TANZIA: Aliyewahi kuwa Rais wa pili wa Zanzibar, Mzee Aboud Jumbe afariki dunia

muda wote huu wakuja Geita na Kuvuka maji wewe upo pembeni unamwanagalia? umemabiwa au umemuona akifanya hivyo?

mimi nilikuwepo Geita kwenye hilo kongamano. nilimuona. sio kuambiwa. Nadhani alikuwa na matatizo ya miguu kutokana na umri wake maana alikuwa akitembea kwa taratibu sana.
 
Hii mbona kama vile hataki serikali katika mazishi yake
 
Kama kweli alifungwa, nani wa kulaumiwa maana aliyemfunga mwenyewe alishakufa long time ago. Nadhani it is better, tusilaum mtu katika hili. Kumbuka yawezekana kama asingefungwa angekuwa kashakufa- wanaofungwa huwa wanakaa miaka mingi sana mfn. Mandela na yeye Jumbe na wengineo.

Wapo WALIOKATISHWA MAISHA Kwa sababu ya muungano, yeye alifungwa-HUONI HIYO NI BAHATI SANA KWAKE????

Poleni sana Wazanzibar, jitokezeni kwa wingi katika mazishi ya mzee Jumbe.
 
Jumbe hakua kizuizini, ameishi kwa Uhuru miaka yote akiwa mji mwema, akienda kokote anakotaka, Kuna wakati alisafiri kwenda arabuni, sijawahi kujua hii dhana ya kizuizini ililetwa na nani na watu wakaishupalia

Tuambie kwanini alikuwa haudhurii kwenye sherehe zote za kitaifa za Zanzibar na Tanzania, wakati karibia Marais waliopita wote wa Muungano na wa Zanzibar walikuwa wakihudhuria?
Humu siyo wote watoto miaka ya tisini.
 
Aboud AJumbe alimsomesha mzee wangu mika kabla ya Mapinduzi..akimsifia sana ..naweza kumuita Mzee Jumbe ni Uamsho wa kwanza alie jitolea kuwaamsha Wazanzibari juu ya Dude Mungano na atahri zake.
Alikua mhanga wa wazi kabisa katika viongozi...
 
Rais ametuma salamu za rambirambi kwa WANANCHI wa Zanzibar?
Hivi suala la uraia si la muungano au? Kuna raia wa Zanzibar na wa wapi kwingine?
Anyways, pumzika vyema Mzee Jumbe

Hee imekua rambi rambi za zanzibar? Si alikua makamu wa nyerere na makamu wa ccm ? Makubwa
 
Hakuna mtanzania atakaye sema wasifu wa kweli kuhusu taabu alizopitia huyo MZEE, ila ndiyo haya tunayasema kila siku, "UKITAKA KUWA MKWELI, JIANDAE KUTENGWA"". Amepitia mengi na magumu, Mwache akapumzike, Roho na Nafsi yake Mungu akafanyie wepesi.

#RestInPeaceDktAboudJumbe
 
Hakuna mtanzania atakaye sema wasifu wa kweli kuhusu taabu alizopitia huyo MZEE, ila ndiyo haya tunayasema kila siku, "UKITAKA KUWA MKWELI, JIANDAE KUTENGWA"". Amepitia mengi na magumu, Mwache akapumzike, Roho na Nafsi yake Mungu akafanyie wepesi.

#RestInPeaceDktAboudJumbe
 
rip ligend,ulipigania maslahi mapana ya zanzibar japo masnitch walikuwa wengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…