Tanzanian actor Steven Kanumba reported dead

Tanzanian actor Steven Kanumba reported dead

Lulu uliambiwa mwanangu, asiyefunzwa na ***** hufunzwa na ulimwengu. Sasa ona utaishia jela kwa kuua bila kukusudia. Umejiharibia maisha yako maana mzimu wa Kanumba hautakuacha kamwe. Haya we!!! Uliyotaka umeyapata!!!!

Jamani msimhukumu Lulu kwakuwa hilo linaweza mpata yeyote kati yetu awe mlokole, kicheche au mtulivu.
Maana nadhani alimsukuma katika kujaribu kujitetea lakini ndio hivyo hakujua kwamba siku ya Kanumba kuaga dunia ndio imefika na yeye ndiye atasababisha.
 
Picha yake ya Mwisho aliyoipost jana katika Blog yake saa 6.01 usiku:

Q3.jpg



'' KANUMBA THE GREAT PIONEER MOTO WA VOLCANO'' NIKIWA KTK OFISI ZA TANZANIA MITINDO HOUSE.

TULIOSAPOTI MPAKA KITUO HIKI KUFIKIA HAPA KILIPO SOMA MAJINA HAPO JUU JINA LANGU LIPO HAPO,KUSEMA UKWELI INAPOKUJA MAMBO YA KUSAIDIA JAMII NAJITAIDI KUTOA NINACHOKUA NACHO MAANA HAPA HUKUMBUKA MANENO YA MWANDISHI ALBERT PINE..''"What we do for ourselves dies with us. What we do for others and the world remains and is immortal."
 

Mkuu acha speculation. Funguka vema unachotaka kuandika watu wakusome vema:


  1. Movie aliyoichezea Nigera ipi na uimefanya nini? Devil Kingdom aliichezea Tanzania na Noah alishiriki.
  2. Movie yake ya Mwisho ni ay Kijiji cha tambua haki
  3. Afya yake ilikuwa na Mushkeli Mkubwa upi wakati kila siku watu wanamwona mitaani yuko fiti hata hiyo Movie yake ya Mwisho?
  4. Kama ni juu ya Ugomvi ndani ya Nyumba kulikuwa na Mdogo wake Kanumba pia. Ugomvi ule ulikuwa na Sauti na hata majirani walisikia sasa kipi ambacho watu watashindwa kuelewa?
  5. Na kanumba Amem-mock God kivipi? Movie ya Devil Kingdom alikuwa anajaribu kuonyesha kuwa utajiri wa shetani hauna upako. Hiyo ni mbaya?
  6. Mkuu, mtu kufa kwa kuanguka jambo la kawaida, hata wewe inatokea unaweza kukosa balance ukaanguka na kufa
  7. Tuache utani katika masuala ya vifo. Sijakufagilia kabisa na nakuona mtu wa ajabu sana katika hili. Si jadi yetu. Umenifanya nikuweke level ya chini sana. Wewe mwenyewe unajua utakufa kifo cha namna gani? Acha kubeza wakati taifa liko katika msiba!
Mkuu hata mimi huyu jamaa nimemshangaa sana alichokuwa anaongea...
 
Kwa sasa siyo wakati muafaka wa kulumbana, cha muhimu kama msiba haujakugusa unaweza kujikalia tu kimya.
Nikuwekee mabandiko yako hapa unayofuraiaga vifo vya watu wengine? ninashangazwa ni kipi kilichokugusa kwenye msiba wa Kanumba? Unafki ni kitu kibaya sana.
 
siku za kuishi duniani si nyingi..unaweza kup0teza uhai kwa namna y0y0te ile..ila unap0fariki mm0ja ni vema wengine tupate s0m0..p0leni sana watanzania w0te kwa kump0teza mtu alieitangaza tasnia ya uigizaji ya tanzania ndani na nje ya nchi bwana amet0a na bwana ametwaa jina la bwana libarikiwe amen!!!!!!!
 
haya mambo yanahitaji kuwa na kifua kipana....
 
Nimesikitichwa na chanzo cha kifo cha Kanumnba.
Inamaana Kanumba ameuliwa na Lulu?
 
namckia steve nyerere hapa klaudi tv. eti anasema mara ya mwisho wamekunywa pombe wote maisha klab. kwa iyo marehem alikuwa mlevi..!
RIP ong'wise Kanu

Tanzania hatuna wasanii wengi wa kujivunia!!! Sina uhakika sana na Kanumba na sioni msaada wake katika harakati za kulikomboa Taifa. Kama wengine wameishia kwenye kufunga ndoa na mafisadi huku wakijua fika wanatokea familia duni walizotelekeza.

Angekuwa mwanamziki mf. FD Q, Mw.FA, ..... au komediani kama Masanja, Joti,..... ungemwona kwenye kampeni za CCM anauza sura.
 
B3.jpg


Movie yake ya Mwisho na Jackline Wopper "Ndoa Yangu" ambayo inatarajiwa kutoka mwezi huu.
 
Wandugu, watu kama akina Kanumba nchi nyingine huwapa VIP passport na huwa wanapewa mazishi ya Kitaifa, nchi zinazotambua mchango wa wasanii hawa katika kukuza jina la taifa husika katika nchi mbalimbali duniani na hata katika maendeleo ya nchi hasa katika kuelimisha nk

J e kanumba anastahili mazishi ya kitaifa?

Hastaili
, amefanya nini kwa utukufu wa Tanzania na watanzania ukiacha wanawake ambao ni chaguo lao!
 
Tanzania hatuna wasanii wengi wa kujivunia!!! Sina uhakika sana na Kanumba na sioni msaada wake katika harakati za kulikomboa Taifa. Kama wengine wameishia kwenye kufunga ndoa na mafisadi huku wakijua fika wanatokea familia duni walizotelekeza.

Angekuwa mwanamziki mf. FD Q, Mw.FA, ..... au komediani kama Masanja, Joti,..... ungemwona kwenye kampeni za CCM anauza sura.
Hivi wewe una akili sawasawa kweli? yani ulitaka Kanumba awe anakwenda kukata mauno kwenye mikutano ya CCM ndio ungemuona ana mchango kwa Taifa? Hivi hao kina Joti wako wameshawahi kupata Airtime DSTV au kutembelea Holywood?
 
Msanii Kanumba hastahili state funeral, please!!! Kumbuka tulishawazika wacheza mpira Sembuli, Zimbwe etc na wasanii Mwinamila, Makongoro, Moses Nyunyusa etc hatujawahi kufanya state funeral. Any way, anything can happen. Kumbuka suala la Babu wa Loliondo alivyopaishwa chat wakati ule!!!
 
Nikuwekee mabandiko yako hapa unayofuraiaga vifo vya watu wengine? ninashangazwa ni kipi kilichokugusa kwenye msiba wa Kanumba? Unafki ni kitu kibaya sana.

tuache itikadi matola
rejao ni binadamu hayuko perfect kwa kila kitu.
 
Back
Top Bottom