TANZIA: Mchezaji wa Mbao FC afariki baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa Mwadui FC

TANZIA: Mchezaji wa Mbao FC afariki baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa Mwadui FC

Mchezaji wa mbao FC, Ismail Khalfani Mrisho afariki baada ya kugongana na mchezaji wa Mwadui FC kwenye mtanange uliochezwa uwanja wa Kaitaba, Bukoba kwa wachezaji walio chini ya miaka 20 (U20).

View attachment 442735
Photo Credit; Faustine Ruta
==================

UPDATE

Mechi hiyo ilikuwa inachezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ambako michuano ya vijana chini ya miaka 20 inaendelea.

Ismail aligongana na beki wa Mwadui FC wakati wakiwania mpira na kuanguka na juhudi za kuokoa maisha yake zilionekana kukakwama.

Wakati mauti yanamkuta Ismail, dakika chache kabla alikuwa amefunga bao dhidi ya Mwadui.

Pamoja na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Kagera, taarifa baadaye zilizopatikana zilieleza, Ismail alifariki palepale uwanjani.
Wamegongana wapi rafu ya dhahiri kabisa ile. R.I.P
 
Wakati akishangilia goli lake kuna style aliitumia,Nadhani inaweza kuwa imechangia kwa kiasi fulani lakini yote kwa yote Mungu ndiye ajuae siri ya kifo,Na hakuna ajuae R.I.P. Ismail.
Na wale waliompa huduma ya dharura ni majanga pia!jamaa alifariki pale miguu ilipoanza kutetemeka! Pale ndio roho ilikuwa inaachana na mwili [emoji25] [emoji25] [emoji25] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144]
 
Ismal Mrisho Alfan, amesafirishwa na gari iliyotolewa na uongozi wa manispaa ya Bukoba kusafirisha mwili wa kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 19 kwenda Mwanza wilayani Ilemela kwa maziko.

Alikuwa amehitimu kidato cha nne, alikuwa anavaa jezi namba nne, alikuwa amefunga goli la nne katika mashindano ya U-20, alitarajiwa kujiunga na academy nchini Marekani baada ya kufuzu katika majaribio, ingawa alirudi nchini kumalizia masomo yake ya sekondari, na ameaga dunia tarehe ya nne ya mwezi 12/2016.
 
Mi nahisi ile shangilia yake ilileta hitilafu labda kwenye moyo. Rafu aliyochezewa ilikuwa ni ya kawaida mno hadi refa hakupiga filimbi.
 
TFF ilichukue tukio hili kama fundisho. Nashauri TFF kwa kushirikiana na chama cha Madaktari waanzishe mafunzo ya huduma ya kwanza kwa watoa huduma wote waliopo mikoani. Kwa jinsi nilivyoliona tukio hili watoa huduma waliokuwepo pale uwanjani walishindwa kumsaidia mchezaji ambae mapigo ya moyo yamesimama. Huduma ya kwanza ingefanyika kiweledi wangeweza kuokuo maisha ya kijana huyu. R.I.P
 
On behalf of myself and the people of Ilembula,.. We say R. I. P
Haaahaahaaa
Kwani kuna Ilembula kwenye Bible?
Mi naongelea Korinto ya kwenye Bible mkuu.
Teh teh
Nimekumisi nyumbani kwetu, hasa kuvuka ule mto Halali kwa mguu. Magari huwa sipandi nikiwa kwetu.
 
Back
Top Bottom