Tanzania's GDP: Hivi tunajua hili?

Tanzania's GDP: Hivi tunajua hili?

Bw. Kamundu ,

GDP - per capita (PPP):
$1,300 (2007 est.)

Source: CIA FACTBOOK

LABDA ukijumlisha URANIUM na madini mengine toka Songea ambayo yanamilikiwa na wenye nchi na ambayo rasmi hayajaingia kwenye vitabu vya hazina na BOT!
 
Bila kujali kama nchi ni ya kibepari au kijamaa mahala pazuri pa kuanzia kuzungumza uchumi ni maandiko ya mwanzo ya Bwana Adam Smith.

Sidhani kuna ugumu kupata maandiko haya katika mtandao. Kwa hiyo mimi nitakwenda moja kwa moja kwa hoja ambayo nataka kuitumia kama msin gi wa kuanza kujenge taifa lilillo makini na linalojizatiti kuongeza GDP per capita yake mwaka hadi mwaka. . Hili sio jingine ila zile njia ambazo Adam Smith alizozianisha kwamba ndizo zinazosaidia kuongeza utajiri wa nchi. Kwa maneno mengine, unapozungumzia GDP per capita, unazungumzia jinsi ya kuzalisha au kuongeza utajiri nchini mwako. Ni vigumu kwa kweli kuoongeza GDP per capita kama nchi yenu imechukua likizo ya kuongeza utajiri wa nchi na badala yake inakwiba fedha ndogo ilipo Hazina kwa matumizi na matanuzi binafsi.

Adam Smith aliandika kitabu kilichoitwa: ' An Inquiry into the Nature and Causes of the Wealth of Nations.' Lengo lake lilikuwa ni kuanzisha mjadala kuhusu kwanini baadhi ya nchi duniani zinaendelea kiuchumi na kuwa na maisha mazuri kwa watu wake lakini nyingine zinaogelea kwenye dimbwi la umasikini mkubwa? Akagundua, kwanza, kwamba ni maendeleo ya kiuchumi peke yake ndiyo yanayoweza kuufagia pembeni umasikini.

Haikuwa vigumu kupata sababu za umasikini wa watu na nchi. Nchi nyingi Ulaya wakati huo zilikuwa masikini wa kutupwa kama Tanzania ilivyo leo. Lakini kazi ilikuwa kupata sababu zinazochangia nchi kuwa tajiri.

Kwa mujibu wa Adam Smith yafuatayo ni baadhi ya mambo yanayoweza kusaidia nchi kuzalisha mali au utajiri kwa wingi zaidi na hivyo nchi kuwa na hali bora zaidi ya kiuchumi na maisha kwa watu wake:

. kuongezeka kwa rasilimali zilizopo nchini (lakini pale tu rasilimali hizo zinapoingia kwenye Mfuko au Hazina ya nchi na sio kwenda nje),
. Ugunduzi au uvumbuzi wa teknolojia mpya ( hili linawezekana kwa nchi iliyo na fungu la Research and Development na linalowasaidia na kuwanyanyua watu waliosoma na wasiosoma mara wanapogungua kitu fulani badala ya kuwakwaza kwa kisingizio chochote kile),
. kuongezeka kwa mgawanyo wa kazi na uzamili au ubingwa katika shughuli mbalimbali ( pale ambapo mwalimu inampasa awe mkulima, mfugaji, mfanyabiashara na kadhalika ni vigumu hili kuwezekana),
. kuongezeka kwa njia bora za mgawanyo na matumizi ya rasilimali katika nchi (kama asilimia kubwa ya rasilimali za nchi inakwenda katika kununua magari ya kifahari, au kulipia mafuta -kitu ambacho kinaendelea na ghali zaidi- au safari na misafara ya kwenda nchi za nje haiishi basi rasilimali zinakosekana katika kuwekeza kwenye maeneo ambayo yangelichangia kuondoa umasikini nchini), na
. kuongezeka kwa kiwango cha matumizi ya rasilimali zilizopo (katika lugha ya menejimenti kuna maneno mawili muhimu. Nayo ni 'effectiveness' na 'efficiency'. 'Effectiveness' ni kuzalisha kile kinachotakiwa na kukubalika na soko, wakati 'efficiency' ni kuzalisha kwa usahihi au kwa gharama inayokubalika. Tuna matatizo katika yote mawili. Na maneno haya mawili yatakuwa yakijirudia tena na tena kadri tunavyoendelea na mazungumzo yetu ya uchumi. La muhimu hapa ni kwamba watu wawili wanaweza kuwa na rasilimali kiasi kile kile lakini mmoja akawa more effective and more efficient na hivyo kutajirika na mwenzake akabaki palepale. Japan haina rasilimali yoyote ya maana ukilinganisha na Tanzania zaidi ya watu wake. Hivi leo ukiwatoa Wajapani wote toka Japani na kuwapeleka Watanzania wote Japani na Wajapani wote wakaja Tanzania kwa sababu ya Watanzania kutomudu effectiveness and efficiency Japan itamasikinika na Tanzania (Ya Wajapani wakati huo ) itatajirika.

Tumeona sababu alizozianisha Mzee Adam Smith, Je, mwenzangu kwa kuangalia hali ya dunia sasa, uchumi wetu ulipo na aina ya uongozi tulion nao unaweza ukaongeza njia nyingine ambazo kwazo nchi inaweza ikatajirika kabla ya mimi kufanya hivyo kwenye makala ijayo? Karibu! Kumbuka usipotumia ni sawa na kama umeingiza au umeongeza kipato pia!
 
PUNDIT

NAAM, hakika ni kazi kujua ni wapi siasa inapoanzia na kuishia na wapi kwa upande mwingine uchumi unapoanzia na unapoishia. Lakini ni rahisi vilevile kujua kuwa nchi inaendeshwa kama nchi inayotanguliza mbele uchumi au inayotanguliza mbele siasa. Tiofauti ya nchi mbili hizi ni kuwa ya kwanza huwa inatesa na pili huwa inateswa!

Lengo la kuanza kunyambua suala hili katika wizara ni kuhakikisha tunapata kazi au majukumu yaliyopo katika nchi kama yalivyo chini ya wizar ahusika. Hili halitatuzuia kuonesha kuwa hatima ya yote ushiriki na ushirikishwaji watu katika kufanya ndoto zilizopo katika maandishi ziwe kweli ni kitu kisichoepukika katika oganaizesheni au jamii yoyote ile hapa ulimwenguni.

Hilo la kwamba nchi hii haiendelei kwa sababu viongozi walio juu hawawajui wananchi walioko chini ni hoja nzito na ambayo hali ya nchi inaweza ikawa ushuda wa kutosha kuonesha kuwa wanaokuja madarakani hawaji kwa lengo la kukunufaisha wewe bali kwa lengo la kujinufaisha wao wenyewe.

Ili nchi iendelee katika nchi yoyote ile VIONGOZI wanapaswa kuchukua EDA ya miaka kadhaa (Kawaida huwa mitatu au minne) huku wakiumua nguvu na rasilimali za nchi ili kwanza kuiweka nchi angalau katika utajiri wa GDP per capita ya dola 2,500.

Eda huwa ni kwa viongozi kujinyima mishahara mikubwa na safari za nje na matanuzi mengine ili wananchi wawe na hali nzuri zaidi kabla ya wao viongozi kuanza kula.

Hili limekuwa gumu kwa viongozi wengi Afrika lakini ndicho kilichofanyika Korea Kusini, Malaysia, Singapore, Botswana na sasa kinafanyika huko Vietnam, Cambodia na Uchina.
 
TANGO,

It takes two to tangle, but one to dangle or hang see here please:

Somo kubwa hapa ni kwamba kuna wanauchumi aina mbili. Wasema kweli na wasema uongo.

Yaani kuna TBC na Redio Uhuru, halafu kuna Redio private na televisheni private.

Angalau sasa tuna nafasi ya kuchagua na kusema hata siku moja sintosikiliza TBC au Redio Uhuru lakini ujue kuna wana nani na wana nanihino ambao wao watasikiliza na ndicho watakachowafunza wananchi huko vijijini ambako FM hazijaona ndani.

UKWELI wazungu wanasema: 'The proof of the pudding is in eating,' kama sijakosea. Yaani ukitaka kujua utamu wa chachandu ni kwenye kula na sio vinginevyo. Hivi wewe na akilizangu kama zangu utakubali uchumu UNAKUA wakati wewe tumbo linavia???

HAKUNA mwanauchumi yeyote msema kweli na mchanga Mungu anaweza akapendwa na serikali kama yetu. Maana hawa wamezaliwa kwenye uongo, wamelelewa kwenye uongo na watakaufa kwenye uongo tu!

FUNGUA macho na mfuatilie Mtanzania huyu aliyeamua kutufungua macho sisi wakina naninhino tulidhani eti uchumi ni ALCADABRA ya ajabu au mazingaombwe kumbe ni kitu rahisi kweli kikielezwa kwa Kiswahili fasaha kama cha Bwana huyu.

Mimi Sammy Sr. wangu, simuachi na mkurugenzi wa JF hakikisha unampamba, kumtia moyo na kumwachia ukumbi atuelimishe sisi wajinga wa nchi hii katika masuala ya uchumi.

NA KINACHOTISHA sasa hivi ni kuwa na nchi yenye chama tawala ambacho hakina hata MCHUMI mmoja mwenye jina duniani wakati asili ya nchii ni kutoa wachumi wenye majina kama Profesa rweyemamu. Malima, Mbilinyi, Amani na kadhalika!
 
KUONESHA KUWA CCM akili ziliwahama kwa muda, hebu angalia baada ya yote sasa wamezuka hao hao CCM na mawakala wao kuanzisha kila aina ya mifuko ya Umoja, ya Ushirikiano, ya Kujikimu na kadhalika.

Mifuko yote hii ilistahili kuanzishwa ili wananchi wamilikishwe uchumi wao wakati ule badala ya kuaifisha vitega uchumi vilivyoorodheshwa na Mheshimiwa Tango.

Sasa angalia kichekesho hiki jamani, eti tuliambiwa mashirika enzi hizo yalikuwa yetu, yaani , mashirika ya umma. Lakini nani anayejua baada ya kutaifishwa mali zote nani kala. Ninachojua mimi ni kuwa sisi wote kina yakhe tumekosa. Na kwa hili naomba kufungua kesi ya kuishtaki serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa kuiba na kurusha mali ya umma kwa niaba yenu Watanzania.

Hii ni miaka ya uwazi na pengine hiyo neema kwa wote inaweza kutujia sisi na wastaafu wa EAC, Walimu, Madaktari, wachoma jua saa zote za mchana, polisi, kwa maneno mengine kwa kuishtaki serikali kwa KUIBA NA KULA MALI YA UMMA mnasemaje wenzangu????

Na maalibino nao wakaishtaki kwa kushindwa KUWALINDA wao kama raia wa nchi hii, walipa kodi na binadamu chini ya haki za binadamu kwa sharia za umoja wa mataifa.


Ni Mimi Akili Mingisana
 
Sammy Jr,
Kwa mujibu wa Adam Smith yafuatayo ni baadhi ya mambo yanayoweza kusaidia nchi kuzalisha mali au utajiri kwa wingi zaidi na hivyo nchi kuwa na hali bora zaidi ya kiuchumi na maisha kwa watu wake:

1. kuongezeka kwa rasilimali zilizopo nchini (lakini pale tu rasilimali hizo zinapoingia kwenye Mfuko au Hazina ya nchi na sio kwenda nje),
2. Ugunduzi au uvumbuzi wa teknolojia mpya ( hili linawezekana kwa nchi iliyo na fungu la Research and Development na linalowasaidia na kuwanyanyua watu waliosoma na wasiosoma mara wanapogungua kitu fulani badala ya kuwakwaza kwa kisingizio chochote kile),
3. kuongezeka kwa mgawanyo wa kazi na uzamili au ubingwa katika shughuli mbalimbali ( pale ambapo mwalimu inampasa awe mkulima, mfugaji, mfanyabiashara na kadhalika ni vigumu hili kuwezekana),
4. kuongezeka kwa njia bora za mgawanyo na matumizi ya rasilimali katika nchi (kama asilimia kubwa ya rasilimali za nchi inakwenda katika kununua magari ya kifahari, au kulipia mafuta -kitu ambacho kinaendelea na ghali zaidi- au safari na misafara ya kwenda nchi za nje haiishi basi rasilimali zinakosekana katika kuwekeza kwenye maeneo ambayo yangelichangia kuondoa umasikini nchini), na
5. kuongezeka kwa kiwango cha matumizi ya rasilimali zilizopo (katika lugha ya menejimenti kuna maneno mawili muhimu. Nayo ni 'effectiveness' na 'efficiency'. 'Effectiveness' ni kuzalisha kile kinachotakiwa na kukubalika na soko, wakati 'efficiency' ni kuzalisha kwa usahihi au kwa gharama inayokubalika.

Tuna matatizo katika yote mawili. Na maneno haya mawili yatakuwa yakijirudia tena na tena kadri tunavyoendelea na mazungumzo yetu ya uchumi. La muhimu hapa ni kwamba watu wawili wanaweza kuwa na rasilimali kiasi kile kile lakini mmoja akawa more effective and more efficient na hivyo kutajirika na mwenzake akabaki palepale. Japan haina rasilimali yoyote ya maana ukilinganisha na Tanzania zaidi ya watu wake. Hivi leo ukiwatoa Wajapani wote toka Japani na kuwapeleka Watanzania wote Japani na Wajapani wote wakaja Tanzania kwa sababu ya Watanzania kutomudu effectiveness and efficiency Japan itamasikinika na Tanzania (Ya Wajapani wakati huo ) itatajirika.

Mkuu shukran kubwa kwa kutupa kipande hicho na Inshaallah, leo jioni nikipata muda nitazungumzia zaidi kuhusiana na biashara ya dunia hii. Hao wenzetu wanafanya kitu gani ambacho sisi na hasa nchi zenye wananchi wenye roho maskini wameshindwa kufanya..
 
Tumeona katika sehemu iliyopita kwamba nchi inaweza ikatajirika au kinyume chake kuondokana na umasikini kwa kufanya mambo kadhaa. Baadhi yake yalikuwa:
. kuongezeka kwa rasilimali zilizopo nchini,
. kugundulika kwa teknolojia mpya,
. kuongezeka kwa kiwango cha matumizi ya rasilimali nchini,
. kuongezeka kwa mgawanyo wa kazi na uzamili, na
. kupanuka na kuboreshwa kwa mgawanyo wa rasilimali katika nchi.

Kwa yakini ukitaka kutathmini mafanikio ya serikali yoyote duniani basi unastahili kuanzia hapa.

Hata hivyo, sintojiingiza sasa hivi katika kutathmini utendaji kazi wa serikali iliyoko madarakani. Hilo kwa sasa nakuachia wewe kwa kuangalia kama serikali yako imemudu kiasi gani kufanya hayo hapo juu yawezekane hapa nchini.

Kwa leo, ninapenda kuuliza je, hizo hapo juu ndio njia pekee ambazo nchi inaweza ikaongeza utajiri wake au kupunguza umasikini wake? Nina hakika jibu lenu litakuwa la hasha!

Hebu tujiulize ni njia gani nyingine ambazo tunaweza kuongeza uzalishaji mali, huduma na hivyo utajiri nchini na wakati huo huo kupunguza kabisa umasikini wa kutisha?

Unaweza ukauliza swali au maswali juu ya hili kwa kutumiia muundo wa serikali au maeneo ya kijiografia au maeneo ya uchaguzi au kisekta, kwa maana ya kilimo, uvuvi, ufugaji, viwanda, biashara, ajiranchizanje, huduma na bila kusahau michezo na muziki.

Hata hivyo, mimi nitauliza kijumla jumla tu kwa kuuliza, je, tunaweza kuongeza uzalishaji mali, utoaji huduma na biashara na hivyo kuongeza utajiri wetu kwa njia hizi:

. kuigeuza serikali a 'Learning Organization' yaani tufanye mamboyetu yaendeshe vizuri kiasi cha kutamanisha serikali zingine kutuma watumishi wao kuja kujifunza uendeshaji serikali nchini kwetu?

. Kugeuza baadhi ya Wizara nchini kuwa Agencies ili sio tu kuongeza ufanisi bali kupunguza gharama za uendeshaji serikali na pengine kuwa katika nafasi ya kuliingizia taifa kipato cha uhakika? Masuala ya kiutawala kama ya Muungano/Afrika Mashariki,Serikali za mikoa na mitaa, Utumishi, Bunge na Mazingira mathalani yanaweza kuendeshwa na agencies kwa ufanisi zaidi kuliko kuwa Wizara kama ilivyo sasa?

. Kutumia balozi zetu kama vituo vya 'intelligence' kuhusu mbinu mpya za kiuchumi, biashara, fedha na rasilimali watu ili tufyonze vilivyo muhimu na kuvitumia haraka kwa maendeleo yetu?

. kutumia balozi zetu kama 'branch' za kibiashara katika kusaidia Watanzania bila upendeleo au ujanja ujanja ili waweze kununua na kuuza vitu nje kwa urahisi?

. Kuzihamasisha benki zetu kufungua matawi nje ya nchi?
. Kurahisisha taratibu za uanzishwaji SACCOS kwa kuondoa masharti magumu wakati wa uanzishwaji SACCOS. Wengi wanakata tamaa kwa sababu wanachama waanzilishi wanashindwa kuweka fedha benki mpaka wapate hati ya SACCOS. Je, hivi ni big deal kuwa na Akaunti ya Muda ili watu waendelee kuaminiana na kulipa au kuweka wanachostahili kwenye akaunti ya SACCOS tarajiwa?
. Kutoa upendeleo kwa benki zinazowakopesha wakulima, wafugaji, wavuvi, wafuga nyuki, wachimbaji madini wadogowadogo na wafanyabiashara na nchi za nje wadogowadogo?
. Uanzsihwaji wa viwanda vidogo vijijini?
. Kununua bidhaa na vifaa toka nje na kuviuza kwa majirani zetu na hususan Kongo, zambia, Malawi, Rwanda, Burundi na kadhalika,
. Kuwashirikisha watu kwa kuwalipa na kuhakikisha wanacholima hakikwami njiani au mashambani bali kinasafirishwa kwa urahisi hadi masoko ya ndani au nje?
. Kuwa na wakala wa maendeleo ya viwanda, wakala wa maendeleo ya biashara ya ndani na nje?

. ATC kuachana na ndege za abirria na kuwa na mijidege mikubwa ya kusafirisha mizigo toka Uarabuni na uchina kuja Tanzania na kinyume chake?
. Kuigeuza Tanzania na hasa miji yetu ya mipakani kama Holili, Horohoro, Mtukula, Isaka, Tunduma, Mbamba Bay, Taveta, Namanga na kadhalika kuwa MASOKO makubwa ya kimataifa kwa kugeuza border posts zetu kuwa kama vile viwanja vya ndege vya kimataifa kwa kuwa na majengo makubwa ya maduka na bohari?

. Kuwa na Wakala wa Umwagiliaji Maji?

. Kurahisisha ubia kati ya wakulima nchini na watu au wakulima wa nje?

. Kuwa na meli za kisasa za uvuvi katika mito, maziwa na bahari zetu?

. Kwa Kampuni za dhahabu, almasi, tanzanite, ruby na kadhalika kulipa royalty kubwa zaidi inayotosha kuipa BOT/Hazina uwezo wa kukidhi mahitaji madogo madogo kama gharama za elimu kwa watoto wetu na ziada ya kuwakopesha wazawa?

. Kufanya miji na vijiji vyetu safi zaidi na hivyo kufanya watalii kukubali kuvitembelea kwa urahisi zaidi,

. Kuhakikisha mali asili yetu inauzwa kwa bei nzuri na kuna uwazi katika biashara hii,

. Hotelii na huduma zingine za kiswahili kama vile usafiri vinaimarishwa na hivyo kuipa nchi hadhi bora zaidi machoni mwa wageni na hususan watalii,

. kuanzisha shughuli za utafiti & Maendeleo kwa madhumuni ya kugundua, kuzalisha na kusambaza nishati mbadala vijijini?

. Kuhakikisha fedha zinazotojka mabarabarani zinarudi kukarabati barabara na sio vinginevyo?

. Kuhakikisha tunakuwa na bandari tatu kama sio nne zinazofanya kazi usiku na mchana bila wizi wala kuinyima serikali mapato ya kodi?

. Kuongeza matumizi ya teknohama kiwango cha kufikia kuwa tunaweza kupunguza gharama zinazotokana na safari, barua na mikutano isiyo na sababu za kutosha,

. Kuanzisha SAMPULI za miradi ya sayansi & teknolojia ili vijana wetu waweze kuiga na kupitia elimu ya ujasiliamali na menejimenti ya biahsara waweze kuanzisha shughuli za kiuchumi zinazoendana na vitu hivyo?

. Kuongeza ubora wa maisha ya walimu na wahadhiri na ubora wa vyuo na shule zetu ili tupate wanafunzi toka nchi za nje?
. Kuongeza ubora wa maisha ya madaktari, manesi na wafanyakazi wa mahospitali na ubora wa vifaa, mitambo na huduma za hospitali zetu ili tuweze kupata wagonjwa toka nchi za nje kwa wingi zaidi?

. Kurahisisha ujenzi wa nyumba kwa kila familia ya Kitanzania?

. Kuifanya miji yetu iwe mizuri na safi zaidi siku zote?


. Kuhakikisha vyombo vyetu vya habari-redio na magazeti vinasikika hadi nje ya nchi na hivyo kupata uwezekano wa matangazo toka nchi za nje?

. Kuwa na magazeti na vitabu vinavyoweza kuuzwa hadi nchi za nje?

. Kuuza au kuruhusu kwenda nje wanamichezo na wanamuziki wengi iwezekanavyo nchi za nje?


. Kuangalia vipengee mbalimbali vya utamaduni wetu vinavyoweza kutumika kutuongezea heshima na mapato zaidi vikitumika kifundi na kwa ustaarabu zaidi?

. Kuhakikisha wahalifu au wenye kufanya makosa mbalimbali barabarani na kwingineko wanalipishwa faini zitakazochangia mifuko yetu ya maendeleo?

. Tunaboresha mbinu za ufugaji na uvivu na hivyo kuwa na biashara nzuri zaidi katika sekta hii?
 
UMUHIMU wa wewe kuchangia mazungumzo haya ni kwamba, chukua mathalani, hili suala la mgawanyo wa kazi na uzamili au kuwa stadi katika fani fulani. Sio rahisi kama linavyoonekana hapa. Utakuta mgawanyo huu wa kazi unashuka hadi kwenye ngazi ya mkoa na wilaya.

Pamoja na watu kugawiwa kazi na majukumu na kubwa mabingwa wa hiki au kile je, wilaya na mkoa nao unaweza ukagawiwa kazi fulani fulani na kuwa bingwa katika eneo fulani?

Au wote na mikoa na wilaya zote tunastahili kufanya yote tu kwa kuwa ndivyo tulivyo au ndivyo tulivyokuta mambo yakifanyika?

Kuna mkoa au mikoa au wilaya zinazoweza kuwa nambari wani katika utalii? uvuvi? nyama ya ng'ombe? maziwa? matunda? viwanda vidogo vidogo? huduma ya elimu? huduma ya afya? usafi? usafirishaji na uchukuzi ? benki na fedha? madini? mafuta? umeme wa jua? na kadhalika na kadhalika? Nini faida ya hili? Nchi itapigaje hatua mbele? Nini hatari au udhaifu wa mbinu hii? Yote haya ni michanuo tu ya mazungumzo endelevu ya uchumi. Mazungumzo yanayooanza lakini vigumu kwisha!
 
" UMUHIMU wa wewe kuchangia mazungumzo haya ni kwamba, chukua mathalani, hili suala la mgawanyo wa kazi na uzamili au kuwa stadi katika fani fulani. Sio rahisi kama linavyoonekana hapa. Utakuta mgawanyo huu wa kazi unashuka hadi kwenye ngazi ya mkoa na wilaya.

Pamoja na watu kugawiwa kazi na majukumu na kubwa mabingwa wa hiki au kile je, wilaya na mkoa nao unaweza ukagawiwa kazi fulani fulani na kuwa bingwa katika eneo fulani?

Au wote na mikoa na wilaya zote tunastahili kufanya yote tu kwa kuwa ndivyo tulivyo au ndivyo tulivyokuta mambo yakifanyika?

Kuna mkoa au mikoa au wilaya zinazoweza kuwa nambari wani katika utalii? uvuvi? nyama ya ng'ombe? maziwa? matunda? viwanda vidogo vidogo? huduma ya elimu? huduma ya afya? usafi? usafirishaji na uchukuzi ? benki na fedha? madini? mafuta? umeme wa jua? na kadhalika na kadhalika? Nini faida ya hili? Nchi itapigaje hatua mbele? Nini hatari au udhaifu wa mbinu hii? Yote haya ni michanuo tu ya mazungumzo endelevu ya uchumi. Mazungumzo yanayooanza lakini vigumu kwisha!"

TUKIWA na GDP per capita ya angalau $1,000 hadi 2,000 tutakuwa sawa na nchi hizi:



Na Nchi GDP pc Makadirio ya mwaka:

169 Pakistan $ 2,100 2003 est.
170 Micronesia, $ 2,000 2002 est.
171 Angola $ 1,900 2003 est.
172 Zimbabwe $ 1,900 2003 est.
173 Sudan $ 1,900 2003 est.
174 Burma $ 1,900 2003 est.
175 Bangladesh $ 1,900 2003 est.
176 Cameroon $ 1,800 2003 est.
177 Mauritania $ 1,800 2003 est.
178 Mongolia $ 1,800 2003 est.
179 Moldova $ 1,800 2003 est.
180 Solomon Islands $ 1,700 2001 est.
181 Gambia, The $ 1,700 2003 est.
182 Uzbekistan $ 1,700 2003 est.
183 Cambodia $ 1,700 2003 est.
184 Laos $ 1,700 2003 est.
185 Haiti $ 1,600 2003 est.
186 Iraq $ 1,600 2003 est.
187 Marshall Islands $ 1,600 2001 est.
188 Senegal $ 1,600 2003 est.
189 Kyrgyzstan $ 1,600 2003 est.
190 Togo $ 1,500 2003 est.
191 Cape Verde $ 1,400 2002 est.
192 Uganda $ 1,400 2003 est.
193 Nepal $ 1,400 2003 est.
194 Cote d'Ivoire $ 1,400 2003 est.
195 Bhutan $ 1,300 2002 est.
196 Rwanda $ 1,300 2003 est.
197 Djibouti $ 1,300 2002 est.
198 Chad $ 1,200 2003 est.
199 Mozambique $ 1,200 2003 est.
200 Sao Tome and $ 1,200 2002 est.
201 Central African $ 1,200 2003 est.
202 Benin $ 1,100 2003 est.
203 Tuvalu $ 1,100 2000 est.
204 Burkina Faso $ 1,100 2003 est.
205 Kenya $ 1,000 2003 est.
206 Korea, North $ 1,000 2003 est.
207 Tokelau $ 1,000 1993 est.
208 Tajikistan $ 1,000 2003 est.
209 Liberia $ 1,000 2003 est.
210 Mali $ 900 2003 est.


KUNA yepi tunayojifunza kutokana kwanza na takwimu hizo hapo juu na jinsi nchi zenyewe zilivyo na kile ambacho wao wanakifanya kwa sasa? Kuna mabalozi wetu huko au wanafunzi wa Kitanzania huko basi watueleze angalau kwa uchache tu?
 
Tanzanian families getting richer, report says
DASSU STEPHEN
Daily News; Wednesday,November 19, 2008 @21:15

Income poverty at the household level has significantly decreased among Tanzanians over the past six years, Deputy Minister for Finance and Economic Affairs Jeremiah Sumari has said. Sumari quoted recent studies in Dar es Salaam yesterday indicating a significant segment of the local population who could not afford basic needs had gone down to 33.2 per cent - from 35.7 per cent between 2001 and 2007.

The deputy minister was speaking during an official opening of a three-day consultative meeting on a National Strategy for Growth and Reduction of Poverty (NSGRP) and Public Expenditure Review (PER). Mr Sumari also said the studies had also shown that food availability was also rising: some 19 out of 100 people in 2007 were able to cater for their food needs as compared to 16 out of 100 people in 2001.

Local experts also say the Gross Domestic Product (GDP) in the country is reported to have increased from 6.7 to 7.1 per cent within the same period of time. The other sectors which have in recent past witnessed a significant improvement included education, health, tourism, infrastructure and communication, said Mr Sumari.

He reiterated that the government through the 2025 development vision will continue to improve living standards among its people in all aspects of life. Speaking in the same occasion, a representative of development partners, Ambassador Tim Clarke, stressed a need for people's participation and good governance as a requisite in fighting poverty among the grassroots. "It very important to make effective and efficient use of public resources….. Dialogue that includes all key stakeholders is also very important in promoting people's development and public ownership," he noted.
 
Wananchi waliosikiliza hii habari watakuwa wameumizwa sana. Katika sehemu ya taarifa hii, alionekana pia huyo mzungu (Tim Clarke) akiongea. Kumuona huyo mzungu katikati yao ilinimaliza nguvu kabisa.




.
 
"Tanzania is a predominantly rural country that is experiencing rapid urban growth. There is a high instance of poverty, and Tanzania is consistently ranked by the annual UN Human Development Index as one of the 20 least-developed countries in the world in terms of the citizens' quality of life. With UN estimates of up to 89 percent of the population living on less than $2 per day, it is not surprising that poor housing conditions are prevalent in both the rural and urban areas of Tanzania..............."

source: Tanzania -- Habitat for Humanity Int'l
 
Tanzanian families getting richer, report says
DASSU STEPHEN
Daily News; Wednesday,November 19, 2008 @21:15

Income poverty at the household level has significantly decreased among Tanzanians over the past six years, Deputy Minister for Finance and Economic Affairs Jeremiah Sumari has said. Sumari quoted recent studies in Dar es Salaam yesterday indicating a significant segment of the local population who could not afford basic needs had gone down to 33.2 per cent - from 35.7 per cent between 2001 and 2007.

The deputy minister was speaking during an official opening of a three-day consultative meeting on a National Strategy for Growth and Reduction of Poverty (NSGRP) and Public Expenditure Review (PER). Mr Sumari also said the studies had also shown that food availability was also rising: some 19 out of 100 people in 2007 were able to cater for their food needs as compared to 16 out of 100 people in 2001.

Local experts also say the Gross Domestic Product (GDP) in the country is reported to have increased from 6.7 to 7.1 per cent within the same period of time. The other sectors which have in recent past witnessed a significant improvement included education, health, tourism, infrastructure and communication, said Mr Sumari.

He reiterated that the government through the 2025 development vision will continue to improve living standards among its people in all aspects of life. Speaking in the same occasion, a representative of development partners, Ambassador Tim Clarke, stressed a need for people's participation and good governance as a requisite in fighting poverty among the grassroots. “It very important to make effective and efficient use of public resources….. Dialogue that includes all key stakeholders is also very important in promoting people’s development and public ownership,” he noted.


No they are not, selective reading and quoting from the report. In fact the absolute number of poor people increased by 1.3 million between 2000/01 and 2007 thanks in part to an uncontrolled population increase.
 
From most of the posts above there appears to be an inherent need for a lesson on understanding national accounts data. GDP calculations only tell you the market value of final goods and services produced in an economy in a given period of time. From this figure alone, there isn't much one can deduce about the finer meaningful points regarding the aspect of life, income generation, productivity, factor markets, etc to name but a few.
 
Jamani tuko kwenye "Information Age" tusichemshane kwa data za 2003 na kutoka kwa taasisi zisizo na "Authority".

Utafiti rahisi kwenye wikipedia utakupa data za IMF na World Bank za 2007
Siitetei Tanzania, bali tufanye mjadala wenye mtazamo sahihi.
 
Ni kweli kwamba gdp sio nzuri katika kusema ni nchi ipi tajiri au masikini mfano equatorial guinea wanairank ya pili duniani kwa utajiri zaidi ya usa ambapo si kweli;lakini watanzania tuna mengi tunayodaiwa kwa habari ya uchumi:kwani maisha ya mtu wa kijijini na mtu wa dar nitofauti kubwa sana je unajua kuwa kuna watu wanalala chumba kimoja na mifugo,wanashinda kwa mlo mmoja kwa siku:
 
GDP kisiwe kipimo pekee cha kusema nchi gani ni tajiri zaidi duniani na nchi gani ni masikini wa kutupa.
Watu wa development studies wana kitu wanaita INDICATORS OF DEVELOPMENT,ambayo ina vitu vingi ma hiyo GDP ikiwa ni kasehemu tu ambavyo kwa pamoja ndivyo vinapima uwezo wa kimaendeleo wa nchi tofauti.
Kuna vitu kama huduma za kijamii kwa mfano shule,hospitali,zahanati,maji safi na salama,kuna walimu wangapi katika nchi,uwiano wa madaktari na wagonjwa,vitanda hospitalini nk
Kuna vitu kama miundombinu,barabara,reli,,anga,simu,mzunguko wa pesa,upatikanaji wa ajira,nk nk
Mambo yako mengi.Kwahiyo unaposema GDP pekee ndiyo kipimo cha maendeleo,si kweli.Inabidi uziangalie hizo indicators zote halafu ndiyo utupangie list ya matajiri na masikini.
Halafu hiyo GDP yenyewe inatafutwaje?iko even?Nchi kama Luxembourg ina watu wasiozidi 500,000(laki tano),hiyo population ni kama mara sita ndiyo ifikie population ya watu wa jiji la Dar Es Salaam kwa mfano.Sawasawa na Rwanda na Burundi ambazo nazo zina idadi ndogo ya watu.
Manake kanchi kenye watu wadogo kama Luxembourg,ni sawa na mkoa fulani wa Tanzania au mji fulani wa Marekani au nchi nyingine kubwa.ukikafanyia hiyo GDP ni sawa labda kwa mfano ufanye GDP kwa sehemu nyingine kwa uwiano huohuo.Kwamfano ukifanya GDP ya mkoa wa Dar Es Salaam,utapata nzuri sana zaidi ya hiyo 600.
Kwahiyo point hapa ni hiyo uneven distribution of incomes in different parts of different populations in a big country like Tanzania.
Ndiyo utaona bajeti ya ulinzi ya Marekani ni zaidi ya bajeti ya nchi tano za ulaya lakini kwenye GDP inashika nafasi ya 2/3/5
Kwahiyo usidanganyike na hizo figure mkuu[/QUOTE



NAKUUNGA MKONO MZEE

Mimi pia sikubaliani na matumizi ya GDP kama kipimo pekee cha umaskini/utajiri. Utafanya kazi kubwa sana kunishawishi kuwa hicho ni kipimo sahihi cha hali nzuri ya maisha. Ethiopia ni nchi iliyochoka sana ukiangalia hali ya maisha kwa sababu taarifa za watu kufa yaani kudead kwa njaa ni ya kawaida sana. Huku mashuleni tunasoma nao na wanaonekana na hali mbaya sana na wanasema wazi jinsi ambavyo hali kimaisha nchini kwao ni duni. Mshahara wa university graduates kwenye public sector mshahara wao ni dola 250 kwa mwezi, hela ambayo si kwamba itanunua vitu vingi kuliko vile amabavyo inenunua Tanzania. Kimsingi tusidumazwe akili na kujiona hatuwezi kabisa eti kwa sababu ya GDP. Hizo ni hadithi za mila za kishenzi tulizoletewa na wakoloni.
 
Hivi leo duniani kuna takriban nchi 231 duniani. Kiuchumi, Tanzania, Malawi, Gaza Strip, Sierra Leone, Somalia na East Timor ndio nchi sita hoibintaaban za mwisho ulimwenguni.

Hadi kufikia sasa katika nchi yetu ilipofikia ni sawa Gaza Strip ya Wapalestina ilipo? Sisi , Gaza na Malawi wote tuna GDP per capita ya dola 600 za Kimarekani. Waliopo chini yetu ni nchi zilizoathirika sana na vita na misukosuko ya kijamii nazo ni Somalia, Sierra Leone na East Timor. Sierra Leone na East Timor baada ya mwaka huu, hata hivyo, lazima ziwe juu yetu kwa hiyo nchi itakayokuwa ya mwisho kabisa itakuwa ni Somalia ikifuatiwa na Tanzania. Tujiulize ni wapi tulipokosea, tunapokosea na tutakapoendelea kukosea? Ya kwamba pamoja na kugundulika utajiri mkubwa wa dhahabu na madini mengine hali ya Watanzania ndio imezidi kuwa mbaya kuliko ya watu wote duniani isipokuwa Somalia.


Unataka ushahidi nenda hapa:

World Facts and Figures - GDP per capita by country


Mkuu Iga, ahsante saana kwa taarifa yako hii.

Lakini inaonekana ni taarifa iliotolewa tarehe 11 May 2004.

Pia kwa mpangilio huo inaonekana kwamba hii ilikuwa "estimate" kwa mwaka 2003, yaani hizo dollar 600.

Sasa kwa kuwa tupo kwenye "current economic situation" ambayo inaandamwa na matatizo ya "credit crunch" na mifumuko ya bei duniani, inabidi tujadili ni vipi Tanzania inaathirika au itaathirika kama sio kuadhirika kiuchumi.

Tunahitaji "reversed decisions" ambazo zitafanya tuanze kujitegemea na kuinuka kiuchumi kwa kuzingatia kuwa kila rasilimali tunayo.

Sasa kwa mujibu wa wikipedia.org, kwa estimate ya 2008 ambayo ni latest na imerekebishwa,Tanzania ina GDP ya $37,031 na inashika nafasi ya 16 miongoni mwa nchi za Afrika.

Hii ni kwa kiasi gani kila mtu anatumia kufanya matumizi kwa mwaka au PPP.

Kwa GDP ya kila mtu (hii inahusu kipato) Tanzania inasimama namba 48 miongoni mwa nchi za Afrika na ni $982 na hii pia ni estimate ya 2008.

Enenda link hii hapa na upate the "general context".

http://en.wikipedia.org/wiki/List_of_African_countries_by_GDP

Tuache ku-"meddle" hizi "figures" ambazo haziteli afya.
 
Hivi leo duniani kuna takriban nchi 231 duniani. Kiuchumi, Tanzania, Malawi, Gaza Strip, Sierra Leone, Somalia na East Timor ndio nchi sita hoibintaaban za mwisho ulimwenguni.

Hadi kufikia sasa katika nchi yetu ilipofikia ni sawa Gaza Strip ya Wapalestina ilipo? Sisi , Gaza na Malawi wote tuna GDP per capita ya dola 600 za Kimarekani. Waliopo chini yetu ni nchi zilizoathirika sana na vita na misukosuko ya kijamii nazo ni Somalia, Sierra Leone na East Timor. Sierra Leone na East Timor baada ya mwaka huu, hata hivyo, lazima ziwe juu yetu kwa hiyo nchi itakayokuwa ya mwisho kabisa itakuwa ni Somalia ikifuatiwa na Tanzania. Tujiulize ni wapi tulipokosea, tunapokosea na tutakapoendelea kukosea? Ya kwamba pamoja na kugundulika utajiri mkubwa wa dhahabu na madini mengine hali ya Watanzania ndio imezidi kuwa mbaya kuliko ya watu wote duniani isipokuwa Somalia.


Unataka ushahidi nenda hapa:

World Facts and Figures - GDP per capita by country

Mheshimiwa mbona hizo data za long time sana.

Latest CIA data iko hapa https://www.cia.gov/library/publications/the-world-factbook/geos/tz.html#Econ

GDP (2007 est) ni $51 billion.
Hata hao Kenya wanaopiga kelele wana $61 billion. Kagepu ka $10 billion tu, I don't think kama kanawarrant kelele zote hizo za kujitapa kama za bwana Gitui.
 
Nakubaliana kabisa na wale wanaosema kwamba GDP haiwezi kutoa picha halisi ya utajiri au umaskini katika nchi, na hasa kama nchi ni Tanzania ambapo sehemu kubwa ya uchumi wetu haiwi haionekani katika takwimu kutokana na ukubwa wa sekta isiyo rasmi huku kwetu. Kwa mawazo yangu kipimo tulicho nacho hapa kinachoweza kukaribia hali halisi ni Household Budget Survey (2001/2 and 2007/8 version found at National Bureau of Statistics Tanzania Official Website) kwa sababu hapa tunapima consumption na siyo production kwa hiyo hata sekta isiyo rasmi inazingatiwa.

Kwa maoni yangu wakati mwingine umaskini wetu unatokana na maamuzi tunayo ruhusu yachukuliwe na viongozi wetu. Nimeambatanisha presentation inayoelezea uchambuzi wa bajeti uliyofanyika katika sekta ya maji hivi karibuni nikijaribu kuelezea point yangu. Tukiendelea kupanga bajeti kila mwaka bila kufuala muelekeo unaoeleweka sijui kama tutafika kweli. Maoni yanakaribishwa.
 

Attachments

Back
Top Bottom