Tanzania yazuia ndege za Kenya Airways kutua nchini. Ni baada ya Kenya kutoruhusu ndege za Tanzania kubeba mizigo Kenya

Tanzania yazuia ndege za Kenya Airways kutua nchini. Ni baada ya Kenya kutoruhusu ndege za Tanzania kubeba mizigo Kenya

Kenya kilichowaumiza zaidi ni ile kufungiwa kuja kuingia mashambani na kununuwa mazao.

Tuliwadekeza sana, akaja Msomali akasema, hapana, kwenda huko.
Mbona wengine wapo wanakuja kununua mahanadi huku kiwangwa kiroho safi tu
Ila wao sasa kwao wanakuwa tofauti sana
Sema dawa yao ni kuwakazia tu watalegea wenyewe

Ova
 
JPM aliwahi kuwapiga ban kama hii akaonekana anaharibu mahusiano, kafunga nchi, hawa si watu wa kuwachekea!!. Kweli tutamkumbuka.
Wao hawakujua kwamba Kenya ndiyo wawekezaji wakubwa tz kwa nchi za afrika Mashariki? Mbali na bidhaa zao kupatikana kwenye kila duka la bidhaa muhimu mitaani. Kimbo, colgate, cadbury, omo, blueband, ice creams, panadol, menthodex, unilever, lifebuoy, palmolive, mchuzi mix, maziwa brookeside. Tukizuia na hizi watajuta kutunyìma leseni.
Bado wananunua kwetu maharage, mchele, korosho, mahindi, mpaka wanakodi mashamba ya vitunguu!! Wakileta ngebe tunachoma na vifaranga tena!
Vifaranga tusichome tuchome hizo Colgate zao na cadbury.
 
Kuna Truvks nyingi za Kenya zinafanya kazi Tanzania.Zinabeba hadi kokoto,makaa ya mawe nk
Wanaleta box za matunda na kiwanda cha kupaki matunda kipo Arusha ila yale maparachichi yanaonekana ni ya Kenya mzigo ukifungwa kwenye kontena unaenda kupakiwa Mombasa sisi tupo kimya tuu kwa sababu hatuna soko la Avocados wao wanafanya kila kitu inabidi iwe kama Ethiopia na Somalia tu wakileta heshima ndio twende sawa...
 
Kumekucha.

Kama kupata tupate wote, kwa nini unazuia ATCL isinlbebe mizigo Tanzania na kutua Kenya.

Nadhani kuna haja ya kutumia forum za kidiplomasia za EAC. Vinginevyo tuambiwe EAC imeshindwa kukutanisha viongozi wake ili kutatua mambo yao kwa amani.

======
Taarifa ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania imeeleza kuwa kwa niaba ya Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeamua kufuta vibali vya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) kuendesha safari za abiria kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia 22 Januari 2024

Taarifa hiyo imedai hatua hii ni baada ya uamuzi wa mamlaka ya anga ya Jamhuri ya Kenya kwenda kinyume na Kifungu cha 4 cha Mkataba wa Maelewano kuhusu Huduma za Ndege, kati ya Tanzania na Kenya yaliyotiwa saini Novemba 24, 2016 Jijini Nairobi

Kufuatia Uamuzi huu, hakutakuwa na safari za ndege za abiria kwa KQ kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia tarehe 22 Januari 2024.

UPDATES:
- Kenya na Tanzania kusuluhisha Mzozo wa Safari za Ndege ndani ya Siku 3

View attachment 2872698
Mabeberu hawataki ATC ya Mama ifue inatishia kuwepo kwao. Freightliner ATC ni ukombozi wa abiria na mizigo yao Kenya hawataki walizoea monopoly.
 
Kenya hufanya hujuma sana za kichini chini kufanya abiria wanaokuja Tanzania kupitia JKIA Jomo Kenyatta International Airport Nairobi kwa kuwaweka masaa kibao ili abiria hao waseme usafiri kwenda Tanzania ni mgumu sana hivyo kama masuala ya kiutalii, biashara n.k bora wamalizie Nairobi Kenya badala ya kwenda 'shamba kijijini' Tanzania ambapo usafiri wa ndege ni mgumu sana...
Noted well, sabotage! Kwa wakenya hili hufanyika kila wakati.
 
Mbona Tanzania hawakuenda kwa mahakama ya EAC kama Uganda walivyo enda huko kuwasilisha kesi ya kutumia Kenya Pipeline kusafirisha mafuta yao? Haya maamuzi yao ni ya hasira na kitoto kulipiza kisasi hivyo.
 
Mbona Tanzania hawakuenda kwa mahakama ya EAC kama Uganda walivyo enda huko kuwasilisha kesi ya kutumia Kenya Pipeline kusafirisha mafuta yao? Haya maamuzi yao ni ya hasira na kitoto kulipiza kisasi hivyo.
Tanzania ni Sovereign state, hivyo Mahakama ni sisi wenyewe, shida yako nini?
 
Back
Top Bottom