Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

SEHEMU YA 5

Kiukweli mama yake Oleg , hakufurahishwa sana na mwanaye huyu mdogo kujiunga kitengoni. Hii ni kwa sababu ya historia na misukosuko aliyopitia .Alimwona kama mwanaye amejiunga na idara ya mashetani waliohusika kuyaharibu sehemu ya maisha yake,Sasa mwanaye naye anajiunga huko Tena .hakika kulimchanganya sana mwanamama huyu. Lakini mwanaye baada ya kurejea kutoka ujerumani mashariki Alimwona mama yake kama Hana furaha kabisa Japo ilikuwa ni kazi yenye status ya Hali ya juu kwa wakati huo. Oleg alimwambia mama yake kwamba hatakuwa anafanya kazi ndani ya KGB hapo Russia Bali kama afisa mwakilishi (balozi ) nje ya nchi ya urusi. Alijaribu kumshawishi sana mama yake asiichukulie kazi ya kitengo in negative way.ila ndio hivyo mwana mama hakuafiki kabisa moyoni mwake Japo hakuwahi onyesha waziwazi. Kwa kifupi Olga na mmewe mzee Anton hawakuwa pride na mwanao kuifanyia kazi kitengo ,lakini watafanyaje Sasa ,kitengo kishamchagua..
Baada ya kurudi kutoka ujerumani mashariki kwenye field yake ya mwisho ,alikutana na rafiki yake, stanislav kaplan kwenye mapumziko mafupi karibu na fukwe za bahari nyeusi. Waliamua kukutana kwa mara ya mwisho kama raia wa kawaida kabla ya kujiunga rasmi kuwa maafisa wa wa ujasusi kwenye nchi zao . Kwa mfano stanislav baada ya kumaliza mafunzo hapo Moscow alitarajiwa kujiunga na idara ya ujasusi ya Czechoslovakia iliyojulikana kama StB. Walikutana ,wakanywa ,wakijipongeza, vilevile wakipeana michapo ya totozi walizozifukuzia,miziki, na zaidi wakipondea mfumo mzima wa kikomunisti uliokuwa unatawala nchi zao. Vilevile stanislav akampa Oleg kijarida kidogo Cha mashairi ya kumponda Stalin kilichoandikwa na Yevgeny Yevtushenko kilichokuwa banned nchini urusi kabla ya kuachana.
Baada ya kutengana na rafiki yake bwana Oleg alihitajika kufika kwenye academy ya KGB iliyojulikana kama "Red banner".elite training academy. Hii akademi ipo porini maili 50 kaskazini ya Jiji la Moscow. Hii akademi ilipewa codename "school 101".
Hapa bwana Oleg pamoja na Maafisa wenzake wa KGB 120 walipewa mafunzo ya mwisho kabisa .walizamishwa kwenye Siri nzito za mfumo wa kisoviet.walifundishwa namna ya kuwatambuana wao kwa wao ,combat skills, kutumia silaha za aina mbalimbali. Vilevile walifundishwa kutumia lugha za uficho wanapowasiliana wao kwa wao. Na la Zaidi na kubwa zaidi walifundishwa namna ya kukwepa kufuatiliwa endapo wanahisiwa ni ma spy .( " surveillance detection). Mafunzo haya pia yalijukulina kama dry-cleaning au proverka kwa kirusi. Hapa wanafundishwa namna ya kuhisi kama unafuatiliwa ,namna ya kukwepa kama unafuatiliwa kwa njia ya kutotambulika na
kumchanganya anayekufuatilia kwa kumkwepa kwa ustadi wa Hali ya juu.
Walifundishwa pia namna ya kutuma na kupokea infos baina yao wakiwapo kazini ,kuacha signal , kutumia wino wa Siri kuandikia,matumizi ya kamera ,vinasa sauti .n.k. Pia maafisa waliotarajiwa kufanya kazi nchi za magharibi walipewa semina za kutosha kuhusu nchi hizo ikiwemo tamaduni , lugha n.k. Walifanyiwa kama ibada ya kukiri imani na kuutumikia mfumo wa kistalini na ukomunisti kwa ujumla.Na mwisho waliapizwa viapo vizito vizito na manuizo ya kutosha na rasmi kuwa maafisa wa KGB.
Baada ya hayo yote bwana oleg alipewa jina lake rasmi la kijasusi.Na mfumo huu wa kupewa jina lako la kispy lilikuwa linafanyika randomly kwa kuchaguliwa jina kwenye list ndefu ya majina yaliyoandikwa kwenye kitabu maalumu. Jina analopewa afisa wa KGB kikanuni lilipaswa kufanana na jina lako rasmi ulilopewa na baba na mama yako. Kwa mfano bwana Oleg alipewa jina la Guardiyetsev. Kulikuwa Kuna sababu ya kupewa jina la kijasusi linalofanana kidogo na jina lako orijino. Hii ilisemekana kwamba ikatokea mtu anakufahamu kwa jina lako halisi , halafu akakuita kwa jina lako hilo, isije ikamchanganya ambaye anakujua kwa jina lako la kijasusi , kwa maana atahisi amesikia vibaya kutokana pseudonym ya majina hayo na yatakavyotamkwa.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa bwana Oleg , na pia kama sehemu ya kuwa afisa rasmi , ilikuwa ni lazima kwa maafisa hao kujiunga na chama Cha siasa Cha nchi yao .communist party. Kulimfanya ku doubt sana lakini ndivyo utaratibu ulivyotaka. Mpaka kufikia majira ya kiangazi mwaka 1963 ,bwana Oleg alikuwa rasmi Sasa ni afisa wa KGB.
Hivyo mwaka huo tarehe 20 august alihitajika kufika makao makuu ya KGB kwenye idara ya FCD. Jengo Hilo la makao makuu lilikuwa na karibu na Kremlin. jengo Hilo lililotumiwa na KGB wakati huo lilikuwa kama hekalu ambalo ni jengo la idara ya bima la urusi. Sehemu ya jengo hili ilikuwa na ofisi za wakubwa wa kitengo,sehemu nyingine ya jengo ilikuwa stoo ya kuhifadhia archives na documents mbalimbali na sehemu nyingine ilikuwa na torture cells.
Baada ya kufika idarani na kuanza rasmi, majukumu yake yalikuwa ni kupitia document na nyaraka za maafisa wa ujasusi waliotumwa nje ya nchi,kupokea taarifa zao za kijasusi na kuzihifadhi. Pia alikuwa na kazi ya kufoji baadhi ya nyaraka kama pasi za kusafiria ,kutengeneza utambulisho bandia kwa majasusi na vilevile kuwapokea waliokuwa wanarudi kutoka kwenye majukumu ya kijasusi.
Mtu aanzapo majukumu ya kazi ya kuajiriwa lazima tapewa orientation za hapa na pale na pia kufahamu wafanyakazi wenzako wa hapo kazini na ma legend wa idarani. Ndivyo ilivyokuwa kwa bwana Oleg. Hapo kwenye idara ya FCD au Derectorates S, Oleg alitambulishwa kwa so called mashujaa wa kijasusi hapo ofisni. Kwa mfano Alitambulishwa kwa bwana mmoja aliyeitwa konon trofimovich au jina rasmi la kijasusi kama Gordon Arnold Lonsdale, aliyekuwa anafanya kazi ya ujasusi kama illegal kwenye nchi nyingine. Jina hili la Gordon Arnold lilitokana na jina la mtoto mdogo wa kanada aliyefariki dunia miaka kadhaa nyuma ,hivyo mwaka 1943 KGB wakaamua kumpa jina hili bwana konon kwa kuwa alikulia marekani tokea akiwa mdogo na kuongea fluent English. Inasemekana huyu alikuwa akiishi London akiwa kama muuza boligamu au bablishi.kazi yake hapo London ilikuwa kukusanya taarifa za kijasusi za jeshi la majini la uingereza na pia kupandikiza majasusi wengine sehemu mbalimbali ndani ya uingereza (Portland spy-ring). Huyu bwana alikuja kukamatwa baada ya uingereza kutonywa na CIA, hivyo akafunguliwa mashtaka ya uhaini .Lakini kesi yake ilisitishwa kusikilizwa na mahakama za uingereza kutokana na mahakama kutokuwa na uhakika na jina lake. Alirudishwa Moscow kutokana na kubadilishana wafungwa (swapping). baina ya uingereza na urusi. Hii ni baada ya kukamatwa kwa mfanyabiashara wa uingereza nchini urusi kwa tuhuma za ujasusi.
Pia Oleg Alitambulishwa kwa bwana mmoja aliyeitwa Vilyam Genrikhovich fisher au jina lingine Rudolf Abel. Huyu alikuwa anafanya ujasusi ndani ya marekani kama illegal na alikamatwa baadaye na kuhukumiwa miaka 20 jela. Lakini marekani walibadilishana na urusi pamoja na mfungwa wa kimarekani aliyeitwa Gary powers aliyekuwa rubani wa ndege iliyotunguliwa ndani ya anga la Soviet aina ya U-2 spy plane mwaka 1962.
Na pia mwisho bwana Oleg Alitambulishwa illegal mwingine aliyekuwa raia wa uingereza aliyejulikana kama Kim Philby. Huyu bwana aliajiriwa na NkVD kabla ya kuwa KGB mwaka 1934 .huyu alikuwa anafanya kazi idara ya ujasusi ya M16 uingereza lakini anatoa Siri za idara yake na kuzituma huko Russia na baada ya kuona mchezo wake ni hatari endapo akikamatwa na uingereza akaamua kutokomea Moja kwa Moja urusi 1963.hili lilifedhehesha sana uingereza wakati huo. Ndivyo ilivyokuwa utambulisho
Bwana Oleg miaka miwili baada ya kujiunga na idara hii ya directorate S alitambua rasmi Sasa ameingia kwenye dunia nyingine kabisa tofauti na binadamu wa kawaida . Hii ni kwa sababu ya kujua mambo mazito katika ulimwengu wa kijasusi ndani ya muungano wa kisoviet.
Mbali na kuwa JASUSI bobevu ,aliamini hataweza kutumwa kama illegal kukusanya taarifa za Siri kwenye nchi nyingine .
 
IMG_20230424_194858_897.jpg

Bwana Oleg akiwa rasmi afisa wa KGB


IMG_20230424_194915_975.jpg

Makao makuu ya idara hiyo y KGB karibu na Kremlin wakati huo
 
SEHEMU YA 5

Kiukweli mama yake Oleg , hakufurahishwa sana na mwanaye huyu mdogo kujiunga kitengoni. Hii ni kwa sababu ya historia na misukosuko aliyopitia .Alimwona kama mwanaye amejiunga na idara ya mashetani waliohusika kuyaharibu sehemu ya maisha yake,Sasa mwanaye naye anajiunga huko Tena .hakika kulimchanganya sana mwanamama huyu. Lakini mwanaye baada ya kurejea kutoka ujerumani mashariki Alimwona mama yake kama Hana furaha kabisa Japo ilikuwa ni kazi yenye status ya Hali ya juu kwa wakati huo. Oleg alimwambia mama yake kwamba hatakuwa anafanya kazi ndani ya KGB hapo Russia Bali kama afisa mwakilishi (balozi ) nje ya nchi ya urusi. Alijaribu kumshawishi sana mama yake asiichukulie kazi ya kitengo in negative way.ila ndio hivyo mwana mama hakuafiki kabisa moyoni mwake Japo hakuwahi onyesha waziwazi. Kwa kifupi Olga na mmewe mzee Anton hawakuwa pride na mwanao kuifanyia kazi kitengo ,lakini watafanyaje Sasa ,kitengo kishamchagua..
Baada ya kurudi kutoka ujerumani mashariki kwenye field yake ya mwisho ,alikutana na rafiki yake, stanislav kaplan kwenye mapumziko mafupi karibu na fukwe za bahari nyeusi. Waliamua kukutana kwa mara ya mwisho kama raia wa kawaida kabla ya kujiunga rasmi kuwa maafisa wa wa ujasusi kwenye nchi zao . Kwa mfano stanislav baada ya kumaliza mafunzo hapo Moscow alitarajiwa kujiunga na idara ya ujasusi ya Czechoslovakia iliyojulikana kama StB. Walikutana ,wakanywa ,wakijipongeza, vilevile wakipeana michapo ya totozi walizozifukuzia,miziki, na zaidi wakipondea mfumo mzima wa kikomunisti uliokuwa unatawala nchi zao. Vilevile stanislav akampa Oleg kijarida kidogo Cha mashairi ya kumponda Stalin kilichoandikwa na Yevgeny Yevtushenko kilichokuwa banned nchini urusi kabla ya kuachana.
Baada ya kutengana na rafiki yake bwana Oleg alihitajika kufika kwenye academy ya KGB iliyojulikana kama "Red banner".elite training academy. Hii akademi ipo porini maili 50 kaskazini ya Jiji la Moscow. Hii akademi ilipewa codename "school 101".
Hapa bwana Oleg pamoja na Maafisa wenzake wa KGB 120 walipewa mafunzo ya mwisho kabisa .walizamishwa kwenye Siri nzito za mfumo wa kisoviet.walifundishwa namna ya kuwatambuana wao kwa wao ,combat skills, kutumia silaha za aina mbalimbali. Vilevile walifundishwa kutumia lugha za uficho wanapowasiliana wao kwa wao. Na la Zaidi na kubwa zaidi walifundishwa namna ya kukwepa kufuatiliwa endapo wanahisiwa ni ma spy .( " surveillance detection). Mafunzo haya pia yalijukulina kama dry-cleaning au proverka kwa kirusi. Hapa wanafundishwa namna ya kuhisi kama unafuatiliwa ,namna ya kukwepa kama unafuatiliwa kwa njia ya kutotambulika na
kumchanganya anayekufuatilia kwa kumkwepa kwa ustadi wa Hali ya juu.
Walifundishwa pia namna ya kutuma na kupokea infos baina yao wakiwapo kazini ,kuacha signal , kutumia wino wa Siri kuandikia,matumizi ya kamera ,vinasa sauti .n.k. Pia maafisa waliotarajiwa kufanya kazi nchi za magharibi walipewa semina za kutosha kuhusu nchi hizo ikiwemo tamaduni , lugha n.k. Walifanyiwa kama ibada ya kukiri imani na kuutumikia mfumo wa kistalini na ukomunisti kwa ujumla.Na mwisho waliapizwa viapo vizito vizito na manuizo ya kutosha na rasmi kuwa maafisa wa KGB.
Baada ya hayo yote bwana oleg alipewa jina lake rasmi la kijasusi.Na mfumo huu wa kupewa jina lako la kispy lilikuwa linafanyika randomly kwa kuchaguliwa jina kwenye list ndefu ya majina yaliyoandikwa kwenye kitabu maalumu. Jina analopewa afisa wa KGB kikanuni lilipaswa kufanana na jina lako rasmi ulilopewa na baba na mama yako. Kwa mfano bwana Oleg alipewa jina la Guardiyetsev. Kulikuwa Kuna sababu ya kupewa jina la kijasusi linalofanana kidogo na jina lako orijino. Hii ilisemekana kwamba ikatokea mtu anakufahamu kwa jina lako halisi , halafu akakuita kwa jina lako hilo, isije ikamchanganya ambaye anakujua kwa jina lako la kijasusi , kwa maana atahisi amesikia vibaya kutokana pseudonym ya majina hayo na yatakavyotamkwa.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa bwana Oleg , na pia kama sehemu ya kuwa afisa rasmi , ilikuwa ni lazima kwa maafisa hao kujiunga na chama Cha siasa Cha nchi yao .communist party. Kulimfanya ku doubt sana lakini ndivyo utaratibu ulivyotaka. Mpaka kufikia majira ya kiangazi mwaka 1963 ,bwana Oleg alikuwa rasmi Sasa ni afisa wa KGB.
Hivyo mwaka huo tarehe 20 august alihitajika kufika makao makuu ya KGB kwenye idara ya FCD. Jengo Hilo la makao makuu lilikuwa na karibu na Kremlin. jengo Hilo lililotumiwa na KGB wakati huo lilikuwa kama hekalu ambalo ni jengo la idara ya bima la urusi. Sehemu ya jengo hili ilikuwa na ofisi za wakubwa wa kitengo,sehemu nyingine ya jengo ilikuwa stoo ya kuhifadhia archives na documents mbalimbali na sehemu nyingine ilikuwa na torture cells.
Baada ya kufika idarani na kuanza rasmi, majukumu yake yalikuwa ni kupitia document na nyaraka za maafisa wa ujasusi waliotumwa nje ya nchi,kupokea taarifa zao za kijasusi na kuzihifadhi. Pia alikuwa na kazi ya kufoji baadhi ya nyaraka kama pasi za kusafiria ,kutengeneza utambulisho bandia kwa majasusi na vilevile kuwapokea waliokuwa wanarudi kutoka kwenye majukumu ya kijasusi.
Mtu aanzapo majukumu ya kazi ya kuajiriwa lazima tapewa orientation za hapa na pale na pia kufahamu wafanyakazi wenzako wa hapo kazini na ma legend wa idarani. Ndivyo ilivyokuwa kwa bwana Oleg. Hapo kwenye idara ya FCD au Derectorates S, Oleg alitambulishwa kwa so called mashujaa wa kijasusi hapo ofisni. Kwa mfano Alitambulishwa kwa bwana mmoja aliyeitwa konon trofimovich au jina rasmi la kijasusi kama Gordon Arnold Lonsdale, aliyekuwa anafanya kazi ya ujasusi kama illegal kwenye nchi nyingine. Jina hili la Gordon Arnold lilitokana na jina la mtoto mdogo wa kanada aliyefariki dunia miaka kadhaa nyuma ,hivyo mwaka 1943 KGB wakaamua kumpa jina hili bwana konon kwa kuwa alikulia marekani tokea akiwa mdogo na kuongea fluent English. Inasemekana huyu alikuwa akiishi London akiwa kama muuza boligamu au bablishi.kazi yake hapo London ilikuwa kukusanya taarifa za kijasusi za jeshi la majini la uingereza na pia kupandikiza majasusi wengine sehemu mbalimbali ndani ya uingereza (Portland spy-ring). Huyu bwana alikuja kukamatwa baada ya uingereza kutonywa na CIA, hivyo akafunguliwa mashtaka ya uhaini .Lakini kesi yake ilisitishwa kusikilizwa na mahakama za uingereza kutokana na mahakama kutokuwa na uhakika na jina lake. Alirudishwa Moscow kutokana na kubadilishana wafungwa (swapping). baina ya uingereza na urusi. Hii ni baada ya kukamatwa kwa mfanyabiashara wa uingereza nchini urusi kwa tuhuma za ujasusi.
Pia Oleg Alitambulishwa kwa bwana mmoja aliyeitwa Vilyam Genrikhovich fisher au jina lingine Rudolf Abel. Huyu alikuwa anafanya ujasusi ndani ya marekani kama illegal na alikamatwa baadaye na kuhukumiwa miaka 20 jela. Lakini marekani walibadilishana na urusi pamoja na mfungwa wa kimarekani aliyeitwa Gary powers aliyekuwa rubani wa ndege iliyotunguliwa ndani ya anga la Soviet aina ya U-2 spy plane mwaka 1962.
Na pia mwisho bwana Oleg Alitambulishwa illegal mwingine aliyekuwa raia wa uingereza aliyejulikana kama Kim Philby. Huyu bwana aliajiriwa na NkVD kabla ya kuwa KGB mwaka 1934 .huyu alikuwa anafanya kazi idara ya ujasusi ya M16 uingereza lakini anatoa Siri za idara yake na kuzituma huko Russia na baada ya kuona mchezo wake ni hatari endapo akikamatwa na uingereza akaamua kutokomea Moja kwa Moja urusi 1963.hili lilifedhehesha sana uingereza wakati huo. Ndivyo ilivyokuwa utambulisho
Bwana Oleg miaka miwili baada ya kujiunga na idara hii ya directorate S alitambua rasmi Sasa ameingia kwenye dunia nyingine kabisa tofauti na binadamu wa kawaida . Hii ni kwa sababu ya kujua mambo mazito katika ulimwengu wa kijasusi ndani ya muungano wa kisoviet.
Mbali na kuwa JASUSI bobevu ,aliamini hataweza kutumwa kama illegal kukusanya taarifa za Siri kwenye nchi nyingine .
Aisee mambo mengi mda mchache wallah mbona hii Dunia ni trust nobody Kwa mtindo huu, kumbe majasusi wanayo mengi vifuani mwao.
Huu Uzi wako una madini mno yakufungua macho, na nimejifunza mengi mhhh but I wonder ka Kwa majasusi wa iliyokuwa USSR waliingia mitengo how about our country jinsi rushwa ni kipaumbdle?
Pia why hao ma illegal majasusi huishwa kuja kudakwa ni Nini huenda wrong hadi kushtukiwa?
 
Aisee mambo mengi mda mchache wallah mbona hii Dunia ni trust nobody Kwa mtindo huu, kumbe majasusi wanayo mengi vifuani mwao.
Huu Uzi wako una madini mno yakufungua macho, na nimejifunza mengi mhhh but I wonder ka Kwa majasusi wa iliyokuwa USSR waliingia mitengo how about our country jinsi rushwa ni kipaumbdle?
Pia why hao ma illegal majasusi huishwa kuja kudakwa ni Nini huenda wrong hadi kushtukiwa?
Kuchomeshwa..kuchomeshana.wao kwa wao .. tutaona huko mbeleni
 
Aisee mambo mengi mda mchache wallah mbona hii Dunia ni trust nobody Kwa mtindo huu, kumbe majasusi wanayo mengi vifuani mwao.
Huu Uzi wako una madini mno yakufungua macho, na nimejifunza mengi mhhh but I wonder ka Kwa majasusi wa iliyokuwa USSR waliingia mitengo how about our country jinsi rushwa ni kipaumbdle?
Pia why hao ma illegal majasusi huishwa kuja kudakwa ni Nini huenda wrong hadi kushtukiwa?
Nakuona umeiwahi shemela cariha
 
SEHEMU YA SITA

Kama afisa yoyote wa KGB ,bwana Oleg alikata shauri na kuamua kuoa licha ya kazi iliyokuwa na majukumu mazito na hatarishi. Alimuoa Yelena Akopian mwanadada aliyekuwa na umri wa miaka 21 , mwalimu wa lugha ya kijerumani. Alikuwa ni nusu mwa Armenia na nusu mrusi na walikutana na oleg kwenye harakati za majukumu ya kazi za ujasusi. Kama tu Oleg, mwanadada huyu alikuwa anapenda maisha ya umagharibi na alikuwa ni wale akina dada wenye itikadi za ufeministi.
Kuoa kwa afisa wa KGB kwa wakati huo ilikuwa pia ni kigezo Cha kupanda ngazi ya cheo. Na ndivyo ilivyokuwa.
Baada ya kufunga ndoa ,mwishoni mwa mwaka 1965 ilikuwa ni siku iliyosubiriwa kwa hamu kubwa . Ilitoka post ya kufanya kazi ya ubalozini nchini Denmark. Ilitarajiwa kazi official ilikuwa ni ku deal na visa na pasi za kusafiria,usajili wa ndoa ,na kazi zingine official kama afisa wa ubalozini . lakini kazi yake Hiyo ilikuwa ni Kama cover kwa juu , majukumu yake kama JASUSI ilikuwa ni kupandikiza majasusi ndani ya nchi ya Denmark,kupokea infos,kutoa fund kwa majasusi na vilevile kuajiri na ku register majasusi. Kwa kifupi alikuwa na majukumu ya kusimamia shughuli zote za ujasusi nchini Denmark.
January 1966 majira ya kuanguka kwa barafu ndio siku bwana Oleg na mkewe Yelena walitua ndani ya Copenhagen. Kwao Jiji Hilo waliona kama wameingia kwenye ulimwengu wa kubuni wa fairy tales. Kwa kifupi Copenhagen lilikuwa ni Jiji safi, la kisasa na la kitajiri. Waliona kama wameingia mbingu nyingine ukilinganisha na Jiji lao la nyumbani la Moscow. Vilabu, maduka ya pombe,vyakula vya kila aina,bendi za miziki,maktaba na bustani za maua ya kila rangi yaliwavutia . Na ni Jiji ambalo everyone minds his/her own business . Na likiwa na polisi wachache mitaani na visa vichache vya uhalifu.
Walifika kituo chao Cha kazi . Ubalozi wa Soviet ndani ya Copenhagen kilichokuwa chini ya mwakilishi /ambassador Leonid yetsev ulikuwa kwenye kitongoji Cha kristianiagade kaskazini mwa Jiji .ilikuwa ni jengo la kisasa lenye bustani za kuvutia,kwao waliona ni kama villa park au aina ya resort ya kisasa . Sehemu ya uwanja wa michezo pamoja na social club. Aliishi yeye na mkewe kwenye apartment ya kisasa na kukabidhiwa Volkswagen beetle pamoja na euro 250 cash kila mwezi kama advance.
Ndani ya ubalozi huo kulikuwa na wafanyakazi 20 Maafisa sita tu kati ya hao walikuwa ni wanadiplomasia na wafanyakazi wa kawaida ila wote waliobaki walikuwa wanafanya kazi kwa niaba ya KGB,GRU. Yaani walikuwa ni majasusi.
Ndani ya ubalozi huo bwana Leonid yetsev ambaye ndie balozi mwakilishi alikuwa anajua kabisa asilimia kubwa ya wafanyakazi wake hapo walikuwa ni incompetent, hawakuwa serious na kazi na wavivu. Wengi wao walitumia pesa vibaya kulewa,kujirusha na totozi n.k kuliko kuzifanyia shughuli za kijasusi.Lakini kwa bwana Oleg alimuona mfanyakazi anayejituma,mchapakazi na pia alikuwa ni mwelewa wa lugha ya ki danish. Bwana Oleg majukumu yake yalikuwa ni kuprocess visa ,kuandaa nyaraka mbalimbali n.k .ila shughuli ujasusi yeye alianza kuzifanya muda wa lunch.Hii Ina maana kwamba wakati wa chakula siyo rahisi kushtukiwa kwa maana wakati mnakula huku mpo mnapiga stori na marafiki zako mnapeana na kubadilishana infos za kijasusi pasipo kushtukiwa kiurahisi.
Majukumu yake makubwa yalikuwa ni kusimamia mtandao mzima wa majasusi waliotapakaa pasipo pia kukutana nao USO kwa USO ,na pia asiwafahamu sura Wala Majina yao kabisa. Kwa mfano Oleg na majasusi wenzake walikuwa wanawasiliana kwa njia ambazo ni ideal zisizoweza kutambulika kiurahisi. Jasusi anaweza kuacha Ganda la chungwa kwenye Yale mabenchi sehemu za umma akimaanisha nipo hatarini, nafuatiliwa.Au unaweza kukuta mbegu za apple zimeachwa mahali ikiwa na maana jasusi huyo anaondoka nchi hiyo. Kwa mfano bwana Oleg siku Moja aliacha msumari uliokunjwa kwenye dirisha la choo Cha umma ,akiwa na maana jasusi Fulani akiuona akachukue kifurushi cha fedha kilichofichwa kwenye dustbin sehemu Fulani ya mji. Na labda jasusi huyo baada ya kupokea fedha hizo ,Ili kuonyesha amepata mzigo ,angeacha kizibo Cha bia kilichokunjwa kwa meno hapo kwenye dirisha la chooni. Hivyo ndivyo mambo ya kijasusi yalivyokuwa Yana operate.
Kwa kuwa bwana Oleg kazi yake kubwa ilikuwa ni kupandikiza majasusi ndani ya Denmark alihitaji pia kupata access ya registration ya raia wa nchi hiyo.
Ni kwamba nchini Denmark ,rekodi za vizazi na vifo vinasajiliwa na kanisa la kiprotestant la nchini humo . Hivyo Oleg aliamua kufanya forgery ya majina kuingizwa kwa ajili ya kazi za kijasusi. Hivyo alianza urafiki na kuwashawishi makasisi wa kilutheri Ili aweze kuwa na access na daftari la rekodi za usajili la kanisa Hilo. Hivyo alifanikiwa kufoji na kuingizwa kwa majina ya raia wa ki danish ambao kiuhalisia hawakuwahi kuwepo . Hii ni kwa sababu majina hayo angeyatumia kwenye ku process visa na kutengeneza alias hapo ubalozini kwa ajili ya majasusi aliokuwa anawajibika kuwasimamia.
Kiukweli mbali na kuwa mfanyakazi hapo ubalozini ,Oleg alionja ladha halisi ya uhuru wa magharibi. Alipenda miziki,watu wake,na pia zaidi uhuru kwenye swala Zima la mapenzi. Ikumbukwe nchi ya Denmark ndio nchi ya kwanza duniani ku legalize homosexuality miaka ya 1960s. Nchi hii swala la ngono lilikuwa ni kipaumbele kwao kama Huku kwetu kipaumbele ni kutafuta Hela .kwao ngono ilikuwa kama ibada na chakula kwao.
Kwa mfano Siku Moja aliwahi nunua majarida mawili Moja likiwa la mapenzi ya jinsia moja kwenye duka kubwa la bidhaa za ngono, kwa ajili ya kwenda kumuonyesha mkewe. Kiukweli haya mambo yalipigwa marufuku nchini mwao . Ni kwamba Oleg alipata a real taste of liberty.
Lakini wanasema ukiwa ugenini ni ugenini tu.
Shirika la ujasusi la Denmark PET( Politiets Efterretningstjeneste) lilikuwa ni shirika dogo Japo lilikuwa effective na vigilant. Majukumu yake yalikuwa ni Yaleyale kama mashirika mengine ya kijasusi duniani . Walianza kumuweka huyu bwana mdogo kwenye radar zao kufuatilia nyendo zake kimya kimya .
Kutokana na itikadi za kikomunisti ni kwamba wa danish yaani hao PET walikuwa na utaratibu wa mara kwa mara wa kufuatilia nyendo za maafisa wa ubalozi wa urusi.Na pia baadhi ya simu za hapo ubalozini zilikuwa zinasikilizwa kwa Siri kwa kuwa zilikuwa tayari zimefanyiwa bugging. Lakini pia ma technician wa KGB nao walikuwa wamefanikiwa kupenyeza mitambo Yao ya kunasa mawasiliano ya pET. Kwa kifupi kila mmoja alikuwa anamwinda mwenzake bila kujua wanawindana.
Oleg na mkewe walikuwa wanasaidizana kusikiliza mawasiliano ya Siri kutoka kwenye ofisi za PET na kuzi decode na kuzitafsiri Hadi kwenye lugha ya kirusi na kuzituma home.
Kwa kuwa bwana Oleg naye alikuwa tayari alikuwa ameshakuwa suspect na idara ya PET, alipewa jina la uficho Ili asisanuke kama naye yupo kwenye radar za majasusi. Alipewa jina la uncle gormsson. Hili lilikuwa jina la mfalme Harald gormsson mfalme wa Denmark wa Karne ya kumi.
Ni kwamba PET walikuwa na mashaka kiasi kama kweli uncle gormsson au Oleg jasusi wa KGB anayefanya kazi chini ya formal diplomatic cover. Wakaamua kuweka mitego ......
Jioni Moja bwana Oleg na mkewe walipokea mwaliko kuhudhuria kupata chakula Cha jioni kwa rafiki yake mmoja aliyekuwa afisa polisi wa kawaida . Wakiwa wametoka kikosi Cha majasusi wa PET waliingia kwenye apartment Yao na kupandikiza vipaza sauti sehemu mbalimbali ndani ya nyumba hiyo. Lakini kwakuwa jasusi ni jasusi bwana Oleg kabla ya kutoka alitilia mashaka huo mwaliko na akaamua kuchukua tahadhari. Kwenye Mlango wa kutokea nje ya nyumba Yao sehemu ya chini kabisa ya mlango alibonyeza matone kadhaa ya super glue . Yaani tone likawa limeshikana na mlango sehemu ya chini na sakafu. Hii ni kwa majibu ya mafunzo aliyopata SCHOOL 101.Wakati aliporudi alikuta ile glue imeachana .Hivyo akajua ndani kwake Kuna watu waliingia na kufanya Yao. Tangia siku hiyo akawa makini na kila atakachokisema na kuongea na mkewe wakiwa nyumbani.
Wanasema taaluma ya ujasusi ni kama mchezo wa paka na panya ,mchezo wa kuviziana na kuwindana.
Ingawaje maafisa wa KGB walikuwa na uwezo wa kukwepa kufatiliwa(dry -cleaning) na majasusi wa PET ,nao pia PET hawakuwa wachache ku target na kuwafuatilia maafisa wa ubalozi wa urusi hapo Denmark hususan kwa target Yao bwana Oleg.
PET ilikuwa inamfuatilia Oleg Hadi mitaa aliyokuwa anatembelea hususan maduka ya kuuza bidhaa za ngono. Kilichowapa alama ya taa nyekundu ni kwamba inakuwaje kwa afisa wa kiurusi anapendelea kusoma majarida ya mapenzi ya jinsia Moja /gay magazine. Kila nyendo za bwana Oleg zilikuwa noted kwa umakini wa Hali ya juu kwenye file lake. Na kwa mara ya kwanza jina lake lilileta question mark.
 
Back
Top Bottom