Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

Tanzania ya sasa ni ile aliyoona Oscar Kambona, Mwalimu Nyerere alikosea sana

Long time no see! Kimsingi mwalimu alituacha sehemu nzuri sana kimaendeleo na kielimu.
Elimu: Uendelezaji wa elimu katika nchi ni jambo la hatua kwa hatua. Ukikurupuka na kuamua ''kufyatua'' vyuo vikuu kama walivyofanya sasa una hasara. Hasara kubwa ni kupata ma-graduate waliyo incompetent na nchi kuelemewa na vijana wasiyo na ajira. Mwalimu alikuwa anaendeleza elimu hatua kwa hatua.
Maendeleo: Nyerere alituachia misingi mingi bora ya maendeleo hasa kwenye sekta ya viwanda na mashirika ya umma. Labda ''kosa'' alilofanya ni kutojua kuwa mwafrika hawezi kusimamia na kuendeleza mali ya umma. Niliwahi kutembelea nchi za Scandinavia na kukuta mfumo wao hauna tofauti kubwa sana na ule Nyerere aliokuwa anajaribu kuujenga. Tofauti ni kuwa wananchi wa Scandinavia ni wachapa kazi na waaminifu kwenye kusimamia mali ya umma.

Alisema mwenyewe kuwa anataka nchi iwe na vyuo vikuu vichache vitakavyotoa majenerali. Iwe na vyuo vya kati kutoa makapteni. Na shule za msingi kutoa utitiri wa wapiganaji. Mfumo huu umepitwa na wakati kwani ata mtu asiye na ajira lakini akiwa na kisomo cha juu anamchango mkubwa kwa jamii kuliko mbumbumbu.

Hata Uingereza alipoiga mfumo huo mambo yamebadilika. Kwa mfano mwaka 1975, asilimia kumi tu ilikwenda University. Kwa miaka ya sasa ni zaidi ya asimilia 40.
 
Alisema mwenyewe kuwa anataka nchi iwe na vyuo vikuu vichache vitakavyotoa majenerali. Iwe na vyuo vya kati kutoa makapteni. Na shule za msingi kutoa utitiri wa wapiganaji. Mfumo huu umepitwa na wakati kwani ata mtu asiye na ajira lakini akiwa na kisomo cha juu anamchango mkubwa kwa jamii kuliko mbumbumbu.

Hata Uingereza alipoiga mfumo huo mambo yamebadilika. Kwa mfano mwaka 1975, asilimia kumi tu ilikwenda University. Kwa miaka ya sasa ni zaidi ya asimilia 40.
kweli zamani ni zamani ina maana hakuwaza elimu kwa watu wote in general
 
Tangu nipo shule ya msingi tulikua tunaaminishwa kwamba Mlm Nyerere ndio "icon" pekee apa nchini, tulikua tunaimba nyimbo nyingi ni za kumsifu, lakini hatukuwahi kuambiwa kua kuna watu wengine ambao bila wao mwalimu "asingetoboa" na pengine tusingemjua kabisa mwalimu nyerere, au story yake ingekua "short lived". Mmoja wa hao watu ni OSCAR KAMBONA.

Nimezaliwa hapa Tanzania miaka ya 90 mpaka nimekua mtu mzima kila kitu ni Nyerere tu. Kambona nilimsikia badae sana baada ya kuskia kisa cha huyu mtu nikawa interested sana kufuatilia stories zake.

kwa mujibu wa maandiko Kambona alikua bega kwa bega na mwalimu ktk kudai uhuru yaani ilikua akitoka mwalimu anaefuata ni Kambona lakini huwezi sikia hichi kitu kinasemwa waziwazi na pengine bila mawazo na support ya kambona mwalimu "angefeli vibaya mno". Kambona ndio mtu aliezima mapinduzi yalioilenga serikali ya nyerere kutoka kwa askari waliotaka kuasi, yaani kwa ufupi ni kwamba Nyerere asinge endelea kua mtawala wa nchi hii kama sio Kambona.

Kambona aliona mbali kuliko mwalimu Tanzania ya sasa ndio aliyoiona kambona lakini mwalimu alipinga, Kambona aliona ubepari ndio utafanya kazi lakini mwalimu aliona ujamaa ndio unafaa, mwalimu "failed miserably" akatupeleka chaka mpaka leo we still pay for his "grave mistake". Mwalimu alikua mbishi na aliamini kwamba yeye ndio ana maono bora kuliko wengine ,chochote kile ambacho kilikua hakiendani na sera zake alikipinga hata kama kilikua "viable". Fikiria mtu mmoja tu kaenda urusi akafurahishwa na mfumo wa ujamaa akaja kuufanyia "experiment" hapa nchini na ukafeli kwasababu alikataa kusikiliza maoni ya watu wengine, kwa wakati huo mwalimu ndio alikua "kila kitu"

Kambona akatofautiana na mwalimu , yeye alitaka ubepari mwalimu alitaka ujamaa. Kutokana na ushawishi mwalimu alishinda japo kambona ndie aliekua sahihi lakini hawakumskiliza. Baadae mwalimu alijua amekosea akaturudisha kwenye Ubepari na bado akaonekana ni "hero" . Kitu ambacho oscar alikiona miaka kadhaa kabla wakati huo mwalimu alikua "blind" almost everyone was blind except the very few including Kambona

Haya leo 2021 TZ hii ya leo ndio kambona aliyoiona na tumechelewa sana, kwa mtazamo wangu bado tupo nyuma kwa miaka 15 kutokana na sera mbovu za mwalimu nyerere

Wote ni marehemu wapumzike kwa amani lakini, mwisho wa siku Oscar Kambona ndio AMESHINDA!!!!! Kwangu mimi shujaa wa kweli nchi hii ni OSCAR KAMBONA na sio mwalimu! Na ndio mtu muhimu sana sawa na mwalimu lakini ndio aliesahaulikia kuliko wote nchi hii, natamani watanzania wengi tuliozaliwa miaka ya 90 wajue habari za huyu shujaaa ambaye ni co-founder wa hii nchi kwangu mimi alichangia 50% ktk kutengeneza taifa hili sawa sawa na mwalimu, yaani ni kama vile "stive wozniak na stive jobs", steve jobs alitumia akili za stive wozniak na credit akajiapa yy mwenyewe

Aliyeweka Nyerere day kama public holiday alitumia vigezo gani ilihali si kweli kwamba Nyerere ndie mtu pekee aliepigania uhuru wa nchi hii

Ukiniambia nichague kati ya Nyerere na Kambona itakua ni Kambona always

UPDATE:
Watu wengi kwenye comments wanasema kwamba ujamaa ulituleta karibu, lakini ujamaa huo huo ndio uliotuletea umaskini, kwa hiyo logic yake ni kwamba mwalimu alichagua umaskini na umoja dhidi ya maendeleo ambayo hatuna uhakika kama yangetugawa, lakini kabla ya yote Kambona alimshauri kwamba kabla ya ku adopt ujamaa tuufanyie kwanza majaribio , tutengeneze vijiji vichache ambavyo vitaishi kijamaa ili tuone hii system itafanya kazi lakini mwalimu alikataa akaiingiza moja kwa moja bila kujua risks zake ni nini kitu ambacho kambona alishakiona


"Oscar Kambona was one of the best presidents Tanzania never had"
refence:
OSCAR KAMBONA: KIONGOZI MAHIRI, MTANASHATI NA RAFIKI KIPENZI WA MWALIMU NYERERE ALIYEISHIA KUWA ADUI YAKE MKUBWA!!! - MICHUZI BLOG (issamichuzi.blogspot.com)

Oscar Kambona - Wikipedia
Nimesoma hivi vitabu ni ukweli mtupu tungekuwa mbali sana
source (chanzo)
*"Bibi Titi and the Treason Trial of 1970," in The East African, Nairobi, Kenya, 10–16 November 1999
*Godfrey Mwakikagile, chapter 13, "Coup Attempts Against President Julius Nyerere.
*Wikipedia
 
Nimesoma hivi vitabu ni ukweli mtupu tungekuwa mbali sana
source (chanzo)
*"Bibi Titi and the Treason Trial of 1970," in The East African, Nairobi, Kenya, 10–16 November 1999
*Godfrey Mwakikagile, chapter 13, "Coup Attempts Against President Julius Nyerere.
*Wikipedia
share apa hvo vitabu kama unavyo
 
Lkn at the end USA ideology zao ndio jibu sahihi. Ujamaa umekazia kuwatawala watu, ikiwemo kuwakandamiza kiuchumi, kumbuka mifumo ya kijamaa uruhusiwi kufikiri zaidi ya anaekutawala, utakiwi kuwa na utajiri au elimu kuliko anaekutawala. Ubepari umekazia uhuru wa kiuchumi KILA mtu avune kadri awezae .
Papy sio kweli kwamba ndio jibu sahihi. Jibu sahihi ingekuwa wao kuwa na kama European Model.

Ambapo makazi (shelter), kazi (empoyment au unemployment), Afya kwa kila mtu (Universal Health Service of course you have to pay through insurance if you work). Lakini itakusaidia sana mbeleni.

Ukimaliza hayo (basic human neeeds) unakuja kwenye Elimu.

Elimu ya ukweli inakufumbua macho, kuiona Dunia tofauti, masoko, oppotunities, gap in the markets, your potential, your abilities to act and react to changing, fluid situation.

Sijui uelewa wako kuhusu neno ujamaa, (Socialism). Kwa kifupi ni undugu, kushirikiana kwa mambo makumbwa ambayo mtu mmoja mmoja hawezi kuyafanya.

Ujamaa is natural, in all human society. Mmasai akienda kuwinda anahitaji washikaji ili arudi salama. Vijiji vyote Tanzania ili ku-survive vinahitaji aina fulani ya social security (Ulinzi Shirikishi, kumsaidia mgonjwa, kupeana kazi, kuwasaidia maskini).

Sababu ziko wazi. Ukiwa tajiri pekee kijijini bila kuwasaidia wengine siku moja utavamiwa na walalahoi na hakuna atayekusaidia.

Ujamaa (Socialism) is old as human and animals. All for greater gòod of society.
 
sawa lakini baadae walimnyanyasa kambona mpaka akakimbia nchi kitu ambacho mwalimu hakupaswa kufanya ,alafu cha ajabu zaidi ni kwamba sijaona sehemu inasema oscar alikua na uchu wa madaraka au alitaka kumreplace mwalimu

Hindsight is 20/20. Lakini kuna ukweli kwamba jina lake, mchango wake, maoni yake, muhimu yawe recognised. He was giant of not only Tanzania politics but African politics.

It was sad to read how he live in London in Council Estate with jobs za kubangaiza. Kwanini asingeishi Afrika like Nigeria for example.

His talent, vision, ideas deserve a Place.
 
Waliokuwa wanapeleka maneno kwa Mzee Nyerere dhidi ya Kambona ni wakina Peter Siyovelwa na Emilion Mzena: Hawa ndiyo waliofanya fitina dhidi ya Kambona, hasahasa Siyovelwa ambaye ndiye alikazia sana jamaa ashughulikiwe.

Lakini upande mwingine wa shilingi wazungu walikuwa hawataki kutoka Tanzania na kuachishwa kazi zao. Earl Seaton anasema moja ya masharti aliyopewa Nyerere kwenye Uhuru wa Tanganyika ni kuhakikisha kwamba hawatawafukuza wafanyakazi wa Tanganyika wenye asili ya Uingereza. Katika hili walifanya kabisa hadi makubaliano ambayo yaliwekwa kwenye karatasi, hivyo haikuwa rahisi kwa Nyerere kuwaondoa.

Yote tisa, kuna mengi yamefichika hapa: Kambona kama waziri alikuwa na nguvu sana wakati uasi unatokea, na kama angekuwa anautaka Uraisi wa Tanganyika basi asingemchelewesha Nyerere. Matukio ya kwenye uasi yanadhihirisha kabisa kwamba Kambona alikuwa ni mtu muungwana. Haingii akilini mtu apange uasi halafu yeye mwenyewe ndiyo asaidie kuwapigia simu waingereza kuja kusaidia kuuzima huo uasi.

Kitu kimoja ambacho nadhani waandishi wengi wanakisahau na kutokitilia mkazo ni kwamba majaribio ya uasi yalifanyika kwenye nchi zote tatu (Tanganyika, Kenya na Uganda), ambazo zilikuwa ni koloni la taifa moja (Uingereza) na majeshi hayo yote (King African Rifles) yalitengenezwa na wao wenyewe. Kikubwa na kinachoshangaza ni kwamba haya mapinduzi yalifanyaka katika kipindi cha mwezi moja: And GUESS WHAT, madai ya wanajeshi kwenye nchi zote tatu yalikuwa yanafanana.
Kwa kifupi ulipangwa kwa Maslahi ya UK. Waje kuufuta baadaye. Kambla ya kuweka masharti fulani.
 
Ubepari ukiendeshwa holels holela ni majanga tu.

Hata ujamaa usiposimamiwa vizuri ni kilio tu. Ndani ya ujamaa Mnaanzisha viwanda, mabenki halafu usimamizi hakuna. Mtegemee maumivu. Kama tulivyoishia kuviuza na mara ingine kwa hasara.

Kama vitu alivyoanzisha Nyerere vingepata usimamizi, tungekuwa tunaongea mengine saa hizi. Ilitakiwa vilindwe, ubunifu uwepo, ushindani uwepo, na nk.

Vitu vingi vilivyoanzishwa nahisi vilikufa kizembe zembe tu - hujuma za wafanyakazi/ viongozi, uzembe zembe, ukosefu wa teknolojia mpya,
 
Hindsight is 20/20. Lakini kuna ukweli kwamba jina lake, mchango wake, maoni yake, muhimu yawe recognised. He was giant of not only Tanzania politics but African politics.

It was sad to read how he live in London in Council Estate with jobs za kubangaiza. Kwanini asingeishi Afrika like Nigeria for example.

His talent, vision, ideas deserve a Place.
How how much we know about him is for TISS to tell us.
nafkiri aliona hatokua salama ndani ya nchi yoyote ya afrika and the funny thing ni kwamba aliishi maisha ya ukata sana lakini huku nyumbanni nyerere & co. walisema kwamba jamaa alikimbia na mkwanja wa kutosha
 
Papy sio kweli kwamba ndio jibu sahihi. Jibu sahihi ingekuwa wao kuwa na kama European Model.

Ambapo makazi (shelter), kazi (empoyment au unemployment), Afya kwa kila mtu (Universal Health Service of course you have to pay through insurance if you work). Lakini itakusaidia sana mbeleni.

Ukimaliza hayo (basic human neeeds) unakuja kwenye Elimu.

Elimu ya ukweli inakufumbua macho, kuiona Dunia tofauti, masoko, oppotunities, gap in the markets, you potential, your abilities to act and react to changing, fluid situation.

Sijui uelewa wako kuhusu neno ujamaa, (Socialism). Kwa kifupi ni undugu, kushirikiana kwa mambo makumbwa ambayo mtu mmoja mmoja hawezi kuyafanya.

Ujamaa is natural all human society. Mmasai akienda kuwinda anahitaji washikaji ili arudi salama. Vijiji vyote Tanzania ili ku-survive vinahitaji aina fulani ya social security (Ulinzi Shirikishi, kumsaidia mgonjwa, kupeana kazi, kuwasaidia maskini).

Sababu ziko wazi. Ukiwa tajiri pekee kijijini bila kuwasaidia wengine siku moja utavamiwa na walalahoi na hakuna atayekusaidia.

Ujamaa (Socialism) is old as human and animals. All for greater gòod of society.

What did you smoke? Ujamaa isn't natural and isn't that old. If it was, we could have seamlessly fitted in without the use of force.
 
Ubepari ukiendeshwa holels holela ni majanga tu.

Hata ujamaa usiposimamiwa vizuri ni kilio tu. Ndani ya ujamaa Mnaanzisha viwanda, mabenki halafu usimamizi hakuna. Mtegemee maumivu. Kama tulivyoishia kuviuza na mara ingine kwa hasara.

Kama vitu alivyoanzisha Nyerere vingepata usimamizi, tungekuwa tunaongea mengine saa hizi. Ilitakiwa vilindwe, ubunifu uwepo, ushindani uwepo, na nk.

Vitu vingi vilivyoanzishwa nahisi vilikufa kizembe zembe tu - hujuma za wafanyakazi/ viongozi, uzembe zembe, ukosefu wa teknolojia mpya,

Kwenye Ujamaa utasimamia nini? Majengo? Zilikuwepo banks, lakini watu walishindwa kuweka pesa kwa sababu ya kipato. Sasa utasimamia nini? Kulikuwepo na viwanda, lakini havikuwa na uzalishaki mzuri. Sasa ulitaka watu wasimamie kugawana kipande cha sabuni.
 
mwalimu "failed miserably" akatupeleka chaka mpaka leo we still pay for his "grave mistake". Ukweli mtupu viongozi ni lazima wawe na utaratibu wa kusikiliza! Lakini vilevile wananchi wengi wanapenda ushabiki sana angalieni sasa kuna watu wanashabikia kila kitu hata mabaya kwa nchi!
 
Fafanua zaidi mkuu.

Hakuna mtu aliyewahi kuishi kwenye Ujamaa. Hata Nyerere mwenyewe hakuwai. Wakati wa utawala wake misaada kutoka kwa mabepari ilikuwa kwenye asilimia 50. Ina maana hata mshahara wake ulitegemea mfumo wa kibepari. Na bila misaada hiyo asingeweza kujenga hospitali au mashule.
 
mwalimu "failed miserably" akatupeleka chaka mpaka leo we still pay for his "grave mistake". Ukweli mtupu viongozi ni lazima wawe na utaratibu wa kusikiliza! Lakini vilevile wananchi wengi wanapenda ushabiki sana angalieni sasa kuna watu wanashabikia kila kitu hata mabaya kwa nchi!

Viongozi wanataka umaarufu kwa kuendeleza umasikini
 
Back
Top Bottom