Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Kwa shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama directorate K. Hii idara ilikuwa na kazi maalumu ya kufanya bugging , kile kitendo Cha kupandikiza vinasa sauti na video camera kwa Siri kwenye ofisi za walengwa maalumu waliokusudiwa , kusikiliza mawasiliano Yao ya simu au pia wakati mwingine kwenye makazi Yao binafsi.

Ilichukua nusu dakika kufungu vitasa viwili vya mlango wa mbele wa chumba namba 220 kwenye ghorofa ya nane katika mtaa wa Leninsky prospekt . Hili lilikuwa ni jumba la ghorofa lililokuwa linakaliwa na maofisa wa KGB pamoja na familia zao.

Kwa Siri sana wanaume waawili waliokuwa wamevalia overall pamoja na gloves kwa haraka haraka wangedhaniwa kuwa ni mafundi tu wa kawaida kwa ajili ya kufanya matengenezo madogo madogo katika jumba Hilo , lakini uhalisia haukuwa hivyo. Baada ya kufungua vitasa vya chumba hicho kwa ustadi na kuingia ndani wakaaanza kufanya kilichowaleta.wanaume hao wawili wakaaanza kuweka camera pamoja na vinasa sauti kwa Siri kwenye sehemu sehemu mbali mbali chumbani maeneo ambayo sio rahisi kushtukiwa. Vinasa sauti viliwekwa ukutani kwenye maiki za simu ya mezani ,pamoja na kwenye Kona za kitanda ,jikoni ,maliwatoni n.k.

Pia kamera ndogo za Siri ziliwekwa kwenye taa za kila Kona ya chumba hicho ,baada ya hapo wakavaa mask usoni na kuanza kunyunyiza vumbi lenye mionzi kwenye nguo na viatu vilivyokuwa kabatini katika Hali ambayo isingeweza kushtukiwa na mlengwa wao. Hili vumbi lingewasaidia ku track movements za huyo mlengwa wao popote aendapo kwa kutumia kifaa kilichojulikana kama Geiger counte. Baada ya kumaliza kilichowaleta wakaurudishia mlango na kuufunga kama walivyoukuta na wakatokomea.

Masaa machache baadaye ,afisa wa ngazi za juu wa KGB alishuka kwenye uwanja wa ndege wa Moscow na shirika la ndege la Aeroflot akitokea London. Kanali Oleg antonyevich Gordievsky alikuwa katika kilele Cha mafaniko ya kazi Yake katika idara ya KGB. Mpaka kufika kuwa afisa wa ngazi za juu kwenye shirika Hilo alipitia vyeo mbalimbali ,amefanya kazi kama balozi kwenye nchi za Scandinavia, uingereza pamoja na hapo Moscow.

Akiwa na miaka 46 aliteuliwa kuwa mwakilishi wa KGB kwenye ubalozi wa USSR hapo London. Kwa kuwa alikuwa jasusi mbobevu alipanda vyeo kwa haraka ndani ya idara kiasi kwamba akawa na uwezo wa kujua Siri nyingi za kijasusi (Disclassfied material) pamoja na mtandao wa kijasusi kwenye mataifa mbalimbali ikiwemo mataifa ya magharibi.

Mwenye muonekano wa mwili wa mazoezi,akiwa hana hofu Wala wasiwasi huku akitabasamu alikatiza katikati ya umati wa watu hapo uwanja wa ndege kwa ajili ya kutafuta teksi imuondoe hapo impeleke anapoishi.
Bwana Oleg afisa wa kijasusi mtiifu wa shirika la KGB aliyependwa na mabosi wake kama asset muhimu waliokuwa nayo kipindi hicho ,pia alikuwa ni JASUSI MTIIFU WA UINGEREZA. Kwa kifupi alikuwa ni double agent.

Akiwa afisa wa KGB tayari alikuwa ni mwajiriwa rasmi wa shirika la kijasusi la uingereza la MI6 kwa miaka takribani 12 .na alipewa jina jina la uficho (codename) la NOCTON.

Na baadaye ikaja semekana alikuwa ndiye JASUSI wa thamani sana enzi zile za vita baridi. Taarifa za Siri alizokuwa anazivujisha kutoka KGB na mipango ya Siri ya USSR zilibadilisha kabisa mkondo wa vita baridi kwa wakati ule. Bwana Oleg aliweza kutoboa Siri ikiwemo mikakati ya nyuklia za USSR..mtandao wa majasusi uliokuwa kwenye nchi za magharibi,pamoja na sera za nje za urusi kwa wakati huo kwa wakubwa wa MI6.

Taarifa alizokuwa anazivujisha bwana Oleg ziliwafanya MI6 na CIA ku share kwa pamoja baadhi ya taarifa, lakini ajabu ni kwamba DG na top officials wa MI6 hawakutaka kutoa identity ya Oleg kwa Margaret thatcher Wala Ronald Reagan waliemwajiri ndani ya Kremlin kwa maaana ya USSR kwa kuwapa sensitive Disclassfied informations. Na kulikuwa na sababu maalumu ya kufanya hivyo.
Pia mkewe bwana oleg hakuwahi kujua mumewe ni spy wa uingereza.

Lakini imekuwaje amekuja ghafla Moscow kwa kuitwa na wakubwa zake? . yaani ni kwa mfano balozi polepole kateuliwa balozi Tz Cuba, lakini ghafla hajamaliza hata miezi mitatu anaitwa nyumbani ghafla ,lazima hata kama ni wewe utajiuliza tu.

Lakini wanasema JASUSI ni jasusi tu . bwana Oleg aliweza kunusa hatari iliyokuwa mbele Yake ,akiwa anakatiza katikati ya watu hapo uwanja wa ndege baada ya kutua ndani ya nafsi yake alihisi upweke uliochanganyika na mashaka . Baada ya kukaguliwa nyaraka zake na hati ya kusafiria na wale maafisa wa passport uwanjani hapo alikabidhiwa akaagwa akaondoka.

Kikawaida kwa wakati huo afisa yoyote hususani mwakilishi akitokea nje ya nchi lazima kunakuwa na courtesy ya maafisa wenzake kuja kumpokea mwenzao airport lakini haikuwa hivyo. Akiwa anaangaza huku na kule asione dalili yoyote ya mapokezi alinotice jambo lisilo la kawaida, kulikuwa na wanaume na wanawake wamesimama hapa na pale uwanjani hapo pasipo jambo la muhimu waliokuwa walikilifanya zaidi ya kushangaa huku na huko.

Lakini bwana huyu akiwa ndani ya teksi alijiambia ikiwa KGB wanajua ukweli kumhusu yeye muda huo angekuwa tayari amewekwa chini ya ulinzi muda huo punde alipokanyaga ardhi ya Russia,aburuzwe Hadi kwenye cell za KGB ahojiwe,ateswe mwisho wa siku auliwe kwa kupigwa risasi ya kichwani .

Mpaka anaingia kwenye teksi Hadi kufika yalipo makazi yake mtaa wa Leninsky prospekt hakuwa anafuatiliwa kwa namna yoyote ile.alikwea lift Hadi ghorofa ya nane kwenye jumba Hilo kitasa Cha kwanza Cha mlango wake kilifunguka na Cha pili vilevile lakini kitasa Cha tatu Cha mlango kilikuwa locked bwana Oleg hakuwahi tumia kitasa Cha tatu kwa kuwa hakuwa na funguo zake, lakini ajabu ni kwamba alikuta kitasa kimefungwa na hapo hapo akahisi Kuna watu waliingia na kutoka wakajisahau wakafunga Hadi kitasa Cha tatu. Alikuwa sahihi . Alikuwa anatiliwa wasiwasi. The spy was being spied upon by his fellow spies.
Kuna huyu mwamba anaitwa Robert fhilip Hansen huyo ni chamtoto.CIA walivuliwa nguo mchanamchana.
Robert_Hanssen.jpg
 
Sehemu 02.

SEHEMU YA PILI

Bwana Oleg Gordievsky alizaliwa ndani ya KGB ,ikamkomaza,ikamtwist vilivyo na almanusura imhuharibie maisha . Kufanya kazi ndani ya idara kubwa ya kijasusi ndani ya muungano wa Soviet,kwake ilikuwa ni heshima kubwa sana na ni kazi iliyokuwa kwenye damu yake. Kwani baba yake amefanya kazi ndani ya shirika Hilo maisha yake yote. Familia ya Gordievsky iliishi kwenye apartment za shirika Hilo na walipewa special treatment na favor maalumu kwa kuwa wao walikuwa ni familia ya kitengo.

Shirika la kijasusi la KGB(komitet gosudarstvennoy bezospasnosti) kwa kiswahili sanifu ni kamati ya ulinzi la kitaifa, ilikuwa ni taasisi imara ya usalama kuwahi kuundwa hapa duniani. Shirika Hili lilizaliwa kutoka kwenye kikundi kidogo Cha majasusi watiifu wa mzee Stalin. Kazi Yake ilikuwa kukusanya taarifa nje na ndani ya muungano wa Soviet ,kutoa ulinzi ndani ya taifa ,pamoja na maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya kijamaa.

Kwa kifupi shirika Hili lilikuwa limetawala nyanja zote za kimaisha kwa wale wote waliokuwa wapo chini ya muungano wa ki Soviet.

Lilikuwa ni shirika lililoajiri na kupandikiza majasusi duniani kote kwa ajili ya ,kukusanya ,kuiba ,na pia kununua taarifa mbalimbali za Siri ikiwemo za kijeshi, kisiasa, silaha pamoja na taarifa za kisayansi na teknolojia. Inakadiriwa kipindi hicho shirika likiwa katika kilele Cha mafanikio ilikuwa na ma agent takribani milioni na zaidi.

Kwa upande wa nchi za kimagharibi hii taasisi ilitazamwa kama zana ya kuwatia watu hofu,kutii wasichokijua,kuwatesa na kuwanyanyasa raia wake kidhalimu. Ilitazamwa kama kundi la kimafia chini ya mwavuli wa kikomunisti lenye kusambaza propaganda za kijamaa zilizopitwa na wakati .

Lakini kwa waliokuwa wanaishi chini ya muungano wa ki Soviet wao walichukulia KGB kama mlinzi wao,alama ya uzalendo na Utiifu kwa taifa na mamlaka,pamoja na ngao ya kuwalinda Raia dhidi ya umagharibi. Kuwa memba wa KGB ilikuwa ni heshima na sifa na pia alama ya ufahari kwa wakati huo.

Hivyo basi bwana Oleg hakuwa na la kupingana nalo zaidi ya kufuata nyendo za mshua wake bwana Anton lavrentyevich Gordievsky, na kuwa afisa wa KGB.

Baba yake Oleg kabla ya kuwa afisa wa KGB ,alikuwa ni mwalimu .lakini baada ya mapinduzi ya mwaka 1917 akaamua kujiunga na kuwa mwanachama rasmi wa chama Cha kikomunisti. Kilichomfanya baba yake Oleg kujiunga na ukomunist ni itikadi za mzee Stalin , ambazo zilikuwa Kali.
Alijiunga na chama Cha NkVD( baadaye sana ilimezwa ndani ya KGB) au taasisi ya kikomunisti kwa ustawi wa watu. Lengo la hii taasisi au chama ni kulinda maslahi ya kikomunisti ,kutoa ulinzi na vilevile kusambaza propaganda pamoja na kupambana na maadui wa urusi. Mzee Stalin alitangazia umma kwamba maadui wa urusi ni mabepari , mashoga,majasusi wa utawala uliopita,wayahudi , maofisa wa serikali wenye mrengo wa kibepari n.k. Hivyo bwana Anton alijitolea kwa udi na uvumba katika kulinda itikadi za kikomunisti. Alijitolea kufundisha propaganda kwenye kambi za kijeshi na taasisi za elimu . Tuseme kwa kifupi alikuwa ni mwenezi kama polepole.
Na katika kipindi hicho watu walianza kuonja ladha ya ukomunisti .watu walipotezwa, wengine walinyang'anywa Mali ,kufungwa na pia wengine walilazimishwa kuhama nchi. Na kubwa zaidi wengi walikufa na njaa kutokana na uzalishaji kuzorota mashamba na maghala kuchukuliwa na serikali. Japo mzee Anton alikuwa ni mwanachama mtiifu kwa chama na serikali lakini nafsi ilikuwa inamsuta.
Alimwoa Olga nikolayevna gornova mrembo wa miaka 24 aliyekuwa anafanya kazi kwenye ofisi za takwimu. Walihamia Moscow kwenye apartments zilizokuwa spesho kwa ajili ya maafisa wa NkVD. Mtoto wao wa kwanza aliitwa Vasili aliyezaliwa 1932. Mtoto wao wa pili alizaliwa miaka sita baadaye yaani 1938,aliyeitwa Oleg antonyevich Gordievsky tarehe 10 October.
Mtoto wao wa tatu aliitwa marina aliyezaliwa miaka Saba baadaye. Kwa kifupi ilikuwa ni familia ya kitengo. Watoto walikuwa vizuri na pia stahiki na treatment za kutosha walizipata kutoka serikalini kwa kuwa ni familia ya KITENGO. Familia ilikuwa na kulelewa katika itikadi za kijamaa ,na watoto walikuwa watiifu na wazalendo kwa serikali ya kisoviet. Waswahili wanasema kila familia Ina Siri zake . kwa nje familia ya mzee Anton ilionekana ni familia Bora na iliyostawi sana na majirani kuweza kuwa admire. Haikuwa hivyo. Mzee Anton nafsi ilikuwa inamsuta sana kwa mabaya aliyokuwa anayafanya kipindi Cha Stalin anashika hatamu. Mfano kupotezwa kwa watu,uporaji wa mashamba na vifo vilivyotokana na njaa.hii ilimsumbua sana nafsini mwake lakini alikausha na Siri yake moyoni. Mkewe , Olga hakuwahi kuukubali ukomunisti lakini atafanyaje ndio anaishi kwenye ndoa yenye itikadi hizo. Sababu ya kuchukia ukomunisti ni kwamba baba yake alinyang'anywa mashine zile za upepo za kuvuta maji ardhini na serikali,pia kaka yake alikamatwa kwa kosa la kupinga sera ya umiliki na kilimo Cha kwa pamoja na kupelekwa huko Gulag Jimbo lililoko mashariki mwa Siberia na kupotelea huko mazima. Pia aliwahi shuhudia majirani zake kipindi hicho wakifuatwa usiku na watu wasiojulikana na kuondoka nao asiwaone tena.


IMG_20230415_092915_487.jpg

Familia ya mzee Anton kushoto na wanao wawili marina na Oleg wakiwa na umri wa miaka kumi hivi

IMG_20230415_092915_489.jpg

Watoto wa mzee Anton Vasili,mdogo wao wa kike marina na Oleg Gordievsky.


Oleg na Vasili walitofautiana kwa umri wa miaka sita hivi.na walikuwa kipindi Cha vita. Kwa mfano Vasili akiwa mdogo, alishuhudia mateka wa kivita wa kijerumani wakipanga gwaride mitaa ya Moscow na kulazimishwa kutembea umbali mrefu wakinyanyaswa na kudhihakiwa kama wanyama. Baba Yao mara nyingi alisafiri sehemu mbalimbali za nchi kueneza propaganda za kikomunisti. Kwa upande wa Oleg ,yeye alikuwa ni mtu wa kujifunza na kusoma vitabu. Kwa umri wake mdogo alijifunza kusoma katekisimu ya ki orthodox yenye mrengo wa kikomunisti. Pia alikuwa ni mtu wa kujifunza lugha na hatimaye alionyesha uwezo mkubwa katika kujifunza kijerumani. Baba yake Oleg alikuwa kila akirudi lazima aje na magazeti yenye itikadi za kikomunisti hivyo akawa na wasaha wa kuyasoma. Ingawaje alikuwa anasoma vitabu vya propaganda dhidi ya magharibi alivutiwa na maswala, kadhaa ikiwemo lugha za huko. Rasmi Sasa Oleg alivyofika umri wa utineja akajiunga tuseme UVCCM ya huko iliyojulikana kama KOMSOMOL.
Oleg alikulia kwenye familia yenye upendo baba yake akiwa mwanachama rasmi wa KGB,na mama yake pia akiwa mke wa afisa ,mama wa nyumbani, lakini ndani ya mioyo Yao Hawa wanandoa wawili walikuwa wanafeki tu kwa nje lakini ndani mwao kulikuwa na vidonda kuhusu madhila ya mfumo mzima wa kikatili wa kikomunisti.hakuna aliyewahi jionyesha kwamba anadukuduku lake dhidi ya mfumo.
Kwa kipindi hicho Cha utawala wa Stalin familia ya Anton Gordievsky waliamini kwamba unaweza ukawa mtiifu kwa serikali ya kikomunisti , lakini ukawa una amini jambo lingine kwa Siri sana Japo ilikuwa ni jambo la hatari ya maisha. Kwa mfano hapa kwetu uwe mtiifu kwa serikali ya ccm lakini ndani ni mwanachama mtiifu kabisa wa upinzani.

Umahiri wa Oleg ulidhihirika akiwa na UVCCM Yao ya KOMSOMOL kwa kupewa medali ya silver kama kijana mwenye akili , shupavu,mwenye bidii katika michezo na vilevile mzalendo haswa kwa nchi yake .licha ya hayo yote Oleg Gordievsky alijifunza kuishi maisha ya aina mbili.
 
Back
Top Bottom