Charles mandela mtt wa simba ulisema ukipata mda utatuonyesha uchum wa tz unamilikiwa na nan nakukumbusha
Wakati TANGANYIKA, sasa ni TANZANIA BARA πΉπΏ, inapata UHURU kutoka kwa UINGEREZA π¬π§ mwaka 1961, HAYATI MWALIMU alipokea nchi ikiwa katika MFUMO WA MAJIMBO, ambapo kulikuwa na MAJIMBO nane [ 8 ], na sio mikoa kama ilivyo sasa hivi.
MAJIMBO hayo ni JIMBO LA KATI, JIMBO LA MASHARIKI, JIMBO LA ZIWA, JIMBO LA KASKAZINI, JIMBO LA NYANDA ZA JUU KUSINI, JIMBO LA TANGA, JIMBO LA MAGHARIBI na JIMBO LA ZIWA TANGANYIKA.
Kwa mamlaka aliyopewa na katiba ya nchi, HAYATI MWALIMU aliunda MIKOA kumi na mitano [ 15 ] na kuiondoa nchi katika MFUMO WA MAJIMBO.
MIKOA hiyo ilikuwa ni ARUSHA, PWANI, DODOMA, TANGA, KIGOMA, KILIMANJARO, MARA, MBEYA, MOROGORO, MTWARA, MWANZA, RUVUMA, SHINYANGA, SINGIDA na TABORA.
Sasa kwenye hii ORODHA YA MIKOA yote, SERENGETI yaani CHUI kupitia kwa HAYATI MWALIMU mwenyewe walikuwa wamehodhi shughuli zote za kiuchumi kwenye kila MKOA husika na hii ilifanyika kwa sababu ya kuimarisha ULINZI na USALAMA kwa upande wa TANZANIA BARA πΉπΏ.
Na hata baada ya MUUNGANO WA TANGANYIKA na ZANZIBAR na kuunda SERIKALI YA TANZANIA πΉπΏ, hawa SERENGETI yaani CHUI kupitia kwa HAYATI MWALIMU mwenyewe waliendelea kujitanua kibiashara mpaka ZANZIBAR, yaani TANZANIA VISIWANI kwa nia ile ile ya kuimarisha ULINZI na USALAMA.
Kwahiyo, kwa kipindi chote cha UONGOZI WA HAYATI MWALIMU, hawa SERENGETI yaani CHUI ndio waliokuwa wameshika UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ kwa asilimia mia moja [ 100% ] kupitia WATU wenye asili ya ASIA na ULAYA kwa malengo ya kuimarisha ULINZI na USALAMA.
Hadi mwaka 2021, MIKOA hiyo ilikuwa imeongezeka na kufikia ishirini na sita [ 26 ], huku HALMASHAURI zote, yaani [ wilaya, miji, manispaa na majiji ] ziliongezeka kutoka arobaini na tano [ 45 ] kwa wakati wa UHURU hadi kufikia mia moja na themanini na nne [ 184 ], lengo likiwa ni kusogeza madaraka kwa WANANCHI na kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii.
MIKOA hiyo ni MARA, MWANZA, SHINYANGA, SIMIYU, GEITA, KAGERA, TABORA, KIGOMA, KATAVI, RUKWA, MBEYA, SONGWE, NJOMBE, IRINGA, RUVUMA, MTWARA, PWANI, MOROGORO, DODOMA, MANYARA, ARUSHA, KILIMANJARO, TANGA, DAR ES SALAAM, UNGUJA na PEMBA.
Mwaka 1972, SERIKALI YA TANZANIA πΉπΏ ilifuta mamlaka za SERIKALI ZA MITAA na kuanzisha MFUMO WA MADARAKA mikoani, mfumo ambao ulizifanya SERIKALI ZA MITAA kuitegemea SERIKALI KUU kwa kila jambo kutokana na WANANCHI kutoshiriki katika maamuzi na pia katika shughuli za maendeleo.
Miaka sita [ 6 ] baadae, MAMLAKA ZA MIJI zilirejeshwa huku mamlaka za wilaya zikirejeshwa mwaka 1984.
Katika moja ya mahojiano aliyowahi kufanya enzi za uhai wake, HAYATI MWALIMU mwenyewe alikiri na kusema ya kwamba anajutia kufuta MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA.
Sasa basi, turudi kwenye ile MADA KUU KUHUSU UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ na walio nyuma yake, yaani WATU wanaomiliki UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ.
Jaribu kuangalia picha hapo juu inayoonesha UTAJIRI WA MIKOA KWA KUANGALIA PATO LA MKOA HUSIKA.
MIKOA KUMI [ 10 ] YA TANZANIA πΉπΏ ambayo inayoongoza kwa UTAJIRI ni:
[1]. DAR ES SALAAM
[2]. MWANZA
[3]. MBEYA
[4]. SHINYANGA
[5]. MOROGORO
[6]. TANGA
[7]. ARUSHA
[8]. GEITA
[9]. KILIMANJARO
[10]. RUVUMA
Hii ndio ORODHA YA MIKOA KUMI [ 10 ] YA TANZANIA πΉπΏ ambayo inaongoza kwa UTAJIRI WA PATO KWA MKOA HUSIKA kwa muujibu wa TAASISI YA TAKWIMU TANZANIA πΉπΏ yaani NBS, mwaka 2021.
Vile vile UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ umechagizwa na SEHEMU KUU TATU - sehemu ya kwanza ikiwa ni SERIKALI YA TANZANIA πΉπΏ yenyewe, sehemu ya pili ikiwa ni JAMII YA SERENGETI yaani CHUI na sehemu ya tatu ikiwa ni JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA π¦.
Na uchambuzi huo unachambuliwa kama ifuatavyo - kuanzia mwaka 1961 hadi mwaka 1985, pale ambapo HAYATI MWALIMU mwenyewe anang'atuka MADARAKANI, UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ ulikuwa umeshikiliwa na JAMII ya SERENGETI yaani CHUI kwa asilimia mia moja [ 100% ].
JAMII ya SERENGETI yaani CHUI ni jamii ambayo anatoka HAYATI MWALIMU mwenyewe na inajumuisha makabila yote ya MKOA WA MARA.
Baadae, kwenye miaka ya themanini yaani 1980's - SERIKALI YA TANZANIA πΉπΏ kupitia SERIKALI ZA MITAA NA TAWALA ZA MIKOA ilianzisha VYAMA VYA USHIRIKA kwenye kila MKOA unaopatikana TANZANIA πΉπΏ ili kulenga na kukuza sekta ya kilimo inayopatikana kwenye MKOA husika.
VYAMA VYA USHIRIKA vilikuwa vinapatikana kila MKOA wa TANZANIA BARA πΉπΏ kwa lengo la kukuza mazao ya kibiashara kwa kila MKOA husika.
MAZAO YA KIBIASHARA yalikuwa kama vile TUMBAKU, KOROSHO, KAHAWA, MKONGE, PAMBA na mazao mengine ya kibiashara ya kufanana na hayo.
Hivi VYAMA VYA USHIRIKA vilikuja kuwa na UCHUMI mkubwa sana kiasi ambacho kilitishia UHAI WA CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ kutokana na wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA kuwa na UCHUMI na UKWASI uliopitiliza uliotokana na UBADHIRIFU, RUSHWA na WIZI wa mali ya UMMA.
Na MIKOA ambayo kulikuwa na VYAMA VYA USHIRIKA vyenye UCHUMI MKUBWA ilikuwa ni MWANZA, SHINYANGA na TABORA. Kwa MKOA WA MWANZA kulikuwa na CHAMA CHA USHIRIKA kilichokuwa kinaitwa NYANZA COOPERATIVE UNION yaani NCU na kwa MKOA WA SHINYANGA kulikuwa na CHAMA CHA USHIRIKA kilichokuwa kinaitwa SHINYANGA REGIONAL COOPERATIVE UNION yaani SHIRECU na kwa MKOA WA TABORA kulikuwa na CHAMA CHA USHIRIKA kilichokuwa kinaitwa WESTERN ZONE TOBACCO GROWERS COOPERATIVE UNION yaani WETCU.
Hivi VYAMA VYA USHIRIKA vya NCU, SHIRECU na WETCU ndio ilikuwa chimbuko la wakaazi wa hii MIKOA MITATU [ 3 ] ya MWANZA, SHINYANGA na TABORA kumiliki UCHUMI wao wenyewe kutokana na shughuli mbali mbali za kibiashara ikiwemo mazao ya kibiashara kama vile TUMBAKU na PAMBA na shughuli za uchimbaji madini ya DHAHABU na ALMASI.
Hali hii iliwafanya wakaazi wa hii MIKOA MITATU [ 3 ] ya MWANZA, SHINYANGA na TABORA yaani MWASHITA au kwa lingine wanaitwa SIMBA π¦ kuingia kwenye ushindani wa kibiashara na JAMII YA SERENGETI yaani CHUI na kufanikiwa kumiliki asilimia thelathini [ 30% ] ya UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ.
Kwahiyo, kuanzia mwaka 1984 hadi mwaka 1995 - UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ ulikuwa unamilikiwa na JAMII mbili tu ambazo ni SERENGETI yaani CHUI na MWASHITA yaani SIMBA π¦. JAMII ya SERENGETI yaani CHUI ilikuwa inamiliki asilimia sabini [ 70% ] ya UCHUMI WA TANZANIA πΉπΏ na asilimia zilizobaki yaani asilimia thelathini [ 30% ] ilikuwa inamilikiwa na MWASHITA yaani SIMBA π¦.
Baada ya mwaka 1995, yaani baada ya kuingia kwa RAIS WA AWAMU YA TATU, Ndugu BENJAMIN WILLIAM MKAPA alikuja na SERA YA UKWELI NA UWAZI ikiambatana na SERA YA UBINAFSISHAJI iliyokuwa inalenga madhumuni ya kuongeza ufanisi katika SEKTA BINAFSI na vile vile aliruhusu SERIKALI iingie kwenye SOKO LA USHINDANI kwa kuruhusu SERIKALI kufanya biashara kwa mtindo wa "ACCORDANCE TO BUSINESS".
Hali hii ilipelekea SEKTA BINAFSI kukua na kumea mithiri ya UYOGA kutokana na uwepo wa SERIKALI katika SEKTA BINAFSI.
Uwepo wa SERIKALI katika SEKTA BINAFSI ulifanya kiwango cha asilimia [%] kwa hizi JAMII MBILI ZA SERENGETI yaani CHUI na MWASHITA yaani SIMBA π¦ kupungua kwenye sekta ya UCHUMI WA NCHI kutokana na uwepo wa SERIKALI katika SEKTA BINAFSI yaani BIASHARA na UCHUMI.
Hali hii iliendelea hivyo hivyo mpaka leo, huku SERIKALI YA TANZANIA πΉπΏ ikiongeza kasi, ubunifu na ufanisi kwenye SEKTA BINAFSI na ikiziacha hizi JAMII MBILI ZA SERENGETI yaani CHUI na MWASHITA yaani SIMBA π¦ kwa kiwango cha UWEKEZAJI WA NDANI YA NCHI.
Hivyo basi, kwa kadri siku zinavyozidi kwenda na hali ya UCHUMI WA NCHI ulivyo - SERIKALI YA TANZANIA πΉπΏ imehodhi asilimia hamsini [ 50% ] ya UCHUMI WOTE wa TANZANIA πΉπΏ na SERIKALI inaendelea kuwekeza kwa kasi ya ajabu ikiwa na malengo ya kuhodhi UCHUMI WA NCHI na JAMII YA SERENGETI yaani CHUI inamiliki asilimia thelathini [ 30% ] ya UCHUMI WOTE wa TANZANIA πΉπΏ na asilimia ishirini [ 20% ] iliyobaki inashikiliwa na JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA π¦.