TANZIA: Mwanahabari mkongwe, Bi Sarah Dumba afariki dunia ghafla akiwa Njombe

Pumzika kwa amani Bi Mkubwa,duh alinichukua alipoteuliwa kuiongoza wilaya ya Kilindi nilijifumza mengi toka kwake upole na ucheshi duh tumbo la ardhi limemeza wengi.
InshaAlla Mungu akupe kauli thabiti uko uendako pole sana mwanangu Sunday na Henry.
 
hata kama alikuwa mwanaccm , tunamuomba Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali inapostahili .
 
OOh Mama Sarah Dumba, ninakumbuka alikuwa anasoma taarifa ya habari external service RTD sauti yake ilikuwa nzuri, kipindi cha mama na mwana alikuwa nasimulia hadith ya ua jekundu. R.I.P mama.
 
Usichanganye na Debora Mwenda
Hapana, nafikiri wewe ni mzaliwa miaka hii ya karibuni, Marehemu Sara Dumba ndiyo nafikiri mtu wa mwanzo kabisa wa kipindi cha mama na mwana! Kwa ufahmu wangu nakumbuka miaka ya themanini na kitu hdithi za kutisha wakati wa jioni tumsikiliza kupitia radio za wakati huo, National MemoryQ,
Rest in Peace Bi Sara Dumba
 
Unafikiri....mi nina uhakika
 
Nikumbushe hadithi moja nione kama ulikuwepo....usije na ua jekundu au akajasembamba maana hizo ni za majuzi tu
 
R.I.P mama Dumba ... nakumbuka kipindi cha mama na mwana tulikuwa tunaitolea macho radio utadhani ni tv.
 
Nikumbushe hadithi moja nione kama ulikuwepo....usije na ua jekundu au akajasembamba maana hizo ni za majuzi tu
Kulikuwa na moja ya binti mfalme, hiyo y ua jekundu ni mojawapo pia, kulikuwa pia na hadith moja ya joka jeusi.
 
Kweli mkuu coz mara mwisho kumuona ilikuwa Njombe kama aka3 iv, kiukweli alikuwa bonge sana na kama ulisema uzee ulikuwa mwing sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…