uwanja wa Namfua mkoani Singida TPL..
Singida United 0-0 Simba SC
02' Mchezo umeanza kwa kasi kwa Simba kuliandama lango la wenyeji na kupata kona mbili ambazo hazikuzaa matunda.
05' Singida United, wanajaribu kujibu mashambulizi ambapo shuti la Maganga limetoka nje sentimita chache lango la Simba.
09' Goooooooooooooooooooaaal gooooooooaaal.. Maddie Kagere anaipatia Simba SC bao la kwanza baada beki wa Singida United kushindwa kuondosha mpira wa hatari ulipigwa na Mohammed Hussein
Singida United 0- 1 Simba SC
14' Singida wanaokoa mpira wa hatari ambao ungeweza kuipatia Simba bao la pili.
Mchezo umechangamka kwa pande zote mbili, Singida wakijihakikishia kusalia TPL, huku Simba wakihitaji ushindi.
15' Singida United 0-1 Simba SC
Kinyombo anakwenda lango la Simba lakini mwamuzi anasema umejiangusha na mpira wanachukua Simba
20' mpira umetawaliwa na Simba, japo Singida ni wenyeji
Free kick kuelekea Simba.Inapigwaaaaa lakini Munishi anadaka bila wasiwasi.
24' mpira umesimama baada ya mwamuzi mpira kumpiga kichwani, madaktari wanaitwa kumpatia matibabu..
Haya mpira unaendelea, TPL uwanja wa Namfua baada ya mwamuzi kupata rabsha na kutibiwa
26' Okwi anapata nafasi safi anapiga lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick
30' Inapigwa free kick kuelekea Simba, sio mbali, inapigwaaa lakini mpira unakuwa hafifu na kudakwa na Munish
35' Singida wapiga pasi za hapa na pale kujaribu kulifikia lango la Simba, anatokea mchezaji wa Singida anapiga nje na kuwa goal kick
Bocco anaambaa na mpira, na anapiga kwake Kagere..Lakini mwamuzi anasema mpira ulitoka nje kabla ya kupiga
40' Singida United 0-1 Simba SC
Simba wanasogea langoni mwa Singida anachukua Okwi mpira anapiga lakini mpira unapaa na kutoka nje na kuwa goal kick
45+2' kuelekea kuwa mapumziko
Naaaaaaam Mpira ni mapumziko uwanja wa Namfua, ambapo Simba wanatoka mbele kwa bao moja bila kwa yai, likiwekwa kambani na Maddie Kagere
Singida United 0-1 Simba SC
Kipindi cha lala kwa buriani kimeanza
46' Singida United ameanza kwa kasi kwa mashambulizi mawili makali ambayo yangeweza kupata bao, lakini mashuti yao yote yametoka nje ya lango.
50' John Bocco shuti lake linashindwa kulenga lango la Singida
Kona inapigwa kuelekea Simba, inapigwa lakini Simba wanaondosha
Mwashuya yuko chini baada ya kupata rabsha, ameinuka anaendelea
Singida United 0-1 Simba SC
Mabadiliko Singida, anatoka Mwashuya na anaingia Juma
61' Goooooooooooooooooooaaal gooooooooooaaaal..John Bocco anaipatia Simba bao la pili kwa kichwa safi baada golikipa kutoka na kuacha lango.
Mpira unaandelea...wakati huo huo golikipa wa Singida anatibiwa baada kupata rabsha.
70' Singida United 0-2 Simba SC
Inapigwa shuti kali lango la Simba SC, golikipa Munish anapangua wakati huo huo Mlipili anaondosha hatari hiyo
75' Anatoka Okwi na anaingia Mkude upande wa Simba SC
Hakuna matumaini kupata bao kama hawatabadilika Singida
Anatoka Maganga na anaingia Michael, upande wa Singida Utd
Na Simba wanafanya mabadiliko..Anatoka Niyonzima na anaingia Dilunga
80' zikiwa zimesalia dakika 10, kumalizika mpira huu, matokeo yakiwa hivi ni Dhahir Simba watakuwa mabingwa wapya
Anachukua Wilson, anapiga mpira unanaswa na Simba na wanapiga pasi fupi
85' Anatoka Maddie Kagere anaingia Triple C Chama upande wa Simba SC
Singida wanapiga mbele. Lakini wanapoteza na kuwahiwa na mabeki wa Simba
90+8' Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa TPL
Naaaaaaaaaaaaaaam..Mpira umemalizika Uwanja wa Namfua ambapo Simba SC wamekuwa Mabingwa Wapya baada ya kuibuka na ushindi wa mabao mawili bila majibu.
Mabao yamewekwa kimiani na Maddie Kagere 09' Na John Bocco 61'
Singida United 0-2 Simba SC
Kwa niaba ya Simba SC na team JF niiiiiii Ghazwat
Mchezo wa Singida United dhidi ya Simba SC, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika tisini
Msimu uliopita Simba SC walitangaza ubingwa rasmi kwenye uwanja huo huo wa Namfua Stadium, wakati walipopepeta na Singida United na wenyeji hao kukubali kipigo cha 1-0
Na leo tena Mei 21, 2019 Mabingwa hao wanahitaji ushindi muhimu ili kuweza kutangaza rasmi ubingwa msimu 2018/2019. Je historia itajirudia au Singida United wanaweza kumsimamisha Simba SC kwa muda?
Usikose ukaambiwa..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 jioni na utakuwa mubashara kupitia Azam Sports 2.
Naaaaaaam mpira umeanza uwanja wa Namfua mkoani Singida TPL..
Singida United 0-0 Simba SC
02' Mchezo umeanza kwa kasi kwa Simba kuliandama lango la wenyeji na kupata kona mbili ambazo hazikuzaa matunda.
05' Singida United, wanajaribu kujibu mashambulizi ambapo shuti la Maganga limetoka nje sentimita chache lango la Simba.
09' Goooooooooooooooooooaaal gooooooooaaal.. Maddie Kagere anaipatia Simba SC bao la kwanza baada beki wa Singida United kushindwa kuondosha mpira wa hatari ulipigwa na Mohammed Hussein
Singida United 0- 1 Simba SC
14' Singida wanaokoa mpira wa hatari ambao ungeweza kuipatia Simba bao la pili.
Mchezo umechangamka kwa pande zote mbili, Singida wakijihakikishia kusalia TPL, huku Simba wakihitaji ushindi.
15' Singida United 0-1 Simba SC
Kinyombo anakwenda lango la Simba lakini mwamuzi anasema umejiangusha na mpira wanachukua Simba
20' mpira umetawaliwa na Simba, japo Singida ni wenyeji
Free kick kuelekea Simba.Inapigwaaaaa lakini Munishi anadaka bila wasiwasi.
24' mpira umesimama baada ya mwamuzi mpira kumpiga kichwani, madaktari wanaitwa kumpatia matibabu..
Haya mpira unaendelea, TPL uwanja wa Namfua baada ya mwamuzi kupata rabsha na kutibiwa
26' Okwi anapata nafasi safi anapiga lakini mpira unatoka nje na kuwa goal kick
30' Inapigwa free kick kuelekea Simba, sio mbali, inapigwaaa lakini mpira unakuwa hafifu na kudakwa na Munish
35' Singida wapiga pasi za hapa na pale kujaribu kulifikia lango la Simba, anatokea mchezaji wa Singida anapiga nje na kuwa goal kick
Bocco anaambaa na mpira, na anapiga kwake Kagere..Lakini mwamuzi anasema mpira ulitoka nje kabla ya kupiga
40' Singida United 0-1 Simba SC
Simba wanasogea langoni mwa Singida anachukua Okwi mpira anapiga lakini mpira unapaa na kutoka nje na kuwa goal kick
45+2' kuelekea kuwa mapumziko
Naaaaaaam Mpira ni mapumziko uwanja wa Namfua, ambapo Simba wanatoka mbele kwa bao moja bila kwa yai, likiwekwa kambani na Maddie Kagere
Singida United 0-1 Simba SC
Kipindi cha lala kwa buriani kimeanza
46' Singida United ameanza kwa kasi kwa mashambulizi mawili makali ambayo yangeweza kupata bao, lakini mashuti yao yote yametoka nje ya lango.
50' John Bocco shuti lake linashindwa kulenga lango la Singida
Kona inapigwa kuelekea Simba, inapigwa lakini Simba wanaondosha
Mwashuya yuko chini baada ya kupata rabsha, ameinuka anaendelea
Singida United 0-1 Simba SC
Mabadiliko Singida, anatoka Mwashuya na anaingia Juma
61' Goooooooooooooooooooaaal gooooooooooaaaal..John Bocco anaipatia Simba bao la pili kwa kichwa safi baada golikipa kutoka na kuacha lango.
Mpira unaandelea...wakati huo huo golikipa wa Singida anatibiwa baada kupata rabsha.
70' Singida United 0-2 Simba SC
Inapigwa shuti kali lango la Simba SC, golikipa Munish anapangua wakati huo huo Mlipili anaondosha hatari hiyo
75' Anatoka Okwi na anaingia Mkude upande wa Simba SC
Hakuna matumaini kupata bao kama hawatabadilika Singida
Anatoka Maganga na anaingia Michael, upande wa Singida Utd
Na Simba wanafanya mabadiliko..Anatoka Niyonzima na anaingia Dilunga
80' zikiwa zimesalia dakika 10, kumalizika mpira huu, matokeo yakiwa hivi ni Dhahir Simba watakuwa mabingwa wapya
Anachukua Wilson, anapiga mpira unanaswa na Simba na wanapiga pasi fupi
85' Anatoka Maddie Kagere anaingia Triple C Chama upande wa Simba SC
Singida wanapiga mbele. Lakini wanapoteza na kuwahiwa na mabeki wa Simba
90+8' Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa TPL
Naaaaaaaaaaaaaaam..Mpira umemalizika Uwanja wa Namfua ambapo Simba SC wamekuwa Mabingwa Wapya baada ya kuibuka na ushindi wa mabao mawili bila majibu.
Mabao yamewekwa kimiani na Maddie Kagere 09' Na John Bocco 61'
Singida United 0-2 Simba SC
Kwa niaba ya Simba SC na team JF niiiiiii Ghazwat