Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

Tarehe 18 Mei 1985: Shirika la kijasusi la KGB kulikuwa na idara iliyojulikana kama Directorate K

11

Jioni Moja tarehe 2 November 1973 , Oleg na mkewe pasua kichwa Yelena ndio kwanza walikuwa wamemaliza dinner,wakasikia mlango ukigongwa . Kwenda kufungua mlango ,Oleg hakuamini alikuwa ni rafiki yake wa siku nyingi bwana stanislav kaplan. alishtuka na vilevile aliogopa kwa wakati mmoja. kwa furaha wanaume Hawa wawili walipeana mikono na kusalimiana kwa furaha akimsihi kuingia ndani.Laiti Oleg laiti angejua bwana stanislav hakuwa peke yake. mkewe alihis kitu kisicho Cha kawaida kwa mgeni wa wakati ule.
Basi bwana Oleg alimkaribisha stanislav na glass ya whiskey na kumtambulisha kwa Yelena na Convo za hapa na pale. Stanislav alimwelezea Oleg kwa Sasa (wakati huo) anafanya kazi kwenye shirika la bima la Canada na amekuja hapo Denmark kwa ajili ya mpenzi wake mdanish. Bwana Oleg alimcheki rafiki yake usoni kwa maelezo aliyokuwa anayatoa ,Kisha akacheki na mkono ambao Stan alikuwa ameshika glass ya whiskey akatambua jambo kwa huyu rafiki yake anamficha. Jasusi ni jasusi tu. Oleg alitambua best yake anamwongopea. Huyu stanislav alitumwa. Stanislav akaendelea kumweleza Oleg jinsi alivyoondoka Czechoslovakia na kutimkia Bulgaria Hadi kufika Canada kupitia ufaransa.
Oleg akawa anapata tu baadhi ya hints kutoka kwa maelezo ya best yake. Baada ya kumaliza whisky alinyanyuka Ili kuondoka na kumwambia kama wangeweza kuonana kwenye mgahawa mmoja hapo mjini Copenhagen waweze kuongea kesho .oleg akakubali.
Na kweli bwana Oleg alifika ila kwa kuchelewa kwenye appointment akijihakikishia hakuwa anafuatiliwa kwa Siri( he was wrong ). stanislav alifika wa kwanza akimsubiri rafiki yake kwenye meza iliyokuwa karibu na dirisha la vioo. Wakawa wanapiga stori mbili tatu , hususan uvamizi wa urusi nchini Czechoslovakia na yaliyoendelea huko na mambo mengine mengi .wakati Hawa marafiki wakiwa wanaongea upande wa pili kachero wa M16 mike Stokes ( muda huo alijifanya kama mtalii akijifanya anasoma tourist guide book[emoji39][emoji39][emoji1]). Alikuwa akiwafuatilia kwa karibu akiwa amekaa kwenye meza iliyo nje ya mkahawa wa jirani ng'ambo ya pili ya barabara . Kumbuka stanislav na Oleg walikuwa wamekaa kwenye meza iliyopo karibu na dirisha hivyo kwa mtu aliye nje ilikuwa rahisi kuwaona kwa uzuri.
Lengo la stanislav ni kujua maoni ya rafiki yake kuhusu nchi yake kuvamiwa na jinsi yeye anavyoshirikiana na mashirika ya kijasusi ya west. Hapa bwana Oleg alikuwa anafanyiwa assessment ya kitaalamu sana . maana taarifa zake A to Z. wanazo. Baada ya kupata mlo wakapeana mikono kuagana na mwishowe stanislav akatokomea kwenye umati wa watu. Hakukuwa na mazungumzo seriously sana waliyoongea au ahadi zozote walizoahidiana . Ila bwana oleg tokea hapo akawa vigilant kuliko kawaida . kwamba Alihisi rafiki yake ametumika kumpima imani kuhusiana na kufanya kazi na idara za ujasusi za west.

stokes na stanislav walikutana hotelini jijini hapo Copenhagen Ili kupeana debriefing za mchakato wao wote na mwisho stokes akaruka kwa ndege Hadi London kupeleka report kwa partner wake guscott na kuchambua vilivyo. kazi nyingine akaachiwa bwana bromhead hapo Denmark.
Ilikuja kubainika kupitia manjagu wa PET kisha wakawatonya M16, Bwana Oleg Huwa anacheza mchezo wa badminton kila asubuhi na mrembo mmoja hivi kwenye kiwanja kimoja kilichopo pembezoni mwa mji kidogo. Huyu mrembo alibainika kwa jina la Ana.
Hivyo bwana bromhead akaamua kufanyia kazi hizi report za ujasusi na kuingia field. Na kweli bwana bromhead akajitosa Hadi kwenye kitongoji hicho asubuhi Moja na kumuona Oleg akiwa na mrembo huyo wakiingia ndani ya kiwanja kimoja.Aliwafuatulia kwa Siri akiwa ndani ya gari ambalo alilitoa namba zile za diplomatic na kuweka private number Ili asiweze kugundulika. Na kweli aliweza kumuona Oleg Gordievsky akiwa na mrembo huyo. bromhead na Oleg kwa mara nyingine tena waliweza kuonana na Oleg hakushtuka alishawahi mwona kwenye hafla kadhaa . Baada ya michezo kumalizika na maongezi ya hapa na pale bromhead akaomba wakutane sehemu wazungumze . Oleg alikubali ila kwa sharti sehemu iwe private kidogo. Wakapendekeza wakutane kwenye hotel Moja inayoitwa Østerport hotel iliyo karibu na railroad inayoelekea zilipo ofisi za ubalozi baada ya siku tatu.. Baada ya kuachana na kuagana , bromhead alipofika ofisini direct akanyanyua simu akawatonya M16 huko London mpango wake kukutana na Oleg privately.
Oleg naye alipofika ofisini mwake naye akamwambia balozi boss wake bwana mogilevchik kwamba Kuna afisa mwenzake mfanyakazi wa ubalozi wa uingereza kamwalika kwenye lunch. Boss wake hakuwa na jibu . Hii taarifa ikafika Moscow Hadi kwa bwana Dimitri Yakushin boss wao. Na kweli naye akamruhusu bwana Oleg asikatae mwaliko aende . maana waliona hii kwao ni chance ya kumtumia bromhead kupata infos za western countries hususan uingereza. Nao upande wa kina bromhead walikuwa na lao kichwani.
 
n
IMG_20230427_103017_687.jpg

Oleg akiwa kwenye mchezo wa badminton
 
Sehemu 02.

SEHEMU YA PILI

Bwana Oleg Gordievsky alizaliwa ndani ya KGB ,ikamkomaza,ikamtwist vilivyo na almanusura imhuharibie maisha . Kufanya kazi ndani ya idara kubwa ya kijasusi ndani ya muungano wa Soviet,kwake ilikuwa ni heshima kubwa sana na ni kazi iliyokuwa kwenye damu yake. Kwani baba yake amefanya kazi ndani ya shirika Hilo maisha yake yote. Familia ya Gordievsky iliishi kwenye apartment za shirika Hilo na walipewa special treatment na favor maalumu kwa kuwa wao walikuwa ni familia ya kitengo.

Shirika la kijasusi la KGB(komitet gosudarstvennoy bezospasnosti) kwa kiswahili sanifu ni kamati ya ulinzi la kitaifa, ilikuwa ni taasisi imara ya usalama kuwahi kuundwa hapa duniani. Shirika Hili lilizaliwa kutoka kwenye kikundi kidogo Cha majasusi watiifu wa mzee Stalin. Kazi Yake ilikuwa kukusanya taarifa nje na ndani ya muungano wa Soviet ,kutoa ulinzi ndani ya taifa ,pamoja na maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya kijamaa.

Kwa kifupi shirika Hili lilikuwa limetawala nyanja zote za kimaisha kwa wale wote waliokuwa wapo chini ya muungano wa ki Soviet.

Lilikuwa ni shirika lililoajiri na kupandikiza majasusi duniani kote kwa ajili ya ,kukusanya ,kuiba ,na pia kununua taarifa mbalimbali za Siri ikiwemo za kijeshi, kisiasa, silaha pamoja na taarifa za kisayansi na teknolojia. Inakadiriwa kipindi hicho shirika likiwa katika kilele Cha mafanikio ilikuwa na ma agent takribani milioni na zaidi.

Kwa upande wa nchi za kimagharibi hii taasisi ilitazamwa kama zana ya kuwatia watu hofu,kutii wasichokijua,kuwatesa na kuwanyanyasa raia wake kidhalimu. Ilitazamwa kama kundi la kimafia chini ya mwavuli wa kikomunisti lenye kusambaza propaganda za kijamaa zilizopitwa na wakati .

Lakini kwa waliokuwa wanaishi chini ya muungano wa ki Soviet wao walichukulia KGB kama mlinzi wao,alama ya uzalendo na Utiifu kwa taifa na mamlaka,pamoja na ngao ya kuwalinda Raia dhidi ya umagharibi. Kuwa memba wa KGB ilikuwa ni heshima na sifa na pia alama ya ufahari kwa wakati huo.

Hivyo basi bwana Oleg hakuwa na la kupingana nalo zaidi ya kufuata nyendo za mshua wake bwana Anton lavrentyevich Gordievsky, na kuwa afisa wa KGB.

Baba yake Oleg kabla ya kuwa afisa wa KGB ,alikuwa ni mwalimu .lakini baada ya mapinduzi ya mwaka 1917 akaamua kujiunga na kuwa mwanachama rasmi wa chama Cha kikomunisti. Kilichomfanya baba yake Oleg kujiunga na ukomunist ni itikadi za mzee Stalin , ambazo zilikuwa Kali.
Alijiunga na chama Cha NkVD( baadaye sana ilimezwa ndani ya KGB) au taasisi ya kikomunisti kwa ustawi wa watu. Lengo la hii taasisi au chama ni kulinda maslahi ya kikomunisti ,kutoa ulinzi na vilevile kusambaza propaganda pamoja na kupambana na maadui wa urusi. Mzee Stalin alitangazia umma kwamba maadui wa urusi ni mabepari , mashoga,majasusi wa utawala uliopita,wayahudi , maofisa wa serikali wenye mrengo wa kibepari n.k. Hivyo bwana Anton alijitolea kwa udi na uvumba katika kulinda itikadi za kikomunisti. Alijitolea kufundisha propaganda kwenye kambi za kijeshi na taasisi za elimu . Tuseme kwa kifupi alikuwa ni mwenezi kama polepole.
Na katika kipindi hicho watu walianza kuonja ladha ya ukomunisti .watu walipotezwa, wengine walinyang'anywa Mali ,kufungwa na pia wengine walilazimishwa kuhama nchi. Na kubwa zaidi wengi walikufa na njaa kutokana na uzalishaji kuzorota mashamba na maghala kuchukuliwa na serikali. Japo mzee Anton alikuwa ni mwanachama mtiifu kwa chama na serikali lakini nafsi ilikuwa inamsuta.
Alimwoa Olga nikolayevna gornova mrembo wa miaka 24 aliyekuwa anafanya kazi kwenye ofisi za takwimu. Walihamia Moscow kwenye apartments zilizokuwa spesho kwa ajili ya maafisa wa NkVD. Mtoto wao wa kwanza aliitwa Vasili aliyezaliwa 1932. Mtoto wao wa pili alizaliwa miaka sita baadaye yaani 1938,aliyeitwa Oleg antonyevich Gordievsky tarehe 10 October.
Mtoto wao wa tatu aliitwa marina aliyezaliwa miaka Saba baadaye. Kwa kifupi ilikuwa ni familia ya kitengo. Watoto walikuwa vizuri na pia stahiki na treatment za kutosha walizipata kutoka serikalini kwa kuwa ni familia ya KITENGO. Familia ilikuwa na kulelewa katika itikadi za kijamaa ,na watoto walikuwa watiifu na wazalendo kwa serikali ya kisoviet. Waswahili wanasema kila familia Ina Siri zake . kwa nje familia ya mzee Anton ilionekana ni familia Bora na iliyostawi sana na majirani kuweza kuwa admire. Haikuwa hivyo. Mzee Anton nafsi ilikuwa inamsuta sana kwa mabaya aliyokuwa anayafanya kipindi Cha Stalin anashika hatamu. Mfano kupotezwa kwa watu,uporaji wa mashamba na vifo vilivyotokana na njaa.hii ilimsumbua sana nafsini mwake lakini alikausha na Siri yake moyoni. Mkewe , Olga hakuwahi kuukubali ukomunisti lakini atafanyaje ndio anaishi kwenye ndoa yenye itikadi hizo. Sababu ya kuchukia ukomunisti ni kwamba baba yake alinyang'anywa mashine zile za upepo za kuvuta maji ardhini na serikali,pia kaka yake alikamatwa kwa kosa la kupinga sera ya umiliki na kilimo Cha kwa pamoja na kupelekwa huko Gulag Jimbo lililoko mashariki mwa Siberia na kupotelea huko mazima. Pia aliwahi shuhudia majirani zake kipindi hicho wakifuatwa usiku na watu wasiojulikana na kuondoka nao asiwaone tena.


View attachment 2588392
Familia ya mzee Anton kushoto na wanao wawili marina na Oleg wakiwa na umri wa miaka kumi hivi

View attachment 2588393
Watoto wa mzee Anton Vasili,mdogo wao wa kike marina na Oleg Gordievsky.


Oleg na Vasili walitofautiana kwa umri wa miaka sita hivi.na walikuwa kipindi Cha vita. Kwa mfano Vasili akiwa mdogo, alishuhudia mateka wa kivita wa kijerumani wakipanga gwaride mitaa ya Moscow na kulazimishwa kutembea umbali mrefu wakinyanyaswa na kudhihakiwa kama wanyama. Baba Yao mara nyingi alisafiri sehemu mbalimbali za nchi kueneza propaganda za kikomunisti. Kwa upande wa Oleg ,yeye alikuwa ni mtu wa kujifunza na kusoma vitabu. Kwa umri wake mdogo alijifunza kusoma katekisimu ya ki orthodox yenye mrengo wa kikomunisti. Pia alikuwa ni mtu wa kujifunza lugha na hatimaye alionyesha uwezo mkubwa katika kujifunza kijerumani. Baba yake Oleg alikuwa kila akirudi lazima aje na magazeti yenye itikadi za kikomunisti hivyo akawa na wasaha wa kuyasoma. Ingawaje alikuwa anasoma vitabu vya propaganda dhidi ya magharibi alivutiwa na maswala, kadhaa ikiwemo lugha za huko. Rasmi Sasa Oleg alivyofika umri wa utineja akajiunga tuseme UVCCM ya huko iliyojulikana kama KOMSOMOL.
Oleg alikulia kwenye familia yenye upendo baba yake akiwa mwanachama rasmi wa KGB,na mama yake pia akiwa mke wa afisa ,mama wa nyumbani, lakini ndani ya mioyo Yao Hawa wanandoa wawili walikuwa wanafeki tu kwa nje lakini ndani mwao kulikuwa na vidonda kuhusu madhila ya mfumo mzima wa kikatili wa kikomunisti.hakuna aliyewahi jionyesha kwamba anadukuduku lake dhidi ya mfumo.
Kwa kipindi hicho Cha utawala wa Stalin familia ya Anton Gordievsky waliamini kwamba unaweza ukawa mtiifu kwa serikali ya kikomunisti , lakini ukawa una amini jambo lingine kwa Siri sana Japo ilikuwa ni jambo la hatari ya maisha. Kwa mfano hapa kwetu uwe mtiifu kwa serikali ya ccm lakini ndani ni mwanachama mtiifu kabisa wa upinzani.

Umahiri wa Oleg ulidhihirika akiwa na UVCCM Yao ya KOMSOMOL kwa kupewa medali ya silver kama kijana mwenye akili , shupavu,mwenye bidii katika michezo na vilevile mzalendo haswa kwa nchi yake .licha ya hayo yote Oleg Gordievsky alijifunza kuishi maisha ya aina mbili.
Mpaka hapa hii story imeandikwa na washinda vita, acha niendelee kuburudika....
 
Back
Top Bottom