Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

Siyo kweli kuwa filosofia ya ubebari ni asiyefanya kazi na asile. Kwenye ubebari unaweza kuwa mchapa kazi mzuri sana sana lakini ukashia kuishi maisha ya kifukara mno.
Kuchapa Kazi sio kupata.Unaweza ukachapa Kazi bila maarifa ya kupata.Kwenye ubepari mzunguko wa pesa ni Mkubwa purchasing power ni kubwa Sana biashara yeyeto inatoka
 
Kuchapa Kazi sio kupata.Unaweza ukachapa Kazi bila maarifa ya kupata.Kwenye ubepari mzunguko wa pesa ni Mkubwa purchasing power ni kubwa Sana biashara yeyeto inatoka
Unajua maana ya ''kuchapa kazi''? Kuchapa kazi ni term inayo-include vipengele vingi ikiwa ni pamoja na maarifa. Kuchapa kazi minus maarifa maana yake siyo kuchapa kazi.
 
Unajua maana ya ''kuchapa kazi''? Kuchapa kazi ni term inayo-include vipengele vingi ikiwa ni pamoja na maarifa. Kuchapa kazi minus maarifa maana yake siyo kuchapa kazi.
Sasa Kama unachapa Kazi na mzunguko mzuri wa pesa zipo mtaani unakuwa vipi masikini sasa.vibarua vimejaa tele, viwanda Kama uyoga, watu wanapesa mfukoni hapa unakuwa vipi masikini sasa.
 
Tangu nipo shule ya msingi tulikua tunaaminishwa kwamba Mlm Nyerere ndio "icon" pekee apa nchini, tulikua tunaimba nyimbo nyingi ni za kumsifu, lakini hatukuwahi kuambiwa kua kuna watu wengine ambao bila wao mwalimu "asingetoboa" na pengine tusingemjua kabisa mwalimu nyerere, au story yake ingekua "short lived". Mmoja wa hao watu ni OSCAR KAMBONA.

Nimezaliwa hapa Tanzania miaka ya 90 mpaka nimekua mtu mzima kila kitu ni Nyerere tu. Kambona nilimsikia badae sana baada ya kuskia kisa cha huyu mtu nikawa interested sana kufuatilia stories zake.

kwa mujibu wa maandiko Kambona alikua bega kwa bega na mwalimu ktk kudai uhuru yaani ilikua akitoka mwalimu anaefuata ni Kambona lakini huwezi sikia hichi kitu kinasemwa waziwazi na pengine bila mawazo na support ya kambona mwalimu "angefeli vibaya mno". Kambona ndio mtu aliezima mapinduzi yalioilenga serikali ya nyerere kutoka kwa askari waliotaka kuasi, yaani kwa ufupi ni kwamba Nyerere asinge endelea kua mtawala wa nchi hii kama sio Kambona.

Kambona aliona mbali kuliko mwalimu Tanzania ya sasa ndio aliyoiona kambona lakini mwalimu alipinga, Kambona aliona ubepari ndio utafanya kazi lakini mwalimu aliona ujamaa ndio unafaa, mwalimu "failed miserably" akatupeleka chaka mpaka leo we still pay for his "grave mistake". Mwalimu alikua mbishi na aliamini kwamba yeye ndio ana maono bora kuliko wengine ,chochote kile ambacho kilikua hakiendani na sera zake alikipinga hata kama kilikua "viable". Fikiria mtu mmoja tu kaenda urusi akafurahishwa na mfumo wa ujamaa akaja kuufanyia "experiment" hapa nchini na ukafeli kwasababu alikataa kusikiliza maoni ya watu wengine, kwa wakati huo mwalimu ndio alikua "kila kitu"

Kambona akatofautiana na mwalimu , yeye alitaka ubepari mwalimu alitaka ujamaa. Kutokana na ushawishi mwalimu alishinda japo kambona ndie aliekua sahihi lakini hawakumskiliza. Baadae mwalimu alijua amekosea akaturudisha kwenye Ubepari na bado akaonekana ni "hero" . Kitu ambacho oscar alikiona miaka kadhaa kabla wakati huo mwalimu alikua "blind" almost everyone was blind except the very few including Kambona

Haya leo 2021 TZ hii ya leo ndio kambona aliyoiona na tumechelewa sana, kwa mtazamo wangu bado tupo nyuma kwa miaka 15 kutokana na sera mbovu za mwalimu nyerere

Wote ni marehemu wapumzike kwa amani lakini, mwisho wa siku Oscar Kambona ndio AMESHINDA!!!!! Kwangu mimi shujaa wa kweli nchi hii ni OSCAR KAMBONA na sio mwalimu! Na ndio mtu muhimu sana sawa na mwalimu lakini ndio aliesahaulikia kuliko wote nchi hii, natamani watanzania wengi tuliozaliwa miaka ya 90 wajue habari za huyu shujaaa ambaye ni co-founder wa hii nchi kwangu mimi alichangia 50% ktk kutengeneza taifa hili sawa sawa na mwalimu, yaani ni kama vile "stive wozniak na stive jobs", steve jobs alitumia akili za stive wozniak na credit akajiapa yy mwenyewe

Aliyeweka Nyerere day kama public holiday alitumia vigezo gani ilihali si kweli kwamba Nyerere ndie mtu pekee aliepigania uhuru wa nchi hii

Ukiniambia nichague kati ya Nyerere na Kambona itakua ni Kambona always

UPDATE:
Watu wengi kwenye comments wanasema kwamba ujamaa ulituleta karibu, lakini ujamaa huo huo ndio uliotuletea umaskini, kwa hiyo logic yake ni kwamba mwalimu alichagua umaskini na umoja dhidi ya maendeleo ambayo hatuna uhakika kama yangetugawa, lakini kabla ya yote Kambona alimshauri kwamba kabla ya ku adopt ujamaa tuufanyie kwanza majaribio , tutengeneze vijiji vichache ambavyo vitaishi kijamaa ili tuone hii system itafanya kazi lakini mwalimu alikataa akaiingiza moja kwa moja bila kujua risks zake ni nini kitu ambacho kambona alishakiona


"Oscar Kambona was one of the best presidents Tanzania never had"
refence:
OSCAR KAMBONA: KIONGOZI MAHIRI, MTANASHATI NA RAFIKI KIPENZI WA MWALIMU NYERERE ALIYEISHIA KUWA ADUI YAKE MKUBWA!!! - MICHUZI BLOG (issamichuzi.blogspot.com)

Oscar Kambona - Wikipedia
Umeandika utumbo wa kiwango cha lami..

Uko biased sana. Asingekuwa yeye kungekuwa na wengine.. [emoji57][emoji57][emoji57][emoji57]
 
Ubebari ni unyonyaji! Ndugu yangu jaribu kutembelea nchi za Scandinavia ndiyo utajua ukweli wa msemu huu. Kule mfumo wao unaweza kudhani ni ujamaa wa aina fulani lakini wananchi wake wana maisha mazuri sana kuliko hata Marekani.

Ubepari ndio unawafanya wanapata huduma zote za kijamii. Ni ubepari ndio unakuza uchumi wao sio huu Ujima
 
Sasa Kama unachapa Kazi na mzunguko mzuri wa pesa zipo mtaani unakuwa vipi masikini sasa.vibarua vimejaa tele, viwanda Kama uyoga, watu wanapesa mfukoni hapa unakuwa vipi masikini sasa.
Hapo ''chacha''! Tashwish yako inaonyesha somo limekuingia. Unakuwa maskini kwa sababu ubebari ni unyama. Utafanya vibarua sana, utamenyeka sana lakini malipo utapewa kidogo. Kumbuka unaweza kukuta viwanda vinamilikiwa na watu wachache na wao ndiyo hupanga malipo.
 
Hapo ''chacha''! Tashwish yako inaonyesha somo limekuingia. Unakuwa maskini kwa sababu ubebari ni unyama. Utafanya vibarua sana, utamenyeka sana lakini malipo utapewa kidogo. Kumbuka unaweza kukuta viwanda vinamilikiwa na watu wachache na wao ndiyo hupanga malipo.
Umasikini unaletwa na sera mbovu za ujamaa za kuwafanya matajiri wawe masikini ili watawaliwe
 
Acha uvivu, uzembe na upumbavu. Tangu Nyerere aache urais ni muda mrefu sana na tungekuwa tuna uongozi mzuri nchi unayoitamani wewe ingeshatengenezwa. Nyerere ni mmoja ya viongozi wazuri sana kutokea. Nchi gani za Afrika zilikuwa na viongozi wazuri enzi za Nyerere ambazo unaweza kutoa kama mfano leo? Mimi naona nchi nyingi zina changamoto kuliko Tanzania mara kumi.
Nyerere alikuwa ni kiongozi mzuri lakini UJAMAA was a disaster: An unmitigated disaster.
 
Tatizo lilianza kwenye uasi wa wanajeshi 1964.

Hata siku ya uasi 1964, wanajeshi walivyoasi, Nyerere akakimbia Ikulu, Kambona ndiye aliyewatukiza. Na baada ya hapo watu wengine wakawa wanasema Kambona ndiye aliyepanga uasi ule.

Wengine waliokuwa hawampendi Kambona wakaona kama Kambona anataka kumpiku Nyerere.

Ikawa habari ya "mafahali wawili hawakai zizi moja".

Ila mpaka mwisho kabisa, Kambona alipokuwa karibu anajiuzulu Nyerere hakutaka kuamini kwamba Kambona anamhujumu.
Waliokuwa wanapeleka maneno kwa Mzee Nyerere dhidi ya Kambona ni wakina Peter Siyovelwa na Emilio Mzena: Hawa ndiyo waliofanya fitina dhidi ya Kambona, hasahasa Siyovelwa ambaye ndiye alikazia sana jamaa ashughulikiwe.

Lakini upande mwingine wa shilingi wazungu walikuwa hawataki kutoka Tanzania na kuachishwa kazi zao. Earl Seaton anasema moja ya masharti aliyopewa Nyerere kwenye Uhuru wa Tanganyika ni kuhakikisha kwamba hawatawafukuza wafanyakazi wa Tanganyika wenye asili ya Uingereza. Katika hili walifanya kabisa hadi makubaliano ambayo yaliwekwa kwenye karatasi, hivyo haikuwa rahisi kwa Nyerere kuwaondoa.

Yote tisa, kuna mengi yamefichika hapa: Kambona kama waziri alikuwa na nguvu sana wakati uasi unatokea, na kama angekuwa anautaka Uraisi wa Tanganyika basi asingemchelewesha Nyerere. Matukio ya kwenye uasi yanadhihirisha kabisa kwamba Kambona alikuwa ni mtu muungwana. Haingii akilini mtu apange uasi halafu yeye mwenyewe ndiyo asaidie kuwapigia simu waingereza kuja kusaidia kuuzima huo uasi.

Kitu kimoja ambacho nadhani waandishi wengi wanakisahau na kutokitilia mkazo ni kwamba majaribio ya uasi yalifanyika kwenye nchi zote tatu (Tanganyika, Kenya na Uganda), ambazo zilikuwa ni koloni la taifa moja (Uingereza) na majeshi hayo yote (King African Rifles) yalitengenezwa na wao wenyewe. Kikubwa na kinachoshangaza ni kwamba haya mapinduzi yalifanyaka katika kipindi cha mwezi moja: And GUESS WHAT, madai ya wanajeshi kwenye nchi zote tatu yalikuwa yanafanana.
 
Waliokuwa wanapeleka maneno kwa Mzee Nyerere dhidi ya Kambona ni wakina Peter Siyovelwa na Emilion Mzena: Hawa ndiyo waliofanya fitina dhidi ya Kambona, hasahasa Siyovelwa ambaye ndiye alikazia sana jamaa ashughulikiwe.

Lakini upande mwingine wa shilingi wazungu walikuwa hawataki kutoka Tanzania na kuachishwa kazi zao. Earl Seaton anasema moja ya masharti aliyopewa Nyerere kwenye Uhuru wa Tanganyika ni kuhakikisha kwamba hawatawafukuza wafanyakazi wa Tanganyika wenye asili ya Uingereza. Katika hili walifanya kabisa hadi makubaliano ambayo yaliwekwa kwenye karatasi, hivyo haikuwa rahisi kwa Nyerere kuwaondoa.

Yote tisa, kuna mengi yamefichika hapa: Kambona kama waziri alikuwa na nguvu sana wakati uasi unatokea, na kama angekuwa anautaka Uraisi wa Tanganyika basi asingemchelewesha Nyerere. Matukio ya kwenye uasi yanadhihirisha kabisa kwamba Kambona alikuwa ni mtu muungwana. Haingii akilini mtu apange uasi halafu yeye mwenyewe ndiyo asaidie kuwapigia simu waingereza kuja kusaidia kuuzima huo uasi.

Kitu kimoja ambacho nadhani waandishi wengi wanakisahau na kutokitilia mkazo ni kwamba majaribio ya uasi yalifanyika kwenye nchi zote tatu (Tanganyika, Kenya na Uganda), ambazo zilikuwa ni koloni la taifa moja (Uingereza) na majeshi hayo yote (King African Rifles) yalitengenezwa na wao wenyewe. Kikubwa na kinachoshangaza ni kwamba haya mapinduzi yalifanyaka katika kipindi cha mwezi moja: And GUESS WHAT, madai ya wanajeshi kwenye nchi zote tatu yalikuwa yanafanana.
kambona sio mtu aliestaili ile treatment, hakua mtu aliekua akipigania madaraka wala hakua mtu wa uchu na madaraka alipigania TZ ile ile aliyokua anapigania nyerere bega kwa bega na mwalimu wote walikua na nia njema ila mwalimu was a fool to the core! kutofautiana tu mtazamo jamaa akamtesa sana mwenzake, mwalimu alikua kiongozi mbaya zaidi kuwahi kutokea Tanzania hii up to nw, he meant well but he persuased the wrong policies foolishly
 
Waliokuwa wanapeleka maneno kwa Mzee Nyerere dhidi ya Kambona ni wakina Peter Siyovelwa na Emilion Mzena: Hawa ndiyo waliofanya fitina dhidi ya Kambona, hasahasa Siyovelwa ambaye ndiye alikazia sana jamaa ashughulikiwe.

Lakini upande mwingine wa shilingi wazungu walikuwa hawataki kutoka Tanzania na kuachishwa kazi zao. Earl Seaton anasema moja ya masharti aliyopewa Nyerere kwenye Uhuru wa Tanganyika ni kuhakikisha kwamba hawatawafukuza wafanyakazi wa Tanganyika wenye asili ya Uingereza. Katika hili walifanya kabisa hadi makubaliano ambayo yaliwekwa kwenye karatasi, hivyo haikuwa rahisi kwa Nyerere kuwaondoa.

Yote tisa, kuna mengi yamefichika hapa: Kambona kama waziri alikuwa na nguvu sana wakati uasi unatokea, na kama angekuwa anautaka Uraisi wa Tanganyika basi asingemchelewesha Nyerere. Matukio ya kwenye uasi yanadhihirisha kabisa kwamba Kambona alikuwa ni mtu muungwana. Haingii akilini mtu apange uasi halafu yeye mwenyewe ndiyo asaidie kuwapigia simu waingereza kuja kusaidia kuuzima huo uasi.

Kitu kimoja ambacho nadhani waandishi wengi wanakisahau na kutokitilia mkazo ni kwamba majaribio ya uasi yalifanyika kwenye nchi zote tatu (Tanganyika, Kenya na Uganda), ambazo zilikuwa ni koloni la taifa moja (Uingereza) na majeshi hayo yote (King African Rifles) yalitengenezwa na wao wenyewe. Kikubwa na kinachoshangaza ni kwamba haya mapinduzi yalifanyaka katika kipindi cha mwezi moja: And GUESS WHAT, madai ya wanajeshi kwenye nchi zote tatu yalikuwa yanafanana.
1964 uasi ulitokea Afrika Mashariki yote, pamoja na Mapinduzi ya Zzanzibar, katika kipindi kifupi sana.

Kuna kitabu kimoja, nafikiri ni "Nyerere of Tanzania" cha William Edgett Smith, kinaelezea jinsi Mkapa alivyokuwa anampelekea maneno Nyerere kwamba Kambona anamsengenya, Nyerere akawa anayapuuza tu mwanzoni.Hata Nyerere mwenyewe hakuamini kwamba ugomvi wake na Kambona utakuwa mkubwa hivyo hapo mwanzoni. Ila inaonekana Kambona alianza kumponda Nyerere, na wapambe hawakupenda.

Kuhusu uasi, watu wanasema Kambona alipanga uasi, ila kama unavyosema, haiyumkiniki.Angepanga, alikuwa na nafasi nzuri ya kufanya mapinduzi ya kijeshi, kwani kuna wakati Nyerere alikimbia Ikulu.
 
1964 uasi ulitokea Afrika Mashariki yote, pamoja na Mapinduzi ya Zzanzibar, katika kipindi kifupi sana.

Kuna kitabu kimoja, nafikiri ni "Nyerere of Tanzania" cha William Edgett Smith, kinaelezea jinsi Mkapa alivyokuwa anampelekea maneno Nyerere kwamba Kambona anamsengenya, Nyerere akawa anayapuuza tu mwanzoni.Hata Nyerere mwenyewe hakuamini kwamba ugomvi wake na Kambona utakuwa mkubwa hivyo hapo mwanzoni. Ila inaonekana Kambona alianza kumponda Nyerere, na wapambe hawakupenda.

Kuhusu uasi, watu wanasema Kambona alipanga uasi, ila kama unavyosema, haiyumkiniki.Angepanga, alikuwa na nafasi nzuri ya kufanya mapinduzi ya kijeshi, kwani kuna wakati Nyerere alikimbia Ikulu.
Hivi kuna uhusiano kati ya huo uasi wa kijeshi wa mwaka 1964 na mapinduzi ya Zanzibar?

Ina maana Kambona alisaidia kutuliza uasi ila aliunga mkono mapinduzi ya Zanzibar yaliyopangwa na rafiki yake Hanga?
 
Siyo kweli kuwa filosofia ya ubebari ni asiyefanya kazi na asile. Kwenye ubebari unaweza kuwa mchapa kazi mzuri sana sana lakini ukashia kuishi maisha ya kifukara mno.

Hoja si kufanya kazi, hoja ni kufanya kazi zenye tija na ndio ubepari unavyotaka.

Sio mtu una amka tu na kuanza kulima lima bila kujua utauzia wapi na kwa nani, sio mtu unakurupuka tu kuomba kazi mahali ili hali hujui hata mahitaji yako yanakuitaji uwe na kipato kiasi gani.

Lazima ujue hivi ndio ufanikiwe la sivyo utabaki kulalamika unanyonywa kumbe ni ujinga binafsi tu
 
Back
Top Bottom