Sawa mkuu ila tutaona ukweli wa ccm kuchukuliwa na hao wasukuma
Najaribu kubahatisha kwa makini, kama ni huyu KIJANA ndio anaendesha HARAKATI ZA KISIASA yaani POLITICAL RALLY ya hao WASUKUMA waliopo ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ kuweza kumiliki CHAMA.
Kitendo cha kumiliki au kuhodhi CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ ni jambo ambalo halitawezekana. Hilo suala walifute kabisa!!
Yaani ni nafuu au vyepesi kukitoa madarakani CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ, kuliko kumiliki au kuhodhi CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ kutoka kwa JAMII YA SERENGETI yaani CHUI.
Na itakuwa BORA na SALAMA zaidi kwa hao WASUKUMA waliopo ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ kutoka ndani ya CHAMA na kuamua kuanzisha CHAMA CHA KISIASA ili wafanye SIASA ZA USHINDANI za kukiondoa madarakani CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ.
Hii njia wakiamua kuitumia itakuwa ni NJIA SAHIHI, SALAMA na BORA kwao na itaongeza AFYA YA KISIASA kwa upande wa TAIFA LA TANZANIA πΉπΏ.
Lakini wakiamua kuendeleza HARAKATI ZA KISIASA yaani POLITICAL RALLY ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ watakuwa wanapoteza muda na watakuwa wanakikomaza na kukiimarisha CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ kwa namna moja ama nyingine.
Kwahiyo ni vyema na busara kuiga kwa waliofanikiwa ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ. Na waliofanikiwa ndani ya CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ ni WATU WA PWANI. Hivyo wanatakiwa kufanya SIASA kama WATU WA PWANI wanavyofanya.
Vile vile ni busara kuiga kwa waliowatangulia na waliofanikiwa chini ya UTAWALA WA CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ. Na waliowatangulia na waliofanikiwa chini ya UTAWALA WA CHAMA CHA MAPINDUZI - CCM βοΈ ni JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA π¦ yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA VYA NCU, SHIRECU na WETCU.
Hao JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA π¦ yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA VYA NCU, SHIRECU na WETCU wamepitia mambo mengi sana. Kebehi! Dharau! Kejeli! Dhihaka na maneno machafu machafu yaliyokuwa yanatumika kuwakashifu hawa JAMII YA MWASHITA yaani SIMBA π¦.
Ilifikia hatua mpaka HAYATI MWALIMU alikuwa anawaita hawa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA VYA NCU, SHIRECU na WETCU kuwa ni WASHOSHA NG'OMBE yaani ni WATU WASHAMBA WASHAMBA.
Lakini hawa waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA VYA NCU, SHIRECU na WETCU walivumilia kwa sababu walikuwa wanajitumbua na walikuwa wanafahamu wanachokitafuta. Hawa waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA walikuwa wanatafuta UCHUMI na wamefanikiwa kwa asilimia zaidi ya mia moja [ 100% ].
Kuna kauli moja maarufu sana kwenye SEKTA YA MICHEZO ambayo iliwahi kusemwa na RAIS MSTAAFU - Ndugu ALLY HASSAN MWINYI, alisema hivi - "TANZANIA πΉπΏ ni KICHWA CHA MWENDAWAZIMU."
Na kuna kauli moja ambayo sio maarufu sana kwenye SEKTA YA MICHEZO ambayo iliwahi kusemwa na HAYATI MWALIMU baada ya HAYATI MWALIMU kuhusishwa na ununuzi wa KLABU YANGA, alisema hivi - "Mimi siwezi kununua na kumiliki TIMU ZA MCHANGANI, wapelekeeni WASHOSHA NG'OMBE ndio wanaweza hiyo shughuli." ππ
Basi kipindi hicho RAIS WA KLABU YA YANGA SC alikuwa ni ABBAS GULAMALI alifanikiwa kuwatafuta na kuwapata hao WASHOSHA NG'OMBE kwenye MKOA WA SHINYANGA na biashara ikafanyika ya kuuza KLABU YA YANGA SC na baadae tena kwenye miaka 1992/93 biashara ilifanyika tena ya kununua KLABU YA SIMBA SC ili kuiokoa isishuke DARAJA.
Baada ya hapo, hao waliokuwa wanaitwa ni WASHOSHA NG'OMBE walifanikiwa kununua KLABU nyingi sana za mpira wa miguu ikiwemo COASTAL UNION FC ya TANGA, PAN AFRICAN FC na AFRICAN LYON FC zote za DAR ES SALAAM.
Sasa hivi wale waliokuwa wanaitwa ni WASHOSHA NG'OMBE yaani WATU WASHAMBA WASHAMBA ndio wameshikilia LIGI KUU YA TANZANIA πΉπΏ kwa kumiliki TIMU ZA MPIRA WA MIGUU 7 kati ya 16 ambazo zinashiriki LIGI KUU.
Na hawa MWASHITA yaani SIMBA π¦ yaani wale waliokuwa wafanyakazi wa VYAMA VYA USHIRIKA VYA NCU, SHIRECU na WETCU ndio wamewafanya JAMII YA MIKOA YA MWANZA, SHINYANGA NA TABORA yaani WASUKUMA kuwa ni JAMII yenye UCHUMI mkubwa baada ya JAMII YA SERENGETI yaani CHUI yaani JAMII ambayo anatoka HAYATI MWALIMU mwenyewe.
Kwahiyo hii yote ni kujaribu kukuonesha ni kwa namna gani mnaweza kufanikiwa kwenye SIASA, hata kwenye MAISHA YA KILA SIKU. UVUMILIVU ndio jambo la msingi, mambo mengine yatabaki kuwa ni SIRI kwa faida ya WATAWALA.