Wambandwa
JF-Expert Member
- Dec 3, 2006
- 2,249
- 832
Kazi gani? Hizi za visasi na wivu au kuteua wapambe watakaompigia magoti?Mwacheni Rais achape kazi!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kazi gani? Hizi za visasi na wivu au kuteua wapambe watakaompigia magoti?Mwacheni Rais achape kazi!
Hayo sio maamuzi magumu. Dalili za uwoga kwa kiongozi mwenye mtazamo kama huoJk hakuwa na Maamuzi Magumu tukasema tunataka Rais Mwenye Maamuzi Magumu
Hadi sasa JK ni shujaa!nasikia kuna mwandishi mmoja kasema tumerudi nyuma miaka 50!Jk hakuwa na Maamuzi Magumu tukasema tunataka Rais Mwenye Maamuzi Magumu
"... kikundi cha watu fulani. .. " real? pathetic!!!!!Maamuzi magumu yenye manufaa kwa taifa na sio maamuzi ya kujinufaisha binafsi kikundi cha watu fulani kama uyu anavyofanya.
haha hatari mnooKudhibiti Maandamano
Si umeona Leo Tundu Lissu na Hellen Kijo kisimba wameandamana wakiwa wameshika Mabango ndani ya Fence ya LHRC ingekuwa zamani ingekuwa Vurugu Mji Mzima
Maandamano yalianzia ndani ya Fence na yakaishia ndani ya Fence hiyo hiyo
Na tusijue kazi anayochapa - kwa mfano mazungumzo ya makinikia yamefikia wapi!Mwacheni Rais achape kazi!
Hizo ni ndoto - wait and see
Maamuzi magumu yenye manufaa kwa taifa na sio maamuzi ya kujinufaisha binafsi kikundi cha watu fulani kama uyu anavyofanya.
Porojo tu,mbona kulikuwa hakuna uwazi wa mikataba hata wabunge hawajui undani hadi baadhi ya mawaziri hawajui.Serikali ya Tanzania inadaiwa kujitoa kwa muda kwenye Mkakati wa Uwazi, Ushiriki na Uwajibikaji yaani Open Goverment Partnership(OGP). Inadaiwa Serikali imeamua kujikita kwenye "kutumbua majipu" kwanza kabla ya kujikita kwenye uwazi.
OGP ilianzishwa mwaka 2011 na ilianza na Serikali 8 hadi 70 na Tanzania ilijiunga 2011 na kutekeleza mipango kazi ya kitaifa 3 hadi sasa (3 National Action Plans).
Ahadi 7 zilizokuwa kwenye Mpango Kazi wa 3 wa Kitaifa wa OGP ni
i) Kutungwa kwa Sheria ya Upatikanaji wa Habari(Access to Information Act)
ii) Bajeti kuwa wazi(Open Budgets)
iii) Taarifa mbalimbali za Serikali kuwa wazi(Open Data)
iv) Uwazi wa masuala ya ardhi ikiwemo taarifa za umiliki wa Ardhi nchi nzima kuweza kupatikana mtandaoni(Land Transparency)
v) Uwazi katika Sekta ya Madini
Ahadi za Nyongeza
(vi) Uwazi katika Sekta ya Afya kwa ujumla(Medical and Health Service Transparency)
(vii) Kuwepo kwa mifumo ya utendaji kazi wa Serikali iliyo wazi kabisa (Performance Management Systems)
Anaandika Mbunge wa Kigoma Ujiji, Zitto Kabwe:
Nimeshangazwa na uamuzi wa Serikali kujiondoa OGP. Hivyo nimeamua kuwasilisha swali Bungeni kutaka maelezo ya Serikali, inayojipambanua kwa kupambana dhidi 11 ufisadi, kujiondoa kwenye jukwaa la Kimataifa linalopigania Serikali kuendeshwa kwa uwazi na uwajibikaji.
Uwazi ( Transparency/Openness ) ni silaha muhimu sana katika vita dhidi ya rushwa na katika kuwezesha ufanisi Serikalini.
Licha ya kwamba Tanzania ilikuwa haitimizi ahadi zote kwenye Action Plans, lakini kulikuwa na msingi kwamba Nchi yetu inaamini katika Uwazi na Uwajibikaji. Uamuzi wa Serikali kujiondoa OGP unarudisha nchi yetu nyuma. Ni uamuzi ambao haukufikiriwa Sawa sawa.
Kujua Zaidi kuhusu OGP:
Msafara wa Kikwete Brazil Kwenye Mkutano wa OGP
OGP announces 15 subnational govt that will be part of a pilot program, Kigoma Tanzania one of them
Mpango Kazi wa Kitaifa wa kuendesha shughuli za Serikali kwa Uwazi Awamu ya Tatu (OGP NAP III)