Tanzania yapata Mkopo wa Dola Mil 278 kutoka Benki ya Dunia

Tanzania yapata Mkopo wa Dola Mil 278 kutoka Benki ya Dunia

Hata baada ya "Kujitawala" sisi wenyewe, bado tuendelee tu kulaumu mfumo? Haiwezekani tukasema sisi tunataka kufanya mambo tofauti kidogo tuonavyo inafaa sisi wenyewe?

Ninajua jibulako mkuu, usihangaike kunijibu hilo swali nililouliza hapo.

Ngoja nitumie muda kidogo kutumia hoja yako hii, nami kuweka ninachoamini juu ya hali yetu hii tuliyomo.

Binafsi ninaamini lawama hasa inaanzia kwetu sisi wenyewe na viongozi wetu wanaotuongoza katika awamu mbalimbali, na hasa hasa hizi awamu za miaka hii ya karibuni.

Tunashindwa hata kufanya mambo madogo madogo yaliyomo katika uwezo wetu, kubadili hali zetu, na badala yake tunasubiri mikopo kama hii, inayojadiliwa hapa.

Wananchi wengi wanaoishi ndani ya nchi yetu sasa hivi ni zao la uhuru wa nchi yetu, wengi wamesoma shule zilizoanzishwa na sisi wenyewe, lakini zikashindwa kuwapa uwezo wa kutumia akili ya kutumia nyezo zilizo katika uwezo wao kubadili mazingira yao. Hata vyoo vya mashimo, inakuwa ni tatizo kwetu, kweli?

Zahanati na vituo vya afya vimejengwa huko vijijini, lakini hatuna uwezo wa kuvifanya vifanye kazi kwa ufanisi. Hatujiulizi inakuwaje?

Kilimo chetu kwa sehemu kubwa ni kilekile alichotuachia mkoloni! Mkulima ambaye amesoma kwenye shule tulizoziendesha sisi wenyewe, hajabadilika, miaka sitini? Tunasubiri mikopo,kama hii, na inapopopatikana, hatujui inakopitia?
Hapo mwanzo, baada ya uhuru, tulisema kukosa watu wetu wenye elimu na utaalam katika mambo mbalimbali ilikuwa ni kikwazo kwetu.
Watu wakasomeshwa, tena kwa wingi na kwa gharama kubwa. Leo hii sidhani kuna eneo ambalo hatuna watu walilolisomea ndani ya nchi hii, lakini huoni kazi za hawa watu, sana sana itakulazimu uende ndani ya CCM, na utawakuta wamejazana huko, wakifanya yao yanayowafaa wao wenyewe, na siyo kunufaisha taifa.

Viongozi wetu sasa wameamua, kwamba sisi hatuwezi kuleta maendeleo katika nchi hii, kwa hiyo njia sahihi na bora iliyopo, ni kuagiza watu toka nje, waje watuletee maendeleo!

Hakuna kiongozi anayetaka kufanya kazi na wananchi hawa, kuwatia moyo na kuwahimiza wajiletee maendeleo ya kweli. Wananchi nao sasa wanawasikiliza viongozi wao, wakisubiri waletewe maendeleo, huku raslimali za nchi yao zikizolewa kama takataka!

Sasa acha tusubiri maendeleo, miaka sitini mingine inayofuata toka sasa! Sijui kama bado utakuwa upo kuyafaidi hayo maendeleo, au vipi mkuu 'BloodofJesus'?
Daah!
 
Mfumo wa elimu yetu umekaa hovyo, haumwandai mtanzania kujitegemea kimaarifa, asipoajiriwa amekwama. Na once anapoajiriwa anawaza kuiba tu yaani kujinufaisha kibinafsi. Mtu anaitwa msomi lakini ni kwa kukariri ideas za hao hao wazungu, najua unajua kuwa huwa tunasoma kufaulu mitihani.

Unaonaje unalima mazao malighafi ambayo huwezi kuitumia. Hadi uwaombe hao hao wazungu wanunue, wasiponunua umekwama. Na wananunua kwa bei wanayokupangia.

Una mali ndani ya ardhi yako madini na vito vya thamani huwezi kuchimba hadi uwaombe hao hao wazungu waje wachimbe!

Unalazimishwa uishi watakavyo ukijidai kujitenga nao wakikupiga "vikwazo" athari zake zinakuwa dhahiri. Kumbuka kilichowatokea nchi ya Zimbabwe kipindi kile cha Mugabe kwenye ishu ya wakulima wa kizungu nchini mwake.

Ukiona tunawakopa, ujue tokea karne nyingi walishajua kuwa tutafika muda ambao lazima tutawakopa tu. "the situation that we are experiencing now is a created one by those people over there"

Nakumbuka wimbo wa mtu mmoja unasema: "the world is not my home"


Jesus is Savior
Naona mimi na wewe "tunazunguka mlemle tu" mkuu wangu 'Blood of Jesus', tunalalamikaaaaa, na hakuna tunachoweza kubadili.

Ninaamini, Katika yote haya tunayolalamikia, tungeweza kuyaweka pembeni na kuamua kufanya hata hicho kidogo kama tungekuwa na VIONGOZI wenye maono ya kuelewa tunatakiwa kufanya nini ili tujisitiri kwa kiasi tuwezacho sisi wenyewe kwa nguvu zetu.

Hakuna sababu ya kupambana na haya mapapa ya dunia, lakini tungeweza kufanya yetu bila kuyaamusha hayo mapapa yatushughulikie kama yalivyomshughulikia Mugabe.

Ninajua kuna njia nyingi za kuwahamasisha wananchi wafanye kweli katika maendeleo yao katika maisha yao ya kila siku, na kuweza kubadili hali zao za maisha kama viongozi wangeamua kulisimamia hili kwa umakini mkubwa.

Na wala sisemi kujitenga na yeyote duniani, la hasha, bali kujua jinsi ya kufanya mambo yetu kutimiza malengo ya nchi yetu bila ya misuguano isiyokuwa na lazima kuwepo.
 
Naona mimi na wewe "tunazunguka mlemle tu" mkuu wangu 'Blood of Jesus', tunalalamikaaaaa, na hakuna tunachoweza kubadili.

Ninaamini, Katika yote haya tunayolalamikia, tungeweza kuyaweka pembeni na kuamua kufanya hata hicho kidogo kama tungekuwa na VIONGOZI wenye maono ya kuelewa tunatakiwa kufanya nini ili tujisitiri kwa kiasi tuwezacho sisi wenyewe kwa nguvu zetu.

Hakuna sababu ya kupambana na haya mapapa ya dunia, lakini tungeweza kufanya yetu bila kuyaamusha hayo mapapa yatushughulikie kama yalivyomshughulikia Mugabe.

Ninajua kuna njia nyingi za kuwahamasisha wananchi wafanye kweli katika maendeleo yao katika maisha yao ya kila siku, na kuweza kubadili hali zao za maisha kama viongozi wangeamua kulisimamia hili kwa umakini mkubwa.

Na wala sisemi kujitenga na yeyote duniani, la hasha, bali kujua jinsi ya kufanya mambo yetu kutimiza malengo ya nchi yetu bila ya misuguano isiyokuwa na lazima kuwepo.
Huu mkwamo sio mdogo mkuu, labda fanya halahala Mungu akupe chance ya kuwa kiongozi mkuu wa nchi labda kuna ambalo litatokea kama unavyoamini.
 
Bora ya Samia mara 100000 kuliko yule sadist wenu aliyekuwa anakopa kimyakimya ...na kuhonga wapinzani wamuunge mkono
Kwamba kwa akili yako Samia yeye wapinzani hawaongi? Au unafikiri Zitto na Mbowe wako kimya kwa sababu wanamuogopa sana?
 
Back
Top Bottom