Tanzania yatajwa kwenye orodha ya nchi zenye mishahara mikubwa Afrika

Tanzania yatajwa kwenye orodha ya nchi zenye mishahara mikubwa Afrika

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,299
upload_2017-8-31_11-57-29.jpeg
Shirika la Numbeo limetoa orodha ya nchi kumi zenye mishahara mikubwa zaidi barani Afrika. Hili ni shirika kubwa zaidi duniani la ukusanyaji wa taarifa za majiji na nchi. Shirika hili linatoa taarifa za mara kwa mara kuhusu hali za maisha duniani ikiwemo gharama za maisha, upatikanaji wa nyumba za kupanga, huduma za afya, foleni za barabarani, uhalifu na kiwango cha uchafuzi wa mazingira.

Zifuatazo ni nchi kumi za kiafrika zenye viwango vya juu zaidi vya mshahara:

1. Libya
Libya ndiyo nchi inayoongoza barani Afrika kwa kuwa na viwango vikubwa vya mishahara. Nchi hii yenye utajiri wa mafuta imejulikana kwa zaidi ya miongo minne ya utawala wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Hayati Muammar Gaddafi na machafuko yaliyofata baada ya kifo chake. Na pamoja kwa machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini humo mpaka sasa yanayosababisha hali ya usalama kuwa tete, kiwango cha kawaida cha mshahara kwa mwezi baada ya makato ya kodi ni shilingi milioni tatu na laki nane (3,800,000)

Ingawa machafuko nchini Libya yamekuwa ni kikwazo kikubwa barani Afrika, kiwango cha hifadhi ya mafuta kwenye nchi hiyo kinachokadiriwa kuwa mapipa bilioni 48 kunaifanya nchi hiyo sio tu kuwa moja ya nchi kumi zenye utajiri mkubwa zaidi wa mafuta duniani lakini pia Serikali yake inawafurahisha wananchi kwa kuwapa viwango vya juu vya mishahara pamoja na kufanya gharama za maisha kuwa chini.

2. Zambia
Jambo kubwa zaidi litakalokufanya uhamie kwenye nchi hii isiyo na bahari ni idadi kubwa ya wanyamapori. Ina mbuga na hifadhi nyingi sana, jambo linaloweza kuwa la kuvutia sana kama moja ya vitu unavyopendelea ni kufanya safari za mbugani. Kiwango cha kawaida cha mshahara kwa mwezi nchini Zambia ni shilingi milioni tatu na laki tatu (3,300,000), na kwa hakika huu ni mshahara mkubwa kwa yeyote yule. Gharama za kodi za nyumba na maisha kwa ujumla nchini Zambia zipo chini. Pamoja na viwango vikubwa kiasi hiki, Zambia kwa sasa inapitia katika mgogoro wa kisiasa na mifumo yake ya kiuchumi na kisheria bado inafata mfumo wa uendeshaji wa kikoloni.

3. Afrika Kusini

Mwisho wa siku kila mmoja anataka kazi yenye mshahara mzuri. Nchini Afrika Kusini, kazi zinazotokana na taaluma za Sheria, Umeneja wa mifumo ya kompyuta na teknolojia, waongoza ndege, udhibiti wa mafuta ya petroli, uhandisi wa majengo na uhandisi wa programu ni baadhi ya ajira zenye mishahara mizuri zaidi nchini humo. Kiwango cha kawaida cha mshahara nchini humo ni shilingi milioni mbili na laki sita (2,600,000+), ingawa wazungu bado mpaka sasa wanaishi maisha mazuri zaidi.

4. Namibia

Uchumi wa Namibia unaendeshwa na sekta ya madini – kuchimba, kusafisha na kusafirisha kwenda nje ya nchi. Sekta ya madini inachangia asilimia 11.5 ya pato la Taifa lakini inaiingizia nchi hiyo zaidi ya asilimia 50 ya fedha za kigeni.

Pia, Namibia ni moja ya nchi tano zinazozalisha madini ya uranium kwa wingi zaidi na pia wana utajiri mkubwa sana wa madini ya almasi. Ingawa uchumi wa nchi hiyo unaathiriwa sana na kupanda na kushuka kwa soko la dunia pamoja na ukame unaoikumba mara kwa mara, mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi nchini humo ni shilingi milioni moja na laki sita (1,600,000) kwa mwezi.

5. Mauritius

Nchi hii ambacho ni kisiwa kilichopo nje kidogo ya pwani ya Kusini-Mashariki mwa Afrika kina historia ndefu ya kuwa na utulivu wa kisiasa, utawala bora pamoja na uwajibikaji wa uwazi wa Serikali yake. Ni moja ya nchi za Afrika zenye uchumi mzuri zaidi ikiwa na idadi ya watu milioni 1.3. Mshahara wa kawaida nchini Mauritius ni shilingi milioni moja na laki tano (1,500,000) kwa mwezi.

6. Tanzania
Hii ni nchi ya sita kwa nchi za bara la Afrika zenye viwango vya juu vya mshahara ambapo mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi unakadiriwa kuwa ni shilingi laki tisa (900,000). Zaidi ya nusu ya wafanyakazi nchini Tanzania wapo kwenye sekta ya kilimo kama njia kuu ya kuwasingizia kipato. Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, Tanzania imeweza kuwa na uchumi imara na unaokua kwa asilimia saba kila mwaka katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Kiwango cha umaskini kimeendelea kupungua na vita dhidi ya Rushwa inayoongozwa na Rais John Magufuli inabaki kuwa msingi imara wa ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

7. Morocco
Tangu mwezi Oktoba mwaka 2016 nchi ya Morocco imekuwa kwenye mgogoro mkubwa sana wa kisiasa. Kwa sasa, nchi hiyo ina muunganiko mkubwa wa vyama vya siasa unaojumuisha vyama sita vya siasa nchini humo. Kilimo bado kinachangia asilimia 15 ya pato la Taifa. Pamoja na nchi hiyo kukumbwa na ukame mkubwa mwaka 2016, bado waliweza kuweka rekodi ya mavuno mengi zaidi ya nafaka. Katika nchi ya Morocco, mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi ni shilingi laki tisa (900,000).

8. Zimbabwe
Mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi nchini Zimbabwe ni shilingi laki nane (800,000). Nchi hii inayoongozwa na Rais Robert Mugabe tangu kupata kwa uhuru wake inatabiriwa kuwa itaweza kuwa na uchumi bora zaidi ya sasa na kupunguza umaskini iwapo itadhibiti hali ya kisiasa na kufikia makubaliano kuhusu kufanyika kwa siasa na sera za ushindani kwenye uwekezaji.

9. Ghana
Nchi hii imepiga hatua kubwa sana kwenye kujenga demokrasia imara. Ni nchi inayosifika kwa kuwa na mfumo huru wa Mahakama pamoja na uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza kwa wananchi na wanaharakati. Mshahara wa kawaida nchini Ghana ni shilingi laki saba (700,000) kwa mwezi. Uchumi wa nchi hii unategemea zaidi sekta ya mafuta, sekta nyingine zisizo za mafuta zina mchango mdogo kwenye uchumi wa nchi hiyo.

10. Algeria
Pamoja na bei ya mafuta kuporomoka kwenye soka la dunia, bado uchumi wa Algeria uliweza kukua kwa asilimia 3.8 mwaka 2016 ingawa pia yategemewa uchumi wake utashuka kati ya mwaka 2017 na 2019. Kiwango cha kawaida cha mshahara nchini Algeria baada ya makato ya kodi ni shilingi laki sita na elfu hamsini (650,000), kiwango ambacho ni kikubwa ukilinganisha na nchi nyingine nyingi za Afrika.

Chanzo: Swahili Times
 
Limeuliza watumishi wa umma kweli?

Yawezekana wakawa wameuliza mashirika binafsi tena ya kimataifa na ma NGO ya kimataifa.

Wametembelea kweli viwanda vya wahindi, makambuni ya wachina, wahindi, wabongo wenyewe kama Sahara Media Group?

Je wameuliza watu wa aina gani hao? Au ma CEO wanaolipwa milioni 40 kwa mujibu wa Rais Magufuli.

Sina imani na huo utafiti. Hawana tofauti na TWASHINDWA ya Tanzania.
 
Inawezekana mshahara wa bosi mkuu umechangia average yetu kupanda.

Marais wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi Afrika. Top ten in (TZS).

1. John Pombe Magufuli
5th President Tanzania
Born: Tanzania 1959
Married
Children: 5
Annual: TZS 422,136,637.00
Monthly: TZS 35,178,053.00
Weekly: TZS 8,118,012.00
Daily: TZS 1,156,539.00

2. Robert Mugabe
President Zimbabwe
Born: 1924 Zimbabwe
Married
Children: 3
Annual: TZS237,451,858.00
Monthly: TZS 19,787,655.00
Weekly: TZS 4,566,382.00
Daily: TZS 650,553.00

3. Uhuru Kenyatta
President Kenya
Born: 1961 Kenya
Married
Children: 3
Annual: TZS 352,435,114.00
Monthly: TZS 29,369,593.00
Weekly: TZS 6,777,598.00
Daily: TZS 965,576.00

4. Ellen Johnson Sirleaf
President Liberia
Born: 1938 Liberia
Children: 4
Divorced
Annual: TZS197,876,549.00
Monthly: TZS16,489,712.00
Weekly: TZS 3,805,318.00
Daily: TZS 542,128.00

5. Jacob Zuma
President South Africa
Born: 1942 South Africa
Married
Children: 20
Annual: TZS 598,026,903.00
Monthly: TZS 49,835,575.00
Weekly: TZS 11,500,517.00
Daily: TZS 1,638,430.00

6. Alpha Condé
President Guinea
Born: 1938 Guinea
Married
Children: 1
Annual: TZS 48,369,823.00
Monthly: TZS 4,030,819.00
Weekly: TZS 930,189.00
Daily: TZS 132,520.00

7. Archibald Lesao Lehohla
Lesotho's Deputy Prime Minister and Minister of Home Affairs and Public Safety and of Parliamentary Affairs
Born: 1946 Lesotho
Married
Children: 2
Annual: TZS 52,923,195.00
Monthly: TZS 4,410,266.00
Weekly: TZS 1,017,754.00
Daily: TZS 144,995.00

8. José Eduardo dosSantos
President of Angola
Born: 1942 Angola
Married
Children: 7
Annual: TZS 178,253,791.00
Monthly: TZS 14,854,483.00
Weekly: TZS 3,427,958.00
Daily: TZS 488,367.00

9. Yayi Boni
President of Benin
Born: 1952 Benin
Married
Children: 5
Annual: TZS 64,386,830.00
Monthly: TZS 5,365,569.00
Weekly: TZS 1,238,208.00
Daily: TZS 176,402.00

10. Edgar Lungu
President Zambia
Born: 1956, Ndola, Zambia
Married
Children: 6
Annual: TZS 123,123,186.00
Monthly: TZS 10,260,265.00
Weekly: TZS 2,367,754.00
Daily: TZS 337,324.00

Salary Survey South Africa – Online Wage, Pay Survey at Mywage.co.za
 
Tuwe makini na hizi takwimu. Baada ya kusoma hilo imebidi nipembue kidogo.
Mshahara sio issue pekee. Tuangalie bei za vitu. Nimechukua mfano wa kilo ya sukari. Angalia huo mshahara, na bei ya kilo kwa baadhi ya nchi6

Tanzania / 900,000 / 2500 +
Zambia/ 3,300,000 / 1,309
Mauritius / 1,500,000 / 1,670
Ghana / 700,000/ 1,400

Kwa mwendo huu, wapi Kuna nafuu?
Kwa vyovyote vile, ni ghali sana Tanzania. Au kwa lugha nyepesi ni ngumu zaidi kumudu maisha Tanzania kwa mshahara
 
Ndio maana tafiti za namna hii hua nazipotezea,mshahara wa laki 9 ndio kima cha chini tangu lini? Figure ni za uongo kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inawezekana mshahara wa bosi mkuu umechangia average yetu kupanda.

Marais wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi Afrika. Top ten in (TZS).

1. John Pombe Magufuli
5th President Tanzania
Born: Tanzania 1959
Married
Children: 5
Annual: TZS 422,136,637.00
Monthly: TZS 35,178,053.00
Weekly: TZS 8,118,012.00
Daily: TZS 1,156,539.00

2. Robert Mugabe
President Zimbabwe
Born: 1924 Zimbabwe
Married
Children: 3
Annual: TZS237,451,858.00
Monthly: TZS 19,787,655.00
Weekly: TZS 4,566,382.00
Daily: TZS 650,553.00

3. Uhuru Kenyatta
President Kenya
Born: 1961 Kenya
Married
Children: 3
Annual: TZS 352,435,114.00
Monthly: TZS 29,369,593.00
Weekly: TZS 6,777,598.00
Daily: TZS 965,576.00

4. Ellen Johnson Sirleaf
President Liberia
Born: 1938 Liberia
Children: 4
Divorced
Annual: TZS197,876,549.00
Monthly: TZS16,489,712.00
Weekly: TZS 3,805,318.00
Daily: TZS 542,128.00

5. Jacob Zuma
President South Africa
Born: 1942 South Africa
Married
Children: 20
Annual: TZS 598,026,903.00
Monthly: TZS 49,835,575.00
Weekly: TZS 11,500,517.00
Daily: TZS 1,638,430.00

6. Alpha Condé
President Guinea
Born: 1938 Guinea
Married
Children: 1
Annual: TZS 48,369,823.00
Monthly: TZS 4,030,819.00
Weekly: TZS 930,189.00
Daily: TZS 132,520.00

7. Archibald Lesao Lehohla
Lesotho's Deputy Prime Minister and Minister of Home Affairs and Public Safety and of Parliamentary Affairs
Born: 1946 Lesotho
Married
Children: 2
Annual: TZS 52,923,195.00
Monthly: TZS 4,410,266.00
Weekly: TZS 1,017,754.00
Daily: TZS 144,995.00

8. José Eduardo dosSantos
President of Angola
Born: 1942 Angola
Married
Children: 7
Annual: TZS 178,253,791.00
Monthly: TZS 14,854,483.00
Weekly: TZS 3,427,958.00
Daily: TZS 488,367.00

9. Yayi Boni
President of Benin
Born: 1952 Benin
Married
Children: 5
Annual: TZS 64,386,830.00
Monthly: TZS 5,365,569.00
Weekly: TZS 1,238,208.00
Daily: TZS 176,402.00

10. Edgar Lungu
President Zambia
Born: 1956, Ndola, Zambia
Married
Children: 6
Annual: TZS 123,123,186.00
Monthly: TZS 10,260,265.00
Weekly: TZS 2,367,754.00
Daily: TZS 337,324.00

Salary Survey South Africa – Online Wage, Pay Survey at Mywage.co.za

Huu uongo ukitazama kwa umakini kama ni kweli magu analipwa kiasi hicho hiyo nafasi ya kwanza hastahili hapo zuma ndo ananstahili, check ua namba zako mkuu
 
Limeuliza watumishi wa umma kweli?

Yawezekana wakawa wameuliza mashirika binafsi tena ya kimataifa na ma NGO ya kimataifa.

Wametembelea kweli viwanda vya wahindi, makambuni ya wachina, wahindi, wabongo wenyewe kama Sahara Media Group?

Je wameuliza watu wa aina gani hao? Au ma CEO wanaolipwa milioni 40 kwa mujibu wa Rais Magufuli.

Sina imani na huo utafiti. Hawana tofauti na TWASHINDWA ya Tanzania.
Kwenye kampuni nyingi za hiyo conclusion huwa wanaipata wapi? Kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi kilichotangazwa na serikali ni Tsh 100,000(laki moja) hizo laki tisa wanalipwa watu gani wa kawaida? Mtoa mada atakuwa amepigwa chenga na kilugha kilichotumika kumfikishia taarifa hiyo! Mshahara wa laki sita ni wa mameneja!
 
Hongera umeshaingiza siku yako, usinisahau balimi moja ukishapitia malipo Lumumba
 
Back
Top Bottom