huyu mtoto namuonea huruma huku simuonei huruma. ni mtoto mdogo mno kukumbwa na visanga kama hivi. na yote hii ni kuvamia maisha katika umri mdogo, kujiona umekua wakati bado una safari ndefu. Watoto wa umri wake wako chuo wanasoma ili wawe na elimu waweze kujitegemea, yeye katika umri huu yuko busy kusaka waume za watu wenye pesa maana bongo limejaa matope, hawezi kutulia akasoma, anataka short cut. Siku zote ukitaka short cut ya maisha, unakumbwa na mikasa kama hii. Hana tofauti na jambazi. Alitamba sana muda si mrefu kwenye kipindi cha Zamaradi kua yeye ni mchaga anaipenda pesa na anajua kuitafuta... kumbe kuitafuta kwenyewe si kwa kujituma akajulikana anachokifanya, bali ni kuvunja ndoa za watu na kuvuliwa pichu... mwenyezi mungu tunusurie watoto wetu wasifikie alikofikia huyo mtoto mdogo mwenye malezi mabovu... nasema mabovu maana mama yake anaonekana kufurahia sana haya maisha ya huyu mtoto. Sidhani hata kama kuna siku ameshawahi kumkalisha chini na kumkemea hii tabia au kumshawishi arudi shule. majaribu anayopitia, ni ujumbe kua amevamia mambo makubwa angali mdogo, hivyo anatakiwa kutulia sasa. Nina imani mwanaume mwenye akili timamu atamuogopa huyu binti kama ukoma, unless kama hujipendi. wako wanaosema siku za hawa wanaume zilifika, sikatai, lakini why always siku zifike ukiwa katika mahusiano na huyu binti...??? something is wrong somewhere, amrudie mungu wake. mke wa huyu marehemu RIP, aliumia sana kwa ajili ya huyu mtoto, machozi yake ndio yameleta majibu kama haya. naomba hili liwe fundisho kwa mabinti wote wenye kupenda short cut katika maisha kwa kuvuruga ndoa za wengine.