TANZIA: Mchezaji wa Mbao FC afariki baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa Mwadui FC

TANZIA: Mchezaji wa Mbao FC afariki baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa Mwadui FC

Inasikitisha sana....Mauti yalivyomkuta Mrisho Khalfan wa Mbao FC.... ANGALIA pia BAO alilofunga na alivyoshangilia dakika chache kabla ya mauti.... Hakika Mungu ni mkubwa....



Hivi mnajua kuwa kuangalia video hizi za Facebook ni lazima uwe na account huko? Akaunti yangu ya Facebook niliifutilia mbali mwaka 2015 baada ya kuchoshwa na "axante beb gd9 2taxem kxho" na kuamua kujiunga JF. Video za YouTube ndo poa bana.

Mrisho Khalfan apumzike salama. Kama amefia uwanjani basi aangalau ameondoka wakati akifanya kitu akipendacho na hakuteseka. Sisi tuliobaki hatujui tutaondokaje. Jina la Bwana na lihimidiwe!
 
Duh hizi first aid za bongo. Kila mtu anavuta mguu wake
 
Duh hizi first aid za bongo. Kila mtu anavuta mguu wake
Ingawa kifo au ajali anapanga muumba lakini upo umuhimu wa kuhakikisha hao watoa huduma wanakuwa na utaalamu wa kutosha pamoja na vifaa stahiki. Hivi unafahamu marehemu alipelekwa hospitali na gari la zima moto?
 
Inadaiwa Ambulance haikuwapo uwanjani, alipelekwa na gari ya fire, pole kwa familia

Apumzike kwa amani ndogo wetu
Nchi ya hovyo hii, hata mie kila siku naliona fire ila sijawahi kuliona ambulance uwanjani
 
Huu ndio uanaume wenyewe unakufa ukiwa Kazini!!!!. Mwenyezi Mungu ampe pumziko lenye Heri na Amani ndugu @IsmailKhalfanMrisho
 
Nimeona video clip yake nimeshindwa kuirudia.... R.I.p Ismail
 
Mchezaji wa mbao FC, Ismail Khalfani Mrisho afariki baada ya kugongana na mchezaji wa Mwadui FC kwenye mtanange uliochezwa uwanja wa Kaitaba, Bukoba kwa wachezaji walio chini ya miaka 20 (U20).

View attachment 442735
Photo Credit; Faustine Ruta
==================

UPDATE

Mechi hiyo ilikuwa inachezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ambako michuano ya vijana chini ya miaka 20 inaendelea.

Ismail aligongana na beki wa Mwadui FC wakati wakiwania mpira na kuanguka na juhudi za kuokoa maisha yake zilionekana kukakwama.

Wakati mauti yanamkuta Ismail, dakika chache kabla alikuwa amefunga bao dhidi ya Mwadui.

Pamoja na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Kagera, taarifa baadaye zilizopatikana zilieleza, Ismail alifariki palepale uwanjani.
Rip Ismail hakuna kifo kinachokosa sababu wengine watakihusisha na nguvu za giza
 
Au goli limemcost,maana bongo kuna ndumba banaa kwenye soccer
 
pamoja na yote, nadhani kuna haja ya kuwa makini katika kupima afya ya wachezaji na kufuatilia maendeleo yao kiafya kila wakati ili kujiridhisha kama wako fit kwa mechi....

Lilikua tukio la kawaida sana katika mchezo jambo ambalo linanishawishi kwamba labda hali yake ya afya haikuwa nzuri.

Pole kwa familia, pole kwa Mbao Fc pole kwa wapenda soka wote..
R.I.P
Mkuu hii hali huwa inatokea sana kwenye michezo kwa mfano hata Marc Vivien Foe hakuwa amegongana na mtu ila alianguka tu peke yake na kifo kilimkuta pale pale .

Kwahiyo hata wakiwapima vipimo vya aina gani bado haitasaida chochote kwa sababu wakati mwingine ni kufeli kwa mishipa ya damu kufanya kazi yake katika hali ya kawaida.

Kifo kipo karibu sana na binadamu kuliko kitu chochote mkuu.
 
Back
Top Bottom